mkuu unataka kusema kwa uchumi wa mtu mojamoja Tanzania ina afadhali kuliko Bangladesh?
mbona hata tukiangalia hizo GDP per capita figures za tanzania na Bangladesh bado zinaonesha sisi ni maskini kuliko hao Bangladesh, sijaelewa hapo.
Sijajikita sana kulinganisha Bangladesh na Tanzania. Nimejikita kwenye heading ya kulinganisha Bangladesh na taifa lolote Afrika, na kuonesha uchumi mkubwa si lazima uwe uchumi mzuri, nchi inaweza kuwa na uchumi mkubwa kutokana na kuwa na watu masikini wengi.
Nimetoa uchumi wa Bangladesh kulinganisha na Seychelles kwa GDP per capita.
Main point, ukubwa wa uchumi si kipimo kizuri cha uzuri wa uchumi. Hata masikini wengi wakiwa pamoja wanatengeneza uchumi mkubwa na kugawana umasikini tu.
Tunavyoilinganisha Bangladesh na Afrika tuangalie angalau GDP per capita.
2021 figures.
Bangladesh $ 2458
Seychelles $ 14,653
Mauritius $ 9,106
South Africa $ 7,055
Botswana $6,805
Cape Verde $ 3,293
Ivory Coast $ 2,549
Kwa hivyo utaona licha ya Bangladesh kuwa na uchumi mkubwa , watu wa Bangladesh hawajaweza kufanya "uchumi" vizuri na kufaidika zaidi kutoka uchumi huo mkubwa kulinganisha na watu wa nchi nyingi za Afrika.
Kitu kingine unachobidi kuelewa ni kwamba, nchi inaweza kuwa na uchumi mkubwa, halafu huo uchumi mkubwa ukawa unachukuliwa na makampuni makubwa ya nje.
Hili ni tatizo kubwa Bangladesh. Tatizo linaloweza ku explain kwa nini Bangladesh on paper ina uchumi mkubwa sana, lakini maisha ya watu ni ya umasikini mkubwa.
Bangladesh wanatengeneza sana nguo na viatu. Kwa cheap labor. Sasa mauzo ya hivi viatu na nguo yanavyofanywa katika soko la dunia, hesabu zinaonesha hela nyingi zimeenda Bangladesh, wakati makampuni makubwa yana njia kemkem za kukwepa kodi na kuhakikisha hela zinabaki kwao, kama vile kununua malighafi na mitambo kutoka kwa international affiliates at inflated prices.
Hapo ndipo utaona nchi inaweza kuwa na uchumi mkubwa, halafu sehemu kubwa ya huo uchumi mkubwa inaenda nje, na wananchi wake wanabaki masikini tu.
Bangladesh na uchumi wake mkubwa imezidiwa mpaka na Ivory Coast (GDP per capita 2021) nchi ya Afrika ambayo imetoka kwenye vita muda si mrefu uliopita.