Jenchede
JF-Expert Member
- Jul 22, 2014
- 237
- 503
Kwa kweli wanaopitisha sheria sijui huwa wanawaza nini hawangalii uhalisia wa maisha. Hawaweki sheria za kumsaidia mwananchi bali kumkomoaNi kweli kabisa utaratibu wa watu wa bima kupanga lazima umuweke mzazi wako ni wa kipuuzi kwa sababu kuna watumishi wengi hawajawahi kuwaona hao wazazi bali wamelewa na kusomeshwa na watu baki .Mfano wajomba shangazi au mama wakubwa au wadogo.Mara nafasi za wategemezi lazima awe mke wa ndoa mpaka uweke cheti hivi hawa mbwa hawajui kuna ndoa za kimila nazo ni halali ?Na watoto lazima uwe umewazaa mtumishi mwenyewe kama huna kizazi nafasi zinabaki huku unaendelea kukatwa mshahara wako.Ifike mahali sheria ibadilishwe Mwenye mshahara aweke watu anaotaka wanufaike kisheria pasipo kupangiwa na hao watu wa bima lasivyo kujiunga na bima ya afya kwa mtumishi iwe ni hiari.
Sent using Jamii Forums mobile app