Udhaifu wa Serikali hii tutakuja ona madhara yake baadaye. Leo ni ishara ndogo mojawapo

Ndio maana Hayati aliwahi kumuambia kama unataka kuachia ngazi achia, mlango uko wazi
Siku njema huonekana/huanza asubuhi, Wahenga walinena. Angeanza kwa vitendo kimya kimya yale anayoyesema kwenye hotuba zake, kwani Ada ya Mwungwana ni vitendo.
 
Umeme ukikatika kidogo utasikia ni sababu ya Rais Samia yuko madarakani, vibaka wakisumbua kidogo ni SSH, sasa eti hata mechi ya Simba/Yanga nayo ni Rais Samia.

Niwaambie Tanzania iko mikono salama chini ya Raia SSH. Tukose umeme, tuamiwe na vibaka, Simba na Yanga wasicheze bado nchi yetu ni nzuri sana kuliko ilivyokuwa chini ya DIKTETA Magufuli
 
watu wanafanya mzaha,lakini ukweli ni kwamba mpaka vibaka na majambazi wana imani na mama[emoji1][emoji1].
maana mama ni mlezi,mama ana huruma,mama ana ubinaadam.kifupi wana uhakika mambo hayataharibika hata iweje.
Hata kaya ambayo Mkuu ni mama, hakuna utaratibu unaoeleweka wa maisha. Ghafla madawa ya kulevya, kwa tani, yameanza kuingizwa nchini, muda si mrefu vijiwe vya wabugiaji vitashamiri
 
nchi hii kwa miaka 6 imekosa watu wanaothubutu.
Labda kama unaongelea kwenye uga wa soka pekee. Lkn kwenye uga wa siasa yupo jemedari aliyethubutu mpk kusababisha umeme wa pacemaker ya mwendazake kukatika, le gendare TAML.
 
 
sawa iko mikono salama hatukatai,ndio maana yanapoibuka madhaifu ya kijinga jinga tunashangaa,matutusa mnapotaka kusema mwendazake aliyafanya kwa udhaifu wake.

leo bimkubwa na miezi 2 tu,tayari maujinga kibao yanatokea pamoja ya kuwa na mikono salama.kwani aliyesema mechi iahirishwe katoa maagizo kwenye serikali ya jiwe!!!!!
 
Wewe unao uhakika alieahirisha mechi sio serikali, bali ni simba na yanga?
Uzuri Mimi sio mshabiki kinandakindaki hivyo bado akili ya kuhoji hayo bado ipo ,ila wengine wanaumwa kabisa kwa yaliyojiri,hata kuongea chochote kwa kuwa matarajio hayajatimia.
 
"Serikali ina ahirisha match ya Simba na Yanga eti sababu Mwinyi anazindua kitabu. Huu ni wendawazimu" Match imehaitlrisha kwa sababu Yanga wamesusa sio Serikali.
Yanga hawajasusa walifika uwanjani muda rasmi uliyopangwa kwa mujibu wa ratiba na kanuni za ligi lakini Simba hawakutokea uwanjani.Bashungwa,Karia na Mo Dewji ambao wote ni Simba ndiyo wanapaswa kulaumiwa.Mganga wao aliwashauri Simba ikicheza saa kumi na moja watafungwa wakaamua kwa ubabe kusogeza mbele muda wa mchezo!
 
Ila mkuu pamoja na kuandika KWA jazba japo binafsi kwangu mpira napenda KWA asilimia 3% tu but kila Jambo hutokea KWA sababu mkuu,Mambo ya sheria au kanuni sizungumzii hapa maana sio kitu muhimu Sana kwangu ila kiroho kila ambalo ulipenda liwe na kushindwa jua pia lipo kusudi la mungu wenda leo apo ulipo ungeondoka na ngeo maana hii mechi nikiwa safarin wa nchi kavu takribani km 925 ili nifike nilipokua naenda nimekuta muitikio mkubwa tu wa mechi hii na Cha kushangaza mungu matokeo anayajua ,Sasa usije weka nyumba,mke,kuacha kazi, kujinyonga, kutembea uchi,n.k jua tu mpira ni Kama kamali na mpaka mda huu simba na yanga wate washindi wanasubili takika 90 KWA wakati na mda mhafaka
 
Una matatizo binafsi wewe na Simba wazee wa kazi, Yanga wametoka uwanjani saa 11 kasoro, hata hivyo hawakuingia uwanjani mlipaswa kufata utaratibu tu hata Simba tulijua muda umebadilishwa na tukatii.
 
Hata kurejea kwa uharifu wa vibaka mijini, hasa Dar, si dalili njema. Ni ishara kuna tatizo lakini linaongelewa na kushughulikiwa kisasa (km hotuba)
Shida tuliyonayo ni kuwa bado kuna ambao wamekwamia awamu iliyopita na bado kujileta awamu ya sita.
 
"Serikali ina ahirisha match ya Simba na Yanga eti sababu Mwinyi anazindua kitabu. Huu ni wendawazimu" Match imehaitlrisha kwa sababu Yanga wamesusa sio Serikali.
We ndo kalaghabaho kabisa.
 
Hayo maujinga hasa ndiyo raha yetu. As long as hatufokewi, hatutekwi, hatuuawi, na wala hatutengwi kimaendeleo kwetu sawa sawa.

Maisha ya Mwendazake ni laana ya kishetani na ndiyo maana mahali anakostahili ni Jejanam tu.

Tuachieni nchi yetu tuishi na ujinga wetu na Rais wetu SSH,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…