Ukwerli gani Majebere, kuwa nauza unga na siku yangu ilikuwa imewadia?
Nimesafiri sana dunia hii nimgekuwa mtu a unga weshanikamata siku nyingi.
Hapo umesahau kidogo mkuu wangu. Hali hiyo ingekubalika sana na kupokelewa na nchi zenye serikali za Kiislamu kama Irani, Saudi Arabia n.k. Ila katika nchi zizizofungamana na dini yoyote kama Tanzania, hilo lisingekubalika.Pole kwa yote yaliyokukuta,hata hivyo elewa watanzania ni wamoja na wanatawaliwa kwa kufuata katika na sheria.Ila uzingatie kuwa suala za vurugu za Mwembe chai na kuvunja mabucha ya nguruwe yasingekubalika katika serikali ya nchi yoyote.
Inabidi uwe/muwe wavumilivu katika kuepusha dini na siasa katika misikiti.
Wewe umesema ulikuwa ktk mkutano kuusiana na ugaidi Afrika mashariki hususani TZ,ila haujasema ni wa dini au siasa?.
Hata hivyo elewa kuwa watu wenye mamlaka ni waoga sana wakijua au kupata taarifa kuwa fulani anajihusisha na siasa nje ya nchi ktk vikao au mikutano mbalimbali,maana anahatarisha maslahi yao.Kwa walichokufanyia wako sawa kabisa hata wewe ungesikia kama ungekuwa kwenye mamlaka usingenyamaza,ila baada ya kujiridhisha umeachiwa.
Endelea kufanya kazi ya mungu wako utapata thawabu,maana ninavyojua mimi hakuna mtu aliyewahi kufanya vita na mungu akashinda labda unayemtumikia siyo MUNGU wa kweli.
huko duniani huwa unaenda kufanza nini?
Ni mfanyabiashara wewe, kama ni kuhubiri hapa home ushahuri mpaka kaliua sikonge na ulyampiti, ushafika kipumbuiko na malampaka kuwasilimisha makafiri, DINI IMO NDANI YAKO WALA SI WEWE UPO NDANI YA DINI.
Unaweza kutuelezea maana ya dini?
Hapo umesahau kidogo mkuu wangu. Hali hiyo ingekubalika sana na kupokelewa na nchi zenye serikali za Kiislamu kama Irani, Saudi Arabia n.k. Ila katika nchi zizizofungamana na dini yoyote kama Tanzania, hilo lisingekubalika.
Ndio maana makundi kwa makundi ya watu wanaingia na kufata mfumo wa Maisha wa Mwenyeezi Mungu nao ni Uislaam.
Mwanakijiji! mzee wetu Mohamed Said ameianza nakala yake kwa kuturudisha nyuma kidogo na habari ya yule Sheikh aliyerudishwa "kwao" Zanzibar halafu akaendelea kutupeleka mwaka 1964 wakati masheikh wengi waliwekwa kizuizini, hakutuacha hapo bali alitukumbusha mwaka 1993 ambapo kulizuka tafrani kati ya askari na Waislamu akamalizia tukio la Sheikh Kishki juzijuzi na Mufti wa Yemen halafu akaunganisha na lilomkuta yeye.
Huu ni mlolongo wa matukio baada ya matukio haiwezekani ulifananishe na tukio moja la Ulimboka au na jingine kama la Ulimboka pale na hapa......mwisho kauli yako imenishangaza sana kwani inaonekana kuihukumu Serikali kuwa na hatia ya utekwaji wa Ulimboka!
Mohamed said ametuletea udhalilishwaji wa Waislamu unaofanywa na vyombo vya dola, wakati ya Ulimboka ndio kwanza uchunguzi unaendelea!
[/QUOT
Tatizo mbona liko wazi hapa. Nafasi nyingi kati ya hizi ulizozitolea mfano ni za KITAALUMA zaidi. Hapewi mtu kwa sababu ya dini yake, nafasi hizi zinapatikana kutokana na sifa za TAALUMA. Tumieni nguvu nyingi sana kuwapeleka watoto wenu shule ili wapate elimu na kujinasua kwenye ujinga unaoendelea kuitafuna jamii yenu. Angalia mfano huu hapa: Kwa kipindi cha miaka saba nilipokuwa shule ya msingi sikufundishwa na mwalimu yeyote MUISLAM, nakumbuka kwenye eneo lote la kata ile yenye shule za msingi tisa hakukuwa na mwalimu hata mmoja MUISLAM. Nilipokwenda shule ya sekondari ambayo ilikuwa na walimu 47 alikuwepo mwalimu mmoja tu MUISLAM. Kwa bahati nzuri nilifauru mtihani wa kidato cha nne na kuendelea na masomo ya high school katika shule ile ile, tulikuwa wanafunzi 46 wa (PGM) tuliochaguliwa kuingia kidato cha tano, katika darasa letu hakuwemo MUISLAM hata mmoja. Nilipokwenda chuo kikuu nilisoma na wanafunzi wachache sana WAISLAM. Kwa mtiririko huu usitegemee kuwaona WAISLAM kwenye nafasi za kiataaluma. Acheni tabia ya kulalalamika tu, jengeni shule, wapelekeni watoto wenu shule, wahimize watoto wenu wasome kwa bidii na acheni tabia ya kuwajaza fikra za kibaguzi watoto wenu.
Kwa hiyo unataka aajiriwe mtu yeyote hata kama hajui kuandika bora tu anajiita muislamu? Walioajiriwa hawana sifa za kuajiriwa kwenye kazi walizopewa? Ninajua nchi hii viongozi ni corrupt, na kwa maana hiyo sitashangaa kuona mtu kapewa kazi asiyostahili (kama kina Sophia Simba, Celina Kombani, Stephen Wassira, Mustapha Mkulo n.k), unataka kutuambia walipewa kwa kuwa wote ni wakristo au walipewa kutokana na incompetence ya aliowapa? Acheni uzuzu nyie watu!
Kwani hao masheikh waliokamatwa mwembechai hawakuhusika kuvunja mabucha ya kitimoto?Mwanakijiji! mzee wetu Mohamed Said ameianza nakala yake kwa kuturudisha nyuma kidogo na habari ya yule Sheikh aliyerudishwa "kwao" Zanzibar halafu akaendelea kutupeleka mwaka 1964 wakati masheikh wengi waliwekwa kizuizini, hakutuacha hapo bali alitukumbusha mwaka 1993 ambapo kulizuka tafrani kati ya askari na Waislamu akamalizia tukio la Sheikh Kishki juzijuzi na Mufti wa Yemen halafu akaunganisha na lilomkuta yeye.
Huu ni mlolongo wa matukio baada ya matukio haiwezekani ulifananishe na tukio moja la Ulimboka au na jingine kama la Ulimboka pale na hapa......mwisho kauli yako imenishangaza sana kwani inaonekana kuihukumu Serikali kuwa na hatia ya utekwaji wa Ulimboka!
Mohamed said ametuletea udhalilishwaji wa Waislamu unaofanywa na vyombo vya dola, wakati ya Ulimboka ndio kwanza uchunguzi unaendelea!
Mohamed Said, kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho hawa ndugu zetu hutuogopa kwa majina tu ya Kiislaam. Hawana zaidi ya uoga, na uonevu wao wote lakini AlhamduliLllah Uislaam ndio dini inayokuwa kwa haraka kuliko dini nyingine yoyote duniani na hususan hukohuko Merekani, ushahidi huu hapa: Fastgrowing Islam winning converts in Western world - CNN