Udhalimu wa Utumwa Zanzibar na Pemba: Mababu zetu waliteswa, walihasiwa, walibakwa, na kuuawa kinyama

Udhalimu wa Utumwa Zanzibar na Pemba: Mababu zetu waliteswa, walihasiwa, walibakwa, na kuuawa kinyama

Mkuu Maalim, bandiko langu hili ni la zaidi ya michango 250 ila bandiko lako ndilo la kwanza kujibu na nadhani pia ndio la mwisho kwa upande wangu!.

Kumbe hizo picha ni fitna tuu na popaganda za chuki tuu dhidi ya Uislamu!.

Asante kutufahamisha, na asante kuchangia uzi wangu huu.

Pasco
Pasco sikutaka kukushirikisha haya manake najua kwa hulka yako na mipaka ulihojiwekea huwa si mtu wa kijiingiza kwenye tom and jerry arguments za udini.

Ila kuna kawaida ya hawa watumwa humu ndani hata wakiwa kwenye zile wanaita Da'awa wakiona hoja inawaelemea wanaanzisha vurugu ili mradi tu wasionekane wameshindwa.

Kimsingi Hoja ulizoweka na ushahidi ulioweka kama ukiupeleka kwa wasomi watakuelewa na dhamira yako inaeleweka. Hauko pro-religious.

Lakini humu hawa vikofia japo,.wanakuelewavizuri sana pengine walishamgeuza mwandishi mohammed said kama kiongozi wao wa daawa. Hivyo hawako tayari ashindwe kwa nguvu ya hoja . Wanafanya hizi vurugu zote intentionaly ku ficha udhaifu wa mohammed said.

Na hapa sitaki kumaanisha mohamed said anao udhaifu La. Namheshimu sana., bali kwa hoja nzito ulizoweka na picha hawa wapambe wamesoma wakaona mohammed said pengine hatoweza kutolea ufafanuzi haya uloandika. Ndio wakaanzisha shutuma dhidi yako.

Hoja umeanzisha vyema na pengine mngefikia consesus nyinyi wawili kama wasingejiingiza team mohamed saidi humu ndani...

Mazingira kama haya yanatoa picha kua unapojadili mohamed saidi haujadilli naye tu bali na team yake ambayo imejengeka either formaly ama informaly.

Pasco ulichoandika hujamtukana mtu wala dini ya mtu. Umeandika hoja hazina udini kabisa. Umebakia kua neutral hata sasa. Integrity yako haina mashaka kabisa. Pasco You are so smart.
 
KIWAVI,
http:// mohammed said anaandika ukweli na ni mtu anaefatilia ukweli na anakwenda deep kwa kila jambo ili apate ukweli haandiki kijuu juu kama wewe tatizo hampendi haki na ukweli mnapotoshwa na waandishi uchwara walioegemea kwenye dini .historia ya kweli ya uhuru wa tanganyika ambayo waislamu ndio waliopigania inawauma sana kwa sababu mohammed ameifanyia reserch ya kina na ukweli inawauma sana go go m said.
 
Kipindi cha ukoloni kuna mambo mengi yamefanyika. Kwa bahati mbaya ukweli halisi wa mambo yaliyokuwa yakifanyika ulifichwa, waliouficha walikufa nao. Watu wa leo tumebaki na historia ya kuunga-unga tu, hakuna mwenye uhakika na historia ya kweli isiyotiliwa shaka.
 
Wana Bodi na wachangiaji:

tuache kukashifiane turudi tujadili mada ya Pasco tukiwa watulivu tujenge hoja.Hoja Yake inahitaji kuwekwa sawa ili kuondoa kasumba ambazo wengi vichwa vyao vimepikwa kasumba.

Nitajaribu kuweka ukweli wa historia hizi kwa kadri zilivoandikwa na watu mashuhuri inshaalalh...
 
pasco,

You can't go back to change your history, but you can start a new history from where you are. Ukisikia mtu anang'ang'ania kuwalaumu waarabu na wazungu, utakugundua kwamba mtu huyo hana roho ya msamaha pia hataki maendeleo....Siku moja nikiwa chuoni hapa USA, one of African american alikuwa ananichukia sana, kwamba tuliwauza,nikamwambia walipouzana babu zetu mimi na wewe hatukuwepo kwanini kujenga chuki kwa kitu ambacho hakipo sasa?

Kama babu zetu waliuza babu zenu basi sisi tutendeane mema..pili nikamwambia babu zetu walilazimishwa tena kwa bunduki wangefanyaje? tatu nikamwambia habari za Yusufu kwenye Biblia ndugu zake walimuuza lakini aligeuza kuuzwa kule kuwa fursa kwa ndugu zake....nikamalizia kwa kumuuliza swali hili kama Marekani isingekuwa na mchanganyiko wa weusi na weupe unafikiri weusi wangeweza kuonekana kuwa ni watu?

Baada ya hapo alianza kunielewa na hatimaye tumewahi kuja wote Tanzania. Mleta mada hii please change your perspective, think positively for the development of this new generation.
 
Kijana baridi inakutesa sana jitie gunzi tu au subiri yamebakia masaa machache kufika saa 10 ukambong'olee mtume mwamedi akupge mboli [emoji23] [emoji23] [emoji24]
Askofu Robinson ameishi katika ndoa ya kishoga kwa takribani miaka ishirini mpaka mwaka 2010 pale ambapo patner wake Mark Andrew alipofariki.

Biblia pamoja misingi ya kanisa la Kianglikani hairuhusu ndoa ya jinsia moja, lakini kinachowashangaza watu duniani ni kitendo cha kuhalalisha hatua hiyo kwa presha ya utandawazi.Barani Afrika nchi ya Afrika ya kusini ilikuwa ni nchi ya kwanza kuruhusu ndoa ya jinsia moja, kuna kipindi bunge la nchi ya Uganda liliwahi ijadili hoja hiyo na ilipingwa vikali japokuwa mwaka jana pia hoja hiyo ya uhalali wa ndoa ya jinsia moja ilirudi bungeni humo na haikupita.

Katika hili kuna mengi ya kujifunza na kumsihi Kristo aingilie kati kuliko kutumia akili na kufikiri kuwa hapa nchini Tanzania jambo hili litawezekan maana hao wazungu ndiyo wafadhiri wetu.Waliotutangulia waliandika tenzi, Nionapo AMANI kama shwari, ama nionapo shida....., Usalama wetu uko katika Kristo Yesu pekee.

Teh teh teh
 
Pasco,hivi kati ya hio michoro hapo juu kuna handaki lenye watumwa? Tulione hilo handaki au hio milango ndo mahandaki?!
 
Bado tatizo lipo kwa Waarabu.....wale wageni wanaojenga viwanja kule Qatar wanalalamika.....Kina dada wanaotoka huku (Tanzania na Kenya) kwenda kufanya kazi nchi za kiarabu wengi wao hawatendewi kibinaadamu...

Kuna bwana aliwahi kutoa habari yake kupitia kipindi cha Njia panda(clouds) anaitwa Samadu (kama sikosei) alielezea madhila aliyokumbana nayo akiwa "utumwani" ikiwepo kuambiwa na wenyeji wake kuwa wao (weusi) wapo duniani kwa ajili ya kuwa Watumwa.
Hapa ndipo ulipo unafiki wetu kiasi kwamba wengine wanahusisha kv ni chuki tu dhidi ya jamii fulani.

Tuachane na Waarabu na turudi hapa nyumbani. Ni matukio mangapi yamepata kutokea yanayohusu udhalilishaji wa kawaida, udhalilishaji wa kijinsia pamoja na ukatili dhidi ya ma-housegirl? Unataka kuniambia hujawahi sikia hapahapa TZ habari za wafanyakazi wa ndani kuchomwa pasi, kupigwa na vitu vyenye ncha kali, kubakwa na mambo mengine kama hayo? Unataka kusema ni mageni hayo kwako?

Rudi kwenye familia. Ni akina mama wangapi wanawafanyia ukatili wa kutisha watoto wa kambo? Ni akina baba wangapi wanabaka mabinti zao?

Ni ujinga kuwa na fikra kwamba jamii fulani eti ni roho mbaya wakati unayoamini wanafanya hufanywa pia na watu wa jamii yenu. Roho mbaya ya mtu haitokani eti kv yeye ni Mwarabu, Mzungu, Mwafrika bali ni mtu mwenyewe! Kusema kwamba eti hawa ni roho mbaya kuliko ni dalili tu ya kutopewa ubaguzi. Ni ubaguzi ku-judge watu collectively instead of in individual basis.
 
Pasco kuna watu ukimsema vibaya mwarab wanaona unaisema vibaya dini yao.ingawa huwa sioni uhusiano upo wapi. Hawa wamekana uafrika wao na kujiona nao ni sehemu ya waarabu na huwatetea wa arabu kwa nguvu zote na kuwa tayari kufa kwa ajili ya waarabu.

Hawa huua hata wenzao kwa ajili ya kuwanusuru au kuwapendelea waarabu. Wakija hapa watakuja na theories mbalmbal za ajab ajab sana. Wanashindwa kuelewa kuwa kuna waarab wakristo ,wasio na dini n.k. waarabu wangekuwa wema hivyo zanzibar wasingefanya mapinduzi na umwagaj wa damu mkubwa namna ile. Wangefanya mapinduz ya nini sasa ikiwa mambo yalikuwa mazur? Ukatili na waarabu zanzibar anayekataa kuwepo ni mtu ambaye tayar ameshafanywa msukule. Huyu huwez mwelewesha akakuelewa. Na sion uhusiano watu wanaoweka wa dini na uarabu. Wanasahau waarab walikuwepo kabla ya dini.

Na ni waarabu hawa hawa wanaouana huko syria,egypt,iraq,somalia n.k kwa tofaut za madhehebu. Huu ni upumbavu maana ujinga unaelimishwa. Ni kama mtu akiona wazungu wamesemwa awatetee kwa sabab anaamin ni wakristo. Nashukuru lakini sijaona wajinga wa namna hiyo linapokuja suala la kukosoa watu wenye elimu hukosoa pasipo kuangalia dini,kabila au rangi.

Subiri waje wakushukie hapa huku mashavu yakiwacheza kqa hasira wakimtetea mwarab
 
Awamu ya pili mlipewa nchi mkaharibu kwa ruksa za kipumbavu mkapewa awamu ya nne mkaishia kuifisidi kwa kushiriana na washkaji na watoto wenu sasa mnaisoma namba mnakimbilia kwa papa. Thread ni ukatili wa waarabu kama vipi anzisha yako ya papa tuje tuchangie
Awamu ya pili ndo watu walifunguliwa toka minyororo ya umasikini hoehoe na wakaanza kuyaishi maisha,ndo maana ya ruxa,kiisha ukafuatia ukapa mkali sana,kabla teena watu hawajaanza kujiachia,muulize pasco kale ka babywalker kanunua katika awamu ipi kati ya nne zilizopita,waabudu sanamu hamna shukrani.
 
Na hao wachina wanafanyana watumwa wao kwa wao japo nao walifanywa watumwa na wajapani!
Huu utumwa sijui nani alisalimika ukiondoa wakaa mbugani wamasai na jamii zifananazo!

Hata,

Kiuhalisia ni vigubu kusema kundi fulani halijawahi kuwa watumwa hata wazungu pia waliwahi kwa matumwa na hawa waarabu na waturuki walishawahi tekwa na Genghis khan
 
mkuu wewe unaona ni sahihi pope kuwala denda watoto?
Mkuu Elungata

Hizo ni picha mnato,huwezi kusema anapiga denda wakati ni picha mnato,ingekuwa video ndio ingekuwa na ushahidi.Hujawahi kuona mtu yupo macho lkn akipiga picha anaonekana kalala?sababu ni kuwa wakati picha ikipigwa yeye alikuwa anapepesa ukope!! Hizo picha za Papa na busu tu, kn sbb ni picha mgando basi unaitengenezea maneno,lkn unapata wapi ujasiri huo kupotosha kiasi hiki?
 
Muongo wewe.
Vasco dagama ndio waanzilishi wa slave trade east africa.
Portugese walikuja kutawala coast ya east africa...kuanzia lamu
Mombasa tanga Dar esalam
Zanzibar
Kilwa na wakateremka mpaka mozambique.
Waliwaua maelfu ya wenyeji walo resist ushenzi wao. ..waliuvunja kabisa mji mkuu wa kilwa ulokua mji wa elimu na ustaraabu..wakaua watu wake..
Pale mombasa pia waliua mamia ya waafrika.
Walipo fanikiwa kuzikalia wakaingia ndani mpaka congo na kuchukua slave kuwapeleka kwao lisbon na wengine kwenye trans antlantic route.
Na wazungu walikuja kununua slaves east afrika na route yao ilikua via cape town to europe or America au brazil .
Ni waarabu ndio walowafurusha wareno east africa...wakabakia msumbiji.
Nitakupa darsa murua kuhusu trade hii wewe na pasco mupate kujifunza .
Na kuacha kusoma uongo mlosomeshwa misionary school kuwa vasco dagama
Livungstone
Bethelow mew diaz ni wazumbuzi...
Ujinga mnao someshwa..walikuja kuvumbua nini ? Ibn batuta alishakuja miaka na miaka na kuandika habari za Afrika mpaka ndani kabisa Huko Zumbabwe.
Huyu alikua mwarabu...yeye ndie mvumbuzi ..hawa wengine ni wakoloni na slave traders
Kaka uarabu umekutawala sana east african slaves ndo unawaona waarabu weusi huko uarabuni na dada na mama zao walizalishwa huku wanaume wakiasiwa.waliokuwepo Europe na america from west Africa.
 
Matatizo yenu mnasomshwa uongo makanisani mwenu na kwenye shule za Kikristo, ndio maana hamjui ukweli in real life (mtabakia wajinga mpaka msilimu).
mkuu, hapa sizungumzii kanisa, wala msikiti, hizo ni imani za watu, huwa sipendi kujadili,

hapa nazungumzia historia aliyopitia mtu mweusi, kadhalilishwa na kuteswa na waarabu, pia na wazungu,

na hadi leo hii bado kuna udhalilishaji wanafanyiwa, sasa watu weusi badala ya kuitafakari hii historia na mambo yanayoendelea kwa sasa ili kupata njia ya kujikwamua , watu mnaanza kushambuliana nyinyi kwa nyinyi, mmoja akin
msifia mwarabu, mwingine akimsifia.

huu ni upuuzi wa hali ya juu kabisa
 
10-Dec-Siku-ya-Uhuru.jpeg
Pasco kuna watu wenye mtindio wa ubongo ukimsema vibaya mwarab wanaona unaisema vibaya dini yao.ingawa huwa sioni uhusiano upo wapi. Hawa wamekana uafrika wao na kujiona nao ni sehemu ya waarabu na huwatetea wa arabu kwa nguvu zote na kuwa tayari kufa kwa ajili ya waarabu. Hawa huua hata wenzao kwa ajili ya kuwanusuru au kuwapendelea waarabu. Wakija hapa watakuja na theories mbalmbal za ajab ajab sana. Wanashindwa kuelewa kuwa kuna waarab wakristo ,wasio na dini n.k. waarabu wangekuwa wema hivyo zanzibar wasingefanya mapinduzi na umwagaj wa damu mkubwa namna ile. Wangefanya mapinduz ya nini sasa ikiwa mambo yalikuwa mazur? Ukatili na waarabu zanzibar anayekataa kuwepo ni mtu ambaye tayar ameshafanywa msukule. Huyu huwez mwelewesha akakuelewa. Na sion uhusiano watu wanaoweka wa dini na uarabu. Wanasahau waarab walikuwepo kabla ya dini. Na ni waarabu hawa hawa wanaouana huko syria,egypt,iraq,somalia n.k kwa tofaut za madhehebu. Huu ni upumbavu maana ujinga unaelimishwa. Ni kama mtu akiona wazungu wamesemwa awatetee kwa sabab anaamin ni wakristo. Nashukuru lakini sijaona wajinga wa namna hiyo linapokuja suala la kukosoa watu wenye elimu hukosoa pasipo kuangalia dini,kabila au rangi. Lakini hawa mandondocha wao humtetea bwana wao kwa hali na mali. Subiri waje wakushukie hapa huku mashavu yakiwacheza kqa hasira wakimtetea mwarab

Bila ya kuja na hotuba ndefu ambayo lengo lake ni ile ile ya kuhimiza chuki ungejaribu kupata ukweli jee ni wazanzibar au watu kutoka nje ya zanzibar ndio waliofanya mapinduzi yaliyopelekea zaidi ya wazanzibar 20,000 kuuliwa na kuzikwa wakiwa hai katika makaburi ya pamoja!

Kwa ufupi ni kuwa 1964 haikupinduliwa serikali ya Sultani bali serikali halali ya wazanzibar ambayo ilipata uhuru kutoka kwa mwengereza tarehe 10/12/1963
UHURUDAY.jpg


Jengine ni kuwa hakuna USHAHIDI wowote ule wa watawala wa kiarabu kuwafanyia wazanzibar UKATILI kama huo unaousema!! Katika historia ya Zanzibar wazanzibar walifanyiwa UKATILI WA KUTISHA na wareno hadi madhila yalipowazidi wakafunga safari kwenda Omani kuomba msaada wa kuwafurusha wareno.

UKATILI mwengine wa kutisha wazanzibar waliupata kutoka kwa watanganyika pale walipokuja kuipindua serikali halali ya Muhammed Shamte january 12 1964 na kuwauwa wazanzibar wasiopungua 20,000!!! Na hili lilifanyika chini ya master plan Nyerere, huyu alikuwa na chuki kubwa ndani ya moyo wake shidi ya wazanzibar na ndio moja katika hotuba yake aliwahi kunukuliwa kuwa kama angalikuwa na uwezo basi angalivichukua visiwa vya Zanzibar na kuvisukumia mbali huko!!! Chuki zake zilitokana na kuwa Zanzibar wakati huo ilikuwa inatowa wazuoni wakubwa wa dini ya kiislamu.
znz-un-1963.jpg
HAPA KWELI PANA SULTANI WA KIARABU!? hii ilikuwa 1963.

UKATILI mwengine mkubwa ambao umewakuta wazanzibar kutoka kwa watanganyika ni ule wa tarehe 27/12/2001 pale Mkapa alipotoa amri na kuuliwa wazanzibar wasiopungua 70 katika maandamano halali.
IMG-20150527-WA0049.jpg
Nikaribuni tu watanganyika walikuwa na hamu ya kuwafanyia tena ukatili wa kutisha wazanzibar lakini M/Mungu akampa hekima maalim Seif na kuzing'amua hila zao hivyo akawazuia wazanzibar watulie majumbani!!!! UMEONAPO WAPI MTU HATA GOBORE HANA LAKINI WATAWALA WAKAJIANDAA NA VIFARU NA MAJESHI.

MWISHO NARUDIA KUWA HAKUNA USHAHIDI WOWOTE ULE UTAKAOPATIKANA KWA MWARABU KUMFANYIA UKATILI MZANZIBAR KULIKO ALIVYOFANYIWA NA WATANGANYIKA, kama mtu anao aulete hapa!!! Sio ushahidi kutoka kwa maaskufu wa mkunazini Unguja
 

Attachments

  • TbNUJqSFRhqYAn-cLZDg33YwRiWWliFvNh1Zk7ADm04=w170-h534-no.jpeg
    TbNUJqSFRhqYAn-cLZDg33YwRiWWliFvNh1Zk7ADm04=w170-h534-no.jpeg
    11.8 KB · Views: 112
Picha zimepigwa na kamera za wazungu!!!!! aliyewapiga nan?wazungu walikua wapi wakati wanapiga hizo picha?......."AU NDO STYLE ZILEZILE ZA KUTUAMINISHA IDDI AMINI ANAKULA NYAMA ZA WATU KWENYE FILAMU"
 
Pasco,

Majibu yako haya hapa umejibiwa.


Na Ahmed Ngwali.

Ukweli kuhusu Utumwa- Zanzibar,( Unguja na Pemba).

Nimeamua kuandika post hii baada ya kusoma post ambayo imeandikwa na PASCO mmoja wa wanajamvi maarufu katika mtandao wa JF.

Post yake ilikuwa na kichwa cha habari kama ifuatavyo:-
UDHALIMU WA WAARABU ZANZIBAR NA PEMBA KWA NDUGU ZETU WALI-TESWA-HASIWA-WALIBAKWA.

Hoja ya Pasco ilitegemea sana report ya commissioner Donald Mackenzie iliotolewa London mwaka 1895.

A report on slavery and slave trade in Zanzibar, Pemba.

Ambayo ilitayarishawa na The British and Sovereign Ant-Slave Society.

Ukweli wa Mambo.

Ikiwa kweli kisingizio cha mavamizi ya Zanzibar ni utumwa basi utumwa ulikuwepo nchi zote duniani, si Zanzibar tu.

Waliofanya biashara za utumwa ni watu wa kabila zote na dini zote, hata Wapagani wa kiafirika.

Lakini waliotia fora kwa ukatili na ukhabithi mkubwa katika biashara ya utumwa ni mataifa ya kizungu na khasa Waingezera na Wamarekani.

Leo wana uso wa kujigamba na kujidai kama eti wao ndio walio ondosha utumwa?

Ushahidi.

1. Sayyid Said bin Sultan alipiga marufuku biashara ya watumwa baina ya mamlaka zake na mataifa yote ya kikristo mwaka 1822.

2. Pia alizuwia kusafirisha watumwa kutoka Afrika kwenda Oman katika mwaka 1845.

3. Sayyid Barghash alipiga marufuku biashara ya watumwa katika mwaka 1872 na akalifunga soko la watumwa lililokuwepo Mkunazini, Zanzibar.

4. Dola za kizungu zilipiga marufuku biashara ya watumwa kwa hiyo inayoitwa Brussels Act katika mwaka 1890 (yaani Zanzibar iliutangulia ulimwengu mzima kwa miaka kumi na nane (18) katika kupiga marufuku biashara ya watumwa)

5. Sayyid Hamoud ambaye pia nae alikuwa Sultan wa Zanzibar alipiga marufuku kabisa utumwa wenyewe katika mwaka 1897 (yaani mwaka huo hapakuwa na mtu yeyote mtumwa katika mamlaka ya Zanzibar).

6. Waingereza walipiga marufuku utumwa Kenya mwaka 1912 (yaani miaka miaka 15 baada ya Zanzibar).

Katika Tanganyika Wajerumani waliendelea na utumwa kwa muda wote waliotawala na baada ya hapo Waingereza waliendeleza utumwa katika Tanganyika mpaka mwaka 1920 (yaani kwa muda wa miaka 23 baada ya Zanzibar).

Huu ndugu zangu ndio ukweli.

Utumwa khasa ulifanywa na wazungu sio waarabu.

Mwisho:

Katika nchi yetu ya Zanzibar sasa tumebaki Na Ukoloni mweusi kutoka Tanganyika licha ya kuwa tunajinata Na kujigamba kwamba tumejikomboa ili tujitawale, lakini hao wanaoripokwa haya inaonekana wazi kwamba wamelevya Na maslahi yao binafsi Na wengine pangu pakavu tia mchuzi hawana kazi hawana bazi wao ni bendera ipepee tu japo wale dongo.
 
Ni stori nzuri tu, lakini mwandishi umechanganya mambo mengi bila ya kufahau hasa nini kilichotokea Unguja na Pemba,kwa ufupi wenyeji waliwaitia Warabu ili waje kuwasahidia kuwaondoe wareno katika hivi visiwa.

kwa mantiki hiyo hamna hata mwenyeji mmoja wa Zazniabr alikuwa Mtumwa,isipokuwa warabu walijaribu kujipendekeza kwa wenyeji kwa kuoana nao,,

Utumwa kweli ulikuwepo Lakini kumbuka si Mwarabu tu ndio waliofanya hiyo biashara bali mpaka wenyeji wa Zanzibar ambao wewe unawaita "Wamatumbwi",kama umesoma historia ya Zanzibar,Mwenyeji wa Zanzibar aliekuwa akiitwa Tiptip alikuwa mfanyabiashara mkubwa wa watumwa..Sio kama biashara ya utumwa ni sifa,sio sifa lakini ukweli ulikuwa huo wazanzibar wenye asili ya kiafrika na wao walikuwa na watumwa..Ki ukweli mwenyeji wa zanzibar hakuwahi kuwa mtumwa

Kitu chengine ambacho unatakiwa ufahau ni kuwa hiyo familia ya waliokuwa masultani wa Zanzibar walikuwa ni watu waliochanganya damu baina ya warabu na wenyeji wa Zanzibar(hao uanowaita wamatumbwi),kwahiyo propaganda kama hizi hazina ueledi katika historia za Zanzibar.Wanasiasa na watu waliokuwa sio wazanizbari ndio wanaleta siasa kama hizi ili kuwatafautisha wazanzibari....

Warabu hawakuwa washenzi kama unavyojaribu kutueleza, utawala wa CCM ni washezi zaidi na wabaguzi kuliko walivyokuwa Warabu, mfano wakati wa utawala wa Sultani walikuwapo Polisi warabu,wahindi na wafrika je hali ya utawala wa sasa iko vipi...,Wauza kahawa mitaani walikuwa warabu(washihiri) je hali ya sasa iko je,Madobi (wafua nguo) walikuwa wahindi je hali ya sasa iko je...,matopasi (wazoa taka )mitaani walikuwa wahindi nk,Mwenyeji wa Zanzibar alikuwa hafanyikazi..

Hali ya sasa Mwenyeji wa zanzibar amekuwa masikini fukara,mwenyeji wa zanzibar hivi sasa ndio anafanya kazi walizokuwa wakifanya wahindi na washihiri na wageni wengine waliokuwa a´wakija zanzibar kutafuta riziki,yaani kwa ufupi ndugu mwandishi chukuwa mfano wa warab wa GULF wanayoishi hivi,ndio walivyokuwa wakiishi wazanzibari wakati huo,,

Nimeattach baadhi tu ya picha za waliokuwa masultan wa zanzibar sasa nambie kuna mwanarabu wa ukweli hapo?hizo zote i picha za wazanzibar kama akina Mohamed Aboud, Salim Ahmed Salim,S eif sharif nk..

Kwa ufupi waafrika kama kawaida yetu,tumeiharibu zanzibar nchi iliyokuwa Empire tumeifanya iwe fukara,Angalia nchi zote za kiafrika ziko hali gani utajua udhofu wetu,wafrika tunangalia mambo kwa hisia kuliko uhalisia kwa namna hiyo tunashinswa hata kujitawala

Mmeirejesha Zanzibar nyuma kimaendeleo na bado mpaka katika karne hii ya leo mnatuletea hadithi z mambo ya miaka 500 iliyopita,,,tunaka twende mbele kimaendeleo makosa waliyoyafanya mabibi na mababu zetu ndio yameshayafanya,hapa tulipo tusonge mbele hatutaki kusikia yaliyopita.....,kila zama zina mambo yake

imagessu.jpg
Jamshid_bin_Abdullah_Al_Said.jpg
Tippu_Tip.jpg
 
Back
Top Bottom