Udikteta Tanzania: Polisi ya Simon Sirro yazuia wanawake kufanya mazoezi ya Jogging

Udikteta Tanzania: Polisi ya Simon Sirro yazuia wanawake kufanya mazoezi ya Jogging

Kama lengo ni kutoa ujumbe wa kudai tume huru, basi polisi wangejulishwa.

Lakini kama lengo ni kutafuta wanachama zaidi wa jogging Club basi hakuna maana ya kuweka neno Tume Huru kwenye fulana zenu, kama nilivyoainisha hapo juu.

Kwa kifupi ni kwamba wapinzani sasa hivi mpo hoi na mnachofanya ni kujitutumua tu.

Tafuteni mikakati na mipango sahihi.
Ndugu yangu hao akina Mama wamefanikiwa sana kufikisha ujumbe.
Kwa polisi kuja alfajiri ile ni uthibitisho kuwa wametumwa na aliekerwa na ujumbe huo.
Ila wangefanya vitu vya kuivutia CCM na kuwafurahisha nyie mawakala wake ndio wangekuwa wamefeli.
 
Serikali inazidi kuwapa Chadema umaarufu

Mama anamuiga Magufuli mtu asiekua na akili

Kati ya akili ya Magufuli na Kikwete,akili ya Kikwete ni milions of miles bigger than that nonsense,ni heri nigeiga ya Kikwete

Mama anaiga matango pori ya Magufuli....ni heri walao atumie hata akili yake binafsi kuliko ya Magufuli aisee
Kwamba Kikwete anaakili kuliko jiwe?

Ni Kikwete huyu huyu aliyekataliwa na Nyerere asigombee urais kisa ni mhuni anayedhani kuwa hapo ikulu ni pahali kula bata?

Ni kikwete huyu huyu aliye anzisha Makundi ya kifisadi ndani ya chama kwa kwa mtu kuhonga pesa ili ateuliwe kugombea urais & ubunge?

Wash your brain and make sure umetakasika ndipo uje hapa kumsifia mzee wa Msoga aka kinara wa upigaji wa kodi na raslimali za nchi
 
Hivi ndiyo akili za Bawacha ndiyo zimefikia hapa, Soma fulana hizo ndiyo ujue polisi wako sahihi kuwazuia. Polisi yetu ni ya wasomi hizo mbinu za kitoto wanazing'amua haraka.
Sijui ni usomi gani unaousifu hapo?
Huo ni uthibitsho kuwa ujumbe umefika na ukamkera MKUBWA aliyewatuma alfajiri ile.
 
Sijui ni usomi gani unaousifu hapo?
Huo ni uthibitsho kuwa ujumbe umefika na ukamkera MKUBWA aliyewatuma alfajiri ile.
Usemi ni kugundua mbinu ya Bawacha kuficha makucha yao ya maandamano kwenye jogging. Angalia ujumbe wao kwenye fulana zao. Hiyo haikuwa jogging ni maandamano

Polisi wasomi wamegundua mapema na kuchukua hatua stahiki. Big up kwa polisi wetu. Watanzania tunaunga mkono polisi wetu.
 
Si kazi ya polisi kuingilia vitu visivyovunja sheria
Ninyi mlipanga maandamano yalojificha nyuma ya jogging.

Ila mkasahau polisi nao wapo kazini.

Kiufundi (technically) hayo ni maandamano yenye ujumbe wa kutaka Tume Huru.

Mnapofanya mambo yenu yawe yamepangwa kiufundi.
 
Usemi ni kugundua mbinu ya Bawacha kuficha makucha yao ya maandamano kwenye jogging. Angalia ujumbe wao kwenye fulana zao. Hiyo haikuwa jogging ni maandamano

Polisi wasomi wamegundua mapema na kuchukua hatua stahiki. Big up kwa polisi wetu. Watanzania tunaunga mkono polisi wetu.
Wakubwa wenu wamesoma ujumbe, wakakereka wakawatuma polisi. Si ndio ujumbe umefika?
 
Wakubwa wenu wamesoma ujumbe, wakakereka wakawatuma polisi. Si ndio ujumbe umefika?
Na nyie kubalini kipigo cha mbwa koko. Wamepigwa na kushikwa shikwa na mwanaume. Ujumbe huu pia umefika. Mwanakulitafuta, mwanakulipata.
 
Ninyi mlipanga maandamano yalojificha nyuma ya jogging.

Ila mkasahau polisi nao wapo kazini.

Kiufundi (technically) hayo ni maandamano yenye ujumbe wa kutaka Tume Huru.

Mnapofanya mambo yenu yawe yamepangwa kiufundi.
Shetani anapojitahidi kukukosoa ujue ndio upo sahihi.
 
Hii polisi itaingia kwenye historia kama ndio polisi hovyo kuliko zote zilizopita kwenye ma IGP wote Tanzania
 
Shetani anapojitahidi kukukosoa ujue ndio upo sahihi.
Tatizo kubwa mlilo nalo ni kushindwa kufikiri uzuri na kupanga mikakati kisomi.

Sanasana mwakimbilia kutusi watu ambao wengine wetu malengo yao ni kuwasaidia.

Acheni kukimbilia kutusi hizo si siasa sahihi.
 
Tatizo kubwa mlilo nalo ni kushindwa kufikiri uzuri na kupanga mikakati kisomi.

Sanasana mwakimbilia kutusi watu ambao wengine wetu malengo yao ni kuwasaidia.

Acheni kukimbilia kutusi hizo si siasa sahihi.
Ushauri wako wafanana na zilezile nyimbo za kina Ndugai, hauhitajiki.
 
Back
Top Bottom