Kamanda SIRO siku zako za kuwa ofisini zinahesabika,soon utastaafu utumishi was UMMA.yuko wapi IGP SAID MWEMA,OMARI MAHITA,ERNEST MANGU nawe utashika njia yao.Ni vyema tukukumbuke kwa heri na mema .kamanda SIRO wewe Ni mtu mdogo Sana katika TAIFA letu jitahidi kuwa muungwana na muadilifu kwa siku chache zilizobaki kukaa ofisini.
Kamanda SIRO Taifa letu lilipofika Ni Vita Kali Kati ya CHADEMA na dola Vita hivi vinaelekea mwishoni kabisa jitahidi kuwa mwema katika kumalizia siku zako za ofisini zilizobaki.
Kamanda SIRO si kwamba CHADEMA imejiandaa kuingia ikulu Kama Bibi harusi Hilo hapana Bali hata Kama itatulazimu kupita kwenye damu na Moto tutapitia.
Kamanda SIRO leo unajiona mwamba,imara na mkubwa kwa nafasi yako ila kumbuka Kuna maisha baada ya kuwa IGP.
Kamanda SIRO unapata wapi mamlaka ya kuzuia watu kufanya mazoezi ili kuimarisha miili yao,Leo unawakataza kufanya mazoezi kwa pamoja kesho unawakataza harusi,misiba,michezo na kutembeleana.
Kamanda SIRO Kama unatafuta huruma ya Bibi wa shungi akuongezee muda wa kustaafu hapo unakosea.kuwa mwema,muungwana na muaminifu kwa siku zako chache za kuwa ofisini zilizobaki.
Kamanda SIRO Kuna wakati utafika umoja w mataifa utaingilia Kati kusuruhisha mgogoro wakati mamia kwa maelfu wamekimbia nchi,wanavilema vya maisha,wapo hospitalini na wangine wamezikwa bila misa Wala swala.
Kamanda SIRO leo CCM wanafanya watakacho katika TAIFA bila bugudha yoyote ,hawasubuliwi ba OCD TISS RPC Wala IGP kesho CHADEMA watakosa uvumilivu nchi itaingia kwenye mtanziko mkali.
Kamanda SIRO hatukulazimishi kufuata maoni Wala ushauri ila ipo siku utaamka saa TISA usiku kuutafuta ushauri.taifa Ni Mali yetu kakuna kundi tukufu Wala duni.