Consigliere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 12,037
- 24,637
Kama kweli Mkuu wa Shule amekimbia shuleni atakuwa amefanya vizuri kwa sababu alikuwa hatakiwi na wanafunzi, alisema Mbaga ambaye hata hivyo, hakutaka kufafanua zaidi chanzo cha mgogoro huo.
Mkuu kile chumba Bado Kipo pale kama msikiti....Juhudi kubwa zimefanywa na baadhi ya walimu Kuwanyang'nya waislamu Kile chumba.....Labda hilo tatizo liwe siku hizi, miaka hii.
Nakumbuka wakati nasoma O-level pale Azania secondary(early 90's), Head master, second master, displini master na academic master walikuwa ni Wakristo.
Kulikuwa na chumba maalumu ambacho kilitengwa kuwa ni sehemu ya kusalia waislamu na kilikuwa kinatumika exactly kama msikiti. kutokana na ibada za waislamu kuwa ni mara tano kwa siku so chumba kile kilikuwa hakitumiwi na watu wengine na palikuwa panaitwa msikitini.
Kwa Wakristo walikuwa wakitumia madarasa kuendesha ibada ambazo zilikuwa zinafanyika kila siku nyakati za jioni na sometimes hall la shule lilikuwa linatumika kuendeshea ibada za kikristo.
Lakini hakukuwa na maneno wala tatizo lolote kama leo hii.
Kweli kabisa mkuu, leo ndiyo tunasituka juu ya mambo haya.Hilo swali lako ni muhimu kujibiwa ili tuchangie tukiwa na uelewa mzuri.
Lakin jambo la msingi hapa ni funzo gani tunapata hapa; Hakuna umuhimu wa kuwa na haya makanisa ama misikiti kwenye taasisi za serikali kama shule!
Uvaaji wa miwani ya mbao kwenye mambo kama haya tutajuta uko tuendako!
Binafsi sioni tatizo na pia sio islamu. Shule niliyosoma ambayo awali ilikuwa shule ya mission na baadaye kutaifishwa na serikali enzi za mwalimu ina kanisa katikati ya shule. Lakini pia kama shule ya Bagamoyo imejengwa na serikali kwa ajili ya wanafunzi wote na ikajenga msikiti katika eneo la shule hilo ni TATIZO!
Hapo kwenye bold. Pole sana kwa kutoyajua maandiko matakatifu. Yaani tatizo lenu ninyi wakristo maandiko hamyajui, na hata kama mkifundishwa hamtaki kuukubali ukweli. Tukubaliane kitu kimoja.... Kwamba huwezi kuwa mkristo kamili bila kwanza kubatizwa (jibu ni ndiyo). Je, ubatizo maana yake ni nini? Jibu, ni kuzaliwa upya ama wengine watasema ni ondoleo la dhambi.... Tuanze na kuzaliwa upya. Hapa inamaana unaingizwa kwenye ulimwengu mwingine wa dini nyingine unakuwa mpya yaani unakuwa mkristo. Tuje na ondoleo la dhambi. Mtoto mdogo anapobatizwa maana yake tunamnwondolea dhambi...? Lakini mbona Yesu anasema watoto hawana dhambi? Maana yake hapa si kumwondolea dhambi bali tunampa dini mpya. Sasa tujiulize dini yake ya awali kabla ilikuwa inaitwaje? Jibu ni uislamu!!!! Kwa kawaida mtu anapozaliwa hutanguliza kichwa (anasujudu-means anakuwa muslim!!!). Na ndio maana mtoto akizaliwa kwa kutanguliza miguu inakuwaga hekaheka kweli mpaka madaktari huwa wanachanganyikiwa. kwa nini wanachanganyikiwa? Au kwa nini mila zingine hufanya tambiko mtu akizaliwa katanguliza miguu???
Ila kwa chuki ya uislamu ama kutopenda kujifunza maandiko watu watabisha mpaka mwaka mpya utaingia. lakini huo ndio ukweli. kwamba binadamu woooooote huzaliwa wakiwa waislamu na ndio maana huwa wanabatizwa ili kuwatoa kwenye dini yao (ya uislamu) kwenda dini hiyo ya ukristo.
Masyopakindi wa Magamba anaendelea kuchochea udini JF!