Wewe jamaa unachokataa sasa hapo ni nini? Halafu umetaja wachezaji waliotokea kwenye generations tofauti tofauti kwa ujumla na wakati mimi point yangu inalenga kuwa na wachezaji wazuri waliotokea kwenye kizazi moja kama ilivyo hivi sasa, hapo ndio tunashidwa kuelewana.
Labda nikuulize ile squad ya akina Rui Patricia,Bruno Alves,Miguel,Roland,Ruben Amorim,Duda,Pedro Mendez,Raul Mereles na Silvio ambayo ilienda kushiriki world Cup ya 2010 unaweza ukalingisha na hii ya sasa hivi ya akina Bernado silva??
Ile squad iliyoshiriki iliyoenda kushiriki Euro 2012 iliyokuwa imejaza wazee kibao akina Helder Postiga, Nuno Gomez,Carlos Martin,Ricardo Carvalho, Ricard Costa unaweza ukailinganisha na hii ya sasa hivi ya akina Raphael Leao??
Squad ambayo ilishiriki World cup 2014 kule brazil yenye midfield mbovu kabisa ya akina Miguel Veloso na Silvestee Velera ambapo walitoka hatua ya makundi unaweza ukailinganishan na hii sasa hivi ya Bruno Fernandez?
Yaani ni kwamba wewe unachotaka kusema hiki kizazi chao cha kisasa ubora wao hauna tofauti na vizazi vilivyopita au?
Halafu unasema eti ukitoa Spain hauna timu nyingine iliyokuwa na wachezaji wazuri kweli? Ronaldo angekuawa anacheza na wachezaji wazuri kama unavyosema angekosa goli hata moja kwenye knock out stage ya world cup tournaments licha ya kushiriki michuano hiyo mara tano???
Kwamba hawa wachezaji wa sasa hivi tunaowaona wakivaa uzi wa Portugal hawana tofauti na hao wa huko nyuma uliowataja au? Kwa hiyo wewe unabishana na Luis Figo ambaye anasema hiki kizazi cha sasa ndio kizazi bora zaidi kuwahi kutokea kwenye historia ya taifa lao?
Kwanza nachokataa ulivyosema Portugal haikuwa na wachezaji wazuri 2008-2017
Huu ni uongo
Wachezaji wazuri waliotokea kizazi kimoja na Ronaldo wapo na nimekutajia mfano ndio hao kina Ricardo carvalho, pepe, Luis nani, n.k na wengine ni hao walikuja mara moja ba kupotea
Squad ya sasa ya kina bernaldo ni bora kuliko ya 2010? Hii haina sana ukweli labda kama unaangalia kwamacho. 2010 Portugal walikuwa nafasi ya 7 kwa ubora, mwaka huu 2024 wapo nafasi ya 6. Kwa utofauti hapo huwezi kuona, hivyo tunasema Portugal ya 2010 na hii ya 2024 zote viwango sawa
Squad ya 2012 iliyoshiriki euro huwezi linganisba na hii ya Sasa? Huu nao ni uongo, kwa mujibu wa wapima ubora FIFA rankings Portugal 2012 walikua nafasi ya 3 kwa ubora nyuma ya Spain na Germany. Ww ubora unaupimaje? Maana katika hata hiyo euro Portugal ndio alitoa changamoto kubwa kwa spain iliiyokua bora kabisa duniani, bila mikwaju ya penalty spain alikua anatolewa
Squad ya 2014 iliyoenda kushiriki world cup nayo umeibeza? Kwa taarifa tu kabla ya world cup portugal bado ilikua nafasi ya 3 kwa ubora duniani nyuma ya Spain na germany
Unasema Ronaldo kukosa goli kwenye knockout stage ndio sababu ya we kuona Portugal haikua na timu nzuri? Hiyo kukosa goli ni la Ronaldo mwenyewe binafsi, maana katika timu hiyo hiyo ya Portugal wapo waliofunga goli kwenye hatua hiyo.
Mchezaji kufunga au kutofunga goli hatua flani haina uhusiano na uzuri au ubovu wa timu. Fernandez mchezaji wa kawaida tu kutoka timu ya kawaida kabisa ya Australia kwenye world cup iliyopita alifunga goli hatua ya knockout. Hii euro tunayoangalia sasa, ile iliyopita top scorer alikua Ronaldo pamoja Schik kutoka Czech, Czech ni timu ya kawaida kabisa lakini Schick ameweza kuibuka top scorer. Hivyo Ronaldo kushindwa kufunga goli knockout stage huo ni uzembe wake wala hauhusiani na uzuri wa wachezaji. Hata huu uzembe messi amewahi kufanya, 2010 hakufunga goli hata moja. Hapo napo ilibidi ilaumiwe Argentina?
Figo kusifia timu ya sasa sio hoja, ndio hufanya hivyo legends wengi. Hii euro Germany wameshinda 5 dhidi ya Scotland, lakini ulimuuliza kocha wa Germany kuhusu scotland bado ataisifia na kusema wana nafasi kubwa kuchukua ubingwa wa euro