UEFA EURO 2024: Special Thread | Final: FT: Spain 2-1 England (Spain aibuka bingwa)

UEFA EURO 2024: Special Thread | Final: FT: Spain 2-1 England (Spain aibuka bingwa)

Ni dhairi kabisa hujanipata kwa usahihi mantiki yangu, umenisosoma kwa juu juu tu kisha ukaona unijibu tena kwa comment iliyojaa mahaba yaliyopitiliza.

Kwanza nikukosoe Ronaldo tangu aanze kushiriki hii michuano ya Euro mwaka huu ni mara ya tano, na katika mara zote 5 amekuwa top scorer wa michuano mara moja tu ambapo ni mwaka 2020/21.

Na pia nikujuze tu Ronaldo katika international career yake ameshiriki hizi major tournaments yaani EURO,WORLD CUP,FIFA CONFEDERATION CUP pamoja na UEFA NATIONS LEAGUE zote kwa pamoja mara 12, sasa katika mara 12 zote alizoshiriki ameibuka kama top scorer mara 2 tu, je unajua sababu???? Ni kwanini kwenye international career ana golden boot chache hivyo na wakati kwenye clubs huwa haipiti misimu miwili anaibuka mfunga bora?

Endapo kama ungekuwa umenielewa mantiki yangu hata usingeona kuna shida kwenye comment yangu.

Yaani hizo goals ambazo wewe unaona amefunga na zinakuridhisha ni ndogo sana kulinganisha na zile ambazo angeweza kufunga endapo kama angecheza na teammates wazuri tangu kipindi yuko kwenye prime(2008-2017) na hata world cup angeweza kuwa nayo leo hii kama hiki kizazi cha akina Bernado Silva,Diaz,Fernandez,Joao Felix angekuwa na anacheza nacha tangu 2010 huko..... nafikiri kwa huu ufafanuzi utakuwa umenielewa sasa.
Portugal ya 2008-2017 ilikuwa na wachezaji wa kawaida?

Huu ni uongo mkubwa, kwa miaka hiyo ukiacha Spain hakuna timu ilikua na wachezaji wazuri kama Portugal
Ricardo, Rui Patricio, Jose bosingwa, Pepe, Paulo Ferreira, Ricardo carvalho, maniche, costinha, Deco, bruno alves, postiga, Tiago, Simao, Quaresma, Nuno gomes, raul meireles, Mendes, Luis Nani, Mourinho, Hugo almeida, Fabio contreao, William carvalho,
Hao wote bawakua wazuri?
 
Back
Top Bottom