Ufafanuzi kuhusu shambulio la gari la watumishi wa TRA eneo la Tegeta, Dar es Salaam

Ufafanuzi kuhusu shambulio la gari la watumishi wa TRA eneo la Tegeta, Dar es Salaam

View attachment 3170012

UFAFANUZI KUHUSU SHAMBULIO LA GARI NA WATUMISHI WA TRA KATIKA ENEO LA TEGETA (Kwa Ndevu)

Dar es Salaam, 06 Desemba, 2024:

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inasikitika kuutarifu Umma kwamba gari yake yenye namba za usajili STL 9923, ikiwa na Watumishi watatu katika doria za kawaida za udhibiti na ukamataji wa magendo na magari yaliyoingia nchini kinyume na taratibu za Forodha na kutolipiwa ushuru, imeshambuliwa na watumishi kuumizwa katika eneo la Tegeta kwa Ndevu, tarehe 05 Disemba, 2024, usiku.

Kadhia hii imetokea baada ya watumishi wa TRA kubaini kwamba gari namba T229 DHZ aina ya BMW X6 ilioingizwa nchini kinyemela bila kulipa kodi za serikali stahiki kwa mujibu wa sheria na kuifuatilia kwa lengo la kuikamata ili kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria za kodi.

Wakati Watumishi wa TRA wanatimiza wajibu wao, walihusishwa na kitendo cha utekaji, kilichopelekea wao na gari kushambuliwa.

Mamlaka ya Mapato Tanzania, inawapa pole watumishi wake waliojeruhiwa wakiwa wanatimiza wajibu wao, pamoja na wengine wote waliojeruhiwa katika kadhia hii, na kuwaombea wapone kwa haraka.

Mamlaka ya Mapato Tanzania inauhakikishia umma kuendelea kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa sheria.

"Pamoja Tunajenga Taifa Letu"

Imetolewa na;

IDARA YA ELIMU KWA MLIPAKODI NA MAWASILIANO

Pia Soma: Tegeta, Dar: ‘Wasiojulikana’ washambuliwa na wananchi kwa mawe
Mwambieni aache kuteka wàtu ona sasa anaumiza wasiohusika!
 
Kama gari mnaijua na ina usajili kwanini msimuite mwenye nayo atoe nyaraka za gari yake? Inakuwaje mnaanza kufuatilia mtu tena usiku?

Nyie ni polisi?
Je mna mamlaka ya kumfuatilia mtu na kumkamata au kukamata mali yake bila kushirikisha vyombo vya ulinzi na usalama?

Hayo yote mmeyataka kwakuwa hali ya usalama wa raia nchini imedhoofu kiasi kwamba sasa raia ni lazima kuwa vigilant la sivyo ni kutekwa na kuuwawa tu.

Wafanyakazi wenu mnatakiwa muwape barua ya onyo kwa kuwa negligent. Wameshindwa kusoma alama za nyakati.
Valid point aione mkuu wa TRA
 
Maswali
1.Gari namba DH usajili wake ni miaka zaidi ya 4 mpaka sasa.
Je , nani aliisajili?
2.Miaka yote hiyo iweje mugundue leo ?
3. Je, gari ina usajili bandia?
Screenshot_20241206-073837.jpg
 
Gari namba DH si ni miaka karibu nane ipo nchini au? Yaani kwa usajili huo inaonesha iliingia nchini mwaka 2016. Sasa kweli tangu kipindi hicho ndyo ije idaiwe hizo kodi kwa kuzingirwa tena usiku? Halafu bila polisi?
Sikia,
Ipo gari Ingine iliyoingia hiyo miaka 8 iliyopita lakin sio hiyo BMW. Sasa hiyo gari Ingine labda ilipata ajali ikawa "Written -Off" ndio number plate zake (plate number) zikahamishiwa kwenye hiyo BMW iliyoingia juzi tu kimagendo.

Angalia hapa chini usajili wa bima hizo number unasoma ni gari ya aina gani
Screenshot_20241206-073837.jpg
 
Shida ni kwamba mmekuja kama watekaji lazima mpigwe mawe tu adios
Wananchi wanahaki ya kutetea maisha yao kwa mtu asiyejitambbulisha rasmi kwa kufuata mujibu wa sheria.

Huu ukamataji haramu na utekaji, haya ndiyo madhara yake.
Wananchi hawana makosa na mimi binafsi safari hii nawapongeza.
Serikali ijisahihishe kiutendaji maana wananchi siyo nguruwe ambao unaweza kuwafanyia upendavyo.
 
Kama gari mnaijua na ina usajili kwanini msimuite mwenye nayo atoe nyaraka za gari yake? Inakuwaje mnaanza kufuatilia mtu tena usiku?

Nyie ni polisi?
Je mna mamlaka ya kumfuatilia mtu na kumkamata au kukamata mali yake bila kushirikisha vyombo vya ulinzi na usalama?

Hayo yote mmeyataka kwakuwa hali ya usalama wa raia nchini imedhoofu kiasi kwamba sasa raia ni lazima kuwa vigilant la sivyo ni kutekwa na kuuwawa tu.

Wafanyakazi wenu mnatakiwa muwape barua ya onyo kwa kuwa negligent. Wameshindwa kusoma alama za nyakati.
sio vigilant tu ni tumekuwa masenari..
 
Wanasiasa bana, sijui wanawachukuliaje wananchi?

Basi, asubuhi Waziri Mwigulu Nchemba akaibuka Instagram na kulaani.

Wananchi nao wamemtolea uvivu (hakuna cha siasa).

Nawarahisishia TRA kupata snapshot ya public reaction kwa Waziri wenu na jinsi wananchi walivyochoka.

Iwe funzo pia kwa Serikali na Mamlaka zake huko tunakoelekea. Hofu HAKUNA TENA

IMG_8739.jpeg

IMG_8713.jpeg
IMG_8714.jpeg
IMG_8718.jpeg
IMG_8719.jpeg
IMG_8720.jpeg
IMG_8715.jpeg
IMG_8716.jpeg
IMG_8717.jpeg
IMG_8721.jpeg
IMG_8722.jpeg
IMG_8723.jpeg
IMG_8724.jpeg
IMG_8725.jpeg
IMG_8726.jpeg
IMG_8728.jpeg
IMG_8729.jpeg
IMG_8730.jpeg
IMG_8731.jpeg
IMG_8732.jpeg
IMG_8733.jpeg
IMG_8734.jpeg
IMG_8735.jpeg
IMG_8736.jpeg
IMG_8737.jpeg
IMG_8738.jpeg
 
TRA mnafanya mambo kama vile shule hamjapitia kabisa.

Yaani kipindi hiki cha utekaji halafu mnawatuma watu wawakamate mtu usiku kwa gari hizo hizo(Land cruiser)?

Pia nina mashaka kama kweli walikuwa wanafatilia gari ambalo halijalipiwa kodi usiku maana kama wangefanikiwa kuteka tungeambiwa ni watu wasiojulikana.

Siku nyingine mkifanya hivyo mnawahatarishia maisha wafanyakazi wenu; tumieni japo akili kidogo ingawa najua hakuna kitu mnajua zaidi ya kutumia nguvu bila hata chembe ya akili..
 
Back
Top Bottom