Ufafanuzi kuhusu shambulio la gari la watumishi wa TRA eneo la Tegeta, Dar es Salaam

Ufafanuzi kuhusu shambulio la gari la watumishi wa TRA eneo la Tegeta, Dar es Salaam

Hii ni ngeni kwako? Fatilia vizuri hao jamaa wana operations zao, intelejensia yao na wanakamata vilevile, haijalishi siku wala masaa.
Sasa hapo ndio wategemee kuumizwa.
Kazi ya ukamataji hiyo itawaghalimu.
 
Tatizo lingine TRA hawapendwii na wananchi. Hivyo ni rahisi sana kwa wananchi kumsaidia anaekimbizwa na tra kurusha mawe ama hata kuwachoma moto tra. Sababu hawawapendi tra

Tafuta post ile ya ajali iliyoua wafanyakazi wa TRA mbeya usome comments zake wananchi walivyoshangilia vifo vyao
Uko sahihi
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inasikitika kuutarifu Umma kwamba gari yake yenye namba za usajili STL 9923, ikiwa na Watumishi watatu katika doria za kawaida za udhibiti na ukamataji wa magendo na magari yaliyoingia nchini kinyume na taratibu za Forodha na kutolipiwa ushuru, imeshambuliwa na watumishi kuumizwa katika eneo la Tegeta kwa Ndevu, tarehe 05 Disemba, 2024, usiku.

Kadhia hii imetokea baada ya watumishi wa TRA kubaini kwamba gari namba T229 DHZ aina ya BMW X6 ilioingizwa nchini kinyemela bila kulipa kodi za serikali stahiki kwa mujibu wa sheria na kuifuatilia kwa lengo la kuikamata ili kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria za kodi.

Wakati Watumishi wa TRA wanatimiza wajibu wao, walihusishwa na kitendo cha utekaji, kilichopelekea wao na gari kushambuliwa.

Mamlaka ya Mapato Tanzania, inawapa pole watumishi wake waliojeruhiwa wakiwa wanatimiza wajibu wao, pamoja na wengine wote waliojeruhiwa katika kadhia hii, na kuwaombea wapone kwa haraka.

Mamlaka ya Mapato Tanzania inauhakikishia umma kuendelea kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa sheria.

"Pamoja Tunajenga Taifa Letu"

Imetolewa na;

IDARA YA ELIMU KWA MLIPAKODI NA MAWASILIANO

Pia Soma: Tegeta, Dar: ‘Wasiojulikana’ washambuliwa na hivi kweli ni sawa kwa watumishi wa TRA kuwa mamraka ya kukamata watu. Bila chombo chenye utalaam wa masuala ya ukamataji kuhusika. Watanzania tutaponea wapi jamani? TRA wakamate , mgombo halimashauri wakamate , usalama wa taifa wakamate, jeshi likamate, polisi wakamate, mahakama zikamate, wakuu wa wilaya na mikowa nao wakamate
 
Inawezekana wao wanaona wanatimiza wajibu. Kukamata kuwe kwa utaratibu na kwa kutimiza vigezo vyote vinavyotakiwa.
Jamii yetu ina taharuki na hawa wanaosemekana ni watu wasiojulikana. Wanachukua watu na so far ni kama vile wameshinda maana hawakamatiki
Kwahiyo, pale raia wanapowaona wasiojulikana wameingia 18 zao, si wanawarahisishia kazi wenye wajibu wa kukamata?
Imani imepotea kabisa kwenye usalama wa raia sababu watu wengi waliopotea hakuna anayejua wameenda wapi. Kwahiyo ikitokea kuna mwanya wa kuzuia kupotezwa kwa raia wengine na watu wasiojulikana, raia wakiweza kudhibiti sina shaka wataendelea kufanya hivyo.
Necessity is the mother of all invetions.
Wana operate kijambaz jambaz hawa nao na wangemtuliza sana sana wangemtoa hela tu wangemuachia
Nakumbuka mbeya kuna jamaa wa TRA walikuwa wanakimbiza gari limebeba magendo jamaa wa TRA Walikuwa mzinga wote walikata moto 😄
Hawakomi tuu

Ova
 
TRA,wameshindwa hata kutaja kifungu Cha Sheria kinachowaruhuau wao kufanya doria ya ukamataji bila polisi
 
A

Ndivyo ilivyo joh, mtu awaye yote asipoteze rasilimali muda na akili zake kufikiria cha kukujibu. Alipuke tu kama unavyolipuka
huko kujitoa muhanga kitaalam ni sawa na ugaidi.

ni aina ya ukataji tamaa wa kiwango cha juu mno. Na Chimbuko lake hua ni uvivu tu,

So,
gentleman kaza buti uondokane na mihemko ya hovyo kama hivyo 🐒
 
Kwahiyo mkono wakushoto unashambulia mkono wakulia au ? Hawakupeana taarifa 🤔🤭🤭🤭
 
Kama gari mnaijua na ina usajili kwanini msimuite mwenye nayo atoe nyaraka za gari yake? Inakuwaje mnaanza kufuatilia mtu tena usiku?

Nyie ni polisi?
Je mna mamlaka ya kumfuatilia mtu na kumkamata au kukamata mali yake bila kushirikisha vyombo vya ulinzi na usalama?

Hayo yote mmeyataka kwakuwa hali ya usalama wa raia nchini imedhoofu kiasi kwamba sasa raia ni lazima kuwa vigilant la sivyo ni kutekwa na kuuwawa tu.

Wafanyakazi wenu mnatakiwa muwape barua ya onyo kwa kuwa negligent. Wameshindwa kusoma alama za nyakati.
Hadi anapata usajili halali, hawakujua kuwa ni mkwepa kodi?
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inasikitika kuutarifu Umma kwamba gari yake yenye namba za usajili STL 9923, ikiwa na Watumishi watatu katika doria za kawaida za udhibiti na ukamataji wa magendo na magari yaliyoingia nchini kinyume na taratibu za Forodha na kutolipiwa ushuru, imeshambuliwa na watumishi kuumizwa katika eneo la Tegeta kwa Ndevu, tarehe 05 Disemba, 2024, usiku.

Kadhia hii imetokea baada ya watumishi wa TRA kubaini kwamba gari namba T229 DHZ aina ya BMW X6 ilioingizwa nchini kinyemela bila kulipa kodi za serikali stahiki kwa mujibu wa sheria na kuifuatilia kwa lengo la kuikamata ili kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria za kodi.

Wakati Watumishi wa TRA wanatimiza wajibu wao, walihusishwa na kitendo cha utekaji, kilichopelekea wao na gari kushambuliwa.

Mamlaka ya Mapato Tanzania, inawapa pole watumishi wake waliojeruhiwa wakiwa wanatimiza wajibu wao, pamoja na wengine wote waliojeruhiwa katika kadhia hii, na kuwaombea wapone kwa haraka.

Mamlaka ya Mapato Tanzania inauhakikishia umma kuendelea kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa sheria.

"Pamoja Tunajenga Taifa Letu"

Imetolewa na;

IDARA YA ELIMU KWA MLIPAKODI NA MAWASILIANO

Pia Soma: Tegeta, Dar: ‘Wasiojulikana’ washambuliwa na wananchi kwa mawe
WEWE MTOA TAARIFA,HAUNA AKILI.

WATANZANIA TUJIFUNZE KUSIMAMIA SHERIA.
NI SHERIA GANI ILIWAONGOZA HAO KWENDA KUMKAMATA MTU KWA KUZIBA GARI BILA ASKARI WALA CHOCHOTE CHA KUTHIBITISHA SIO WATEKAJI?
 
ukweli mchungu ,hao jamaa walikuwa wanafanya uhalifu katika vazi la tra .Ingawa kuna mambo mengi sana juu ya hili , serikali ya Samia iamke na ijitafakari, jambo la kwanza maswala ya utekaji, yameshamiri mbili uchaguzi wa serikali za mitaa ccm kushinda asilimia 99 maoni ya wananchi yanayotolewa juu ya tukio hili ,it is a clear picture kwamba nchi imegawanyika
 
Back
Top Bottom