BB Pharma consultancy Ltd
New Member
- Jan 24, 2017
- 4
- 2
Ndugu msomaji wetu, mfanyabiashara na Mjasiriamali.
Leo tunataka kukujuza juu ya undani wa biashara ya vipodozi hapa Tanzania. Biashara ilioyoenea sana lakini wengi kwa kutokutambua, huifanya bila kufuata utaratibu..na matokeo yake huwa si rafiki hata kidogo kibiashara.
ELIMU hii, kama si wewe, basi inaweza kumsadia ndugu, rafiki au jamaa.
KARIBU SANA.
Kwa Tanzania, na kwingineko duniani, vipodozi hujumuishwa ndani ya kundi kubwa la bidhaa za afya (Healthcare products). Biashara ya vipodozi ni moja kati ya biashara zinazodhibitiwa kisheria (regulated business), na usimamizi wa biashara ya bidhaa hizi kwa Tanzania bara unafanywa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA).
Biashara hii ya vipodozi pia ni moja kati ya biashara zilizoenea sana hapa nchini; karibu kila mtaa (hasa maeneo ya mijini), hutapita hatua chache bila kukuta duka la vipodozi. Na ni biashara ambayo soko lake ni kubwa na linaendelea kukua siku hadi siku.
Kwa bahati mbaya, maduka haya mengi yamekuwa yanauza vipodozi ambavyo havijasajiliwa na TFDA, ukiachilia mbali maduka yenyewe pia mengi kutokutambuliwa na Mamlaka.
Na kama nilivyogusia hapo juu, biashara hii ni “regulated business” hivyo kwa mujibu wa sheria na kanuni za Tanzania, kuuza vipodozi visivyosajiliwa ama kuuza vipodozi bila kibali ni kosa kisheria. Mimi na wewe ni mashaidi kwani mara nyingi tumeona na kusikia maduka mengi ya vipodozi yakifungwa na bidhaa kuharibiwa na Mamlaka husika, sababu mojawapo ikiwa ni kufanyika kwa biashara hii kinyume na taratibu.
Mbali na uvunjaji wa sheria, pia ni muhimu tukajua ya kwamba, uuzaji huu wa VIPODOZI visivyosajiliwa una madhara makubwa sana yakiwemo yale ya kiafya kwa jamii yetu ya watanzania.
Kwa haraka haraka, inaweza kuonekana kwamba kukwepa kufuata utaratibu na kuifanya biashara hii kinyemela haina shida sana, LAKINI shida ipo, tena kubwa sana; mojawapo ni hiyo ya kukamatwa kwa kuvunja sheria na biashara yako inaweza ikawa ndo mwisho wake.
Njia pekee ya kuepukana na haya yote ni kuhakikisha UNARASIMISHA biashara yako.
Sasa basi, pamoja na kupata TIN na lesseni ya biashara, mchakato wa urasimishaji wa biashara ya vipodozi una mambo mengine mawili (02) muhimu ya kufuata.
(1) JAMBO LA KWANZA: Kusajili bidhaa zako, ama kuhakikisha unauza bidhaa zilizosajiliwa na TFDA.
(2) JAMBO LA PILI: Kupata kibali cha biashara kutoka TFDA.
Ukifanikiwa kuyafanya mambo haya mawili, basi utafanya biashara yako raha mustarehe bila bugdha yoyote ile.
Hata hivyo, utafiti wetu mfupi ulionesha kwamba, UGUMU uliopo katika zoezi zima la usajili wa bidhaa hizi za afya pamoja na upatikanaji wa vibali ndiyo umekuwa sababu kuu ya wajasiriamali na wafanyabiashara wengi kushindwa kusajili bidhaa zao na kurasimisha biashara zao pia.
Kufuatia changamato hii, tumeona, kama kampuni ni vyema kufanya juhudi za dhati kutoa elimu, ufafanuzi na msaada wa kitaalamu utakao kusaidia wewe msomaji wetu na mfanyabiashara katika zoezi zima la usajili wa biashara yako na bidhaa zako.
Makala hii ni ndefu sana, hatuwezi kuiweka yote hapa, hata hivyo usijali ndugu msomaji wetu tunanjia mbili za wewe kuweza kuipata kwa urefu wake;
(1) Ya kwanza, fuata hii link inakupeleka moja kwa moja.. http://pharmaregtz.com/sites/default/files/Mambo Makuu 2 lazima kuyajua..pdf
(2) Ya pili-- Comment email address yako au tutumie kwenye sms au email yetu ya support@pharmaregtz.com nasi tutakutumia makala yote ndani ya muda mfupi. Pia, tukipata email yako tutakuunganisha moja kwa moja na mtandao wetu wa email na hivyo utakuwa unapata taarifa mbalimbali zitakazo kusaidia wewe, au jamaa yako katika biashara hii ya VIPODOZI na bidhaa nyingine za afya (kama vile dawa, vifaa tiba na vyakula).
Leo tunataka kukujuza juu ya undani wa biashara ya vipodozi hapa Tanzania. Biashara ilioyoenea sana lakini wengi kwa kutokutambua, huifanya bila kufuata utaratibu..na matokeo yake huwa si rafiki hata kidogo kibiashara.
ELIMU hii, kama si wewe, basi inaweza kumsadia ndugu, rafiki au jamaa.
KARIBU SANA.
Kwa Tanzania, na kwingineko duniani, vipodozi hujumuishwa ndani ya kundi kubwa la bidhaa za afya (Healthcare products). Biashara ya vipodozi ni moja kati ya biashara zinazodhibitiwa kisheria (regulated business), na usimamizi wa biashara ya bidhaa hizi kwa Tanzania bara unafanywa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA).
Biashara hii ya vipodozi pia ni moja kati ya biashara zilizoenea sana hapa nchini; karibu kila mtaa (hasa maeneo ya mijini), hutapita hatua chache bila kukuta duka la vipodozi. Na ni biashara ambayo soko lake ni kubwa na linaendelea kukua siku hadi siku.
Kwa bahati mbaya, maduka haya mengi yamekuwa yanauza vipodozi ambavyo havijasajiliwa na TFDA, ukiachilia mbali maduka yenyewe pia mengi kutokutambuliwa na Mamlaka.
Na kama nilivyogusia hapo juu, biashara hii ni “regulated business” hivyo kwa mujibu wa sheria na kanuni za Tanzania, kuuza vipodozi visivyosajiliwa ama kuuza vipodozi bila kibali ni kosa kisheria. Mimi na wewe ni mashaidi kwani mara nyingi tumeona na kusikia maduka mengi ya vipodozi yakifungwa na bidhaa kuharibiwa na Mamlaka husika, sababu mojawapo ikiwa ni kufanyika kwa biashara hii kinyume na taratibu.
Mbali na uvunjaji wa sheria, pia ni muhimu tukajua ya kwamba, uuzaji huu wa VIPODOZI visivyosajiliwa una madhara makubwa sana yakiwemo yale ya kiafya kwa jamii yetu ya watanzania.
Kwa haraka haraka, inaweza kuonekana kwamba kukwepa kufuata utaratibu na kuifanya biashara hii kinyemela haina shida sana, LAKINI shida ipo, tena kubwa sana; mojawapo ni hiyo ya kukamatwa kwa kuvunja sheria na biashara yako inaweza ikawa ndo mwisho wake.
Njia pekee ya kuepukana na haya yote ni kuhakikisha UNARASIMISHA biashara yako.
Sasa basi, pamoja na kupata TIN na lesseni ya biashara, mchakato wa urasimishaji wa biashara ya vipodozi una mambo mengine mawili (02) muhimu ya kufuata.
(1) JAMBO LA KWANZA: Kusajili bidhaa zako, ama kuhakikisha unauza bidhaa zilizosajiliwa na TFDA.
(2) JAMBO LA PILI: Kupata kibali cha biashara kutoka TFDA.
Ukifanikiwa kuyafanya mambo haya mawili, basi utafanya biashara yako raha mustarehe bila bugdha yoyote ile.
Hata hivyo, utafiti wetu mfupi ulionesha kwamba, UGUMU uliopo katika zoezi zima la usajili wa bidhaa hizi za afya pamoja na upatikanaji wa vibali ndiyo umekuwa sababu kuu ya wajasiriamali na wafanyabiashara wengi kushindwa kusajili bidhaa zao na kurasimisha biashara zao pia.
Kufuatia changamato hii, tumeona, kama kampuni ni vyema kufanya juhudi za dhati kutoa elimu, ufafanuzi na msaada wa kitaalamu utakao kusaidia wewe msomaji wetu na mfanyabiashara katika zoezi zima la usajili wa biashara yako na bidhaa zako.
Makala hii ni ndefu sana, hatuwezi kuiweka yote hapa, hata hivyo usijali ndugu msomaji wetu tunanjia mbili za wewe kuweza kuipata kwa urefu wake;
(1) Ya kwanza, fuata hii link inakupeleka moja kwa moja.. http://pharmaregtz.com/sites/default/files/Mambo Makuu 2 lazima kuyajua..pdf
(2) Ya pili-- Comment email address yako au tutumie kwenye sms au email yetu ya support@pharmaregtz.com nasi tutakutumia makala yote ndani ya muda mfupi. Pia, tukipata email yako tutakuunganisha moja kwa moja na mtandao wetu wa email na hivyo utakuwa unapata taarifa mbalimbali zitakazo kusaidia wewe, au jamaa yako katika biashara hii ya VIPODOZI na bidhaa nyingine za afya (kama vile dawa, vifaa tiba na vyakula).