Ufahamu kuhusu nyota za angani

Ufahamu kuhusu nyota za angani

Kama nilivyo ahidi ifuatayo ni ile nyongeza.

Nyota zinazaliwaje?
Kabla ya nyota kuzaliwa inaanza kama sayari ya kawaida wakati vumbi na hewa (sana sana hydrogen) ikijikusanya. Kadri hii hewa na vumbi vinavyoongezeka basi gravity nayo pia inaongezeka. Tukichukulia ukubwa/uzito wa jua letu kama kiwango (solar-mass) basi mkusanyiko wowote ule wa vumbi na hewa chini ya 0.013 solar-mass (1.3% ukubwa wa jua letu) hiyo itakuwa ni sayari (planet) tu. Kuanzia ukubwa wa 0.08 solar-mass na kuendelea gravity inakuwa kubwa sana (kilo moja hapa duniani ukiipeleka huko itakuwa na uzito wa kilo bilioni 100 na zaidi). Huu mgandamizo mkubwa wa gravity unafanya joto kupanda zaidi ya nyuzi milioni 15 celcius. Hili joto na mgandamizo wa gravity ndio kibiriti kinachofanya hydrogen ichanganyike ketengeneza helium na kutoa nguvu hizi za nyuklia (fusion). Hivi ndio jua linavyozaliwa.

Nyota zinakufaje?
Maisha ya nyota yanategemea sana na ukubwa wake. Nyota ndogo zinaishi muda mrefu sana (zinachoma hydrogen yake taratibu taratibu) kuliko nyota kubwa. Kwa mfano, nyota ndogo kama jua letu inategemewa kuwaka kwa miaka bilioni 10 wakati nyota kubwa sana kama Betelgeuse zinategemewa kuwaka kwa miaka million 10 tu.

Wakati nyota inawaka kunakuwa na uwiano (equilibrium) wa nguvu ya gravity na nyuklia. Gravity inakandamiza chini wakati milipuko ya nyuklia inasukuma vitu nje. Uwiano huu unaendelea hata baada ya hydrogen ikiisha. Baada ya hydrogen kuisha helium nayo italipuka kinyuklia kutengeneza Carbon na Oxygen. Baadae carbon nayo italipuka kunyuklia kutengeneza iron (chuma). Mara tu nyota inapoanza kutengeneza chuma (iron), mchezo umekwisha. Chuma ni kama maji yanayouzima huu mlipuko wa nyuklia mara moja. Milipuko ya nyuklia ikiacha, ule uwiano (equilibrium) wa gravity na nyukilia unakuwa haupo tena na gravity inashinda. Kila kitu huanguka chini na mlipuko mkubwa sana wa mwisho hutokea na mwanga mkubwa sana (super nova) huonekana.

Vitu viwili vinatokea wakati wa hii super nova. Kwanza, madini nzito zaidi ya chuma (iron) yanatengenezwa kama vile dhahabu, urani, nk. Hii ndio maana dunia yetu pamoja na sisi tunaitwa vumbi la nyota (star dust) kwa saababu kama hizi super nova zisingetokea basi dunia yetu na sisi tusingekuwepo. La pili linaliotokea baada ya kishindo (collapse) ni kuwacha tumba (core) ndogo sana lakini yenye uzito (density) mkubwa wa ajabu. Hii tumba ndio ijulikanayo kama BLACK HOLE.

(For correctness sake, not all stars die and turn into black holes. For instance, our sun is too small to turn into a black hole. When it dies it will collapse into a dense core with properties nowhere close to those of black holes)

Black holes na makaburi ya nyota.
Black holes zinazotokea baada ya nyota kubwa sana (super massive stars) ku-collapse ni vitu vya ajabu sana. Chupa moja ya bia (ujazo wa 0.5 lita) ya hii black-hole ina uzito wa zaidi ya tani 3,000,000,000,000. Gravity inayotokana na hizi black holes ni kubwa kiasi ya kumeza kitu chochote kile (majua, sayari, nk) kinachoikaribia. Hii gravity ni kubwa kiasi cha kumeza hata mwanga (even light cannot escape it) na ndio maana zinaitwa BLACKHOLE kwa sababu hazionekani (mwanga pia unamezwa). Kuwepo wa black hole kunajulikana tu kwa vitu inavyovimeza au vinavyo izunguuka. Usiku ukitoka nje angalia juu. Ukiona ukanda wa nyota nyingi basi huo ndio mkusanyiko wetu wa nyota (Galaxy yetu) unaoitwa MILKYWAY. Katikati ya hi
i galaxy yetu lipo hili black hole moja ambalo jua letu na nyota nyingine zote zilizopo kwenye hii galaxy yetu zinalizunguuka. Ukitaka kujua hii blackhole yetu iko wapi angalia juu na kama unaijua constellation ya Virgo basi usawa huo ndipo lilipo.

Natumaini hii itasaidia pa kuanzia katika kuzijua nyota.

cc. Mwamba028, 2013 Globu
Iron Lady

Lecture nzuri kiasi.... Sema wanasayansi wetu sijui hawpo updated ama ndo kukariri...

Bingwa wa sayansi kashasema balckhole doesnt exist! Sasa sijui kwanini mnapoteza energy kuzungumzia na kuelezea something which doesnt exist....
 
mkuu kifyatu mimi naomba kukurudisha nyuma
1. super nova ni nini na zinalipuka mara ngapi ili sisi tupate hizo faida zake
2. tunaonaje ama kujuaje kwamba supernova imetokea
3. blackhole na usalama wa dunia vimekaaje
4. UFO's ni nini?
samahani kama maswali yamekuwa mengi lakini hii mada imekuwa interesting kwangu kuliko bunge lla katiba!!


Usijali mkuu nitajaribu kudadavua zaidi hii mada. Sote tuko hapa JF kujifunza.

1. super nova ni nini na zinalipuka mara ngapi ili sisi tupate hizo faida zake
Super nova inapolipuka hutengeneza black hole na vumbi linalobaki hujikusanya na kutengeneza sayari kama dunia yetu. Baada ya hizi sayari kutengenezwa basi zinapitia process ya evolution. Kama sayari ina vigezo vizuri kama dunia yetu (joto, maji, nk.) basi maisha yanaweza kuanza kwa hii njia ya evolution (from simple amino acids, to DNA, to one-celled organisms, to multi-celled creatures to humans, animals, fish, etc.)

2. tunaonaje ama kujuaje kwamba supernova imetokea
Nyota kubwa zinapokufa zinalipuka kama super nova. Hakuna anaejua lini super nova itatokea. Wataalam wa anga wameelekeza darubini zao angani na mara kwa mara wataona sehemu ambayo palikuwa na kanyota kadogo mara panatokea mwanga mkubwa sana. Hapa ndio wanajua super nova imetokea.

3. blackhole na usalama wa dunia vimekaajeo jua letu.
Usiiogope black hole. Hii ni center of gravity kama lilivyo jua letu. Sayari zetu zinalizunguuka jua na hatuogopi kuwa litatumeza. Hivyo hivyo, nyota zilizoko kwenye galaxy yetu (milkway) zinaizunguuka hiyo black hole na hazitamezwa. Vitu vinavyomezwa na black holes ni vile vinavyo sesereka na kuikaribia.

4. UFO's ni nini?
UFO ni kifupi cha Unidentified Flying Object au kitu kilichoko angani ambacho hakijulikani. Kuna dhana kuwa hivi ni vyombo vya viumbe vitokavyo kwenye sayari nyingine zaidi ya dunia yetu. Pia inaaminika kuwa serikali kama za marekani wamevikamata lakini wanafanya siri. Hii dhana siwezi kuithibitisha lakini kama ni kweli basi tujipange. Kuna watu waliotoa ushuhuda kuwa walitekwa na hivi viumbe vilivyokuja na hizi UFOs na kufanyiwa majaribio. Mimi sina sababu ya kutowaamini lakini bado hatujaona ushahidi (physical evidence).

Mara nyingi hizi UFO unakuta ni ndege za majaribio (kwa mfano marekani walipokuwa wanajaribu stealth jets. alieziona wakati huo asingejua ni kitu gani na angeziita UFO). Wakati mwengine ni matufe ya kupimia hali ya hewa (weather baloons).

Jibu zuri kwako ni kuwa hata mimi sijui UFO ni nini. Ni hati hati tu kama nilivyoainisha hapa.
 
Lecture nzuri kiasi.... Sema wanasayansi wetu sijui hawpo updated ama ndo kukariri...

Bingwa wa sayansi kashasema balckhole doesnt exist! Sasa sijui kwanini mnapoteza energy kuzungumzia na kuelezea something which doesnt exist....

Ni bingwa gani wa sayansi aliesema blackhole does not exist. General relativity has predicted it theoretically, and astronomical observation have proved their existence.

Naomba unijuze (maana sote tunajifunza) kama kuna sayansi mpya iliotokea mwezi huu inayothibitisha kuwa blackholes hazipo. Kuna any scientific paper ninayoweza kuiona inayothibitisha unachosema?
 
Hii mada imenifanya ni load mambo mengi ambayo mwanzo nilikuwa nayajua lakin nilikuwa siyaelewi likin leo nimeyaelewa zaid...!!
ila pia kuna mambo ambayo nilikuwa nataka kuelewa zaid..
Hivii hii "THE BIG BANG THEORY" ni kweli ndio chimbuko la mwadaam yan Element au chembechembe ambazo binaadam ameumbwa nazo ni zao la hio Theory ¡¡¡
Na pia je kuhusiana na elimu ya nyota inavohusika kwenye utabiri, kutoa ishara ,Bahati na mengineyo Mfano mm kuna nyota tatu zimekaa mstari na nyingine kama umbo Pyramid ambazo ni tofauti na nyingine thou zina change position kutokana na rotation ya dunia, but kitu ambacho najiuliza how can i interprate that sign ni hayo 2 nilikuwa naomba kueleweshwa na sio kuyafaham.

Big bang ndio inayoaminiwa kuzalisha matter kutoka nishati (pure energy). Einstein alituonyesha kuwa unaweza kuanza na matter (kama uranium au hydrogen) yenye uzito m na kutengeneza nishati E kwa kanuni ya E = mC[SUP]2[/SUP]. (C = speed ya mwanga). Big bang inaigeuza hii process. Unaanza na nishati E na unaigeuza kuwa matter m.

Binaadam hakutokea wakati wa big bang. Ni baada ya hydrogen iliyotengenezwa na big bang kutengeneza nyota, nyota kufa (super nova) vumbi la hizi nyota kugeuka sayari (kama dunia yetu) ndipo evolution ikachukua mkondo wake na sisi viumbe tukatokea.

Utabiri wa nyota - Astrology
Wataalam wa anga wa zamani sio tu walikuwa wanatafuta uelewa wa nyota zimejipangaje, sayari na mizunguuko yake (fani inayojulikana kama Astronomy) lakini pia walikuwa wanajaribu kuona kama kuna uhusiano wa maisha yako na wapi jua, mwezi, sayari, na nyota zilipo ulipozaliwa, na sasa (fani inayojulikana kama Astrology).

Dhana hapa ni kuwa kama mwezi unaweza kuvuta maji ya bahari na kuleta high na low tides, basi kwa nini hauwezi kumuathiri binaadamu ambae aslimia 80 ya mwili wake ni maji. Wengi wanaamini kuwa wakati wa full moon basi wangonjwa kwenye psychiatric wards wanacharuka sana. By extension, jua, sayari nyingine na makundi ya nyota pia yanaweza ku-shape maisha yako.

Mimi sina utaalam wa utabiri wa nyota (astrology) kwa hiyo naomba wale waliobobea katika astrology watujuze.
 
4. UFO's ni nini?
UFO ni kifupi cha Unidentified Flying Object au kitu kilichoko angani ambacho hakijulikani. Kuna dhana kuwa hivi ni vyombo vya viumbe vitokavyo kwenye sayari nyingine zaidi ya dunia yetu. Pia inaaminika kuwa serikali kama za marekani wamevikamata lakini wanafanya siri. Hii dhana siwezi kuithibitisha lakini kama ni kweli basi tujipange. Kuna watu waliotoa ushuhuda kuwa walitekwa na hivi viumbe vilivyokuja na hizi UFOs na kufanyiwa majaribio. Mimi sina sababu ya kutowaamini lakini bado hatujaona ushahidi (physical evidence).
Mara nyingi hizi UFO unakuta ni ndege za majaribio (kwa mfano marekani walipokuwa wanajaribu stealth jets. alieziona wakati huo asingejua ni kitu gani na angeziita UFO). Wakati mwengine ni matufe ya kupimia hali ya hewa (weather baloons). Jibu zuri kwako ni kuwa hata mimi sijui UFO ni nini. Ni hati hati tu kama nilivyoainisha hapa.
penye red:
kwa kuongezea tu kuhusu UFOs Hizi story za UFOs, zilianza kipindi cha Hilter ambapo inadaiwa alipanga kuunda secret society yake ambayo alitaka iwe na nguvu kuliko Vatican(St Peters church), na pia alishaadraft michoro ya UFOs ambayo haitofautiani na hii inayodaiwa kujitokeza miaka ya leo.
german ni taifa la kwanza kuunda submarine, kuruka na Parachute,Baloons, radar.Na muundo wa kofia za kijeshi za marekani umetokana na kuigiza ule wa jeshi la ujerman enzi za Hitler.Wanasayansi walioiwezesha US kwenda kwenye space ni wa kutoka ujerman. Na ideas za UFOs zilianza kwao.

wernher von braun(german scientist) aliyechukuliwa na wenzake kwenda marekani kupitia mpango wa ''Operation paper clip'' baada ya vita kuu ya Pili aliwahi kukaririwa akisema wanapata msaada wa alliens baada ya kuulizwa iliwezekanaje kwa german kuweza kuunda technolojia kubwa ndani ya muda mfupi.wamarekani wanamtambua kama father of rocket.
(ukifuatilia makala nzima utaona Alliens na UFOs is almost the same thing kwani vyote vinasemekana kutokea sayari nyingine nje ya dunia)

marekani kuna eneo linaitwa Area 51(Area fifty one).Ukisoma makala nyingi ni eneo maarufu zaidi kwa UFOs kushuka duniani, lakini miaka ya karibuni baada ya kuanguka kwa USSR limegundulika ni eneo la kutengeneza na kujaribisha vyombo vya kisayansi vya jeshi na space kwa siri la marekani.

na kwa kuongeza ni kuwa mwaka jana, UFO ilionekana middle East(iran, palestine na Israel) lakini baada ya siku kadhaa Iran wakatamba kuwa wamerusha drone kikaingia kwenye anga ya Israel bila kutambulika, japo Israel ilikataa.
THIRDPHASEOFMOON » Breaking News UFOs Over Middle East! Could This Be a Sign?

binafsi kitu nachoweza kusema ni kuwa UFOs ni technology ya juu inayoundwa na binadamu na sio viumbe vinavyodhaniwa kushuka duniani kutokea sayari nyingine.


 
penye red:
kwa kuongezea tu kuhusu UFOs Hizi story za UFOs, zilianza kipindi cha Hilter ambapo inadaiwa alipanga kuunda secret society yake ambayo alitaka iwe na nguvu kuliko Vatican(St Peters church), na pia alishaadraft michoro ya UFOs ambayo haitofautiani na hii inayodaiwa kujitokeza miaka ya leo.
german ni taifa la kwanza kuunda submarine, kuruka na Parachute,Baloons, radar.Na muundo wa kofia za kijeshi za marekani umetokana na kuigiza ule wa jeshi la ujerman enzi za Hitler.Wanasayansi walioiwezesha US kwenda kwenye space ni wa kutoka ujerman. Na ideas za UFOs zilianza kwao.

wernher von braun(german scientist) aliyechukuliwa na wenzake kwenda marekani kupitia mpango wa ''Operation paper clip'' baada ya vita kuu ya Pili aliwahi kukaririwa akisema wanapata msaada wa alliens baada ya kuulizwa iliwezekanaje kwa german kuweza kuunda technolojia kubwa ndani ya muda mfupi.wamarekani wanamtambua kama father of rocket.
(ukifuatilia makala nzima utaona Alliens na UFOs is almost the same thing kwani vyote vinasemekana kutokea sayari nyingine nje ya dunia)

marekani kuna eneo linaitwa Area 51(Area fifty one).Ukisoma makala nyingi ni eneo maarufu zaidi kwa UFOs kushuka duniani, lakini miaka ya karibuni baada ya kuanguka kwa USSR limegundulika ni eneo la kutengeneza na kujaribisha vyombo vya kisayansi vya jeshi na space kwa siri la marekani.

na kwa kuongeza ni kuwa mwaka jana, UFO ilionekana middle East(iran, palestine na Israel) lakini baada ya siku kadhaa Iran wakatamba kuwa wamerusha drone kikaingia kwenye anga ya Israel bila kutambulika, japo Israel ilikataa.
THIRDPHASEOFMOON » Breaking News UFOs Over Middle East! Could This Be a Sign?

binafsi kitu nachoweza kusema ni kuwa UFOs ni technology ya juu inayoundwa na binadamu na sio viumbe vinavyodhaniwa kushuka duniani kutokea sayari nyingine.



Nimekupata mkuu. Nakubaliana na wewe. Unajua kama sio upumbavu wa Hitler kuanzisha lile varangati wakati wa vita vya pili vya dunia, basi leo Ujerumani ingekua super power kabambe kiteknolojia. Wanasayansi wa kijerumani wameleta michango mingi ya teknolojia tunazozitumia sasa.

Big up mkuu.
 
nimekupata mkuu. Nakubaliana na wewe. Unajua kama sio upumbavu wa hitler kuanzisha lile varangati wakati wa vita vya pili vya dunia, basi leo ujerumani ingekua super power kabambe kiteknolojia. Wanasayansi wa kijerumani wameleta michango mingi ya teknolojia tunazozitumia sasa.

Big up mkuu.
definitely yes.... Mkuu.
 
NYOTA ni kama jua lakini ziko mbali sana na dunia kushinda jua.NYOta ni kubwa kushinda jua.

Mkuu jua ndio nyota kubwa kuliko zote. So a sun is a star too
Msaada zaidi: just google ''Sun"

Ni kweli jua ndiyo nyota kubwa kuliko zote kwenye mfumo wetu wa jua (solar system) ambao una sayari 9 tu. Nyota unazoziona zinang'aa ziko mbali mno, wala haziko kwenye mfumo wetu huu wa kwetu, yaani ziko nje ya solar sytem. Jirani ya mfumo wetu, yaani jirani yetu aliye karibu sana na mfumo wetu wa jua (hayuko kwenye mfumo wetu) ni nyota inayoitwa alpha centauri, ambaye yuko umbali wa unaokadiriwa kuwa 4.4 light years kutoka hapa kwenye mfumo wetu wa jua, kwa maana kwamba umbali huo, ni umbali ambao ukiwa na ndege au chombo kingine chochote kile chenye uwezo wa kutembea kwa kasi ya km laki3 kwa sekunde moja (300,000km per second), au sawa na roundtrip zaidi ya 10 za kutoka Dar kwenda Mwanza (na kurudi), au zaidi ya 20 za Dar Mwanza, kwa sekunde moja tu, kinaweza kuchukua muda wa miaka 4.4 kufika kwa jirani yetu nyota ya alpha centauri ambaye ndiyo jirani aliye karibu zaidi na sisi.

Mbali na hayo, jirani yetu kwenye galaxy yetu, yaani galaxy ambayo iko karibu sana na sisi kwenye universe inaitwa andromeda na iko umbali unaokadiriwa kufikia 2,000,000 light years (miaka-mwanga millioni mbili). Hii ndiyo galaxy iliyo karibu sana na sisi, hakuna nyingine ambayo ni jirani na sisi kuzidi hii.

Hata hivyo, the entire universe ambayo ina millions of galaxies, inasemekana kwamba inatanuka kwa kiwango cha mara 300 trillion trillion kwa sekunde moja,..., jaribu ku-imagine hii scenerio, yaani possibly naweza kufananisha na kitu kilicho kidogo size ya mchanga kiwe kinatanuka na kuwa size ya tuseme, Tanzania nzima (mfano) kwa sekunde moja, halafu mtindo huo huo ndiyo uendelee kwa kutanuka namna hiyo kila umbile linalopatikana kila baada ya sekunde moja, you can imagine how incomprehensible the size of the universe is. Unaona maajabu haya ya ulimwengu huu tunaoishi? Who's behind all these mystical, miraculous and adventurous actions and creations? Are they really by coincidencial, randomly unorganised forces only? Really no thanks!

Ndugu yangu kusema ukweli mimi kuna kipindi nilikuwa naamini kuwa Mungu yupo, sasa hivi siamini tu ila pia nimeshahakikisha kwa evidence ambazo siwezi kuziprove kwa mtu mwingine, na hivyo nakusihi wewe uamini kuwa Mungu yupo and there is a day utahakikisha kama mimi nilivyohakikisha. You believe by hearing, you prove by seeing or experiencing. Kitu kikishakuwa knowledge maana yake kimeshadevelop beyond faith level!
 
Usijali mkuu nitajaribu kudadavua zaidi hii mada. Sote tuko hapa JF kujifunza.

1. super nova ni nini na zinalipuka mara ngapi ili sisi tupate hizo faida zake
Super nova inapolipuka hutengeneza black hole na vumbi linalobaki hujikusanya na kutengeneza sayari kama dunia yetu. Baada ya hizi sayari kutengenezwa basi zinapitia process ya evolution. Kama sayari ina vigezo vizuri kama dunia yetu (joto, maji, nk.) basi maisha yanaweza kuanza kwa hii njia ya evolution (from simple amino acids, to DNA, to one-celled organisms, to multi-celled creatures to humans, animals, fish, etc.)

2. tunaonaje ama kujuaje kwamba supernova imetokea
Nyota kubwa zinapokufa zinalipuka kama super nova. Hakuna anaejua lini super nova itatokea. Wataalam wa anga wameelekeza darubini zao angani na mara kwa mara wataona sehemu ambayo palikuwa na kanyota kadogo mara panatokea mwanga mkubwa sana. Hapa ndio wanajua super nova imetokea.

3. blackhole na usalama wa dunia vimekaajeo jua letu.
Usiiogope black hole. Hii ni center of gravity kama lilivyo jua letu. Sayari zetu zinalizunguuka jua na hatuogopi kuwa litatumeza. Hivyo hivyo, nyota zilizoko kwenye galaxy yetu (milkway) zinaizunguuka hiyo black hole na hazitamezwa. Vitu vinavyomezwa na black holes ni vile vinavyo sesereka na kuikaribia.

4. UFO's ni nini?
UFO ni kifupi cha Unidentified Flying Object au kitu kilichoko angani ambacho hakijulikani. Kuna dhana kuwa hivi ni vyombo vya viumbe vitokavyo kwenye sayari nyingine zaidi ya dunia yetu. Pia inaaminika kuwa serikali kama za marekani wamevikamata lakini wanafanya siri. Hii dhana siwezi kuithibitisha lakini kama ni kweli basi tujipange. Kuna watu waliotoa ushuhuda kuwa walitekwa na hivi viumbe vilivyokuja na hizi UFOs na kufanyiwa majaribio. Mimi sina sababu ya kutowaamini lakini bado hatujaona ushahidi (physical evidence).

Mara nyingi hizi UFO unakuta ni ndege za majaribio (kwa mfano marekani walipokuwa wanajaribu stealth jets. alieziona wakati huo asingejua ni kitu gani na angeziita UFO). Wakati mwengine ni matufe ya kupimia hali ya hewa (weather baloons).

Jibu zuri kwako ni kuwa hata mimi sijui UFO ni nini. Ni hati hati tu kama nilivyoainisha hapa.

Mkuu unajibu vizur sana, heshma yako
 
Ni kweli jua ndiyo nyota kubwa kuliko zote kwenye mfumo wetu wa jua (solar system) ambao una sayari 9 tu. Nyota unazoziona zinang'aa ziko mbali mno, wala haziko kwenye mfumo wetu huu wa kwetu, yaani ziko nje ya solar sytem. Jirani ya mfumo wetu, yaani jirani yetu aliye karibu sana na mfumo wetu wa jua (hayuko kwenye mfumo wetu) ni nyota inayoitwa alpha centauri, ambaye yuko umbali wa unaokadiriwa kuwa 4.4 light years kutoka hapa kwenye mfumo wetu wa jua, kwa maana kwamba umbali huo, ni umbali ambao ukiwa na ndege au chombo kingine chochote kile chenye uwezo wa kutembea kwa kasi ya km laki3 kwa sekunde moja (300,000km per second), au sawa na roundtrip zaidi ya 10 za kutoka Dar kwenda Mwanza (na kurudi), au zaidi ya 20 za Dar Mwanza, kwa sekunde moja tu, kinaweza kuchukua muda wa miaka 4.4 kufika kwa jirani yetu nyota ya alpha centauri ambaye ndiyo jirani aliye karibu zaidi na sisi. Mbali na hayo, jirani yetu kwenye galaxy yetu, yaani galaxy ambayo iko karibu sana na sisi kwenye universe inaitwa andromeda na iko umbali unaokadiriwa kufikia 2,000,000 light years (miaka-mwanga millioni mbili). Hii ndiyo galaxy iliyo karibu sana na sisi, hakuna nyingine ambayo ni jirani na sisi kuzidi hii. Hata hivyo, the entire universe ambayo ina millions of galaxies, inasemekana kwamba inatanuka kwa kiwango cha mara 300 trillion trillion kwa sekunde moja,..., jaribu ku-imagine hii scenerio, yaani possibly naweza kufananisha na kitu kilicho kidogo size ya mchanga kiwe kinatanuka na kuwa size ya tuseme, Tanzania nzima (mfano) kwa sekunde moja, halafu mtindo huo huo ndiyo uendelee kwa kutanuka namna hiyo kila umbile linalopatikana kila baada ya sekunde moja, you can imagine how incomprehensible the size of the universe is. Unaona maajabu haya ya ulimwengu huu tunaoishi? Who's behind all these mystical, miraculous and adventurous actions and creations? Are they really by coincidencial, randomly unorganised forces only? Really no thanks!
Ndugu yangu kusema ukweli mimi kuna kipindi nilikuwa naamini kuwa Mungu yupo, sasa hivi siamini tu ila pia nimeshahakikisha kwa evidence ambazo siwezi kuziprove kwa mtu mwingine, na hivyo nakusihi wewe uamini kuwa Mungu yupo and there is a day utahakikisha kama mimi nilivyohakikisha. You believe by hearing, you prove by seeing or experiencing. Kitu kikishakuwa knowledge maana yake kimeshadevelop beyond faith level!

Mkuu ulivyoanza umenikuna haswaa ila ulipofika kwenye swala la imani hahahaaa give me a break kidogo. Just tell us how did u come to raealise kuwa hakuna Mungu?
 
Ni kweli jua ndiyo nyota kubwa kuliko zote kwenye mfumo wetu wa jua (solar system) ambao una sayari 9 tu. Nyota unazoziona zinang'aa ziko mbali mno, wala haziko kwenye mfumo wetu huu wa kwetu, yaani ziko nje ya solar sytem. Jirani ya mfumo wetu, yaani jirani yetu aliye karibu sana na mfumo wetu wa jua (hayuko kwenye mfumo wetu) ni nyota inayoitwa alpha centauri, ambaye yuko umbali wa unaokadiriwa kuwa 4.4 light years kutoka hapa kwenye mfumo wetu wa jua, kwa maana kwamba umbali huo, ni umbali ambao ukiwa na ndege au chombo kingine chochote kile chenye uwezo wa kutembea kwa kasi ya km laki3 kwa sekunde moja (300,000km per second), au sawa na roundtrip zaidi ya 10 za kutoka Dar kwenda Mwanza (na kurudi), au zaidi ya 20 za Dar Mwanza, kwa sekunde moja tu, kinaweza kuchukua muda wa miaka 4.4 kufika kwa jirani yetu nyota ya alpha centauri ambaye ndiyo jirani aliye karibu zaidi na sisi. Mbali na hayo, jirani yetu kwenye galaxy yetu, yaani galaxy ambayo iko karibu sana na sisi kwenye universe inaitwa andromeda na iko umbali unaokadiriwa kufikia 2,000,000 light years (miaka-mwanga millioni mbili). Hii ndiyo galaxy iliyo karibu sana na sisi, hakuna nyingine ambayo ni jirani na sisi kuzidi hii. Hata hivyo, the entire universe ambayo ina millions of galaxies, inasemekana kwamba inatanuka kwa kiwango cha mara 300 trillion trillion kwa sekunde moja,..., jaribu ku-imagine hii scenerio, yaani possibly naweza kufananisha na kitu kilicho kidogo size ya mchanga kiwe kinatanuka na kuwa size ya tuseme, Tanzania nzima (mfano) kwa sekunde moja, halafu mtindo huo huo ndiyo uendelee kwa kutanuka namna hiyo kila umbile linalopatikana kila baada ya sekunde moja, you can imagine how incomprehensible the size of the universe is. Unaona maajabu haya ya ulimwengu huu tunaoishi? Who's behind all these mystical, miraculous and adventurous actions and creations? Are they really by coincidencial, randomly unorganised forces only? Really no thanks!
Ndugu yangu kusema ukweli mimi kuna kipindi nilikuwa naamini kuwa Mungu yupo, sasa hivi siamini tu ila pia nimeshahakikisha kwa evidence ambazo siwezi kuziprove kwa mtu mwingine, na hivyo nakusihi wewe uamini kuwa Mungu yupo and there is a day utahakikisha kama mimi nilivyohakikisha. You believe by hearing, you prove by seeing or experiencing. Kitu kikishakuwa knowledge maana yake kimeshadevelop beyond faith level!

km laki 3 kwa sekunde?? Duuh! Hivi hizi research nani alizifanya mpk kugundua viwango hivyo au ndo wanakisia tu?
then hapo kwenye Mungu mkuu Makanyaga sijakupata kabisaaa
 
Last edited by a moderator:
Thanks Mkuu Makanyaga. Umeeleweka vizuri sana. Hili la kuwa Mungu yupo halina mjadala isipokuwa kila mtu ana fikra zake. Atakae amini sawa na asiyekubali hiyari yake. Binadamu tumepewa akili ya kuchanganua mazuri na mabaya.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Usijali mkuu nitajaribu kudadavua zaidi hii mada. Sote tuko hapa JF kujifunza.

1. super nova ni nini na zinalipuka mara ngapi ili sisi tupate hizo faida zake
Super nova inapolipuka hutengeneza black hole na vumbi linalobaki hujikusanya na kutengeneza sayari kama dunia yetu. Baada ya hizi sayari kutengenezwa basi zinapitia process ya evolution. Kama sayari ina vigezo vizuri kama dunia yetu (joto, maji, nk.) basi maisha yanaweza kuanza kwa hii njia ya evolution (from simple amino acids, to DNA, to one-celled organisms, to multi-celled creatures to humans, animals, fish, etc.)

2. tunaonaje ama kujuaje kwamba supernova imetokea
Nyota kubwa zinapokufa zinalipuka kama super nova. Hakuna anaejua lini super nova itatokea. Wataalam wa anga wameelekeza darubini zao angani na mara kwa mara wataona sehemu ambayo palikuwa na kanyota kadogo mara panatokea mwanga mkubwa sana. Hapa ndio wanajua super nova imetokea.

3. blackhole na usalama wa dunia vimekaajeo jua letu.
Usiiogope black hole. Hii ni center of gravity kama lilivyo jua letu. Sayari zetu zinalizunguuka jua na hatuogopi kuwa litatumeza. Hivyo hivyo, nyota zilizoko kwenye galaxy yetu (milkway) zinaizunguuka hiyo black hole na hazitamezwa. Vitu vinavyomezwa na black holes ni vile vinavyo sesereka na kuikaribia.

4. UFO's ni nini?
UFO ni kifupi cha Unidentified Flying Object au kitu kilichoko angani ambacho hakijulikani. Kuna dhana kuwa hivi ni vyombo vya viumbe vitokavyo kwenye sayari nyingine zaidi ya dunia yetu. Pia inaaminika kuwa serikali kama za marekani wamevikamata lakini wanafanya siri. Hii dhana siwezi kuithibitisha lakini kama ni kweli basi tujipange. Kuna watu waliotoa ushuhuda kuwa walitekwa na hivi viumbe vilivyokuja na hizi UFOs na kufanyiwa majaribio. Mimi sina sababu ya kutowaamini lakini bado hatujaona ushahidi (physical evidence).

Mara nyingi hizi UFO unakuta ni ndege za majaribio (kwa mfano marekani walipokuwa wanajaribu stealth jets. alieziona wakati huo asingejua ni kitu gani na angeziita UFO). Wakati mwengine ni matufe ya kupimia hali ya hewa (weather baloons).

Jibu zuri kwako ni kuwa hata mimi sijui UFO ni nini. Ni hati hati tu kama nilivyoainisha hapa.

Yaani mkuu pamoja sana! kama ingekuwa shuleni tunafundishwa kwa namna hii interesting nisingepata division 4 hahah!!! 1. sasa mkuu hii dhana ya dunia kuwa duara inakuwaje? maji kupwa na kujaa kama dunia ingekuwa duara si maji yangekuwa yanapotea? hii ndio imekaaje?
2. ni kweli kuna jua lingine?
3. pamoja na idadi ya mito inayomwaga maji baharini kwa nini bahari haijai?
nasubiri darasa kwa sana mkuu
 
Yaani mkuu pamoja sana! kama ingekuwa shuleni tunafundishwa kwa namna hii interesting nisingepata division 4 hahah!!! 1. sasa mkuu hii dhana ya dunia kuwa duara inakuwaje? maji kupwa na kujaa kama dunia ingekuwa duara si maji yangekuwa yanapotea? hii ndio imekaaje?
2. ni kweli kuna jua lingine?
3. pamoja na idadi ya mito inayomwaga maji baharini kwa nini bahari haijai?
nasubiri darasa kwa sana mkuu

1. sasa mkuu hii dhana ya dunia kuwa duara inakuwaje?
Dunia ni duara. Sayari inapoanza kuumbika inaweza kuwa ndogo na sio duara. Lakini kadri vitu vingine (meteorites, commets, sayari nyingine) vinapojiunga (zinavutwa na gravity ya hii sayari inayoumbika) huu mgongano hufanya miamba inawaka na kuyeyuka kama uji. Katika hali hii gravity na mzunguuko wa hii sayari huifanya iwe duara. Baada ya miaka mingi kupita sehemu ya nje ya hii sayari hupoa na kuwa kama ardhi yetu lakini ndani bado miamba inakuwa kama uji. Mara kwa mara huu uji hujitokeza nje kama volkano. Mlima kilimanjaro ndivyo ulivyotengenezwa.

Maji kupwa na kujaa kama dunia ingekuwa duara si maji yangekuwa yanapotea? hii ndio imekaaje?
Kumbuka dunia ina mdogo wake aitwae mwezi. Huu mwezi una gravity yake. Maji baharini huvutwa na hii gravity ya mwezi. Upande mwezi ulipo ndiko maji yanapoelekea na maji kujaa wakati ule upande mwengine (ambako mwezi haupo) maji hupwa.

2. ni kweli kuna jua lingine?
Jua letu ni hili hili moja. Lakini kila nyota angani ni jua lengine bali majua hayo yako mbali sana.

3. pamoja na idadi ya mito inayomwaga maji baharini kwa nini bahari haijai?
Bahari haijai kwa sababu jua linafyonza (evaporation) maji na kuwa mawingu. Upepo unapeperusha haya mawingu kuelekea sehemu zenye misitu na milima. Huko yale maji katika mawingu yanageuka kuwa mvua. Mvua inajaza mito na kupeleka maji baharini na huu mzunguuko unajirudia. Hii ndio maana watu wanaambiwa wapande miti ili kuleta mvua.
 
Back
Top Bottom