Ufahamu kuhusu nyota za angani

Ufahamu kuhusu nyota za angani

Kwahiyo hakuna nyota zinazotembea ?

Nyota zinatembea. Kwa mfano jua letu linaizunguuka blackhole iliopo katikati ya galaxy yetu ya milkway. Lakini mzunguuko wa hizi nyota huwa taratibu sana na inachukua maelfu hata mamilioni ya miaka kuona badiliko lolote lile za nyota zilipo.

Vitu vinavyofanana na nyota angani ambavyo vinatembea kwa kasi tunayoweza kuiona ni sayari (zinabadilisha nafasi kwa masiku au miezi) na satellites (ambazo zina kasi kama ya ndege au zaidi).
 
Mie naomba unifahamishe kuhusu nyuklear,kiwanda cha nuec kinaweza chukua gharama tshs? Kukijenga?
 
nyota ni ndogo sana kuliko dunia, ni kama mwezi. zinategemea mwanga wa jua. na nyota ulizoona zinazobadilika kutoka rangi kutokea ya blue kwenda ya kijani ni kutokana na kuzibwa na miti na bahari .na ukiona nyekundu ujue hapo kuna radi na mvua inanyesha.

Hahahahàaaaaa usinichekeshe mkuu, are you serious?
 
Mkuu ulivyoanza umenikuna haswaa ila ulipofika kwenye swala la imani hahahaaa give me a break kidogo. Just tell us how did u come to raealise kuwa hakuna Mungu?

Labda umemwelewa vibaya mkuu kasema mungu yupo..lbd umesoma kwa haraka!
 
Mie naomba unifahamishe kuhusu nyuklear,kiwanda cha nuec kinaweza chukua gharama tshs? Kukijenga?

Sidhani wamiliki wa hii dunia (UN-Bodies) wataturuhusu kufanya hivyo. Angalia varangati linaloipata Iran.

Lakini kitaaluma tunaweza. Mchakato mzima ndio huu:


  • Tunachimba madini ya urani ambayo tunayo hapa bongo.

  • Tunachuja takataka na kupata yellow cake (uchafu wa kutupa ni hatari sana kiafya. Umewaathiri watu wengi Chad - fuatilia kwenye YouTube).

  • Yellow cake tunaiunguza na kupata hewa yake.

  • Hewa tunaiingiza kwenye centrifuges kupata urani nzuri (concentrate - 3.7%).

  • 3.7% ya urani tunaweza kuiingiza kwenye centrifuges nyingine tukafikia uzuri (concentrates) wa 20% (viwango hivi vya 3.7% mpaka 20% tunaweza kuvitumia kwa kuzalisha umeme.)

  • Ukitaka ubora wa kutengenezea bomu la nyuklia basi unapaswa uendelee kuboresha purity ya hii madini ya urani zaidi ya 20%.

Sidhani sisi wabongo tunataka kufanya hiki. Kwa hiyo hata gharama za kufanikisha kitu hiki hazina maana kwetu.
 
Pia,kuna uwezekano kila palipo na mfumo wa jua pana viumbe hai,mfano mfumo wetu wa jua ulio na sayari 8?


Hapana sio kweli. Lakini uwezekano huo ni mkubwa sana kutokana na uwingi wa majua.

Kama tunazungumzia viumbe hai kama sisi (carbon-based) basi tunahitaji hilo jua liwe na sayari kama dunia yetu na vikorombwezo vyote. Lakini sio lazima uhai uwe carbon-based. Kunaweza kuwa na uhai unaotumia madini nyingine kama silicon ambayo inaweza kuhimili joto kubwa zaidi ya tunalolihimili sisi binadam.

Ukweli ni kuwa kuna nyota (majua) nyingi sana kwenye galaxy yetu na galaxy nyingine. Kufikiria kuwa kwote huko hakuna uhai ila hapa kwetu tu ni kujidanganya.
 
Mkuu Kifyatu vipi kuhusu wanasayansi je huwa wanakwenda anga za mbali au hutumwa vyombo tu. Na nilisikia kujengwa kwa vituo vya utafiti wa anga huko kwenye sayari nyengine je ni kweli? Na vifaa na vyombo vinavyokuwa huko vinatumia power source ya aina gani?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kifyatu vipi kuhusu wanasayansi je huwa wanakwenda anga za mbali au hutumwa vyombo tu. Na nilisikia kujengwa kwa vituo vya utafiti wa anga huko kwenye sayari nyengine je ni kweli? Na vifaa na vyombo vinavyokuwa huko vinatumia power source ya aina gani?

Majibu ni kama yafuatayo:

Vipi kuhusu wanasayansi je huwa wanakwenda anga za mbali au hutumwa vyombo tu?
Kati ya hapa duniani na mwezi wetu binaadamu wamesafiri sana. Hata hivi sasa kuna wanasayansi kadhaa kwenye kituo cha utafiti angani (International Space Station) wakiendelea na tafiti zao. Kituo hiki siku zote kina watu. Huwa wanabadilishana tu mara kwa mara.

Nilisikia kujengwa kwa vituo vya utafiti wa anga huko kwenye sayari nyengine je ni kweli?
Ni kweli lakini kwa sasa hakuna kituo chenye binaadam. Nitakupa mifano michache ya vyombo vya tafiti vilivyokwenda kwenye sayari.

Mars: Safari za kwenda Mars zilianza tangu 1960. Nyingi zilipeleka vyombo kupitia tu au kuizunguuka. Sasa hivi kuna magari 2 (Rovers zilizotua 2003 na 2011) yaliotua na kuendelea na utafiti. Lengo ni kuona kama baadae wanaweza kujenga kituo cha kudumu ili watu waende.

Saturn: Mwaka 2004 chombo kiitwacho Cassini-Huygens kilifika Saturn. Cassini kinaizunguuka hii sayari hata leo. Mdogo wake Huygens kilitua kwenye mwezi mmoja wa Saturn uitwao TITAN na kuona kuwa unafanana sana na dunia yetu na kuwa una mito, maziwa na mvua. Lakini mvua hii sio ya maji bali ya Methane (methane ni hewa hapa kwetu lakini ni kama maji kule kwa ajili ya baridi kali)

Kuna vyombo vingi sana vilivyopelekwa angani. Vingine vinazunguuka sayari, vingine vinatoswa ndani ya sayari kuona kuna nini, na vingine vinaendelea tu kusafiri na kuna vinavyotoka sasa kwenye solar system yetu lakini bado vinawasiliana nasi.

Vifaa na vyombo vinavyokuwa huko vinatumia power source ya aina gani?
Vyombo vyote viendavyo angani hasa kama vimepangiwa kwenda masafa marefu vinatumia vyanzo viwili vya nishati.

  • Kwanza vinakuwa na solar panels kutengenezea umeme kutokana na mwanga wa jua.
  • Lakini chanzo cha muhimu sana kwa vyombo hivi ni nguvu za nyuklia. Hivi vyombo vinakuwa na nuclear reactors zinazotengeneza umeme na kuutumia moja kwa moja au kuuhifadhi kwenye batteries. Chanzo hiki cha nishati ni muhimu sana hasa ikifikia kuwa chombo kiko mbali sana na jua mpaka jua kuonekana kama nyota tu.
 
Jua ni miongoni mwa nyota inaonekana kubwa kwa vile iko karibu na sayari yetu dunia kila nyota ina sayari zake jua ina sayari tisa na mwezi mmoja lakini nyota hizi pia zipo ndani ya Galaxy mfano sisi tupo ndani ya milky way ndio nyota ya jua na nyota zingine zingine
 
Back
Top Bottom