Ufahamu wasifu wa Mwanasheria Mkuu mpya wa Serikali, Dkt. Adelardus Kilangi

Mkuu Petro E. Mselewa, huko ulikoipata hii biography hawajamtendea haki huyu Dr. A Dr (Professor), wanamuita Mr. Adelardus Kilangi!!!! Yaani wameanza Mr halafu huko ndani ndo wanaweka mataito ya ukweli. Tuheshimu shule za watu.......
 
Na akirudi mjengoni yule anayetibiwa kule nje, nadhani hapo ndo nafasi hiyo ya AG ndani ya mjengo, itampendeza zaidi...... Maana hata waliopita muziki waliucheza.
 
Omba wewe kazi utapewa maana unaonekana unawajua sana watu
nilishafanya kazi Attorney general mkuu, naijua hiyo ofisi, hata huyo jamaa namfahamu vizuri tu. hata hivyo namtakia yote mema, cha muhimu ni kusoma tu. kwenye masuala ya sheria, asikudanganye mtu, academicians huwa hawafanyi vizuri, ila wale waliopractice sheria iwe mahakamani au kwenye maofisi ndio huwa wanajua kwasababu wameshapitia matatizo mbalimbali katika utendaji na wanazijua hizo ofisi. that's why TULIA ATKSON hakufaa kabisa deputy attorney general baada ya kutolewa ulecturer udsm, huyo naye alikuwa st.augustin...you get the picture?
 
Wasukuma ni zamu yao kutesa
 
Huyu jamaa namfahamu kama mtu mwenye roho nzuri kutokana na jinsi alivyokuwa anaishi VIZURI na malecturer wenzake na wanafunzi wa sheria pale SAUT.

Sijashangaa yeye kupata nafasi hiyo maana wengi aliowasaidia walimuombea mema.
 
Si kweli kuwa aliondoka kwa sababu ya kugoma kuosha vyombo na wala darasa zima halikufukuzwa. Endapo darasa zima lilifukuzwa ilikuwaje classmate wake Mhashamu Flavian Kasala akabakia wakati walikuwa darasa moja huko Kipalapala? Nadhani ungefanya utafiti Kilangi aliingia lini Kipalapala na hayo yakuosha vyombo yalitokea lini! Kukuelimisha hili suala lilifanywa na mashemasi ndio walikuwa hawaoshi vyombo, kwa mujibu wa utaratibu. Lakini alipoingia gombera mpya aliamua kila mwanachuo aoshe vyombo, kupinga suala hilo mashemasi wote waligoma na kwa kuwa ni mashemasi walisimamishwa mwaka mzima 1993 na kisha kupadirishwa majimboni kwao. Kilangi ameondoka miaka mitatu baadaye 1996.
 
Imezoeleka kuwa ukiwa ndani ya ccm uelewa wako lazima some time uuweke pembeni ili ufuate matakwa ya chama katika harakati za kutekeleza ilani ya chama.

Tunayo mifano mingi ya wasomi na wenye upeo wa juu waliokuwa wajengaji wazuri wa hoja kwa wakati wao, lakini walipojumuishwa katika serikali ya ccm mpya ghafla walionekana kama hawana kitu kichwani na walidiriki kuyakana hata Yale waliyowahi kuyapigani kipindi cha nyuma! Hapa nawazungumzia watu kama akina Polepole, Kafulila, Machali na Kitila Mkumbo.

Sasa nije kwa Dr Kilagi ambaye alijipatia umaarufu siku za hivi karibuni kwa kuonesha kuijua sheria vizuri na kuitolea ufafanuzi bila kupepesa au kubase upande Fulani ili spate sifa kama wengine wafanyavyo.
Je baada ya kujumuishwa katika serikali ya ccm mpya atakuwa yuleyule tuliyemzoea aua atabadilika kama wengine?
 
Kifupi ukitaka kudumu kwenye uongozi wa awamu hii ukubali kuwa muongo na chizi! "Ndege wafananao huruka pamoja"
 
Hapa nawazungumzia watu kama akina Polepole, Kafulila, Machali na Kitila Mkumbo.
Umetumia kipimo gani kuonesha/thibitisha kuwa hao uliowataja wamepungukiwa kwenye mental competences zao?
 
Mtarban, wapi kuonesha weledi wa sheria? Tupe mifano
 
As if hujui mambo ya siasa hasa za kibongo , cc prof. LiPUMBA, Muhongo na wengineo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…