Ufugaji Mbuzi wa kienyeji (Asili) kibiashara

Ufugaji Mbuzi wa kienyeji (Asili) kibiashara

Nimepata eneo la kama heka 12 nataka kufuga mbuzi. Mpango ni kulizungushia uzio nipande nyasi na miti spesho kwa malisho ya mbuzi, so naomba mwenye ujuzi anielekeze nyasi na miti sahihi ya kupanda humo ili wawe wanajilisha. Ila naomba kujua Boar Goats madume kwa hapa Tz wanapatikana wapi na bei yao ili niwapandishe kwa majike ya kienyeji.
Kwanza naomba nikupongeze sana kw hilo la kuthubitu ktk ufugaji huu. Sasa naomba nikushauri kitu, kwanza kabisa kabla huja nunua Mbegu naomba ujitahidi upate nafasi upite kwenye masahmba ya wafugaji ambao tumeshaanza iliuweze kupata ABC za ufugaji wa Mbuzi. hii itakusaidia sana kuweza kujua hizo mbegu juu ya uangalizi wake na jinsi ya kuzihudumia kuanzia usafi,upandishaji matunzo baada ya kuzaa na jinsi ya kupishanisha baba asimpande mtoto au ndugu wasipandane.
Pia nakusahuri wakati wa kunua Mbegu usiagize ufike kwa wahusika ili uweze kuchaguwa na kuangalia kwa kina kile unachokihitaji hasa hapo umegusia kuhusu Boer kum cross na jike wa local hapo kuna mtihani wakujua ubora wa jike kwaajili ya kumjumlisha na hao madume wa kubwa. Nakushuri uingie ktk page Ya Mbogo Ranches' kuna semina wanaendesha kwaajili ya ufugaji itakusaidia sana. Kuhusu Mbegu nakushauri uwasiliane na Mbogo ranches, Mavuno ranches, ASAS Afrifarmtz hapo utapata hitaji lako bila shaka, cross wapo hata kwa wafugaji wenzako wapo nao pia ukihitaji unapata bila ya shaka.
Nakuombea kila la kheri ktk wazo lako Mungu akubariki sana na kukujaalia kila yaliyo mema ktk ufugaji huu. Karibu sana kwangu msaada wa kwanz akama upo Dar karibu Kibamba kwa Mangi ujie tujifunze pamoja na tufuge pamoja bure gharama yako ni nauli tu ya kufika ghapo, Barikiwa sana.
 
Hongera sana mkuu, hii ndio nataka kuifanya
Kwa pure Boer ni ghali ila wapo UG na tz wanacross wengi wao kwa hiyo utapata mix
Boer bei imechangamka na wapo Kalahari pia

Ukosikia mtu anauza bora uende mwenyewe kwa gharama zako hata kama ni maili 200 ukajionee mazingara yao
Muhimu zaidi certification zote maana kama Kenya na Uganda unaonyeshwa kila kitu waliponununuliwa mpaka makuzi yao na dawa wanazopewa nk
Uwe makini sana kuhusu majani yapo mengi hata kwenye insta wamejaa wafugaji na mbuzi pia utapata idea nyingi na humu pia wapo watu wema ila usiamini sana mpaka umeridhika na kila kitu
Kati ya sahauri bora sana hii, Mungu akubariki sana na mkuu ni vyema sana kuchukuwa tahadhari sana wakati wa kununua Mbegu. Na nijambo jema sana kumshauri yalio mema mfugaji mwenzetu.
 
Sio sana nina mpango pia wa kulirutubisha kwa mbolea japo pia nimeshauriwa kuwa katika hizi nyasi nazopaswa kupanda zipo zinazo rutubisha ardhi kiasili.
Ni kweli Nyasi zipo nyingi na kuna baadhi ya wafugaji wenzetu wanaagiza nnje mbegu za hizo nyasi na kunawale wataalamu wa shamba la malisho ya majani VIKUGE Kongowe wanatoa shauri mzuri na Mbegu za majani bila shaka kabisa.
 
Hawa ni F1 wa Boer na kienyeji na wanakuwa vyema sana kikubwa nacho wasisitiza wafugaji wote lazima kwenda shambani mwenyewe kuchagua na kujiridhisha. Huyu yupo kwangu kibamba. Mbarikiwe sana .
20240211_184058.jpg


Sent from my SM-N960W using JamiiForums mobile app
 
Kati ya sahauri bora sana hii, Mungu akubariki sana na mkuu ni vyema sana kuchukuwa tahadhari sana wakati wa kununua Mbegu. Na nijambo jema sana kumshauri yalio mema mfugaji mwenzetu.
Kweli kabisa mkuu
Ntakuja nikuone unipe mawili matatu pia
 
Nawaomba muingie kwenye page ya Mbogo ranches mtaona kunawengine walikwenda last week kwenye mafunzo kwa vitendo. Na utaratibu wameuonyesha humo jinsi ya kushiriki mbarikiwe sana.
Screenshot_20240212-131015_Instagram.jpg
Screenshot_20240212-130958_Instagram.jpg


Sent from my SM-N960W using JamiiForums mobile app
 
Kwanza naomba nikupongeze sana kw hilo la kuthubitu ktk ufugaji huu. Sasa naomba nikushauri kitu, kwanza kabisa kabla huja nunua Mbegu naomba ujitahidi upate nafasi upite kwenye masahmba ya wafugaji ambao tumeshaanza iliuweze kupata ABC za ufugaji wa Mbuzi. hii itakusaidia sana kuweza kujua hizo mbegu juu ya uangalizi wake na jinsi ya kuzihudumia kuanzia usafi,upandishaji matunzo baada ya kuzaa na jinsi ya kupishanisha baba asimpande mtoto au ndugu wasipandane.
Pia nakusahuri wakati wa kunua Mbegu usiagize ufike kwa wahusika ili uweze kuchaguwa na kuangalia kwa kina kile unachokihitaji hasa hapo umegusia kuhusu Boer kum cross na jike wa local hapo kuna mtihani wakujua ubora wa jike kwaajili ya kumjumlisha na hao madume wa kubwa. Nakushuri uingie ktk page Ya Mbogo Ranches' kuna semina wanaendesha kwaajili ya ufugaji itakusaidia sana. Kuhusu Mbegu nakushauri uwasiliane na Mbogo ranches, Mavuno ranches, ASAS Afrifarmtz hapo utapata hitaji lako bila shaka, cross wapo hata kwa wafugaji wenzako wapo nao pia ukihitaji unapata bila ya shaka.
Nakuombea kila la kheri ktk wazo lako Mungu akubariki sana na kukujaalia kila yaliyo mema ktk ufugaji huu. Karibu sana kwangu msaada wa kwanz akama upo Dar karibu Kibamba kwa Mangi ujie tujifunze pamoja na tufuge pamoja bure gharama yako ni nauli tu ya kufika ghapo, Barikiwa sana.
Ntatafuta muda nikutembelee Chief nami nijifunze mawili matatu.
 
habari za leo kusema ukweli hasa la wamangati ni changamoto kubwa sana maana hao jamaa bana wanambinu nyingi sana za uwizi na kununuwa viongozi wa vijiji kwamaana hata muwashtaki vipi hamna anae wagusa. wamasai sio waizi na ndio nawatumia mimi kwenye ufugaji shida yao ni kutaka kufuga kwa kieneyeji kama walivyo zoea kwao. Mimi wameshanifanya nikaliacha Shamba kongowe ya Mlandizi na mabanda yakaanguka ndani. Wamangati ni wabaya sana kuliko unavyo fikiria.

Pole sana mkuu,usifanye ufugaji karibu na jamii hizi ni wezi sana wa mifugo.
 
Nawasalimini kwa jina la Mungu nakuja tena na taarifa juu ya uletaji wa Mbuzi kutoka Namibia naomba mwenye kuhitaji awasiliane na MAVUNO RACHESE.0713 282 715/ 0713 54 44 11, tuta kuhudumia kwa kadiri ya uhitaji wako. mbegu tunazo leta. Boer majike/madume. Red kalahare Mjike/madume. Savannah Majike/Madume.
Karibuni sana Mbuzi hawa wote wanatoka Namibia ktk Mashamba ya wazalishaji wa Mbuzi.
 
Ndio maana nawa sisitiza kutembelea wafugaji wenzenu itatusaidia kujifunza zaidi ktk kukuza kipato na kufuga vyema. Hata Taliri pia wana toa Mbegu nzuri za Mbuzi, gogo white, blended na wengineo hao wana zalishwa na vituo vya serekali TALIRI.
Hawa TALIRI wapo wapi mkuu? Mimi ni mfugaji lakini nafuga hawa wa kienyeji.
 
..wafugaji wanasema beberu akipanda binti yake kutatokea kitu kinaitwa " inbreeding."

..nimeangalia kwenye mtandao madhara ya inbreeding ni kama yalivyoelezwa hapo chini.

The most obvious effects of inbreeding are poorer reproductive efficiency including higher mortality rates, lower growth rates and a higher frequency of hereditary abnormalities. This has been shown by numerous studies with cattle, horses, sheep, swine and laboratory animals.
Kuepusha jambo hili ni kuwa na madume mengi tofauti yatasaidia kuimarisha genes na hilo tatizo halitakuwepo.
 
..hebu tumuite MUBENDE atusaidie kama hii inaweza kuwa njia ya kusaidia kuepuka inbreeding.
Habari za leo ni kweli inawezekana kuwa na madume zaidi ya mmoja shambani mwako na pia unatakiwa uweze kuwatenganisha na majike ikiwezekana uwachunge tofauti tofauti na unachanganaya jike na dume pale unapo taka kuwapandisha. Pia unaweza kutumia njia ya kuwafunga kifaa maalumu cha kuwazuia madume kupandi hasa unapoona majike walio kwenye heat ni watoto wa huyo dume.
Na kikubwa lazima ujue mzunguko wa majike wako wanapandawa mwezi gani na unataka kuzalisha na dume gani, hapo sasa itategemea una majike wangapi na una madume wangapi.
 
Habari za leo ni kweli inawezekana kuwa na madume zaidi ya mmoja shambani mwako na pia unatakiwa uweze kuwatenganisha na majike ikiwezekana uwachunge tofauti tofauti na unachanganaya jike na dume pale unapo taka kuwapandisha. Pia unaweza kutumia njia ya kuwafunga kifaa maalumu cha kuwazuia madume kupandi hasa unapoona majike walio kwenye heat ni watoto wa huyo dume.
Na kikubwa lazima ujue mzunguko wa majike wako wanapandawa mwezi gani na unataka kuzalisha na dume gani, hapo sasa itategemea una majike wangapi na una madume wangapi.
naomba univumilie nieleze nilivyokuelewa.

1.unakuwa na madume wengi.

2.unawatenga madume hao na majike.

3. majike wakiwa kwenye heat unaachia dume mmoja ashughulike nao.

4. Ni lazima kujua kila mbuzi ktk zizi lako ametokana na beberu na jike yupi.

Cc Mzee Kijana
 
naomba univumilie nieleze nilivyokuelewa.

1.unakuwa na madume wengi.

2.unawatenga madume hao na majike.

3. majike wakiwa kwenye heat unaachia dume mmoja ashughulike nao.

4. Ni lazima kujua kila mbuzi ktk zoezi lako ametokana na beberu na jike yupi.

Cc Mzee Kijana
Mungu akubariki sana umeelewa vyema kabisa na pia kuna njia ya kutaka kuzalisha majike mf 20 au 30 kwa pamoja kwa Dume utakalo kuwa umelichaguwa toka ktk kundi la madume wako.
Unawachoma majike ulio wachaguwa sindano maalum ya kuavia mayai mara moja wanaingia kwenye jito basi unawakutanisha na Dume ulilolichagua, hapo utapata wanazaa kwa wakati mmoja baada ya hapo unajua hawa watoto ni wa Dume A kwahiyo nawapandisha kwa Dume c. Hii ni njia nzuri pia ya kitaalamu ila inahitaji maandalizi ya kutosha kwaajili ya wale watoto watakao zaliwa kwa kipindi kimoja. Barikiwa sana.
 
Mungu akubariki sana umeelewa vyema kabisa na pia kuna njia ya kutaka kuzalisha majike mf 20 au 30 kwa pamoja kwa Dume utakalo kuwa umelichaguwa toka ktk kundi la madume wako.
Unawachoma majike ulio wachaguwa sindano maalum ya kuavia mayai mara moja wanaingia kwenye jito basi unawakutanisha na Dume ulilolichagua, hapo utapata wanazaa kwa wakati mmoja baada ya hapo unajua hawa watoto ni wa Dume A kwahiyo nawapandisha kwa Dume c. Hii ni njia nzuri pia ya kitaalamu ila inahitaji maandalizi ya kutosha kwaajili ya wale watoto watakao zaliwa kwa kipindi kimoja. Barikiwa sana.
Dume mmoja kwa wakati mmoja? S atakua anakojoa upepo
 
Back
Top Bottom