Ufugaji nyuki wa kisasa

Asantee mkuu, japo umejibu kwa kuchelewa lakini ninasaidiwaje Mimi ninayetoka mkoani(Moro)?

Daima toa bila kukumbuka na Pokea bila kusahau
 
Asantee mkuu, japo umejibu kwa kuchelewa lakini ninasaidiwaje Mimi ninayetoka mkoani(Moro)?

Daima toa bila kukumbuka na Pokea bila kusahau
Pole sana kwa kuchelewa kujibu;

Mizinga yetu inakufikia hapo ulipo.
Aidha kama Tenda ni kubwa, tutaandaa vifaa vyote na kuja kuvionganishia hapo site kwako.

Kuna huduma ya Starter Kit kwa Wafugaji wapya;
Kwa huduma hii utalipia 3.5M.
Utapewa;
- Mizinga 10 ya kisasa iliyo na nyuki.
- Mavazi pair 2 yaliyo kamili kwanzia juu hadi chini.
- Vifaa vyote vya kulinia asali; brush, folk and hive tools.
- Bomba la moshi (Smoker)
- Tutakupatia Mtaalamu wa kuusimamia mradi wako kwa mwezi mmoja akikupatia mafunzo.
- Vifaa vya kuhifadhi asali
- Package za asali.

Na ushauri na saha.

Pia, tutakupatia soko la asali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asanteee sanaaa mkuu, basi Ni wajibu wangu Sasa kuwatafuta,. Natumai Mambo yakienda vizuri nitawatafuta mkuu
Daima toa bila kukumbuka na Pokea bila kusahau
 
Je unafahamu kuwa mdudu nyuki anaweza kukupatia mazao zaidi ya 7 kutoka kwenye Mzinga mmoja tu wa kibiashara?

Ndiyo, Shirika la kitaaluma linalojulikana kama "Penury Root-out Alliance - Tanzania" (www.pratanzania.org) limevimbua Mzinga Bora unaoitwa "PRA MODERN BEEHIVE".

Mzinga huu unakuwezesha kuvuna mazao kama;
1. Asali (Honey)
2. Chavua (Pollen)
3. Nta (Beeswax)
4. Gundi (Propolis)
5. Supu (Bee Soup)
6. Jeli ya Kifalme (Royal Jelly)
7. Sumu ya Nyuki (Bee Venom)



Sent using Jamii Forums mobile app
 

Attachments

  • IMG-20190113-WA0002.jpeg
    48.7 KB · Views: 145
  • 9b3a8b7e0426f854405344399bb241bf.jpeg
    36.2 KB · Views: 169
  • IMG-20190107-WA0008.jpeg
    116 KB · Views: 158
  • IMG-20190115-WA0024.jpeg
    67.7 KB · Views: 165
  • IMG-20190113-WA0013.jpeg
    102.1 KB · Views: 152
Naomba kuuliza yafuatayo

1. Unaweza kuelezea matumizi ya hizo bidhaa mfano chamvua? Na jelly

2. Naweza kutumia nyumba ambayo walikuwa wanaoshi watu kisha wakahama ikiwa ina madirisha yenye nondo tu na iko porini?

3.sehemu ya kufugia Nyuki ni lazima iwe na maua yanayoonekana au likiwa pori tu, tuna assume hapo maua yapo?

Kwenye chumba kimoja kama cha kuishi inaweza kuwekwa mizinga mingapi ya kisasa?


Asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante,

1. Matumizi ya Chavua na Jeli ya Kufalme ni mengi sana katika afya za binadamu, jama kinga na tiba ya magonjwa mengi sana. Mada hii nitaiongelea baadae.

2. Ni muhimu sana Kutambua aina ya miti na aina ya maua yanayopatikana eneo husika. Utatakiwa kujua Msimu wa hio miti kutoa maua ili kuhakikisha kwamba maua yanakuepo kwa muda wote au kipindi kirefu.
Tafafhali hudhuria Mafunzo ili kupata hii elimu.


3. Kuhusu idadi ya mizinga inayotosha kawika chumba, itategemea na mambo kadha wa kadha;
i. Aina ya nyuki
ii. Aina ya mazao ambayo unataka kuvuna

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nina nyuki shambani kwangu wako kwenye mti, nikisema niwaweke kwenye mizinga unadhani itanichukua mda gani kupata mizinga ya kutosha kuendesha mradi?

Hiyo mizinga ya PRA MODERN BEEHIVE hutoa lita ngapi za asali? na mzinga moja mnauza je?

Swali lingine; nyuki wakiingia kwenye mzinga inachukua miezi mingapi kupata asali?
 
Nataka nione shamba darasa lenu..lipo wapi?
Je makundi yenu ya nyuki yana ubora gani??maana kuna makundi ambayo ni hardwork hivyo kwa kipindi kifupi mzinga unakuwa umejaa,na je nnaweza pata malikia ambao ni wapole(russian bee queen type)?
kwa mwezi mnaweza zalisha malkia wangapi??
 

Nitajitahidi kuwepo kwenye mafunzo yatakayo fanyika Zanzibar mwezi ujao, japo mda unaonekana kuwa tatizo kwangu.

kabla ya kuhudhulia kwenye mafunzo ninahitaji kuamua kwanza kama nafanya mradi huu ama lah; ili kufanya uamuzi sahihi nahitaji uafafanuzi zaidi kutoka jibu lako namba moja.

Kwa uzoefu wako, unadhani ianweza kuchukua mda gani kwa kundi moja kujaza mizinga 10+ kama elimu ya kuzalisha na kugawa na kuhamisha imetumika? ukizingatika kuwa sehemu mradi utakapofanyika kuna maji ya kutosha na chakula (pembezon mwa mto ambapo panalimwa matikiti, migomba na mahindi N.k

Asante sana.
 
Ahsante kwa jibu zuri,
Mambo matatu ya muhimu;

1. Sisi tukikupatia Mzinga, tunakupatia na nyuki wake. Ilikuondoa tatizo la Ukosefu ma Makundi ya nyuki kwenye Mizinga iliyopo shambani.

2. Kuwepo na kila kitu shambani sio sababu tosha ya kasi ya ugawaji wa makundi, pamoja na mambo yote elimu itakusaidia kupata ujuzi ambao utakusaidia kufanya maamuzi.
- kundi moja linaweza kugawanywa na kutosha Mizinga Mipya mitatu, miwili au mmoja, hivyo hakuna kanuni Maalumu Bali ni kwa kutumia ujuzi.

3. Hata hivyo kwa kawaida nyuki wanaweza kutengeneza Malkia wapya kati ya 11 - 49. Na kila Malkia anatakiwa awe na kundi jipya la nyuki.

Tafadhali, ni muhimu kufika kwenda mafunzo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu , Asante kwa maelezo mazuri na yenye tija.Nina maswali machache;
1. Uhakika wa masoko wa bidhaa za nyuki upoje?
2. Ipi bidhaa ghali zaidi katika bidhaa za nyuki?
3.Kwa mtu ambaye hana eneo lake binafi mna mpango gani wa kumuwezesha ili awekeze hapo.Kwa mfano, tumeona kampuni nyingine zinatoa maeneo yao halafu wateja wanawekeza kwenye mradi kwa makubaliano maalum
4.Kwa mtu mwenye eneo lake ,je huwa mnafanya survey na kumshauri kama linafaa au halifai?? na kama halifai mnaweza mkalifanya lifae?
 
Ahsante sana.

Napenda kukutaarifa kuwa Shirika la PRA Tanzania ni wanunuzi wakubwa wa Mazao yote ya Nyuki.
Katika Mazao yote, Sumu ya nyuki ndilo zao lenye thamani ya juu sana.
Kwasasa tuna Miradi katika Mikoa kama Tanga, Singida, Arusha, Mara etc.

Kazi yetu kubwa ni kuhakikisha Watanzania wote wanapata elimu hii ili kuongeza kipatao

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Maswali mengine kutokamajibu namba 2 na 3

-- Garama zenu za mzing apamoja na Nyuki ni shilingi ngapi?
- Je inatumia mda gani kwa nyuki kuzalisha malkia 11 - 49 (wastani)

Asante.
 
Maswali mengine kutokamajibu namba 2 na 3

-- Garama zenu za mzing apamoja na Nyuki ni shilingi ngapi?
- Je inatumia mda gani kwa nyuki kuzalisha malkia 11 - 49 (wastani)

Asante.
Mizinga ipo ya bei tofauti tofauti, ukinunua Mizinga yetu nyuki tunatoa kama huduma.
Ila usiponunua Mizinga yetu, Tunauza Makundi ya Nyuki Tshs.30,000/=.

Mizinga ipo ya;
A. 75,000/=
B. 120,000/=
C. 150,000/=
D. 180,000/=
Tofauti ni idadi ya Mazao ambayo utavuna kwani kuna vifaa mbalimbali vinaongezeka ili kukuwezesha kuvuna hayo mazao.

Uzuri ni kwamba, Tunatengeneza Mizinga inayoingiliana. Yaani hata ukinunua Mzinga A, tunaweza kukuletea vifaa vya kuongezea ikawa B, au C na hadi kuwa D, ambao ni Mzinga kamili unaoweza kuvuna mazao yote 7 na kukuzalishia Malikia wengi kwa muda mfupi.

Malkia 11 - 49 wanazalishwa kwa hali ya kawaida (Naturally), ila kama ukitumia Tevhnolojia unaweza kuzalisha Malkia hata zaidi ya 300 kwa muda wa miezi 6 tu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Karibu RAFIKI ASALI ujipatie elimu ya ufugaji na kilimo Nyuki kutoka kwa wataalamu na wenye elimu ya sayansi na teknologia ya ufugaji Nyuki na mazao yake
Habari yako mkuu, nimevutiwa ma kichwa cha habari hapo nje, sasa nimeingia ndani ili nipate hiyo elimu kuhusiana na mzee nyuki na asali yake lakini nimeambua patupu sasa bado hijaiweka au mpaka tubadilishane namba za sim au tukutane pm?.
Naomba itendee haki heading ya uzi wako
Ni hayo tu mkuu.

Wasalaam.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Boss mi nina Mizinga kama 40 but nyuki wanasuasua kuingia niliwawekea nta lakini nimeambulia patupu nitumie njia gani waingie??
 
He ningependa kujua eneo lako la ufugaji. Sababu nta tunatumia kama kuwavuta nyuki lakini cha msingi ni sehemu ya ufugaji Nyuki. Labda kama utakua tayari tungepata muda wa kuonana na kukushauri nini cha kufanya.
 
Boss mi nina Mizinga kama 40 but nyuki wanasuasua kuingia niliwawekea nta lakini nimeambulia patupu nitumie njia gani waingie??
Bosi wangu nta tunatumia katika kuwavutia nyuki lakini ufugaji wa nyuki unahitajika kwanza kua na eneo ambalo ni sahihi la Ufugaji. Kama utahitaji tungeweza kuwasiliana ili niweze kutembelea eneo lako na kukushauri cha kufanya. 0758789957 kwa mawasiliano zaidi
 
Nimekuelewa xana mkuu ila kama nivyoandika katika Uzi wangu lakini ukitaka kujua mengi naomba tuwasiliane
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…