Ufugaji wa kisasa wa Nyuki: Faida, Utaalam na Masoko

Ufugaji wa kisasa wa Nyuki: Faida, Utaalam na Masoko

Ndugu,

Idadi ya mizinga inayoweza kukaa kwenye mti mmoja wa muembe mmoja hutegemea sana ukubwa wa mti husika. Ouput ya mazao ya nyuki haitegemei mti mmoja tu, nyuki wanauwezo wa kutembea zaidi ya kilometa tatu toka kwenye mzinga wao hivyo output ya mazao ya nyuki itategema sana plant density na bee fodder plants zilizopo kwenye eneo nyuki watakaloweza kwenda.

Swali kwako: Hiyo mzinga yako unategemea kuitundika muda wote wa ufugaji?

Kama utalenga ufugaji mkubwa, ningekushauri utundikaji wa mizinga kwenye miti ufanyike wakati wa kutega makundi tu. Na siku 45 baada ya kupata kundi la nyuki kwenye mzinga unashusha mzinga wako kwenye jukwaa. Njia hii ni nzuri na inarahisisha sana ukaguzi wa mzinga yako na itakupunguzia gharama za kuwa na watu wengi wa kupanda kwenye miti.

Tazama picha nilizoambatanisha hapa za mzinga iliyotundikwa na mfano wa mzinga iliyo kwenye jukwaa.
Kiukweli jamaa unajua sana
 
Sifa za eneo:-
1. Miti, uoto wowote wa asili na mimea mbalimbali kama mazao ya chakula na biashara (alizeti, mahindi etc)
2. Maji ni muhimu kwan hutumika kama sehemu ya chakula cha nyuki pia nyuki hutumia maji kurekebisha hali ya hewa ndan ya mzinga
3. Eneo la shamba la nyuki lazima liwe ni salama kwa mizinga, mazao yake, mifugo, binadamu na mahali kusiko na maadui wa nyuki. (Kuthibiti hayo yote kujengea nyumba ya nyuki ni njia nzuri na salama zaidi)
4. Kivuli cha kadri na kinga ya upepo ili kuwapunguzia nyuki kazi ya ubebaji maji kwaajili ya kupunguza joto.


Sent from my iPhone using JamiiForums

Mkuu asante kwa ufafanuzi, maji unayozungmzia hapa ni mto au hata kisima mtu unaweza tu kuchimba? Na je kama ni mto au kisima kiwe umbali gani toka kwenye mizinga? Mimi ninaeneo ninataka kufuga nyuki tatizo hamna maji jirani yapo kama meter 500 hivi toka shambani napo ni kisima kilichochimbwa na wachina wakati wa kutengeneza barabara. Natanguliza Shukrani kwa uzi huu mzuri
 
na unaposema mnanunua 1kg=7000 that means mnapima na je kama muuzaji kaleta kwny ndoo ya 20 lita kwa uzoefu wako hiyo itakuwa na kg.ngapi.pili kama mimi nina asali nimeshaivuna tayari mnaweza kununua asali yangu pia?asante
 
Kwa ufugaji wa kibiashara nashauri angalau mtu kuwa na mizinga kuanzia 50 kwenda mbele.

Hesabu yake:
1hive = 12kgs/harvest (Minimum)
Ndani ya mwaka 1 unaweza kuvuna mara 5, hivyo;

50 Hives = 600kgs

600Kgs * 5 harvest = 3000Kgs

Wholesale price:
1kg = 7000 Tshs
3000Kgs = Tshs 21,000,000/=

NB: Katika mahesabu hayo tumefanya katika range ya chini sana.

Bei ya mzinga mmoja ni Tshs 150,000/=


Sent from my iPhone using JamiiForums

Samahani mkuu.

Unaponunua huo mzinga unapata hiyo kit yote au unanunua separate?
 
Hi Patrick,

Kwanza pole kwa kuchelewa kujibu, natumaini bado sijachelewa kukupatia jibu.

Maji ya kisima ni sahihi na kwa umbali huo bado sio shida kwa nyuki kwani wana uwezo wa kufuata majia hata zaidi ya kilomita 3.

Karibu.
0753 196849
Mkuu asante kwa ufafanuzi, maji unayozungmzia hapa ni mto au hata kisima mtu unaweza tu kuchimba? Na je kama ni mto au kisima kiwe umbali gani toka kwenye mizinga? Mimi ninaeneo ninataka kufuga nyuki tatizo hamna maji jirani yapo kama meter 500 hivi toka shambani napo ni kisima kilichochimbwa na wachina wakati wa kutengeneza barabara. Natanguliza Shukrani kwa uzi huu mzuri
 
Kit yetu inaanzia mizinga 12 ambayo inajumuisha;

Mizinga 12
Machine ya kukamulia 1
Chujio 1
Practical training
Hive tool 1

Naomba tuwasiliane kwa namba 0753196849 kwa maelezo zaidi

Samahani mkuu.

Unaponunua huo mzinga unapata hiyo kit yote au unanunua separate?
 
Asali zipo za aina nyingi kutokana na maua husika nyuki waliyotumia kutengeneza asali na uzito hutofautiana. Ila ndoo ya lita ishirini inaweza fikia kg 35 hadi 40

Tuwasiliane kwa 0753196849 kwa maelezo zaidi.

na unaposema mnanunua 1kg=7000 that means mnapima na je kama muuzaji kaleta kwny ndoo ya 20 lita kwa uzoefu wako hiyo itakuwa na kg.ngapi.pili kama mimi nina asali nimeshaivuna tayari mnaweza kununua asali yangu pia?asante
 
Mnawezeshaje wajasiriamali wadogo wasio na mtaji?
Nina eneo zuri la kufuguia nyuki pia Nina mizinga michache ya kisasa na kienyeji
Je mnaweza kuniamini Kwa kunikopesha mizinga na vifaa huku nikilipa Kwa mavuno ninayopata??
 
Mnawezeshaje wajasiriamali wadogo wasio na mtaji?
Nina eneo zuri la kufuguia nyuki pia Nina mizinga michache ya kisasa na kienyeji
Je mnaweza kuniamini Kwa kunikopesha mizinga na vifaa huku nikilipa Kwa mavuno ninayopata??

Swali zuri sana mkuu mm sijaanza bado ila nipo kwenye eneo ambalo nyuki ni wengi mpaka kero ila tatizo mtaji
 
Hilo shamba darasa lenu la Dodoma lipo sehemu gani?? Mimi nipo Dodoma napenda kuja kujionea
 
Kit yetu inaanzia mizinga 12 ambayo inajumuisha;

Mizinga 12
Machine ya kukamulia 1
Chujio 1
Practical training
Hive tool 1

Naomba tuwasiliane kwa namba 0753196849 kwa maelezo zaidi

Gharama za hiyo Kit nzima ni kiasi gani?
 
Hilo shamba darasa lenu la Dodoma lipo sehemu gani?? Mimi nipo Dodoma napenda kuja kujionea

Msalato mnadani, ukifika ofisi tutakupatia maelekezo zaidi na kupata ratiba kamili. 0689 658811
 
Habari wakuu,mie ni mmoja wa wafuga nyuki,naombeni contact za Mrimba Rubi yule anafuga nyuki Dodoma na za msimamizi wa shamba la M P....na kama kuna shamba ambalo mtu anaweza tembea akajifunza..Asanteni.
 
Me nina Diploma ya ufugaji nyuki kutoka Beekeeping Training Institute-Tabora
Sim:0764 458 513
npo tayar kukusaidia
 
Habari wakuu,mie ni mmoja wa wafuga nyuki,naombeni contact za Mrimba Rubi yule anafuga nyuki Dodoma na za msimamizi wa shamba la M P....na kama kuna shamba ambalo mtu anaweza tembea akajifunza..Asanteni.

me nina diploma ya nyuki kutoka Beekeeping Training Institute-Tabora pia Mwaka jana nilijitolea kwa miez miwili katika shamba la PM.
Simu:0764 458 513
 
Back
Top Bottom