Ufugaji wa kuku chotara na kienyeji kwa mijini ni hasara tupu

Ufugaji wa kuku chotara na kienyeji kwa mijini ni hasara tupu

HEeeenHeeee. Inabidi kucheka tu, kwa mawazo kama haya.

Kwa hiyo unategemea faida kutokana na ufugaji wa kuku wa kienyeji hao 200, huku ukiwalisha pumba za mahindi, pumba za mchele laini na mtama katika hiyo miezi mingapi 6?

Nenda kawadanganye wasiojua kitu kuhusu ufugaji wa kuku.

Hizo pumba pekee utazipata wapi, na kwa bei gani unajua?

Umechanganua gharama za ufugaji huo, na mwisho wa siku ukaona unabaki na faida?

Kwanza, ni kuku gani wa kienyeji utamuuza katika miezi 6, na kwa kuwalisha lishe kama hiyo unayobainisha hapo?

Miezi sita kuku wa kienyeji hujapata yai la kutotolesha, wewe tayari unadai kuwazalisha?

Hiyo miti shamba, huko bustanini kwako inaota tuu, kienyeji, hahitaji kamwe gharama yoyote?
Tena nikwambie, usilogwe, ukadhani kuku wa kienyeji hadhuriki na magonjwa yanayowadhuru hao unaowaita "kuku wa maabara" Salmonella hachagui kuku wa maabara wala wa kienyeji, coryza inafyeka kila aina ya kuku, halafu unakuja hapa na kutalka kudanganya watu?

Kama wewe ni mfugaji wa kuku wa kienyeji, usidhani unayo nafuu yoyote kuhusu magonjwa yanayoangamiza kuku wengine wote.
Code:
Kama wewe ni mfugaji wa kuku wa kienyeji, usidhani unayo nafuu yoyote kuhusu magonjwa yanayoangamiza kuku wengine wote.
Narudia tena kusisitiza kuwa,kuku wa kienyeji ni kuku wa asili na ufugaji wake ubaki kuwa wa asili.Hayo magojwa unayo ya sema,kuku huyo wa kienyeji ujitibu mwenyewe kupitia majani anayotafuta na kula mwenyewe.Wewe dili na chanjo 2 nilizotaja.
Unasema mitishamba inakawia kukua,lakini uzingatii ni mitishamba ipi!!.Hivi muarovela unahitaji muda gani hadi uanze kutumika?,mpampai unahitaji muda gani hadi uanze kutumia majani yake?,Mtunguja (ntulantu),mpilipili kichaa,majani ya maboga,nayo yanahitaji muda mrefu kukua?

Kwani kipi uanza katika ufugaji kati ya kuandaa mazingira ya kufugia na kununua kuku hata uone kuwa mitishamba itakuwa bado kukua?
myonyo.jpg
images%2B%25289%2529.jpg
images%2B%25288%2529.jpg
download%2B%25288%2529.jpg
download%2B%25283%2529.jpg
 
Huyu hapa ni jogoo wa miezi 9,iliyotolewa mwaka jana mwezi 3 na ndiyo kwanza kaanza kuwika.Matemba aliozaliwa nao,wengi kwa sasa wanalea vifaranga.
Mkuu!Mimi nazungumza ninacho kifanya na siyo kusikia.
Mtetea uanza kutaga kati ya miezi 6-7 na wakati huo jogoo uanza kujifunza kuwika.View attachment 2474523View attachment 2474526
Siyo peke yako unayefuga.

Unapoleta taarifa za upotoshaji hapa kuvuruga mipango ya wasiojua utaambiwa ukweli bila kufichwa.

Kuku wa kienyeji, miezi sita hatagi yai hata moja, huo ni uongo unaousema hapa bila aibu.

Sasa umetafuta huyo kuku na kumweka hapa, hiyo kweli ndiyo sampuli wakilishi wa kuku wengi wa kienyeji hapa Tanzania?

Sasa nikuulize, nieleze aina ya 'strain' ya huyo kuku ni ipi, au hata hujibidishi kujua, wewe unafuga tu?

Mara unazungumzia "kuku wa maabara" bila hata kujua unamaanisha kitu gani! Una hakika huyu kuku siyo wa "maabara"?
 
Code:
Kama wewe ni mfugaji wa kuku wa kienyeji, usidhani unayo nafuu yoyote kuhusu magonjwa yanayoangamiza kuku wengine wote.
Narudia tena kusisitiza kuwa,kuku wa kienyeji ni kuku wa asili na ufugaji wake ubaki kuwa wa asili.Hayo magojwa unayo ya sema,kuku huyo wa kienyeji ujitibu mwenyewe kupitia majani anayotafuta na kula mwenyewe.Wewe dili na chanjo 2 nilizotaja.
Unasema mitishamba inakawia kukua,lakini uzingatii ni mitishamba ipi!!.Hivi muarovela unahitaji muda gani hadi uanze kutumika?,mpampai unahitaji muda gani hadi uanze kutumia majani yake?,Mtunguja (ntulantu),mpilipili kichaa,majani ya maboga,nayo yanahitaji muda mrefu kukua?

Kwani kipi uanza katika ufugaji kati ya kuandaa mazingira ya kufugia na kununua kuku hata uone kuwa mitishamba itakuwa bado kukua?View attachment 2474575View attachment 2474576View attachment 2474577View attachment 2474578View attachment 2474579
Wewe bwana usihadae watu na habari za kipotoshaji namna hii.

Hii ni sawa na "dawa za miti shamba" tu wanazotumia binaadam, sasa kwa maisha ya siku hizi huwezi kumwambia mtu yeyote wa kawaida ategemee miti shamba tu kwa magonjwa yanayowasumbua binaadam siku hizi.

Naona katika majani yako hukuweka 'Aloe vera', au umesahau?

Sasa niambie, ni wapi Tanzania hii huko vijijini unapokuta wafugaji wa kuku wa kienyeji wakiwa na bustani za namna hiyo ili kuku wao wajihudumie kila wanaposhambuliwa na magonjwa!

Acha kupotosha watu, hili ndilo ninalokusisitizia hapa.
 
Nimeanza kula broiler,, lakini hazina radha kabisa, ni kama unakula karatasi tu, nimeamua mwezi ujao, nirudi tu kwenye beef,,
Yaani kuku wa kisasa, hawana radha, kabisa🤷🏼‍♀️
 
Nimeanza kula broiler,, lakini hazina radha kabisa, ni kama unakula karatasi tu, nimeamua mwezi ujao, nirudi tu kwenye beef,,
Yaani kuku wa kisasa, hawana radha, kabisa🤷🏼‍♀️
Hujajua mapishi yake.

Pamoja na kwamba hawana ile radha aliyonayo kuku wa kienyeji, lakini akitengenezwa huwezi kuachana naye tena.
Kuna njia mbalimbali za kuwapika hao kuku.

Wewe umechemsha tu basi au?
Jaribu na mapishi ya KFC (Kentucky Fried Chicken) na wengine wanaotengeneza 'fast Food', hutaacha tena kuwala hao kuku.

Hata kwa kuchemsha tu, kuna njia nzuri za kufanya hivyo. Usiwapike wawe tepetepe.
 
Hujajua mapishi yake.

Pamoja na kwamba hawana ile radha aliyonayo kuku wa kienyeji, lakini akitengenezwa huwezi kuachana naye tena.
Kuna njia mbalimbali za kuwapika hao kuku.

Wewe umechemsha tu basi au?
Jaribu na mapishi ya KFC (Kentucky Fried Chicken) na wengine wanaotengeneza 'fast Food', hutaacha tena kuwala hao kuku.

Hata kwa kuchemsha tu, kuna njia nzuri za kufanya hivyo. Usiwapike wawe tepetepe.
😂,Ngoja ntajaribu, maana huu mwaka natafuta kitambi cha kuombea mikopo bank,, napanga kula sana nyana nyama🤷🏼‍♀️
 
😂,Ngoja ntajaribu, maana huu mwaka natafuta kitambi cha kuombea mikopo bank,, napanga kula sana nyana nyama🤷🏼‍♀️
Dah!

Sasa unaanza na yai, au kuku mwenyewe!

Maana hicho kitambi hadi ukipate utakuwa umetumia kitita kwelikweli kwa hayo manyamanyama utakayokula, ambayo bei yake siyo mchezo.

Uje upate kitambi, hadi hapo unakwenda "kuomba mkopo bank", utaambiwa huna dhamana ya kutosha kukopeshwa!
 
Wewe bwana usihadae watu na habari za kipotoshaji namna hii.

Hii ni sawa na "dawa za miti shamba" tu wanazotumia binaadam, sasa kwa maisha ya siku hizi huwezi kumwambia mtu yeyote wa kawaida ategemee miti shamba tu kwa magonjwa yanayowasumbua binaadam siku hizi.

Naona katika majani yako hukuweka 'Aloe vera', au umesahau?

Sasa niambie, ni wapi Tanzania hii huko vijijini unapokuta wafugaji wa kuku wa kienyeji wakiwa na bustani za namna hiyo ili kuku wao wajihudumie kila wanaposhambuliwa na magonjwa!

Acha kupotosha watu, hili ndilo ninalokusisitizia hapa.
Kijijini wao uamini katika kilimo na ufugaji wa ngombe kibiashara.Kuku kwao hawaoni kuwa ni kitu cha biashara kinachoweza wakwamua.Tunao fuga kibiashara huko vijijini ni sisi watu wa mjini.Kumbuka unapoanza uwekezaji huu,lazima uweke pesa siyo chini ya m2-5,maana ni lazima uweke fensi ya waya kulizunguka shamba lako.
 
Siyo peke yako unayefuga.

Unapoleta taarifa za upotoshaji hapa kuvuruga mipango ya wasiojua utaambiwa ukweli bila kufichwa.

Kuku wa kienyeji, miezi sita hatagi yai hata moja, huo ni uongo unaousema hapa bila aibu.

Sasa umetafuta huyo kuku na kumweka hapa, hiyo kweli ndiyo sampuli wakilishi wa kuku wengi wa kienyeji hapa Tanzania?

Sasa nikuulize, nieleze aina ya 'strain' ya huyo kuku ni ipi, au hata hujibidishi kujua, wewe unafuga tu?

Mara unazungumzia "kuku wa maabara" bila hata kujua unamaanisha kitu gani! Una hakika huyu kuku siyo wa "maabara"?
Nasisitiza!Wewe siyo mfugaji bali ni miongoni mwa watu mnaoishi ndani ya yale mlipandikizwa vichwani huko mashuleni ili hali hampo katika ufugaji.Huyo jogoo ni jogoo asilia kabisa na wanapatikana kwa wingi sana maeneo ya Kaliua,Sikonge,Mpanda n.k.
Kwa pale Kaliua,kuku hao unawapata kwenye mabanda tu ya kuuzia kuku hapo sokoni.
Mkuu!Nimeingia katika ufugaji tangu 2013 mpaka leo nafanya.
Hayo mambo yenu ya kukaririshwa darasani,huwezi niletea mimi nikakuelewa.
 
Kijijini wao uamini katika kilimo na ufugaji wa ngombe kibiashara.Kuku kwao hawaoni kuwa ni kitu cha biashara kinachoweza wakwamua.Tunao fuga kibiashara huko vijijini ni sisi watu wa mjini.Kumbuka unapoanza uwekezaji huu,lazima uweke pesa siyo chini ya m2-5,maana ni lazima uweke fensi ya waya kulizunguka shamba lako.
Haya.
Sasa rejea kwenye msingi wa mada hii, toka mwanzo.
Ukishaamua kuwa mfugaji wa hao kuku wa kienyeji kibiashara, na ukawekeza kama ulivyoeleza hapa, mafensi na takataka zingine; hao kuku 78 waliotajwa kwenye mada hii hata ufanye uchawi wa namna gani hawatakuingizia faida yoyote katika kazi hiyo.
Hiyo itakuwa ni biashara kichaa.

Kwa hiyo, baada ya mizungushano yooote, tokea huko mwanzo, hatimaye sasa hapa mwisho tumekubaliana kwamba ufugaji wa kuku wa kienyeji, katika soko letu hili la sasa, na katika mazingira tuliyonayo, ni kazi ngumu sana ya kukuingizia faida na kuwategemea kuku hao kuwa chanzo cha pato.

Kumbuka, sisemi kamwe kwamba huwezi kuwa mfugaji wa kuku hao halafu usipate faida. Lakini itabidi uwe ni mfugaji mkubwa kweli kweli, pengine hupungui kuku 5,000 au 10,000 kwa mpigo, ili uwe unapata faida ya ufugaji huo.

Vinginevyo, unaweza kufanya kazi ya kuuza hao kuku, lakini siyo mfugaji. Wewe kazi yako ikawa ni kukusanya tu hao kuku toka huko vijijini na kwenda kuwauza mjini kwa faida.

Hao wanaokuuzia wewe, (wafugaji wadogowadogo) wao hawaingizi faida, na wala hawajui kabisa gharama za ufugaji wao ni kiasi gani, kwa sababu hawaweki kumbukumbu.

Nadhani hadi hapa tutakuwa tumeelewana vizuri sasa.

Lengo ni lipi hasa?
Kutowapotosha vijana kuona kwamba kazi ya ufugaji wa kuku wa kienyeji ni rahisi, na ndiyo njia nyepesi ya kuwapa riziki haraka haraka.

Tusiwapotoshe, tuwape ukweli kamili ili waupime wao wenyewe na kufanya maamuzi wanayoona yanafaa.
 
Nasisitiza!Wewe siyo mfugaji bali ni miongoni mwa watu mnaoishi ndani ya yale mlipandikizwa vichwani huko mashuleni ili hali hampo katika ufugaji.Huyo jogoo ni jogoo asilia kabisa na wanapatikana kwa wingi sana maeneo ya Kaliua,Sikonge,Mpanda n.k.
Kwa pale Kaliua,kuku hao unawapata kwenye mabanda tu ya kuuzia kuku hapo sokoni.
Mkuu!Nimeingia katika ufugaji tangu 2013 mpaka leo nafanya.
Hayo mambo yenu ya kukaririshwa darasani,huwezi niletea mimi nikakuelewa.
Kwa hiyo kwa kuonyesha picha ya huyo jogoo (kuchi), ndiyo unataka tukutambue wewe kuwa ni mfugaji wa kuku wa kienyeji, na kwamba unajua njia zote za kuwafuga hao kuku kwa faida?

Sijaona ushahidi wowote katika maandishi yako hapa kwamba unao ufahamu mzuri wa ufugaji.

Ninachoona hapa ni habari za upotoshaji tu, kuwahadaa wasioijua kazi hii waone kwamba unauelewa na kazi hiyo, hata bila ya kuonyesha ushahidi halisi wa mafanikio yako.

Kama umeanza ufugaji 2013, tueleze sasa hivi wewe unao kuku wangapi hapo shambani kwako; na je, ni kazi hiyo hiyo unayoitegemea kukuingizia pato au kuna kazi ya ziada unayofanya kuchangia pato lako?

Kama wewe ni mfugaji tokea 2013, na bado huamini kamwe kwamba kuku wa kienyeji anadhurika na magonjwa yanayowadhuru kuku wengine wowote, na kwamba tegemeo lako pekee ni miti shamba..., ufugaji wako unayo kasoro kubwa. Siku utakayoingiliwa na gonjwa mlipuko na kufyeka kuku wako wote, hapo ndipo utakapotambua kuwa kweli bado kazi hiyo huijui.
 
Nasisitiza!Wewe siyo mfugaji bali ni miongoni mwa watu mnaoishi ndani ya yale mlipandikizwa vichwani huko mashuleni ili hali hampo katika ufugaji.Huyo jogoo ni jogoo asilia kabisa na wanapatikana kwa wingi sana maeneo ya Kaliua,Sikonge,Mpanda n.k.
Kwa pale Kaliua,kuku hao unawapata kwenye mabanda tu ya kuuzia kuku hapo sokoni.
Mkuu!Nimeingia katika ufugaji tangu 2013 mpaka leo nafanya.
Hayo mambo yenu ya kukaririshwa darasani,huwezi niletea mimi nikakuelewa.
Unaposema "kuku asilia" hata hujui hao kuku aina ya kuchi wametokea wapi, hadi wakafika hapa Tanzania.

Pole yako.
 
Nimefatilia Uzi vizuri sana. Binafsi nipo mjini kabisa Tena temeke.ninao kuku wa kienyeji matetea 78,kuchi jogoo wadogo 8,jogoo wakawaida wakubwa7.huu mradi unanisogeza sana kiuchumi..naiona faida kwani mradi unajiendesha wenyewe kupitia kuuza mayai.mimi nauza mayai trei 12500.na kwa Kila Trey nasave7000 as profit.iliyobaki ni vyakula dawa na kurepea Banda.kuna namba ya kusave gharama ntawaeleza
Mkuu hongera.
kwa siku unakusanya mayai mangapi kwa hao tetea? Nipo dsm nina lengo la kufuga kienyeji kwa lengo la kuuza mayai,naomba mbinu za kupunguza gharama za uzalishaji na issue za chanjo na madawa ya kienyeji kama huwa unatumia..maana chanjo na madawa ya kununua dukani yanaongeza sana gharama
 
Kuchi ni aina ya kuku wa kienyeji wako sana huko anako taja mdau binafisi nimewala sana Urambo, kuna utapeli sana kwenye wale kuku
Kuwepo sana huko alikotaja, haina maana hiyo ndiyo asili ya kuku hao.

Nadhani huelewi maana ya neno 'asili'.

Hao kuku asili yao si hapa. Wameletwa toka nje miaka michache tu iliyopita. Hawakuwepo hapa nchini..

Ndiyo, wanafugwa kama kuku wa kienyeji, lakini hilo halina maana asili yao ni hapa nchini, au Afrika.
 
Unaposema "kuku asilia" hata hujui hao kuku aina ya kuchi wametokea wapi, hadi wakafika hapa Tanzania.

Pole yako.
Endelea kukariri hivyo hiyvo mkuu.Lakini ukijiuliza swali hili ndiyo utajua nini nasema.Kama kuku huyo ni kuku kutoka nje,je,alifikishwa lini katika mikoa ya Tabora,Mpanda na Singida?.Unaijua station ihitwayo Saranda?Kawaulize wazee wako hao wa huko mikoa ya pwani nini walikuwa wanashangaa katika nyama ya kuku hapo Saranda miaka ya 70 huko!.
 
Kuwepo sana huko alikotaja, haina maana hiyo ndiyo asili ya kuku hao.

Nadhani huelewi maana ya neno 'asili'.

Hao kuku asili yao si hapa. Wameletwa toka nje miaka michache tu iliyopita. Hawakuwepo hapa nchini..

Ndiyo, wanafugwa kama kuku wa kienyeji, lakini hilo halina maana asili yao ni hapa nchini, au Afrika.
Kaka!Hilo jina la kuchi ndiyo jina labda geni lakini kuku hao wamekuwepo miaka mingi tu.
 
Kuchi ni aina ya kuku wa kienyeji wako sana huko anako taja mdau binafisi nimewala sana Urambo, kuna utapeli sana kwenye wale kuku
Miaka ya 80 huko sisi tunakua,watu wa mikoa ya pwani walikuwa wanaogopa kula nyama za kuku hapo Saranda station kwa madai eti zile siyo nyama za kuku kwa kuwa eti ni kubwa na ndefu![emoji23][emoji3][emoji23]Wakifikiri eti ni nyama za ndege wakubwa wasiowajua wao na kumbe ndiyo hawa kuku ambao leo wanahitwa kuchi eti!.[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Endelea kukariri hivyo hiyvo mkuu.Lakini ukijiuliza swali hili ndiyo utajua nini nasema.Kama kuku huyo ni kuku kutoka nje,je,alifikishwa lini katika mikoa ya Tabora,Mpanda na Singida?.Unaijua station ihitwayo Saranda?Kawaulize wazee wako hao wa huko mikoa ya pwani nini walikuwa wanashangaa katika nyama ya kuku hapo Saranda miaka ya 70 huko!.
EEeeenHeeeee!

Sasa umebaki kuhololoja tu, huna hoja tena!

Sasa hapa unataka wasomaji wa mada hii waelewe kitu gani?

Hujaeleza hao kuku asili yao hasa ni wapi! Kwa sababu hujui.
 
Back
Top Bottom