Je uko field au unafugia kwenye not book..ama ndio wale wa business plan..Ila ungekuwa unapajua kilwa kivinje ningekuunganisha na jamaa flani anafanya biashara ya brawn's na kukodi maboti ili umsikie.mana tuponaye tokea alifu kwa ujiti...alianza kwa hasara ndani ya miaka mnne akauza heka heka nne za ninazo singino kwa ajili ya madeni..familia ikaja juu wengine wakasema kalogwa.wakaanza kumsomea na kuuogesha kombe kwa nguvu..Ila Leo pita tu kilwa uulize kayuyu ni nani alafu ulete habari zako na nadharia hapa..wewe hujawahi kufanya biashara wewe..na pia uliza tu mabasi ya Masha Allah historian yake...Yani vijana wengi wameenda shule kukariri miterminologies ya kuzungu lakini kichwani weupe tu.elimu halusi ni elimu yetu ya mazingira ambao Kuna mbuzi inaniita Mimi mvuta bange bila hata kujua hata hiyo bange ni Nini..
Ngoja nikusahihishe makosa yako, ikionyesha kwamba kisomo kiko chini kabisa; na kwa maana hiyo uelewa wa mambo unakuwa mgumu kwako.
1. "not book"
2. "flani"
3. "brawns"
4. "mana"
5. "alifu kwa ujiti"
6. "mnne"
7. "heka hekanne za ninazo singino"
8. "wakasema kalogwa wakaanza kumsomea nakuuogesha kombe kwa nguvu."
9. "historian yake"
10. kukariri miterminologies ya kuzungu"
Kwa hali ya kawaida, isingenilazimu niorodheshe haya hapo juu, kwa sababu najua huu ni mtandao wa JF, unakusanya kila takataka mtu anayoweza kuifikiria.
Maana yangu ya kuyaweka makosa yako hayo hapo juu katika andiko fupi tu lenye mistari pungufu ya kumi, ni kuonyesha uwezo wako halisi ulionao katika kufafanua na kueleza mambo, kuwa ni mfinyu sana.
Mtu mwenye hali ya aina hiyo, hana uwezo wa yale anayojigamba kuwa anauwezo nayo.
Kwa mfano: umekwishadai hapa hapa kwenye mada hii, kwamba wewe ni bingwa sana katika eneo la ufugaji kiasi kwamba umeweza hata kushiriki kwenye tafiti za kuzalisha kuku, na kutengeneza chanjo za asili za kuku!
Kutokana na uandishiwako tu, inaonyesha wazi wewe ni tapeli tu, tena asiye na uwezo hata wa kushawishi hao anaotafuta kuwatapeli.
Nilipoanadika mara ya kwanza kuhusu "uvutaji bangi", sababu kubwa ilihusiana na kusoma unayoandika humu. Mtu wa akili za kawaida haandiki na kujieleza jinsi unavyofanya wewe.
Sasa basi, kama wewe siyo mvuta bangi, basi utakuwa na kasoro ya kipekee katika akili zako.
Kuhusu ufugaji wa kuku, kazi hiyo huiwezi. Pengine nikupe ushauri wa sehemu nyingine unakoweza kwenda kuuza maneno ya hadaa kwa wasomaji watakaopenda kusikia hekaya zako. Jaribu sasa kilimo cha matikiti. Nenda kawaeleze wasomaji jinsi ulivyokwisha fanikiwa katika kilimo hicho.
Nilishafunga mjadala huu nawe, lakini ninajikuta bado nipo hapa nawe. Sasa ninaufunga rasmi. Sina la ziada ninaloweza kukusaidia juu yake.