We hapo umeshatobozea, jitahidi dawa tu, mimi niliwahi kufuga kuku wakafika 57, nikajisahau kuendeleza dawa, kilicho nikuta kila siku nikawa nakula kuku tatu hadi nne nanyingine kutupa, toka hapo hadi leo sijajipanga kufuga ingawa moyo ninao,pia kama una alovela wapatie uwezavyo ila isichukue zaidi ya siku nne mwaga na weka tena, pia otc ya unga inasaidia, pia dawa ya viroboto hakikisha viroboto haviwapati, safisha banda kila siku, hapo watasema unadawa, pamoja mkuu
Aisee hembu niambine mwenzenu mbumbumbu.
Hivi Kuku wa Kienyeji kwa Kiingereza wanaitwaje?
Na hawa Juju wengine(maana hata jina lao sijui niwekeje)wanaitwaje?
Sasa akili yangu inaniambia
-Kuku wa Kienyeji wanaitwa LOCAL CHICKEN
-Sasa hawa wengine(tumezoea kuita wakizungu)inakuwaje,maana FOREIGN CHICKEN mhhh,hapa huwa nacheka mwenyewe
Hembu mtujuze wataalam
Usituletee mambo ya jukwa la mapenzi na facebook huku tafadhali. huku ni serious brains tu.
Vipi mayai ya kienyeji ya kula tu huitaji??Habari wafugaji!
Naitaji mayai ya kuku wa kienyeji kwa ajiri ya kutotolesha nipo dsm,naitaji tray 10.
Kama unayo ni pm tufanye biashara.
Wakuu tujuzane
Nimeona wafugaji wengi wa Ng`ombe wanafanikiwa saana wakiwa karibu na Madktari wa Mifugo hiyo na changamoto kuwa ndogo kwao.Hasa pale wanapokuwa katika hatua za Mwanzo.Kipindi cha mpito kama miaka miwili hivi.Then muda unavyokwenda Mfugaji anakuwa anaongeza uwezo na kupunguza kumuita Dokta kira mara.
Sasa hembi nijuzeni kwenye ufugaji wa Kuku.
Ningependa kujua wapi Unaweza kupata Dokta/mtaalam wa Upande wa Ufugaji wa Kuku,na je mfano kama je inawezekana kuingianae mkataba wa kumlipa kwa mwezi Mshahara na allowance ya mafuta ili kila wiki kwa uchache awe anakuja site.
Kwa wazoefu inawezaku cost kiasi gani?
Maana mie kwa muono wangu,naona hii ndio move nzuri kwangu kuanza nayo.Ili nikianza nianze kwa mfumo wa kuwa karibu sana na Mtaalam.Maana expection ni kuanza na Kuku 4000 wa kienyeji kwenye free grazing kwenye hekari zangu kama 15 hivi.Kwa Kutenga groups in each Acre
Wadau naomba mchanganuo hapo na njia nyepesi,Manual readings ninazo nyingi ila kuwa na trainer on site ni bora zaidi pia
Kifaranga wangu mmoja wa wiki 3 alitoka njee ya uzio akaenda kuzurura, nliporudi jion nkamrudisha ndani. Kesho yake narudi jion tena namkuta anasinzia then akafa the next day. Sasa naona wale wengine aliokua nao banda moja nao wameenza kusinzia, no vidonda wala mafua. Ni ugonjwa gani huu.