Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Ufugaji wa Kuku wa Kisasa: Fahamu Mbinu, Faida, Changamoto na Masoko

Digna thanks kwa ushauri wako. nimeenda kwa mtaalamu mmoja kanipa antibiotic Tylosin 75% ndo nawapa pamoja na Oligovit.

Thanks a lot kwa ushauri wa kuwasafisha macho. Nitafanya hivyo then nitatoa feedback.
 
Pole ndugu yangu lakini usife moyo, cha msingi hapo ni kuwa na umakini ktk chanjo, jitahidi unapowapa chanjo za Gumboro au Newcastle inakuwa ni asubuhi umeondoa vyombo vya maji karibu saa moja ukiwaacha wale na kuwa na kiu. Baada ya hapo wawekee maji na hakikisha hata walio dhaifu wanasogezwa ili wanywe chanjo.

Magonjwa ya hewa jitahidi banda lako kuwa na mzunguko mzuri wa hewa yaani hewa iwe inatembea vizuri, pia jaribu kuwa na kasehemu ka kuwatenga wagonjwa hata kwa kutumia mabox au waya hapo bandani huku ukiendelea kuwatibia wote kwa pamoja. Kila mara kagua na tenga yoyote unayeona ana dalili za ugonjwa ili usiambukize banda zima. Aliyekushauri uwape vitamin ni sawa maana zinaongeza nguvu ya mwili kujikinga au kujijenga hasa kwa wagonjwa.

Nimekushauri kuhusu chanjo kwani magonjwa mengi huwa yanaua kwa kiwango kikubwa iwapo kuku ni dhaifu au tuseme multiple infection, pili hewa ni nzito haitembei hivyo vidudu vimo bandani, tatu kuku hawapewi vitamini ya kutosha na hivyo hawana nguvu ya kustahimili ugonjwa wowote.
Tupe feedback kwani hapa tunafunzana mengi.

Kwa watalaamu na wafugaji wazoefu.

Nini kuku wale weusi (black Australorp) . wako wiki ya 5, nilianza nao 130 na sasa wamebaki 90 maana wanakufa karibu kila siku lazima afe mmoja au wawili. wanaanza kuvimba macho na hatimaye kufa. Daktari alisema ni ukosefu wa vitamini. nimewapa vitamin aina ya Introvit A pamoja na dawa ya typhoid lakini wapi. wanaendelea kufa tu!!

Hebu nipeni maoni, huo unaweza kuwa ugonjwa gani maana naona sijapata dawa muafaka. naambatanisha picha!!
 
Huo ugonjwa unaitwa ndui. Ilitakiwa uwape chanjo ya ndui walipofikia umri wa miezi miwili. Hivyo cha kufanya wape dawa yoyote ya antbiotic na dawa za mafua pia wape vitamin unaweza kuokoa baadhi.ole sana
 
Cha msingi ni kufuata ratiba ya chanjo kwa makini. Mimi kwa mara ya kwanza nilikuwa na kuku 700 wakafa 500 na kubaki 200 kwa kukosa hewa na kukosa chanjo ya new castle. Ikanibidi niongeze ukubwa wa banda. Sasahivi mambo ni mazuri. Pia Hakikisha una dawa ya OTC 20% inatumika kama first aid ya magonjwa mbalimbali.
 
Kwa zahma hii ya biashara ya mayai mimi naona hii ni kaburi la wafugaji wadogo wadogo --
 
Mara nyingi huwa naona ujasiriamali unalipa kuliko kuajiriwa.

We unaajiriwa ili hatimae ulambe angalau 1mil a month wakati mwenzako anapata mara 2 mpaka 3 ya iyo.Inauma.
Tatizo la Tz mitaji ndo issue
 
Digna thanks kwa ushauri wako. nimeenda kwa mtaalamu mmoja kanipa antibiotic Tylosin 75% ndo nawapa pamoja na Oligovit.
thanks a lot kwa ushauri wa kuwasafisha macho. nitafanya hivyo then nitatoa feedback.

Mambo yalikwendaje Kanyagio?
 
Mambo yalikwendaje Kanyagio?

Digna nashukuru kwa kukumbushia, kwa ufupi ni kuwa hiyo dawa iliwasaidia sana. kwa sasa kuku wangu wanataga nakula matunda. though changamoto lipo kwenye soko. ila najjitahidi kulitafuta.

Kikubwa katika biashara hii ni mfanyakazi ambaye ni mchapakazi, mpenda kazi na mwaminifu. namshukuru mungu kwamba nimepata mfanyakazi wa aina hii. kikubwa inabidi kumlipa angalau vizuri. mimi wangu namlipa 100,000/= na kila wiki nampa 10,000/= za chakula na nimempa nyumba nzuri ya kuishi hapo kwenye project location (note: location nimeikodisha).
 
Haya let me share with you some graphs of my poultry project. hii ni project iliyoanza mwezi wa August 2011 kwa kuku 630 layers. mnano mwezi wa 9 mwishoni tuliongeza kuku wengine 450. kuku wa awamu ya kwanza walianza kutaga tarehe 1 December 2011 na hawa wa phase 2 walianza kutaga tarehe 1 February 2012. kwa ujumbla walikufa kuku kama 80 na hivyo tumebakiwa na kuku 1000. kumbuka mabanda nimeyakodisha na nalipa hela kidogo kidogo. ila mabanda haya niliyafanyia renovations. ufugaji unafanyikia Dar es salaam. December na january mwanzoni soko lilikuwa zuri maana tuliuza tray kwa 6500 hadi 7000/= ila sasa limeshuka kwa sababu trei ni Tsh 5500. Chakula (layers mash) kimepanda kutoka 32500/= kwa mfuko wa 50kg hadi 34500/=. ila hatukati tamaa.
expenditure summary.png

income and expenditure summary.png

Mwenye utaalamu wa kukuza image anisaidie.
 
Haya let me share with you some graphs of my poultry project. hii ni project iliyoanza mwezi wa August 2011 kwa kuku 630 layers. mnano mwezi wa 9 mwishoni tuliongeza kuku wengine 450. kuku wa awamu ya kwanza walianza kutaga tarehe 1 December 2011 na hawa wa phase 2 walianza kutaga tarehe 1 February 2012. kwa ujumbla walikufa kuku kama 80 na hivyo tumebakiwa na kuku 1000.

Kumbuka mabanda nimeyakodisha na nalipa hela kidogo kidogo. ila mabanda haya niliyafanyia renovations. ufugaji unafanyikia Dar es salaam. December na january mwanzoni soko lilikuwa zuri maana tuliuza tray kwa 6500 hadi 7000/= ila sasa limeshuka kwa sababu trei ni Tsh 5500. Chakula (layers mash) kimepanda kutoka 32500/= kwa mfuko wa 50kg hadi 34500/=. ila hatukati tamaa.
View attachment 50000

View attachment 50001

mwenye utaalamu wa kukuza image anisaidie

Mpaka sasa umepata faida au vipi? Umeeleza kwamba mradi mpaka ulipofikia umegharimu milioni ishirini, tatal revenue milioni saba, na net revenue milioni kumi na tatu. Je, faida kiasi gani?
 
Mpaka sasa umepata faida au vipi? Umeeleza kwamba mradi mpaka ulipofikia umegharimu milioni ishirini, total revenue milioni saba, na net revenue milioni kumi na tatu. Je, faida kiasi gani?

Kifuku, siyo kurahisi ku-break even ndani ya muda mfupi. so far net revenue ni negative 13m, that mean I need to minimize this number to zero then I will start to make positive profit. So kwa ufupi so far sijapata net profit ingawa kwa sasa mapato yanazidi matumizi. inawezekana watu wa business/financial management wakawa na mtazamo mwingine; lakini kwa upande watu nitaanza kuhesabu kuwa this is real profit hadi pale nitakapo break even
 
Hongera sana Kanyagio, na asante kwa kuleta feedback hapa kuanza kupata faida taratibu tu usikate tamaa. Ushauri wangu, ongeza idadi ya kuku, tafuta na nunua eneo lako, tengeneza chakula mwenyewe kwa kusaga kwa wingi.

Hata hivyo umejitahidi sana kaza buti!
 
Wana jamii naomba msaada kwa wale wanaofuga kuku wa kisasa (broilers) mie kumbukumbu zao zinanipa shida japo faida napata lakini nashindwa kutenganisha hesabu za kila batch kwa kuwa ukianza na vifaranga wiki ya kwanza baada ya wiki mbili nachukua wengine tena na baada ya hapo kuku wa batch ya kwanza wanashirikiana chakula na madawa.

Kwa wenzangu mliopiga hatua kwenye hili naomba mwanga.
 
Habari wadau!

Mwenye kufahamu jinsi ya kutengeneza chakula cha broiler msaada tafadhali.
 
Nipo Dar nataka nianze biashara hii ya kuku wa mayai ila nataka kijana mtaalam mwenye uzoefu naweza mpata wap? na maeneo mazuri ya kuweka banda ni wap nina plot bagamoyo kma heka 2 na plot ya "20 kwa 30" Goba panafaa kujenga banda la kuku 2000?

Ujenzi wa banda la kuku wa mayai (kuku 2000) linagarimu kiasi gani cha fedha? mchoro stracture yake naweza ipata wap la kisasa na economical! ntashukuru kwa majibu yenu

Dr wa Ukweli, ulifanikiwa kuanza mradi huu? Plz nipatie information hii (ujenzi wa banda la kisasa, wapi napata ramani na garama zake zikoje?) THAX
 
Napenda kuwapongeza Mlachake (mleta UZI), Mama Joe, ELNINO, FUSO na wadau woote waliotupia ujuzi na uzoefu wao hapo kuhusiana na ufugaji wa kuku mbalimbali, binafsi naona mchango wao ni wa kutukuka na unafaa kuigwa na Watanzania wote wapenda maendeleo, kwa kuwa mawazo yao yatawasaidia wengi JF members na na wasio member. Mbarikiwe sana kwa utayari huu.

Mwenyezi Mungu awazidishie.
 
Back
Top Bottom