Ufugaji wa Samaki: Pata ushauri, mawazo na michango kuhusu ufugaji samaki. Jifunze changamoto, utaalamu na masoko ya Samaki

Wadau mimi nina fuga samaki aina ya sato na vifaranga nilichukua SUA..mpaka sasa wana kama miezi 6.5 lakini uzito wao sio wa kuridhisha sana kwani 1 anafika gramu 150 mpaka 190..nina mabwawa 4 yote yanasamaki.

Je uzito huu na umri wao ni sawa kweli, wataalam naomba msaada
 

Pole sana mkuu! Ndaha,inaonyesha kwenye ufugaji wako wa samaki kutakuwa na mojawapo ya matatizo ndiyo maana samaki wako wanakuwa na kuongezeka uzito wao taratibu,inaweza kuwa ni mojawapo ya matatizo hayo hapo chini kama ifuatavyo:

1)IDADI KUBWA YA SAMAKI KWA MITA MRABA MOJA - Hii inamaanisha kwamba ukubwa wa bwawa lako ni mdogo ukilinganisha na idadi ya samaki waliopo bwawani kwa hiyo samaki wanakosa nafasi na hewa ya oxygen ya kutosha.

2)CHAKULA- Chunguza mchanganyiko wa chakula unachowapatia samaki wako je kina virutubisho vya kutosha(mfano: Protini,wanga,mafuta na madini muhimu) kwa kuzingatia ratio ya kitaalamu na chakula cha samaki kinatakiwa kiwe katika mfumo wa punje ndogondogo(pelletes) na siyo vumbi ili samaki aweze kula mchanganyiko wote kwa urahisi.

3)JINSIA YA SAMAKI- Pia kuna uwezekano samaki unaowafuga kwenye bwawa moja wakawa na jinsia tofauti(kike na kiume) hivyo kuzaliana,na kwa samaki aina ya sato(tilapia) uweza kuzaliana kwa haraka sana na kuongezeka ndani ya muda mfupi hivyo kupelekea kuwa na idadi kubwa ya samaki kwenye bwawa dogo na hivyo kupelekea samaki kukua taratibu.

4)HALI YA HEWA- Samaki haina ya sato ukua na kuongozeka taratibu sana kwenye maeneo yenye hali ya hewa ya ubaridi,hivyo wafugaji wa samaki kwenye maeneo ya baridi wanashauriwa kufuga samaki wao kwenye mabwawa ndani ya Greenhouse(Chumba maalumu) ili kuweza kudhibiti kiwango cha joto kisiwe kidogo wala kikubwa sana kuwawezesha samaki kukua vizuri.

5)MAJI-Maji ya kwenye bwawa la samaki yanatakiwa yawe na oxygen ya kutosha muda wote,hivyo unashauriwa kubadili maji mara kwa mara pindi unapogundua samaki wako wamepungukiwa na hewa ya oxygen(Mfano: samaki wanaonekana juu ya maji muda wote wakitafuta oxygen au uchafu na chakula vimejaa kwenye maji na kufunika bwawa lote kwa juu),pia maji ya kufugia samaki hayatakiwi yawe na kemikali za aina yoyote ili kulinda ustawi na ukuaji wa samaki wako.

6)ASILI YA UDONGO NA MAJI- PH ya udongo na maji huathiri ukuaji wa samaki kwa kiasi kikubwa,endapo udongo na maji ya kwenye bwawa vitakuwa na kiwango kikubwa cha acid (kwa mabwawa ambayo hayajajengewa),hivyo unashauriwa kupima na kujua asili ya udongo wa sehemu unapotarajia kuchimba bwawa la kufugia samaki wako.

Ni hayo tuu Mkuu kwasasa,ngoja na wataalamu wengine waje kuchangia hapa kwa msaada tofauti!
 
Hivi haiwezekani kuchkua hiyo mbegu na kuileta huku Dar?

Moja ya Watalaam waliopo pale Kinguluira ni mzaliwa wa pande zile za Igowole, na anajua ninachosema hapa, nilipomuuliza kwa nini wasisambaze mbegu ile maeneo mengi, alinijibu kuwa mchakato wa kufanya hivyo bado haujaanza.

Nikamuuliza pia kwa nini yule samaki adimu duniani, ila yupo Morogoro hatangazwi ili afugwe zaidi, jibu ni lile lile,hakuna hela ya kufanyia utafiti. Huyu samaki wa morogoro anaitwa Mjonga, ni mtamu balaa, ila anapotea mdogo mdogo sababu ya uharibifu wa mazingira. Inaaminika yupo Morogoro tu kule Kilombero.

Hawa wa Igowole inawezekana kwa juhudi binafsi. Serikali bado wanawaza uchaguzi 2015.
 
Ndgu zangu wana jf, mimi nina shamba na bustani ambayo ina maji maji ya kutosha ,
nataka kuanzisha mradi wa ufangaji wa samaki,,

naomba mwenye ufaham zaidi kuhusiana na ufungaji wa samaki na utaratibu.....! anijuze

asanten sana
 
Mkuu Search uzi wa Malila - Pata ushauri, michango, mawazo juu ya Ufugaji wa Samaki.
Utapata mengi zaidi. Kila la Kheri.
 
samaki wakue haraka chakula kiwe cha pallets,pumba itakula kwakoii,o
 

Mkuu asante kwa ufafanuzi...bila ya kuwa na interest na ufanyacho ni kazi bure!!
 
Bwana Ndaha, je vifaranga ulivyochukua vilikuwa na gram ngapi? Je, una rekodi ya joto la maji kwa kipindichote cha ufugaji ( au ulifuga msimu wa joto au baridi?).
 

Mkuu mimi nafugia Mkuranga kijijini Msorwa.
 
Niliamua kufanya utundu kidogo,
Mwaka huu mvua ilinyesha vizuri na hivyo kambale walizaliana sana. Sasa mimi nikapiga mbiu kwa madogo kule Mkuranga karibu na shambani kwangu kwamba nanunua kambale. Nimepata kambale wengi sana, na bado nawakusanya. Kasheshe ni chakula. Mdau mmoja alinitembea na kunihakikishia kunipa formula ili nitengeneze chakula changu mwenyewe, hasa floating pellets.

Hawa kambale pori wako vizuri.
 
Mungu akubariki nirushiekaka zqkukuwakienyeji
 
Ni samaki wa aina gani hao na hao ambao hizaliana ni kwa muda hani na kwa kiwango gani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…