Elections 2010 Ufunguzi wa Kampeni ya Chadema Jangwani 2010

Nilijua tu watakata.

Dawa ni watu leo hii hii kuandamana hadi TBC na kuwawekea barua.

Wakimaliza, Dr. Slaa amwambie LIVE Boss wa TBC 1 na maboss wengine kuwa watunze data ili Mhuni anayekata siku zote maelezo ya Slaa basi ashitakiwe kulingana na uhujumu wake. Nawasikitikia kwamba, watapanda peke yao Kizimbani wakati mwenzao Kikwete atakuwa na IMUNITE.

Mijitu mingine bana, wee sijui Mhando siji nani, anza kukusanya virago, CCM weee.......
 
....Mkuu, haya maneno naomba mkutano uishe kwanza salama ndio uyaseme. ameishasema mchangiaji mmoja hapa, hawakawii hawa kukata umeme na kudai kuwa kuna waya umetafunwa na mamba Kihansi



I hate to say this but here goes... I TOLD YOU SO !!!! Ni vizuri Watanzania Tukaandika haya majina ya wahusika wa TBC wanaofanya haya madudu ili siku ya siku tuwashughulikie! Huku ni kutafuta uvunjivu wa Amani. Yaani marudio ya kipindi cha Muziki ni Muhimu zaidi kuliko hotuba za wanasiasa wetu???
 
Huu ni udikteta wa hali juu, CCM oneni aibu Mrudieni Mungu, La sivyo Kikwete utalaanika vibaya sana! acha kuibia raia wema, acha kuua raia wema, kikwete ona aibu!
 
Aisee!! wampe glucose au Padri Slaa amtoe mapepo mabaya Alhaj Mohammed Nyange ( Bob Makani ) Pole sana kamanda wa udongo get well soon.... I hope "umefunguiia"

duuuh... kuna madongo mengine inabidi mtu ucheke kwa sana tu!!! lol
 
TBC wanaendeshwa kwa kodi zetu, lakini hawatuheshimu, hawajali watanzania, wanajali yao wanayojua, labda niseme tu kuwa hii nchi mpaka tuchapane ndo heshima itakuwepo. Tutakapo amua siku moja kuingia TBC na kuwatoa watangazaji pale, harafu tukarusha hewani matangazo yetu wenyewe ndoo watajua kuwa hela yetu inatuuma.
 


Regia nakupigia kwenye Zain inaita tu.

Tafadhali pokea na uniunganishe Live nipate kutuma updates wana JF wapate haki yao
 
wakuu nashukuru sana kwa kutubrief tulio mbal na jangwan na pia tbccm please mlio karibu endeleen kutujuza wanajamvi
 
Mbona majina yamelalia upande mmoja wa dini tena ya kikristo, na ukichanganya na mgombea Padri sina imani na Chadema

Kaka, hujasoma vizuri... Halima Mdee (Muislam), Anna Maulidah Komu (Muislam), Alhaji (Muislam), lakini haya ni baadhi tu ya majina... Usituletee porojo zako! Kama CHADEMA ni chama cha Wakristo, mbona wameanza kampeni na dua ya Kiislam, iliyosomwa na Hassan Yahaya Hussein?

Ongea POINT! Usilete mzaha!

CHADEMA INAKUBALIKA kwa Waislam na Wakristo! Inakubalika, na Watanzania walio wengi. Kama wewe ni mwanachama wa Chama Cha Mafisadi (CCM), hilo ni shauli lako!
 
Huu ni udikteta wa hali juu, CCM oneni aibu Mrudieni Mungu, La sivyo Kikwete utalaanika vibaya sana! acha kuibia raia wema, acha kuua raia wema, kikwete ona aibu!

Wewe Mwita wewe, fanya hima basi na kile kikosi cha sheria tuwashitaki hawa!!!! :glasses-nerdy:
 
Invisible hapokei Mkuu.

Nipe namba yake nyingine. Nitumie kwenye SMS
 
Nimepata habari kwa habari kwa mtu wangu aliyepo uwanjani kuwa wanachama wenye hasira walitaka kuwashushia kibano waandishi wa TBC wakiongozwa na Marini Hassan waliopo uwanjani, lakini wakajitetea kuwa kuna tatizo la kiufundi limetokea na hivyo wanalifanyia kazi.

Hotuba zimesimama kwa muda kusubiria TBC warekebishe hilo tatizo, sasa sijui watasubiri kwa muda gani.
 
Regia nakupigia kwenye Zain inaita tu.

Tafadhali pokea na uniunganishe Live nipate kutuma updates wana JF wapate haki yao

I am really proud of you bro. You show so much care in making sure we all are informed. Ubarikiwe na kuongezewa ndugu!

Steve Dii
 
Superman, ubarikiwe. Siandiki mengi ili kutokukupotezea muda.

Invisible na Regia na wengine kazi safi .......
 

MwanaHaki, ni vizuri kwenye UKWELI kutoongopa, haisaidii kitu kuongopa. Naijua vizuri familia ya kina Halima Mdee, Halima ni MKRISTO, kama alivyo Baba na Mama yake, bali ndugu wengi wa Baba yake ni WAISLAMU. Nikija kwa Anna Komu, alikuwa anaitwa Maulidah kabla ya kubadili dini na kuwa Mkristo. Hivyo Halima Mdee na Maulidah Anna Komu wote ni Wakristo.

Ukiwa katika haki uongo wa nini?.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…