Kwanini wamgeuzie kibao? Kwani amewakamata au hata kuwasumbua ma don? Wahangaike naye kwanini na hajagusa maslahi ya don hata mmojaKuna uwezekano pia ma don wa unga wanamgeuzia kibao?
Tutazame pande zote.
Huo ugaidi wa kuteka watu maarufu tu tena wenye muelekeo fulani fulani ndiyo ugaidi gani? Labda watu wa siasa na hizo siasa zao ndiyo wanataka kuwaletea watu hofu ila sie wengine huku mitaani hakuna hofu hizo kabisa. Tumepigiwa kelele za njaa na sasa mnakuja na ugaidi.
Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni.A strong tiss will ensure there is no terrorism except when and where they are the terrorists themselves. Hivi kama utawala unadulterated katiba (pamoja na mapungufu ya hiyo katiba) kuna umuhimu na u lazima wa ku terrorise walipakodi? Kweli?
Hujajibu swali langu. Kama wewe ndiyo ungekuwa umefanyiwa huo ugaidi ungependa wengine wakae kimya ili lengo la magaidi lisifanikiwe?
Hiv walio ua na kudhulu mapadri zenj ni kina nani? Hiv walio waumiza wale mabinti wa kizungu zenj ni kina nani? Kule Rufiji, Amboni na Kilindi je Tuwaiteje mkuu?Mjadala maridhawa neno gaidi kwa tanzania yetu limekuwa rahisi ndio haya matokeo yake ndugu zetu wanaishia magerezani kisa tu walitoa mihadhara kwa sababu ya kulikuza hili neno gaidi,labda niseme magaidi wengi wafanyapo shughuli zao hutoa taarifa na kwa uwazi si uwazi wa mimi na wewe kuona isipokua hata kipande kidogo cha clip tutashuhudia sasa hapa kwetu tuna vikundi vya wahuni kama vile komando yosso panya road na kiboko msheli bado hatujakuwa na magaidi wa kututia hofu ila tunajitia hofu!
Nashindwa kuelewa kwa nini serikali tukufu ya CCM iko kimya_ hata wabunge wake wanapokuwa wanakabiliwa na matishio ya kutekwa?
Watanzania hatuwezi tukakaa kimya eti tuwakomeshe magaidi kwa kimya chetu!!!.
FaizaFoxy Ndugu yangu nitaumia kiasi gani nikisikia umetekwa na kuteswa?
Je moyo Wangu utahimili kukaa kimya kweli?
Nitafanya niwezalo . Nikishindwa kulipa kisasi basi nitaandika.
Kamwe sitokaa kimya.
Kuna watekaji walitajwa kwa majina na miongoni mwao ni Ramadhan Igwondu, je alichukuliwa hatua gani?
Serikali yetu ya Leo imekuwa Crime Organiser ndio maana iko kimya na hata kwa maswali mazito inakuja na majibu mepesi.
Hiv walio ua na kudhulu mapadri zenj ni kina nani? Hiv walio waumiza wale mabinti wa kizungu zenj ni kina nani? Kule Rufiji, Amboni na Kilindi je Tuwaiteje mkuu?
Umeandika sana Dada yangu,Kinachoendelea sasa hivi Tanzania ni ugaidi (terrorism).
Lengo la ugaidi ni kuwatia watu hofu na kufikisha ujumbe kwa wengi kwa njia ya hofu.
Matukio yanayoongelewa sana kwenye vyombo vya habari na mitandao yote ya kijamii mpaka nchi za nje kwa sasa ni hayo, kuanzia watu kutekwa, kutolewa bastola hadharani, mauaji ya Kusini huko, watu kukutwa kwenye viroba, kupotea kwa watu na mengi mengineyo, yote yanaashiria ugaidi.
Magaidi hujitokeza na kusema sisi ndiyo tuliyoyafanya hayo ili waogopwe au matakwa yao yatimizwe au hukaa kimya na kuwachochea kivingine kwa lengo hilo hilo.
Matukio ya ugaidi yanapotokea pia hujitokeza wengine ambao hutumia fursa hiyo kufikisha ujumbe wao kwa njia tofauti.
Kwa yanayotokea Tanzania, ukweli ni kuwa, kuna wanaofanya huo ugaidi wa kutisha na kuna wanaotumia huo gaidi kama ni fursa kwao kufikisha ujumbe wao ama kwa kuongezea ugaidi mwingine au kwa kuendeleza hofu kwenye jamii na vyombo husika.
Watanzania tunachotakiwa kufanya ni kukaa kimya na kufunga hii mijadala yote na kuwacha kuripoti matukio yote ya kigaidi ili kushindana na ugaidi.
Gaidi kama matukio yake hayaongelewi kazi yake inakuwa haijafanikiwa.
Kila tunapoyaongea na kuyasambaza ndiyo furaha ya magaidi na ndiyo lengo lao, wengi wajawe na hofu.
Kwanini? Mie sijuwi.
Ugaidi wa ccm ni tofauti na wa ISSI, Al shabab , Boko Haram, kina Koni, IRA.... wakat huu unataka uhuru zaidi na matakwa yao yatekelezwe... wa CCM unataka watu wakae kimya tu wasiwakosoe.... ndo maana wa hao wengine publicity inaweza uondoa kama jamii itaweza kaa kimya (japo si rahisi), lakini wa ccm ukikaa kimya ina maana unakuwa umekubaliana nao na wao wanakuwa wameshinda.... tuseme hapana, tupige kelele na walioko ndani ya system wasio penda uonevu watupe habari sahihi ili tuwaumbue... ahsante Mange Kimambi kwa kuwa gwiji kwenye kuja na facts kwa haya majangiri (in Manges tone)
..
Huo ndio ukweli tuwanyamazie magaidi wasiwe na misifaKinachoendelea sasa hivi Tanzania ni ugaidi (terrorism).
Lengo la ugaidi ni kuwatia watu hofu na kufikisha ujumbe kwa wengi kwa njia ya hofu.
Matukio yanayoongelewa sana kwenye vyombo vya habari na mitandao yote ya kijamii mpaka nchi za nje kwa sasa ni hayo, kuanzia watu kutekwa, kutolewa bastola hadharani, mauaji ya Kusini huko, watu kukutwa kwenye viroba, kupotea kwa watu na mengi mengineyo, yote yanaashiria ugaidi.
Magaidi hujitokeza na kusema sisi ndiyo tuliyoyafanya hayo ili waogopwe au matakwa yao yatimizwe au hukaa kimya na kuwachochea kivingine kwa lengo hilo hilo.
Matukio ya ugaidi yanapotokea pia hujitokeza wengine ambao hutumia fursa hiyo kufikisha ujumbe wao kwa njia tofauti.
Kwa yanayotokea Tanzania, ukweli ni kuwa, kuna wanaofanya huo ugaidi wa kutisha na kuna wanaotumia huo gaidi kama ni fursa kwao kufikisha ujumbe wao ama kwa kuongezea ugaidi mwingine au kwa kuendeleza hofu kwenye jamii na vyombo husika.
Watanzania tunachotakiwa kufanya ni kukaa kimya na kufunga hii mijadala yote na kuwacha kuripoti matukio yote ya kigaidi ili kushindana na ugaidi.
Gaidi kama matukio yake hayaongelewi kazi yake inakuwa haijafanikiwa.
Kila tunapoyaongea na kuyasambaza ndiyo furaha ya magaidi na ndiyo lengo lao, wengi wajawe na hofu.
Kwanini? Mie sijuwi.
Swali ni kwamba nani anaefadhili hivi vikundi vya kigaidi duniani jibu ni baadhi ya Serikali duniani hivyo sishangai kuona hapa Tanzania mambo kama hayo yanaibuka kwani chokochoko huanza mdogo mdogo kama hivyo hatimae hukomaa na mambo kwenda mrama kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.