Ugali unaopikwa kwa Unga wa mahindi (dona) hatari kwa afya ya binadamu

Ugali unaopikwa kwa Unga wa mahindi (dona) hatari kwa afya ya binadamu

Watu wengi kwa sasa wamependelea kula ugali uliopikwa kwa unga wa mahindi usiokobilewa, maarufu 'dona'. Pamoja na kwamba mahindi uhifadhiwa kwa madawa ili yasiharibike (athari kwa fedha) kuna tatizo lingine kwa afya zetu yasemekana.

Tahadhali na unga wa dona, ni hatari kwa afya kwa sababu ya sumu inayoitwa 'aflatoxin" ambayo huwa ndani ya kiini cha mbegu ya mhindi. Ukikobolewa kiini uondolewa na kubaki unga mweupe (sembe).

Wengi sasa hawependi kula ugali wa sembe kwa sababu ya kukosa protini (iliyomo kwenye kiini). Lakini hasara ya kukosa hiyo protein ni ndogo sana kulinganisha na madhara ya "aflatoxin" itakayosababisha "cancer" mwilini mwa binadamu.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
Kamaa sijaweka dawa! Kuna tatiizo apo
 
Mzee hiyo sumu hata kama ipo kimsingi imeshathibitika haina madhara yoyote yale kuogopwa. Hicho kimekua chakula kikubwa sana cha wabantu tangu enzi na enzi. Sio ishu. Nimezaliwa mpaka Leo nakula ugali was mahindi. Mababu zetu wamekula. Sio ishu wala nini hiyo nadhani
Naamini wewe siyo kati ya wale waliohusisha kipindupindu na uchaguzi, ati mbinu za CCM watu wasikusanyike.

Nimezungumzia afya zetu kwa kudokeza uwezekano wa kutumia dona iliyo na sumu. Chakula chochote kisipotayarishwa vizuri kinakuwa sumu. Hatuhitaji takwimu kuthibitisha hilo, ila mfano ni mlipuko wa magonjwa ya kuambukiza kama vile kipindupindu.

Ukweli ni kwamba "fungus" huzalisha hiyo sumu ya "aflatoxin" ambayo huleta kansa. Na Vyakula vya nafaka, na vinginevyo vikivunda ni hazina ya "fungus".

Kwamba umekua ukila ugali wa dona, uendelee kufanya hivyo, ni heri kwako. Kumbuka tu mazingira ya sasa hivi siyo salama kamwe. Nenda Ocean Road Hospital uone wagonjwa wa kansa - aina mbalimbali ikiwamo magonjwa ya ngozi.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
 
Watu wengi kwa sasa wamependelea kula ugali uliopikwa kwa unga wa mahindi usiokobilewa, maarufu 'dona'. Pamoja na kwamba mahindi uhifadhiwa kwa madawa ili yasiharibike (athari kwa fedha) kuna tatizo lingine kwa afya zetu yasemekana.

Tahadhali na unga wa dona, ni hatari kwa afya kwa sababu ya sumu inayoitwa 'aflatoxin" ambayo huwa ndani ya kiini cha mbegu ya mhindi. Ukikobolewa kiini uondolewa na kubaki unga mweupe (sembe).

Wengi sasa hawependi kula ugali wa sembe kwa sababu ya kukosa protini (iliyomo kwenye kiini). Lakini hasara ya kukosa hiyo protein ni ndogo sana kulinganisha na madhara ya "aflatoxin" itakayosababisha "cancer" mwilini mwa binadamu.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
kabla haujakimbilia aflatoxin mbona kuna sumu kibao zitolewazo na midaladala mibovu, moshi wa maroli yaendayo na kutoka bandarini, magari yaliyopigwa marufuku ulaya kwa kuchafua hali ya hewa na kuuzwa africa.
 
Naamini wewe siyo kati ya wale waliohusisha kipindupindu na uchaguzi, ati mbinu za CCM watu wasikusanyike.

Nimezungumzia afya zetu kwa kudokeza uwezekano wa kutumia dona iliyo na sumu. Chakula chochote kisipotayarishwa vizuri kinakuwa sumu. Hatuhitaji takwimu kuthibitisha hilo, ila mfano ni mlipuko wa magonjwa ya kuambukiza kama vile kipindupindu.

Ukweli ni kwamba "fungus" huzalisha hiyo sumu ya "aflatoxin" ambayo huleta kansa. Na Vyakula vya nafaka, na vinginevyo vikivunda ni hazina ya "fungus".

Kwamba umekua ukila ugali wa dona, uendelee kufanya hivyo, ni heri kwako. Kumbuka tu mazingira ya sasa hivi siyo salama kamwe. Nenda Ocean Road Hospital uone wagonjwa wa kansa - aina mbalimbali ikiwamo magonjwa ya ngozi.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
mkuu huo utafiti umefanywa na taasisi gani? nimr amref muhas cuhas au tdfa?
 
kabla haujakimbilia aflatoxin mbona kuna sumu kibao zitolewazo na midaladala mibovu, moshi wa maroli yaendayo na kutoka bandarini, magari yaliyopigwa marufuku ulaya kwa kuchafua hali ya hewa na kuuzwa africa.
Kwa hiyo tusipeana taarifa kuhusu afya zetu! Mh, hiyo nayo busara!!!
 
Watu wengi kwa sasa wamependelea kula ugali uliopikwa kwa unga wa mahindi usiokobilewa, maarufu 'dona'. Pamoja na kwamba mahindi uhifadhiwa kwa madawa ili yasiharibike (athari kwa fedha) kuna tatizo lingine kwa afya zetu yasemekana.

Tahadhali na unga wa dona, ni hatari kwa afya kwa sababu ya sumu inayoitwa 'aflatoxin" ambayo huwa ndani ya kiini cha mbegu ya mhindi. Ukikobolewa kiini uondolewa na kubaki unga mweupe (sembe).

Wengi sasa hawependi kula ugali wa sembe kwa sababu ya kukosa protini (iliyomo kwenye kiini). Lakini hasara ya kukosa hiyo protein ni ndogo sana kulinganisha na madhara ya "aflatoxin" itakayosababisha "cancer" mwilini mwa binadamu.

TAFAKARI CHUKUA HATUA

mwengeso tafadhali tunaomba uthibitisho wa hicho unachokisema! Any reference?
 
Jamaa anashawishi tule sembe tuharibu office... Kiukweli sioni mantiki hapo sumu inakuwa juu sio ndani ya Kiiini. Pili dawa hizi za ku preserve nafaka zina muda wake wa ku expire. Hivyo muda wa Matumizi ufiki zitakuwa hazina makali. Mbali na hapo unashauriwa kuyaosha kabla ya kwenda kuyasaga. Wanaume tuleni dona sembe ni majanga.
 
mwengeso tafadhali tunaomba uthibitisho wa hicho unachokisema! Any reference?
Ukisoma michango kwenye hii "post" yangu, hilo swali lako litakuwa na majibu toshelezi. Wataalam wa TFDA watatujuza ili akina "Thomaso" waamini.
 
Watu wengi kwa sasa wamependelea kula ugali uliopikwa kwa unga wa mahindi usiokobilewa, maarufu 'dona'. Pamoja na kwamba mahindi uhifadhiwa kwa madawa ili yasiharibike (athari kwa fedha) kuna tatizo lingine kwa afya zetu yasemekana.

Tahadhali na unga wa dona, ni hatari kwa afya kwa sababu ya sumu inayoitwa 'aflatoxin" ambayo huwa ndani ya kiini cha mbegu ya mhindi. Ukikobolewa kiini uondolewa na kubaki unga mweupe (sembe).

Wengi sasa hawependi kula ugali wa sembe kwa sababu ya kukosa protini (iliyomo kwenye kiini). Lakini hasara ya kukosa hiyo protein ni ndogo sana kulinganisha na madhara ya "aflatoxin" itakayosababisha "cancer" mwilini mwa binadamu.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
Kila kitu apa duniani kina faida na hasara, unachotakiwa kuangalia faida nyingi zipo upande gan, then unafanya maamuzi magum.
 
Siyo kila dona ni hatari...bali dona ambayo haijaandaliwa vizuri....ili kuepusha kupatikana kwa hyo sumu ni vyema mahindi yakatunzwa vizuri ili yasishambuliwe na fangasi waitwao Aspergilus flavus..fangasi wanaoshambulia mahindi ndiyo ambao huzalisha hyo sumu...iwapo nafaka zitakauka vizuri na kuhifadhiwa sehem isokuwa na unyevu unaweza saidia kupungusa mashambulizi....vilevile mahindi kabla ya kusagwa ni vyema yakachambuliwa na kuondolewa Yale ambayo ni mabovu au yaliyotoboka....

Kitu kinachosababisha dona isiwe salama siyo aflatoxin tu bali ata dawa (pesticides) zinazotumika kuhifadhia hayo mahindi...kwani wakulima na wafanyabiashara wengi hawafahamu matumizi sahihi ya dawa hivyo kusaga mahindi yakiwa bado yanadawa na hivyo kuzalisha unga wenye dawa au sumu..ili kuepuka hili ni vyema mahindi yakaoshwa vizuri kabla hayajasagwa na siyo kuyaloweka kwa maji kidogo kama wanavyofanyaga mashineni
Emelezea murua kabisa, maana hata mm nilikua najua aflatoxin inazalishwa na baadhi fungus
 
mwengeso tafadhali tunaomba uthibitisho wa hicho unachokisema! Any reference?
Tafiti nyingi zimefanyika hapa nchini na mabingwa ikiwamo TFDA. Labda usome ya Shirima et al. (2015): A Perspective Study of Growth and Biomarkers of Exposure to Aflatoxin and Fymonisin during Early Childhood in Tanzania. It was concluded from the study that "exposure to fumonisin alone or coexposure with aflatoxin MAY CONTRIBUTE to child growth impairment".
 
mara sembe inakufanya upate ugonjwa wa kusahau sahau mara dona cancer jaman tule nn sasa?
 
tupeane taarifa zilizofanyiwa utafiti
Tafuta na soma hiyo tafiti niliyomjibu "Thomaso" mwenzio. Narudia tena, "post" yangu yahusu afya zetu na siyo "siasa" au "udaku" ambazo wengi tunashabikia kwa sababu zinahusu 'watu' na 'matukio'.
 
Toa ushauri sasa tule nini,mawe au miti?
Ushauri. unga wa mahindi yasiyokobolewa (dona) ni bora kwa afya kwakuwa una virutubisho vyote kuliko unga wa mahindi yaliyokobolewa (sembe).

Zingatia yafuatayo ili hayo madhara aliyoyasema mtoa mada usiyapate.

Dona linahitaji usafi wa hali ya juu wakati wa kuuanda. hivyo unapaswa ufanye yafuatayo.
1. pepeta vizuri mahindi ili kutoa uchafu na vumbi
2. Chambua mahindi vizuri utoe mahindi yaliyooza na uchafu mwingine.
3.osha mahindi vizuri. kama yanadawa hakikisha unaosha zaidi ya maramoja ili dawa yote itoke
4.anika mahindi kwenye jua
5. hakikisha yamekauka vizuri ndipo upeleke kusaga
6. unaposonga ugali hakikisha uji unachemka vizuri ndipo usonge. unaposonga hakikisha unaiva vizuri hadi unukie ndipo upakue.

Hii itasaidia kufanya dona ibakie kuwa bora . dona ya kununua dukani, supermarket nk..... haishauriwi ununue huko kwani hujui wanavyolianda, wafanyabiashara wanaangalia hitaji (demand) ya wateja hivyo huweza kupeleka kusaga pasipo kuzingatia kanuni hapo juu.
 
Eleza hiyo aflatoxin inafikaje kwenye kiini just to know if it's something we can avoid or reduce effect.
 
Ndio wale wale watoto wa mjini wala viepe na vitu laini hata sembe ipo humo..Mwanaume wa kweli anakula "Dona"
 
Watu wengi kwa sasa wamependelea kula ugali uliopikwa kwa unga wa mahindi usiokobilewa, maarufu 'dona'. Pamoja na kwamba mahindi uhifadhiwa kwa madawa ili yasiharibike (athari kwa fedha) kuna tatizo lingine kwa afya zetu yasemekana.

Tahadhali na unga wa dona, ni hatari kwa afya kwa sababu ya sumu inayoitwa 'aflatoxin" ambayo huwa ndani ya kiini cha mbegu ya mhindi. Ukikobolewa kiini uondolewa na kubaki unga mweupe (sembe).

Wengi sasa hawependi kula ugali wa sembe kwa sababu ya kukosa protini (iliyomo kwenye kiini). Lakini hasara ya kukosa hiyo protein ni ndogo sana kulinganisha na madhara ya "aflatoxin" itakayosababisha "cancer" mwilini mwa binadamu.
TAFAKARI CHUKUA HATUA



WADAU TUJIFUNZE KUSOMA NA KUPANUA WELEDI WETU KATIKA KUCHANGANUA BAADHI YA MAMBO, SIYO KUKURUPUKA TU NA MADA KAMA ZA NAMNA HII:

KUHUSU Aflatoxin (Nimecopy na kupaste toka Wikipedia), someni kwa faida ya hii thread.

Aflatoxins are poisonous and cancer-causing chemicals that are produced by certain molds (Aspergillus flavus and Aspergillus parasiticus) which grow in soil, decaying vegetation, hay, and grains. They are regularly found in improperly stored staple commodities such as cassava, chili peppers, corn, cotton seed, millet, peanuts, rice, sorghum, sunflower seeds, tree nuts, wheat, and a variety of spices. When contaminated food is processed, aflatoxins enter the general food supply where they have been found in both pet and human foods, as well as in feedstocks for agricultural animals. Animals fed contaminated food can pass aflatoxin transformation products into eggs, milk products, and meat.

SASA TAHADHARI YA UNGA WA DONA INATOKA WAPI? ilitakiwa uelezee hiyo toxicity inafikaje kwenye unga (siyo dona pekee) na njia za kufanya kujikinga kwa faida ya wana jamvi siyo kupost tu. Kama hujui kitu ni bora kuuliza kuliko kujifanya mjuaji.....
 
Back
Top Bottom