Ugali unaopikwa kwa Unga wa mahindi (dona) hatari kwa afya ya binadamu

Ugali unaopikwa kwa Unga wa mahindi (dona) hatari kwa afya ya binadamu

Duniani kila kila mtu ni mtaalamu leo mwingine kaja na utaalamu wa ugali.
Wakati huo ugali wa dona yeye mwenyewe ndio kakulia tena na maharage alikua wapi kuufanyia utafiti miaka yote kisa leo kapata tuhela kila kitu anakula cha supermarket ugali wa dona anauona sio inshu tena.
 
Wakuu alichosema huyu jamaa mleta mada sio kigeni kwangu maana niliwahi kusikia kitu kama hicho. Nilisikia kwamba ugali wa dona la mahindi linatengeza sumu ikiwa utakuwa unakula kila siku pamoja ya kwamba unga wa dona una virutubisho vya kutosha. Pamoja na hayo, unga wa sembe ni hatari zaidi.
Unahatari gani?
 
Watu wengi kwa sasa wamependelea kula ugali uliopikwa kwa unga wa mahindi usiokobilewa, maarufu 'dona'. Pamoja na kwamba mahindi uhifadhiwa kwa madawa ili yasiharibike (athari kwa fedha) kuna tatizo lingine kwa afya zetu yasemekana.

Tahadhali na unga wa dona, ni hatari kwa afya kwa sababu ya sumu inayoitwa 'aflatoxin" ambayo huwa ndani ya kiini cha mbegu ya mhindi. Ukikobolewa kiini uondolewa na kubaki unga mweupe (sembe).

Wengi sasa hawependi kula ugali wa sembe kwa sababu ya kukosa protini (iliyomo kwenye kiini). Lakini hasara ya kukosa hiyo protein ni ndogo sana kulinganisha na madhara ya "aflatoxin" itakayosababisha "cancer" mwilini mwa binadamu.

TAFAKARI CHUKUA HATUA
Ah! Mnatuchanganya bana.
 
Ni upumbavu kuweka kitu cha Google hapa! ni kiwango gani cha hiyo sumu ndo kinakuwa na madhara kwa binadam, namaanisha katika kipimo cha ppm?
Mkuu tarttiib usiwe na jazba mleta mada kasema ni dokezo kwa hiyo ni nafasi muafaka kwa wenye taaluma hiyo kutujuza ukweli.
 
Jamaa anashawishi tule sembe tuharibu office... Kiukweli sioni mantiki hapo sumu inakuwa juu sio ndani ya Kiiini. Pili dawa hizi za ku preserve nafaka zina muda wake wa ku expire. Hivyo muda wa Matumizi ufiki zitakuwa hazina makali. Mbali na hapo unashauriwa kuyaosha kabla ya kwenda kuyasaga. Wanaume tuleni dona sembe ni majanga.
Wanaofahamu kuhusu kuyaacha mahindi yaishe dawa ni wachache sana..wengi huwa hawazingatii hlo....kwani ww unaponunua mahindi huwa unauliza yamepuliziwa dawa lini ili uyahifadhi kwanza?
 
Daah!...kama na dona sumu basi hakuna chakula tena

Ila hata kama kuna huyo "aflatoxin" kwenye dona bado virutubisho vya dona vinaweza kua ni vingi kuliko hiyo sumu. Aflatoxin iko kwenye karanga na siyo mahindi.You are doing business ya sembe. Very hopeless.






Na kabla ya kusonga ugali ule uji hua unachemka kwa centigrade nyingi sana hiyo sumu bado inabaki salama?
 
Pana ka ukweli flan kwa alichosema mtoa mada haswa kama uvunaji na uhifadhi wa mahindi hayo haukuzingatia ubora mfano kutokaushwa vizuri ama kuhifadhiwa sehemu ya unyevu nyevu sana kabla ya kusagwa. Embu angalia hii link toka chuo kikuu cha Cornell: Cornell University Department of Animal Science
 
Ni upumbavu kuweka kitu cha Google hapa! ni kiwango gani cha hiyo sumu ndo kinakuwa na madhara kwa binadam, namaanisha katika kipimo cha ppm?
Samahani jana nikikosea kidogo kiwango cha aflatoxini B1 hakitakiwi kuzidi 5ppm na total aflatoxin haitakiwi kuzidi 10ppm...iwish this will be helpful to to u
 
Mnataka wanaume wote tuwe legelege na wala chipsi tukose nguvu za kiume. ?
 
Daah!...kama na dona sumu basi hakuna chakula tena

Ila hata kama kuna huyo "aflatoxin" kwenye dona bado virutubisho vya dona vinaweza kua ni vingi kuliko hiyo sumu

Na kabla ya kusonga ugali ule uji hua unachemka kwa centigrade nyingi sana hiyo sumu bado inabaki salama?
Duh, mkuu nani alikwambia sumu inapunguzwa na joto?
 
TETESI duh ngoja nikapike dona nile nitarudi nikimaliza

Lakini mbona Wazee wetu walikula hadi leo wanapeta tu.
 
Tat
sumu hiyo haiwez penya kama mahindi yako yatakua yamekauka vizuri, vinginevyo itabaki ktk ganda la nje hivyo unapaswa kuyaosha vizuri na kuyaanika iliyakauke tayar kwa kusaga.
Kwani ni wewe uanaeandaa hiyo sembe? Wary hawaoshi wanasaga hivyo hivyo, prepare yours vinginevyo hiyo ni tahadhari uichukue
 
Unasababisha kansa ya ubongo, kupungukiwa na kinga, na kutokuwa na uwezo wa kujamiiana kwa mwanaume,

Wa dona hauna madhara, na kama yapo ni madogo sana ambayo yanadhibitiwa na hyo mahidi kwenye kinga..
Kansa kivipi....kupungua kinga kivipi....kutokua na uwezo wa kujamiiana kivipi...then ni vipi dona uwe salama alaf sembe isiwe salama ilihali mahindi ni yale yale...?do you have any facts coz watu hapa wanaelezea ni vipi dona unaweza isiwe salama...na wewe tueleze ni vipi sembe unaweza sababisha hayo matatizo
 
Watu tumekula dona tangu kuzaliwa mpaka leo ndio uniambie kuna sumu.sikuelewi aisee
 
Siijui hiyo sumu kama ni kwwli ipo au ipo, ila wengi wapo hatarini kwa magonjwa kwa sababu hawajui kuanda Unga wa Dona..
Mimi naamini Unga Mzuri wa Dona ni ule ambao mmelima wenyewe na mbegu mlizozipanda ni zile mlizozivuna wenyewe(hapa sio zile mbegu za mahabala)...
 
Back
Top Bottom