Ugomvi wa Jirani na Mke/Mchepuko wake, Ulivyonigombanisha na Mke wangu

Ugomvi wa Jirani na Mke/Mchepuko wake, Ulivyonigombanisha na Mke wangu

Mnawatoaga wapi wanawake waropokaji?
Kwenye suala la mahusiano, mwanamke mwenye mdomo usio na breki kwangu hanaga nafasi.
Kusaidia majirani ni kuzuri lkn usiwe peke yako unaweza kuchomwa kisu ukawaacha wao wanakulana
😀😀😀angeenda ageuziwe yeye kivao watu huwajui wagombane usiku wa manane ujifanye kiherehere kwenda kusuluhisha
 
Ungefanya chochote, hata ku simpasize ba Mwanamke, yani kweli unasikia ugomvi, nyumba kimya, mtu anatoka na gari usifanye kitu?

Hata kupiga simu police, labda kutoka nje sio busara, kaa na mwanamke onyesha concern naye, fanya jambo fulani, mke ni kumpety pety tu.

Amekuona tu u cant protect a Woman, ans probably u can't protect her, mimi siwezi kulala kabisa na kamwe nikisikia hizo sauti za mwanamke akipigwa.

Talk to your wife, admit a mistake in a way, and rudisha atmosphere nzuri, ume act like a boy, and not a Man, if she is worried, handle her, mbona ni rahisi sana, sio jambo dogo wala ulilofanya, ujawajibika.
Yaani una-suggest kuwa majirani wanagombana na wewe huna mazoea nao halafu ukimbilie kichwa kichwa? You are not serious! Kwa taarifa yako unaweza kuuawa mapema sana. Kuna kisa kimoja kilitokea, jamaa alikimbilia ugomvi wa jirani ile kuingia ndani akalimwa shaba na ilikuwa bahati hakufa. Na mbaya zaidi yule mwanamke aliyekuwa anapigwa alikuja ku-side na mumewe na kudai jirani aliingia bila kubisha hodi wakadhani ni mwizi.
 
Si mchezo kuna kipindi niliwahi ingilia ugomvi tena ulikuwa Mwanamke na Mwanamke, ile kesi ilitafsiriwa vibaya mno.

Ikaonekana walikuwa wanapigana kwa sababu yangu ilihali siwafahamu kabisa yani.
Niliwakuta tu njiani wanadundana.
Ulifanya vizuri sana. Jirani unayeweza kukimbilia ugomvi wake kwa haraka ni yule ambaye una mazoea naye. Bora hata ufikishe habari kwa balozi wa shinda kuliko kujiingiza kwenye ugomvi wa mume na mke usiye na undugu naye au urafiki au ukaribu.
 
Acheni umbeya wewe na mkeo kuingilia umbeya wa watu ungeenda wangekugeuzia kibao, niliishi sehemu mke na mume daily kupigana nilikuwa siamulii na wakidundana kesho mahaba ka yote kimoyo moyo nilikuwa nasema uaneni tu mtajiju nani wakuwa shahidi wa jamhuri
 
Acheni umbeya wewe na mkeo kuingilia umbeya wa watu ungeenda wangekugeuzia kibao, niliishi sehemu mke na mume daily kupigana nilikuwa siamulii na wakidundana kesho mahaba ka yote kimoyo moyo nilikuwa nasema uaneni tu mtajiju nani wakuwa shahidi wa jamhuri
Ila haya maisha yana mambo mengi sana kwa kweli.

Kuna mahusiano yanapitia nyakati ngumu sana.
 
Yaani una-suggest kuwa majirani wanagombana na wewe huna mazoea nao halafu ukimbilie kichwa kichwa? You are not serious! Kwa taarifa yako unaweza kuuawa mapema sana. Kuna kisa kimoja kilitokea, jamaa alikimbilia ugomvi wa jirani ile kuingia ndani akalimwa shaba na ilikuwa bahati hakufa. Na mbaya zaidi yule mwanamke aliyekuwa anapigwa alikuja ku-side na mumewe na kudai jirani aliingia bila kubisha hodi wakadhani ni mwizi.

Unajua kusoma na kuandika? Nimesema angafanya chochote, hata kutoka sebuleni, kukaa na mwanamke, ku symphasize, na kutoa taarifa taarifa police....

Sijui mnajibu mkiwaza nini, ingekuwa ni mimi kwenye hiyo case nisingetoka, na ningelala na mke kwa amani sana bila gubu, ni art tu ya kuishi na mwanamke.

Kama kutoka nje si sawa na sio usalama, jamaa angetoka kitandani akakaa na huyo mwanamke akamwelewesha asingeelewa?
 
We jamaa ni mimi kabisa. Am that kind of person sipendagi kuingilia mambo ya watu. Hasa ugomvi. Yaan ugomvi mnaanzisha wenyewe halafu mimi niingilie, hell no. Mi uwa hata nikikuta watoto wanagombana, sijishughulishi nao kabisa. Naendelea na mambo yangu. Wazichape, atakayeshindwa awe na adabu.
 
Wakuu, nimesema mke au mchepuko wa jirani kwasababu sina uhakika kama ni mke wake ama vipi.

Sisi tunaishi eneo moja tulivu sana, eneo moja wapo huku Bunju.
Tunakaribia Miaka Miwili tokea tuhamie.

Tuna jirani yetu, amehamia hana hata Mwezi so hatufahamiani zaidi ya kuonana njiani hasa nyakati za Asubuhi.
Jamaa huwa anampeleka mtoto wake kupanda school bus [emoji590], huyo mtoto anaweza kuwa class Four au Three.

Ni kijana mpole sana, kwa mwonekano.
Kutoka kwenye Nyumba yake hadi kwetu ni kama mita 10-15.
Na nafikiri kwenye hiyo nyumba anaishi na huyo mtoto tu, au sijui kwasababu nimewahi kuwaona wao tu na ni asubuhi tu, Tunaokaa Nje ya mji tunaamka mapema sana kukimbizana na foleni, na tunarudi mida imeenda.

Sasa juzi kumetokea varangati ambalo limeleta mtafaruku.
Mida ya Saa Sita kasoro hivi usiku, tulianza kusikia kelele za Mwanamke kama vile anadai kitu, kutokea kwa jirani yetu huyo, zilianza chini chini hivi na baadae zikapanda.
Niliweza kusikia maneno machache na Jamaa akawa anaongea kwa hasira na kwa nguvu.

Wakaanza kutukanana, tusi kubwa ni kuitana Malaya, Jamaa anamwambia huyo Mwanamke wewe ni Malaya tu, yeye anamjibu Malaya ni wewe na baba yako, na maneno mengine mengine wakati huo kama vile kuna kitu wanagombania, inawezekana ni funguo.

Huyo Mwanamke anasisitiza jamaa ampe, mwamba kakaza, sasa sijui alikuwa amemshika kwasababu purukushani zilikuwa kubwa, Jamaa anamwambia atampasua, anamjibu huwezi kunifanya kitu ma.l.aya mkubwa wewe!!.

Hapo wife wangu yuko Dirishani anawasikiliza, mimi niko Kitandani sikutaka kuamka kabisa, gafla yule Mwanamke akapiga yowe moja la juu kabisa, kwa nyumba zilivyo sisi ndio tuko nao karibu kuliko nyumba za majirani wengine. Mabishano yao yalikuwa yamedumu kama dakika 15 hivi

Baada ya lile yowe la mwisho, nikasikia mkurumo wa gari, Wife akaniambia huyo jamaa anaondoka amka ukamzuie au ujue amemfanyia nini huyo Mwanamke, nikashtuka kidogo! Ile natafakari kwenye ile nyumba taa za ndani zikazimwa.

Wife akaniambia kuna mtu, huko ndani ila Kelele za yule Mwanamke na Jamaa hazikusikika tena. Wakati wote huo wife alikuwa anatamani niende nikaamulie huo ugomvi ambao sijui lolote.

Sasa gafla naona wife anachukua mto wake (pillow) anasema anaenda kulala chumba kingine, simply kwasababu nilishindwa kutoka na kuanza kunilaumu kwa mambo yasiyokuwa na kichwa wala miguu, ananiambia sina msaada wowote ule.

Wakuu kosa langu hapo ni lipi?
Unawezaje kuingilia ugomvi ambao hujui ulikotokea?
Naambiwa nina roho mbaya, kisa sikwenda na mimi dirishani kujaribu kuangalia kinachoendelea.

Ndoa ina miaka 6 hii ila bado sijamfahamu vizuri huyu wife wangu...Nahisi ana vichembe chembe vya u feminist.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kama kawaida yao, mwanamke anaweza kumuona wa maana sana muuza bucha alimuongeza kifundo kimoj cha nyama na akadharau aliyempa 10k akanunue kilo yahio nyama. Wanawake wanatabia za kulipuka from small things halafu akakomalia kabisa. Huna baya mkuu, nilipoanza kusoma uzi nilikua najiambia mimi nisingeenda kuamulia wala nini hadi mwisho wa uzi na wewe hukwenda. Ww ni kama mm tu.

We mpuuze tu atalala ataacha. Ukimpa attention na kuanza kutaka yazungumzike ndio atakaza fuvu ku prove kuwa una hatia. Mwache awe analala chumba kingine, usuulize, kuwa normal kabisa kama hakuna jambo lolote. Atajirudi mwenyewe tu
 
Unajua kusoma na kuandika? Nimeeema angafanya chochote, hata kutoka sebuleni, kukaa na mwanamke, ku symphasize, na kutoa taarifa taarifa police....
Usinichekeshe tena. Jirani akigombana kwake, wewe ukikaa sebuleni kwako na kusikitika na mke wako utasaidia nini? Alichafanya ndicho alichatakiwa kufanya. Mtu huna ukaribu naye, hujui ni nini imetokea halafu uite polisi?
 
Mf angeenda. Akakutane na kisu kinarushwa, kimpate cha uso.

Angemlaumu nani?
Mke wake angebaki na majuto kwanini kamwambia aende.
Mfano wangeuwana pale, angejiskiaje watu wamepoteza maisha na hakufanya chochote?
 
Alitaka uwe mstari wa mbele kama wale mgambo wanaotangulizwa vitani ili wafe wa kwanza.

Kahama chumba muulize anachotaka, yaani wewe ukafe kisa ugomvi usioujua.

Miaka ya nyuma kidogo hapo mbezi walimpiga mbaba risasi kwenye saa nne usiku, hata polisi hawakuonekana mpaka hali ilipotulia.
 
Back
Top Bottom