exalioth
JF-Expert Member
- Jun 22, 2016
- 2,263
- 3,897
Habari zenu wana JF,
Kuna jambo ambalo limenitokea jana yaani hadi sasa nina hofu ata chakula hakiliki, ninahitaji ushauri kwenu makaka zangu na madada pia.
Kuna jamaa mmoja anaishi na mke na watoto inavyosemekana juzi usiku saa2 kuamkia jana alitoka kazini hakumkuta mke wake alielekezwa na watoto alikoelekea mama yao, akafuatilia akamkuta kwenye boma la nyumba wakiwa wanafanya mapenzi kwa kuwa ilikua giza hakumjua ni nani aliekuwa na mke wake jamaa katimua mbio.
Akamkamata mke akampiga akimuuliza ulikua na nani baada ya kipigo kuzidi akataja "ni yule mwenye saloon ya kike".
Ndugu zangu nimeumia sana nimetajwa mimi mwanamke simjui hanijui, hajawahi hata kuingia saloon kwangu.
Kiufupi mimi ni kijana miaka 21 nina saloon ya kike kiukweli mama mzima kanifanyia kitendo cha kikatili. Mume wake jana alipelekwa polisi, kinachoniuma kila mtu kitaa ananiambia kuwa mimi walinikosakosa ugoni nikakimbia.
Sina raha kwa kweli nipeni msaada wa mawazo yenu na ushauri nina maswali mengi kichwani kuna nini kati ya mimi na yaye kitaa kizima ameamua kunipa beef na mme wake nilishamkosea nini?
Nashindwa nimalizie wapi asanteni karibu kwa mawazo yenu.
Kuna jambo ambalo limenitokea jana yaani hadi sasa nina hofu ata chakula hakiliki, ninahitaji ushauri kwenu makaka zangu na madada pia.
Kuna jamaa mmoja anaishi na mke na watoto inavyosemekana juzi usiku saa2 kuamkia jana alitoka kazini hakumkuta mke wake alielekezwa na watoto alikoelekea mama yao, akafuatilia akamkuta kwenye boma la nyumba wakiwa wanafanya mapenzi kwa kuwa ilikua giza hakumjua ni nani aliekuwa na mke wake jamaa katimua mbio.
Akamkamata mke akampiga akimuuliza ulikua na nani baada ya kipigo kuzidi akataja "ni yule mwenye saloon ya kike".
Ndugu zangu nimeumia sana nimetajwa mimi mwanamke simjui hanijui, hajawahi hata kuingia saloon kwangu.
Kiufupi mimi ni kijana miaka 21 nina saloon ya kike kiukweli mama mzima kanifanyia kitendo cha kikatili. Mume wake jana alipelekwa polisi, kinachoniuma kila mtu kitaa ananiambia kuwa mimi walinikosakosa ugoni nikakimbia.
Sina raha kwa kweli nipeni msaada wa mawazo yenu na ushauri nina maswali mengi kichwani kuna nini kati ya mimi na yaye kitaa kizima ameamua kunipa beef na mme wake nilishamkosea nini?
Nashindwa nimalizie wapi asanteni karibu kwa mawazo yenu.