Ugoni bila kutenda nimeumia sana

Ugoni bila kutenda nimeumia sana

exalioth

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2016
Posts
2,263
Reaction score
3,897
Habari zenu wana JF,

Kuna jambo ambalo limenitokea jana yaani hadi sasa nina hofu ata chakula hakiliki, ninahitaji ushauri kwenu makaka zangu na madada pia.

Kuna jamaa mmoja anaishi na mke na watoto inavyosemekana juzi usiku saa2 kuamkia jana alitoka kazini hakumkuta mke wake alielekezwa na watoto alikoelekea mama yao, akafuatilia akamkuta kwenye boma la nyumba wakiwa wanafanya mapenzi kwa kuwa ilikua giza hakumjua ni nani aliekuwa na mke wake jamaa katimua mbio.

Akamkamata mke akampiga akimuuliza ulikua na nani baada ya kipigo kuzidi akataja "ni yule mwenye saloon ya kike".

Ndugu zangu nimeumia sana nimetajwa mimi mwanamke simjui hanijui, hajawahi hata kuingia saloon kwangu.

Kiufupi mimi ni kijana miaka 21 nina saloon ya kike kiukweli mama mzima kanifanyia kitendo cha kikatili. Mume wake jana alipelekwa polisi, kinachoniuma kila mtu kitaa ananiambia kuwa mimi walinikosakosa ugoni nikakimbia.

Sina raha kwa kweli nipeni msaada wa mawazo yenu na ushauri nina maswali mengi kichwani kuna nini kati ya mimi na yaye kitaa kizima ameamua kunipa beef na mme wake nilishamkosea nini?

Nashindwa nimalizie wapi asanteni karibu kwa mawazo yenu.
 
duuuh pole sana mkuu isije ikawa ni mbinu za kibiashara wakufukuzishe mtaa kijanja,INAONEKANA UNAPATA KIPATO KIZURI AU HUYO DADA ALIKUWA ANAKUPENDA TOKA KITAMBO AKAONA BORA AKUTAJE WEWE HATA KIKISANUKA AHAMIE KWAKO.DAAAH ILA BINAMU WABAYA AISEE SASA AKIKUFANYIA KITU MBAYA NA MZIGO HUJALA ITAKUWAJE.

THEN NENDA KAREPORT KITUO CHOCHOTE CHA POLICE WAKUPE ULINZI LIKITOKEA LA KUTOKEA
 
duh mtafute huyo mke wake muulize kwa nini kakutaja wewe? utakuwa ulikuwa kwenye list yake

Siungi mkono hoja, huyo mwanamke ni shetani na laana hafai kusogelewa.

Mimi nashauri dogo achunguze taratibu kimya kimya mpaka amjue muhusika wa ugoni wa huyo mama hlf awatafutie timing ya kuwaumbua kusafisha jina lake
 
Kaka fanya hivi... karipoti kituo cha polisi.... kuhusu hii ishu..
Usiache ukaumia hivi hiv kwa kes ya kusingiziwa... karipoti pia na kwa mwenye kiti wa mtaa
 
Mmhhh, huyo mama muuaji! Yawezekana kataja kijana wa saloon ya kike lakini nyingine si wewe! Hilo suala katoe taarifa polisi kwani huyo mama anahatarisha maisha yako. Aitwe ahojiwe ili atoe ufafanuzi. Pia hiyo itakuwa kinga kama mumewe ana mpango wa kukudhuru akiamini kuwa ni mgoni wake. Angalizo:- Hii ni kama umesingiziwa. Kama unamkula huyo mama hama huo mtaa haraka. Mke anauma aisee!!!!
 
Nenda kwa Mwenyekiti wa Mtaa muelezee ukweli halisi,muombe yeye na Mtaa mzima Wakulinde na Wakupiganie maana muda wowote utafanyiwa kitu mbaya.

M/kiti akishakuelewa maana mpaka sasa kama ni Makini atakua kashajua ukweli,nendeni Polisi na mkaripoti huko.

Hizo ni hila za Walimwengu tu ndugu.
Pole sana.
 
Hiyo kiukweli ni beef ila cha kufanya mtafute huyo mama akwambie kwanini amekutaja wewe na ingekuwa vzuri mme wake awepo ukiwa unamuhoji
 
Duuuhhhh kazi kweli kweli kweli.

Tumeumbwa wengi, kama jambo hujafanya na "Mwenyezi Mungu" mwingi wa Rehema ni shahidi wa Hilo. Wasiwasi wako nini.

Kilicho muhimu jichunguze tabia yako. Ni vizuri kujijengea "TASWIRA" nzuri kwenye jamii ili hata ukisingiziwa jambo basi jamii ikutetee na si wewe ujitetee.
 
Habari zenu wana jf, kunajambo ambalo limenitokea jana yaani hadi sasa ninahofu ata chakura hakiliki,ninahitaji ushauri kwenu makaka zangu na madada pia,

Kuna jamaa mmoja anaishi na mke na watoto inavyo semekana juzi usiku saa2 kuamkia jana alitoka kazini hakumkuta mke wake alielekezwa na watoto alikoelekea mamayao, akafuatilia akamkuta kwenye boma la nyumba wakiwa wanafanya mapenzi kwakua ilikua giza hakumjua ninani aliekua na mkewake jamaa katimua mbio,

akamkamata mke akampiga akimuuliza ulikua nanani baada ya kipigo kuzidi akataja "niyule mwenye saloon ya kike". ndugu zangu nimeumia sana nimtajwa mimi mwanamke simjui hanijui,hajawai ata kuingia saloon kwangu.

kiufupi mimi nikijana miaka 21 nina saloon ya kike kiukweli mama mzima kanifanyia kitendo cha kikatili. mme wake jana alipelekwa polisi, kinachoniuma kila mtu kitaa ananiambia kua mimi walinikosakosa ugoni nikakimbia,

sina raha kwakweli nipeni msaada wa mawazo yenu naushauri nina maswali mengi kichwani kunanini kati ya mimi na yaye kitaa kizima ameamua kunipa beef na mme wake nilisha mkosea nini.

nashindwa nimalizie wapi asanteni karibu kwa mawazo yenu.
Usije ukajiua bure...
Kama hukufanya hakuna haja ya kuhofu chochote...!!
 
Kwann unakuwa mwoga? Au haukufikia kama jamaa uliishia kumnawa juu juu kwahiyo kaamua kukudondoshea jumba bovu
 
Back
Top Bottom