Uhalisia wa matokeo ya kidato cha nne 2012: Nini kimepelekea kufeli huku?

Uhalisia wa matokeo ya kidato cha nne 2012: Nini kimepelekea kufeli huku?

Heri yetu tuliosomea chini ya miembe miaka ilee

Mkuu kuna shule ina majengo ya madarasa 14, yenye madawati yakutosha, walimu ndiyo usiseme..matokeo yake yanatisha! shule idadi ya 0 ni 203! noma jamani! tena noma.
 
Daaaaaaaah mungu mojaaaa haya serikali dhaifu na elimu ndio washaitia siasa za maji taka. Umaskini na amani wavikai pamoja.
 
Hii inaitwa FUKU(Fundisha kadiri unavyolipwa) unalipwa kidogo fundisha kidogo
 
bila kujua limpatalo binadamu kalichuma mwenyewe kwa mikono yake
kwa uwezo waliokuwa nao wakalishika vilivo baraza la mitihani NECTA, ikawa ni kuwafelisha wasio kuwa wa imani yao,
kwa gharama zozote, wale waliofelishwa wakawa hawana pa kwenda wakawa hawawezi kujenga hoja, kwa sasa sio tu walalamikaji bali wamekuwa wauwaji
 
Kihesa! ipo iringa mjini. wana 0. zipatazo 191! cjui tumlaumu nani hapa.
 
kati ya watahiniwa 397,136 waliofanya mtihani, walifaulu ni 126,847 (daraja i-iv)

daraja I- 1,641 (0.4%)
daraja II- 6,453 (1.6%)
daraja III- 15,426
(3.9%)
daraja IV- 103,327
(26.0%)
daraja 0- 240,903
(60.7%)

sasa wanaoweza kwenda form 5 na 6 ambao ni kuanzia daraja la I-III jumla yao ni 23,520 (elfu ishirini na tatu mia tano na ishirini) kati ya wanafunzi 397,136 (laki tatu tisini na saba elfu mia moja thelasini na sita)
hii ni sawa na 5.9224%.

HII NDIO NCHI YETU NA VIJANA WAJAO WA KUJENGA TAIFA, TUNAWAITA TAIFA LA KESHO.
Data zina matatizo kidogo maana ukijumlisha haifiki 100% inafika 92.6
 
Nimeshangaa sana kwa shule kama hiyo yenye jina kubwa tu kutoa matokeo kama hayo.
Tutafika kweli??
 
Waziri kawambwa ametoa sababu nyepesi za kuanguka kwa ufaulu wa watahiniwa wa kidato cha nne 2012 .
Ametaja
1.ukosefu wa waalimu

2.ukosefu wa maabara

3.ukosefu wa maktaba

mimi nampinga kwani ni shule kama ilboru,mzumbe,kibaha,msalato,minaki,arusha sec, na nyingine nyingi zimefeli kulinganisha na miaka kadhaa iliyopita.

Je maabara,maktaba,vitabu na walimu wa shule hizi wemeenda wapi?
 
Serikali DHAIFU elimu MULUGO
 
  • Thanks
Reactions: awp
Data zina matatizo kidogo maana ukijumlisha haifiki 100% inafika 92.6

Hata mimi nimesikia kupitia Radio One Stereo ya kamba, jumla ya wanafunzi 420, *** (laki nne na ishirini na......) walifanya mtihani. Waliopata daraja la zero, waliofeli, ni 200, **** (laki mbili na.....). Tunaomba mwenye uchambuzi sahihi atuletee.
 
Hii ndio Tanzania bhana...tatizo halipo kwa serikali tatizo ni kwa sisi kuipa hiyo serikali mamlaka halafu watoto wao wanasoma kuleeeeeeeeeee wa kwetu hapa.....Dah Muumba wa mbingu na ardhi tuepushe na balaa lijalo.
 
Wadau mliopo kwenye source hepu tuwekeeni hayo matokeo maana hiyo web ya Serikali ipo busy kinoma
 
Hata mimi nimesikia kupitia Radio One Stereo ya kamba, wanafunzi 420, *** (laki nne na ishirini na......). Waliopata daraja la zero, waliofeli, ni 200, **** (laki mbili na.....). Tunaomba mwenye uchambuzi sahihi atuletee.

nadhani kesho wataleta uchambuzi mzuri au kwenye kuingiza data hapa JF jamaa amesahau tarakimu moja
 
Kweli huku ndio chama kilichoshika hatamu kinakotupeleka?? Basi conclusion ni kwamba level hii ya elimu haina maana kwa ufaulu huu!
 
Back
Top Bottom