Wazifute wakati ndo wamewekeza kwenye ujinga!!!!!!!
Unachokiona na kusikia ni matokeo ya mipango madhubuti ya serikali. Zunguka Nchi nzima kuanzia kaskazini-kusini, mashariki -magharibi, uniambie kama utamkuta mtoto wa kiongozi yeyote wa serikali ya Tanzania anaesoma s.t Kayumba au hata shule za kata. Hii ina maanisha shule za serikali hazina mchungi, zinajiendea zenyewe! Na kwa mantiki hiyo serikali haiwezi kuona umuhimu wa kuboresha elimu kwa shule zake, ili iweje ili hali watoto wao hawasomi huko???
Ili uwe sehemu ya suluhisho, lazima kwanza uwe sehemu ya tatizo. Kwa serikali, elimu kushuka kwa kiasi kikubwa namna hiyo, sio issue kwao. The big issue ni kuiba na kupeleka watoto wao nje wakapate elimu bora na matibabu bora. Watanzania waliowengi watateseka sana na mfumo uliopo kwa leo. Sio chadema wala ccm wenye uwezo wa kuboresha elimu yetu. Nikitazama upande wa pili wa shilingi, hakuna kiongozi yeyote wa upinzani anaesomesha mtoto shule zetu za serikali, hili halina ubishi sababu nao sio sehemu ya matatizo ya Watanzania!!!! Watapiga kelele pale madhara yanapotokea, lakini sio kutatua tatizo.
Watasema, fulani ajiuzulu, fulani apishe uchunguzi.........etc. Lakini swali ni je, kwa nini hawakuyapigia kelele kabla ya matokeo??? Ni ukweli usiopingika kwamba, viongozi wetu wanatafuta cheap popularity sana kutoka kwa watanzania. Ni dhahiri kuwa wanajua mfumo wa elimu yetu ni mbovu na ndio maana watoto wao hawapelekwi shule za kata. Na kwa kujua hilo, wanatambua wazi kuwa matokeo hayataweza kuwa mazuri hata kwa gharama za uchawi!!! Ila wanasubiri bomu likishalipuka, nao wanaibuka kila mtu na jukwaa lake.
Lakini pia kuna swala lingine ambalo lipo wazi kabisa. Mwaka huu mwanzoni, serikali ililazimika kuchelewesha matokeo ya darasa la saba kutokana na kuanguka kwa watoto wetu. Kilichotokea, kila mtu anakijua. Badala ya kupeleka sekondari waliopata vigezo vya kujiunga na sekondari kama sheria inavyosema, wao walilazimika kupunguza alama za ufaulu. Which means idadi ya wajinga imeendelea kujiunga na kidato cha kwanza.
Katika hili wadau tuwe na subira kwani huu ni mwanzo wa matokeo mabaya. Sipendi anguko hili kwa sababu miaka michache ijayo hatutaweza kuwajibu hawa jamaa watakapoamua kujua ni kwa nini elimu imeporomoka kwa kiasi kikubwa na sisi tukanyamza kimya wakati tatizo lilikuwa na dalili toka mwanzo!!!!!!!!!!
Mleta mada, kwa kifupi sana; ccm haiwezi kuzifuta shule za kata kwani wao wanafurahia haya matokeo. Kwao wanapendezwa sana na watu wanapokuwa wajinga sababu ni rahisi sana kuwaburuza na kuwarubni na kanga, pombe, t-shirt................etc.
Hawa watu miaka ijayo hawana kazi, so hata wakinunuliwa kwa 5000 ili wawape kura inawezekana kabisa.