Uhamiaji hawaoni aibu kutoa passport laki mbili kwenye nchi yenye watu milioni 55?

Ni mambo ya ajabu sana haya.
Kwani siwezi kuwa na pesa zangu nikahamua niende kutembea kama kutalii ughaibuni au kuangalia na kujifunza kuhusu masoko ya bidhaa flani au fursa flani ya kibiashara au ajira?
Tena zako na umeshalipa Kodi zako zote .Mfano umepokea mshahara Mfano public au private sector Chao Serikali kupitia TRA walishachukua kwa Nini kilichobaki usijirushe nacho nje ya nchi ukitaka?
 
Rwanda passport inspatikana ndani ya massaa matatu.macimum toka uwakilishe ombi lako
Nchi ndogo hiyo watu wamebanana, serikali inatafanya jitihada kuwaondo raia wake kiaina.
 
wewe jamaa ni pimbi sana kutengeneza kile kijitabu chenye vikaratasi vichache vile unasema kuna unyeti na gharama sasa
Tatizo siyo karatasi bali teknolojia iliyojificha kwenye hizo karatasi.
 
Ukienda uhmiaji kutaka passport wanakuuliza unatakwa kwenda wapi? Hapo ndipo utajua kuwa ili upate passport Tanzania lazima uwe na safari.
 
Uko sahihi!
 
Hatuwezi kuboresha hili mkuu? Tuka increase access?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akili zingine duh. Una mawazo kama ya Babu yangu aliyefariki 1927.
 
Misifa ya kijingajinga tu imejaa....
 
Credit to Uhamiaji though. Basically hawataki kuwe na msululu mreeeeefu wa kila "tom and Jerry" anayetaka kuomba passport bila safari ya uhakika, in the process kuwacheleweshea wenye safari za ukweli. Kwa uzoefu wangu, hilo swali la "unaomba passport kwenda wapi" unaweza kulijibu kirahisi tu kwamba "ninajiandaa kwenda Kenya/Uganda/Rwanda/Burundi" kwa safari binafsi. End of story. Unapowapa majibu ya mashaka kwamba unataka passport sijui kwenda shule Canada, hapo unawapa nafasi ya kukudai vitu vingine kama invitation/admission letters etc.

Sidhani kama kuna mtu ambaye ameshanyimwa passport kwa kushindwa kujibu vizuri swali linalohusu lengo la kuomba passport.
 
Tangu ujiunge humu leo umeongea point.siku zingine ulikuwa unavuta Jani chooni??
 
Uhamiaji ujinga mtupu mkuu, Imagine mtu una kitambulisho cha NIDA halafu bado wanataka wakuhakiki kama ni raia, si upumbavu uliopitiliza huo. HALAFU KULE KUMEJAA URASIMU SANA WANAKUWEKEA VIKWAZO ILI UWAPE CHOCHOTE NDIO LAKO LIFANIKIWE. Sasa unaomba passport unaulizwa ya nini? Ingekuwa watu hatuhitaji kupaa majuu unawambia tu nahitaji passport nikajiunge AL SHAABAB.
 
Huna passport we mchawi
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakikuuliza ya nini? unawajibu ya kunywea bia
 
Tupe mchanganuo wa iyo passport moja kutengeneza

 
mkuuu una akili za kizungu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya yote ni matokeo ya elimu za kukaririshwa.

Hili suala la kuwapa Uhuru wananchi kutoka nje ya nchi,ni moja ya njia ya kuongeza kipato na ujuzi mbali mbali kwa raia.

Fikiria hata pale kijijini tu,familia ya watu wanaosafiri sana ndiyo angalau ina maendeleo kuliko wale wasio safiri kabisa

Watu huchuma mbali na kuleta kwao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…