Uharaka unahitajika kwenye maamuzi ya CHADEMA

Uharaka unahitajika kwenye maamuzi ya CHADEMA

Kuna chawa ndani ya chama wanawajaza hofu wenzao kuwa mbowe akiachia uongozi chama kitanunuliwa na ccm.

Wanataka tuamini kuwa hakuna mwenye uwezo kuongoza, isipokuwa mbowe.

Wanasahau kuwa naye ni mwanadamu, na wakati wake ukifika ataondoka duniani.
Kati ya Uongozi wa Edwin Mtei, Bob Makani na Freeman Mbowe ni Mwenyekiti yupi aliyeipa mafanikio Chadema?
 
Kuna chawa ndani ya chama wanawajaza hofu wenzao kuwa mbowe akiachia uongozi chama kitanunuliwa na ccm.

Wanataka tuamini kuwa hakuna mwenye uwezo kuongoza, isipokuwa mbowe.

Wanasahau kuwa naye ni mwanadamu, na wakati wake ukifika ataondoka duniani.

Katika dhana za kipuuzi ni hii ya kusema kiongozi fulani ndio nguzo ya chama. Matokeo yake ndio haya kiongozi anakaa madarakani zaidi ya miaka 10, hata yale mazuri yake yanaanza kuharibika.

Kwa utafiti wangu niliofanya ambao sio rasmi, kiongozi yoyote wa kuchaguliwa akikaa madarakani zaidi ya miaka 10, ubora wake huanza kupungua na mazuri yake hufifia. Mfano wa viongozi hao ni
  1. Nyerere
  2. Moi
  3. Mugabe
  4. Gadaffi
  5. Paul Biya
  6. Museveni
  7. Albashir
  8. Saddam Hussein
Kiongozi kama Mandela amebaki bora na kuwa kiongozi mzuri kwani hakukaa madarakani mrefu. Mbowe alipaswa kukaa pembeni baada ya blunder ya Lowassa, au kama hakuona sawa kuachia baada ya kosa lile, basi hakupaswa tena kugombea uwenyekiti wa CDM uchaguzi uliopita. Mbowe alishafanya vizuri miaka yake 10 ya kwanza, alipoanza kukaa zaidi ya miaka 10, ndio anafikia huku ambapo anakosa ufanisi, na kuishia kuingia kwenye miafaka sijui maridhiano ya kihuni.
 
Mbowe alipaswa kukaa pembeni baada ya blunder ya Lowassa, au kama hakuona sawa kuachia baada ya kosa lile, basi hakupaswa tena kugombea uwenyekiti wa CDM uchaguzi uliopita.
Mawazo mazuri sana; bahati mbaya ukija na mawazo kama hayo ndani ya chama unaonekana msaliti. Utakuwa na bahati sana usipoundiwa zengwe la kufukuzwa uanachama.
 
Mawazo mazuri sana; bahati mbaya ukija na mawazo kama hayo ndani ya chama unaonekana msaliti. Utakuwa na bahati sana usipoundiwa zengwe la kufukuzwa uanachama.

Sijui huko chamani wanafanyaje, lakini sisi huku mitandaoni tunawapa ukweli wao. Tunaheshimu mchango wao kwa walipokifikisha chama, lakini hatuna nafasi ya kuendekeza udhaifu. Tunaweza kufanya siasa bila kutegemea chama chochote, kwani hicho chama kilikuwa platform rasmi tu ya kufanyia siasa.

Ni muda sahihi wa Mbowe kupisha mawazo mapya, maana kafikia mwisho, asijifiche kwenye propaganda za CCM kuwa Mbowe akae pembeni. Tunajua propaganda ni zipi, na ukweli ni upi.
 
Chadema walikanyaga chechele 2015 , shujaa mwendazake apumzike kwa amani.
 
Katika dhana za kipuuzi ni hii ya kusema kiongozi fulani ndio nguzo ya chama. Matokeo yake ndio haya kiongozi anakaa madarakani zaidi ya miaka 10, hata yale mazuri yake yanaanza kuharibika.

Kwa utafiti wangu niliofanya ambao sio rasmi, kiongozi yoyote wa kuchaguliwa akikaa madarakani zaidi ya miaka 10, ubora wake huanza kupungua na mazuri yake hufifia. Mfano wa viongozi hao ni
  1. Nyerere
  2. Moi
  3. Mugabe
  4. Gadaffi
  5. Paul Biya
  6. Museveni
  7. Albashir
  8. Saddam Hussein
Kiongozi kama Mandela amebaki bora na kuwa kiongozi mzuri kwani hakukaa madarakani mrefu. Mbowe alipaswa kukaa pembeni baada ya blunder ya Lowassa, au kama hakuona sawa kuachia baada ya kosa lile, basi hakupaswa tena kugombea uwenyekiti wa CDM uchaguzi uliopita. Mbowe alishafanya vizuri miaka yake 10 ya kwanza, alipoanza kukaa zaidi ya miaka 10, ndio anafikia huku ambapo anakosa ufanisi, na kuishia kuingia kwenye miafaka sijui maridhiano ya kihuni.
Umeandika ukweli mtupu
 
2015 isingekuwa kupokea wale mamluki wa CCM chadema ingekuwa na nguvu kubwa sana katika siasa za Tanzania
 
Kama ni hivyo na kwa maana baada ya pale chadema ilikufa , kwanini mmezuia siasa za majukwaani ?
Haikufa, na haìwezi kufa as long as wafuasi wasioweza kufikiri wanaongezeka kila siku.

Mnatembelea kwenye migongo ya wajinga sawa na ccm. Hamna tofauti wala hakuna unafuu utakaopatikana ccm wakiondoka akaingia chadema. Wote matapeli.
 
Kama ni hivyo na kwa maana baada ya pale chadema ilikufa , kwanini mmezuia siasa za majukwaani ?
ili wajifunze na kujipanga maana hawajui au wamesahau malengo yao kama chama cha siasa.
 
Hivi dalili za chama kufa huwa zikoje, kama siyo hizi zilizoelezwa na mleta bandiko? Au mnasubiri mpaka mkutano mkuu wa chama utamke kuwa chama kimekufa ndiyo mtaamini kuwa chadema is no more?
Vyama vyote vilivyokufa (nccr, cuf) vilianza hivyo hivyo, mara wanatwangana ngumi kwenye vikao, vikao vya kikatiba haviitishwi, nk.
Chadema haiwezi kuepuka.
 
Katika dhana za kipuuzi ni hii ya kusema kiongozi fulani ndio nguzo ya chama. Matokeo yake ndio haya kiongozi anakaa madarakani zaidi ya miaka 10, hata yale mazuri yake yanaanza kuharibika.

Kwa utafiti wangu niliofanya ambao sio rasmi, kiongozi yoyote wa kuchaguliwa akikaa madarakani zaidi ya miaka 10, ubora wake huanza kupungua na mazuri yake hufifia. Mfano wa viongozi hao ni
  1. Nyerere
  2. Moi
  3. Mugabe
  4. Gadaffi
  5. Paul Biya
  6. Museveni
  7. Albashir
  8. Saddam Hussein
Kiongozi kama Mandela amebaki bora na kuwa kiongozi mzuri kwani hakukaa madarakani mrefu. Mbowe alipaswa kukaa pembeni baada ya blunder ya Lowassa, au kama hakuona sawa kuachia baada ya kosa lile, basi hakupaswa tena kugombea uwenyekiti wa CDM uchaguzi uliopita. Mbowe alishafanya vizuri miaka yake 10 ya kwanza, alipoanza kukaa zaidi ya miaka 10, ndio anafikia huku ambapo anakosa ufanisi, na kuishia kuingia kwenye miafaka sijui maridhiano ya kihuni.
Momentum of Lowasa ndio iliwapa wabunge wengi hadi wahuni kama Lijualikali nao wakapata ubunge kirahisi tu.

Sijui huwa mnatumiaga vigezo gani kujuwa mchango wa mtu ni nini?
 
Kuna chawa ndani ya chama wanawajaza hofu wenzao kuwa mbowe akiachia uongozi chama kitanunuliwa na ccm.

Wanataka tuamini kuwa hakuna mwenye uwezo kuongoza, isipokuwa mbowe.

Wanasahau kuwa naye ni mwanadamu, na wakati wake ukifika ataondoka duniani.
Mbowe alikuwa na umuhimu wake katika chama kwa wakati maalum. Sasa nyakati ni tofauti, hawezi kuendelea kuwa na umuhimu ule ule katika nyakati mbalimbali.
 
Haikufa, na haìwezi kufa as long as wafuasi wasioweza kufikiri wanaongezeka kila siku.

Mnatembelea kwenye migongo ya wajinga sawa na ccm. Hamna tofauti wala hakuna unafuu utakaopatikana ccm wakiondoka akaingia chadema. Wote matapeli.
Wachawi nchi nzima walilipwa Chadema ife , lakini wapi !!
 
Kwenye hili la kuchelewa kuchukua maamuzi nakubaliana na ww kabisa, nimewahi kuhoji humu. Pia suala la kuzingatia muda hata kwenye press zao ni tatizo sugu. Kitengo cha habari ni kama kimekufa kwani naona hata website iko down!

Mambo haya na madhaifu mengine kadhaa ndio yanapelekea mimi kutaka Mbowe akae pembeni kama mwenyekiti ili aingie mtu mpya na mbinu mpya, kwani kwa sasa ni sahihi kabisa kwake kukaa pembeni
Kubadilisha sura za viongozi huku tabia za wanachama zikiendelea kubaki zile zile ni sawa na kupoteza muda, hakuna maana.

Kwangu ni bora tungeanza kwanza kubadilisha mindset za wapenzi na wanachama, wajue haki zao na jinsi ya kuzipigania ili kuyafikia malengo, ndipo tuje kuwaza kubadilisha sura za viongozi.

Hili wazo la kukimbilia kubadilisha sura za viongozi pekee tusiwe tunaliimba tu kama wimbo, kufanya hivyo kwangu huliona kama wazo la kibinafsi, tunakaa pembeni na kuona madhaifu ya viongozi kila wakati, huku madhaifu yetu tukiwa hatuyaoni.

Kwa hii mentality, tutaendelea kubadilisha sura za viongozi miaka yote, lakini tatizo letu la msingi hatutakaa tulimalize, tutaendelea kusumbuliwa na CCM mpaka tuamke, wala sio kubadilisha sura za viongozi, jambo ambalo kwangu ni dogo sana.
 
Back
Top Bottom