Uhujumu Uchumi: Idd Simba na wenzake waachiwa huru katika kesi ya kuhujumu shirika la UDA

Uhujumu Uchumi: Idd Simba na wenzake waachiwa huru katika kesi ya kuhujumu shirika la UDA

DPP akili yake nina Shaka nayo,weledi wake pia ninahofu nao. Elimu yake nayo naitilia Shaka mno! Kwa mabilioni yaliyoibwa UDA alafu ufute kesi kiulaini hivi ....you must be kiding!.

...........ma PhD na mdigiri kibao, maamuzi ya ngumbaru !
 
Siku zote ukweli unabaki kuwa kweli na siku zote MAHAKAMA ZINATAKA USHAHIDI PASI NA SHAKA ILI MTU ATIWE HATIANI.

Hongera mchumi mahiiri unaetambulika kimataifa Mzee Wetu Iddi Mohamed Simba.
 
Nimesoma na kurudia mara mbilimbili lakini sijashangaa; siwezi kushangaa kwa sababu hakuna cha kushangaza.
Kisidumu Chama Cha Mapinduzi!
Hata kwa wana CCM this is a disgrace!
Mtu anaye divert hela ya umma kuingia mfukoni mwake anashindaje on technicalities?

Na hicho chama na wizi kitadumu vipi?
 
Du , hela ya umma anaingiza kwenye akaunti yake , halafu hana shitaka la kujibu?
Ufisadi at its highest.
Ningekuwa Hosea naenda likizo bila malipo!!!

Wapi imesemwa ni haramu pesa kupitia kwenye akaunti yake. kama hapakuwa na akaunti ya kuaminika, kwa nini isipitie kwake? Simba kamwibia nani? acheni majungu.......................
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam leo hii imemwachiria huru Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), Idd Simba pamoja na Mkurugenzi wa Bodi hiyo ambaye alikuwa Diwani wa Kata Sinza (CCM), Salum Mwaking’inda vile vile Meneja Mkuu wa shirika hilo Victor Milanzi na Mkurugenzi wa Kampuni ya Simon Group , Simon Kisena waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi wa shirika hilo.

Mahakama imewaachia huru washitakiwa kwa sababu Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk Eliezer Feleshi alliwasilisha hati ya kutokuwa na haja ya kuendelea kuwashitaki washitakiwa hao chini ya kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002.

Simba anayetetewa na wakili maarufu nchini Alex Mgongolwa walifikishwa na mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Mei 27 28 mwaka jana wakikabiliwa na makosa ya kula njama, matumizi mabaya ya madaraka na kughushi na hujumu uchumi.

Hivyo kuanzia sasa, washitakiwa hao wapo huru.





 
Hizi ndiyo habari zinazowafurahisha watawala wetu. Maana kwenye hiyo michongo ya KIFISADI nao wamo.
 
mahakama ya hakimu mkazi kisutu dar es salaam leo hii imemwachiria huru mwenyekiti wa bodi ya shirika la usafiri dar es salaam (uda), idd simba pamoja na mkurugenzi wa bodi hiyo ambaye alikuwa diwani wa kata sinza (ccm), salum mwaking'inda vile vile meneja mkuu wa shirika hilo victor milanzi na mkurugenzi wa kampuni ya simon group , simon kisena waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi wa shirika hilo.


Mahakama imewaachia huru washitakiwa kwa sababu mkurugenzi wa mashitaka (dpp), dk eliezer feleshi alliwasilisha hati ya kutokuwa na haja ya kuendelea kuwashitaki washitakiwa hao chini ya kifungu cha 91(1) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai ya mwaka 2002.

simba anayetetewa na wakili maarufu nchini alex mgongolwa walifikishwa na mahakamani hapo kwa mara ya kwanza mei 27 28 mwaka jana wakikabiliwa na makosa ya kula njama, matumizi mabaya ya madaraka na kughushi na hujumu uchumi.

Hivyo kuanzia sasa, washitakiwa hao wapo huru.






...........habari hii ilishatoka jana dk. 10 baada ya tukio....
 
Wanafungwa wale wezi wa kuku tu; wezi papa kama wakina Idd Simba, Yona,Mramba etc wao kesi zao zinatajwa mahakamani kama geresha kwa wadanganyika!!! Serikali ya Vasco Dagama haifungi mafisadi bali inawapandisha vyeo kama alivyofanyiwa SHIMBO na haitashangaza Idd Simba nae akapewa ubalozi kwani hawa wanashirikiana na mkweree kuiibia nchi.
 
Hii ndiyo Bongo na mambo, vituko vyake ni zaidi ya utalii!
 
Gazeti la Mwananchi la leo limeripoti kuwa Mwenyekiti wa bodi ya UDA, Bw. Iddi Simba na wenzake wamefutiwa kesi hiyo namba 3/2012 ya Uhujumu Uchumi. Katika kesi hiyo Iddi Simba na wenzake walikuwa wanashitakiwa kwa ubadhilifu ulioisababishia UDA hasara ya shilingi Bilioni 8.4. Kesi hiyo imefutwa na DPP kwa maelezo kuwa hakusudii kuendelea kuwashitaki washitakiwa hao.

Mawazo yangu.
Nakumbuka Kesi hii ilifunguliwa na PCCB dhidi ya Iddi Simba na wenzake kufuatia hasara tajwa hapo juu. PCCB pengine walikuwa na mashahidi wa kuthibitisha tuhuma hizo Mahakamani ndio maana kesi ikafunguliwa. Ajabu sasa kabla haijaanza kusikilizwa DPP kaifuta, na mamlaka ya DPP hayahojiwi na mtu yeyote kwa mujibu wa Katiba na Sheria zetu.
Sasa nimemuelewa Dr. Edward Hoseah alipowalaumu wabunge wiki iliyopita kwamba wamempa mamlaka ya kupambana na rushwa lakini wamemnyang'anya kwa upande mwingine. Kabisa kwa mtaji huu amefungwa mikono. Ni mawazo yangu tu lakini.
 
Gazeti la Mwananchi la leo limeripoti kuwa Mwenyekiti wa bodi ya UDA, Bw. Iddi Simba na wenzake wamefutiwa kesi hiyo namba 3/2012 ya Uhujumu Uchumi. Katika kesi hiyo Iddi Simba na wenzake walikuwa wanashitakiwa kwa ubadhilifu ulioisababishia UDA hasara ya shilingi Bilioni 8.4. Kesi hiyo imefutwa na DPP kwa maelezo kuwa hakusudii kuendelea kuwashitaki washitakiwa hao.

Mawazo yangu.
Nakumbuka Kesi hii ilifunguliwa na PCCB dhidi ya Iddi Simba na wenzake kufuatia hasara tajwa hapo juu. PCCB pengine walikuwa na mashahidi wa kuthibitisha tuhuma hizo Mahakamani ndio maana kesi ikafunguliwa. Ajabu sasa kabla haijaanza kusikilizwa DPP kaifuta, na mamlaka ya DPP hayahojiwi na mtu yeyote kwa mujibu wa Katiba na Sheria zetu.
Sasa nimemuelewa Dr. Edward Hoseah alipowalaumu wabunge wiki iliyopita kwamba wamempa mamlaka ya kupambana na rushwa lakini wamemnyang'anya kwa upande mwingine. Kabisa kwa mtaji huu amefungwa mikono. Ni mawazo yangu tu lakini.

only in foolish country like yours, nchi zingine upumbavu wa namna hii huwez kuukuta.

suala lake moja la kuhujumu uchumi wa nchi pale alipotoa akaunti yake zilipwe pesa za uda na simon Group lilikuwa kosa kubwa sana kisheria la kumpa zawadi ya kifungo mwizi huyu na ikumbukwe huu ulikuwa mkakati wa kuhujumu makampuni yaliyokuwa yanaidai uda, so walipima na kuona iwapo simon Group atailipa pesa ya manunuzi ya uda kupitia acc yake basi pesa hiyo itamezwa na deni lilipo as standing order, wakaamua watumie accouny ya Iddi Simba, sasa leo mnasema hakusudii kuendelea kumshitaki huu si wehu! io siku hawa wote wataenda mahakamani!wanajidanganya tu.
 
Na kama hakuna ushahidi wa kutosha basi DPP angeiachia Mahakama ndio iseme hivyo kuwa ushahidi hautoshi. Vitu vingine vinakera sana.
 
Na kama hakuna ushahidi wa kutosha basi DPP angeiachia Mahakama ndio iseme hivyo kuwa ushahidi hautoshi. Vitu vingine vinakera sana.

Ikifutwa na mahakama kuna gharama za kusafisha jina la mtu na ni hela ya mlipakodi ingetumika!
 
Tajiri hafungwi duniani labda mbinguni tu.
 
Nilikua nashangaa, kuna kuna mbwea au mbwa koko gani anaweza kumfunga mzee wa SAIGON...
 
Kwangu mimi hawali ya yote, nadhani kuna mkanganyiko wa kisheria katika suala hili; nijuavyo mimi hii kesi inahusu hujuma ya uchumi, na hivyo baada ya DPP kutoa baraka zake kesi hiyo ilikuwa inatakiwa iendeshwe na Taasisi ya kuzuia rushwa, katika hali hiyo, sioni namna ambapo DPP huyo, anaweza kuingilia mchakato wa uendeshaji wa hiyo kesi. Lakini zaidi ya hapo Watanzania wana haki ya kujua ni nini hatma ya fedha zao zilizowekwa kwenye akaunti ya Iddi Simba. Nasema hivyo kwasababu maelezo yaliyotolewa hapo awali yalikuwa yakikinzana; Kwa mujibu wa aliyekuwa Meneja Mkuu wa UDA fedha hiyo ililipwa katika akaunti ya Simba kuepusha hisimezwe na O.D iliyokuwa ikidaiwa kampuni hiyo; lakini kwa mujibu wa Simba mwenyewe, malipo yaliyowekwa kwenye akaunti yake ni ujira wake kutokana na ushauri elekezi alioutoa kwa wanunuzi wa UDA.
 
Back
Top Bottom