Uhuru Day: Tuliposahau Hadhira ilikuwa pia na Wageni Waalikwa

Uhuru Day: Tuliposahau Hadhira ilikuwa pia na Wageni Waalikwa

Kupiga hatua ni pamoja na kujifunza kutokana na makosa.

Kwa kuangalia tukio la jana, umuhimu wa kuwa na moderators (@mods) unaonekana wazi.

Pana haja ya kuwaandaa moderators katika hadhira kutegemeana na wageni waalikwa.



Kwa kweli kubeza majanga ya Nzige wakati waathirika wapo kulikuwa fyongo.

Kubeza vita na machafuko kwingine wakati waathirika wapo hakukuwa sawa.

Kujinasibu na kina Joe Biden nako ilikuwa ni kituko kingine mbele za wageni wetu.

Funga kazi hili la kushangaana ati kuwa baba zetu ndiyo wasafiri.

Mbele za wageni wetu?

Hiiiiii bagosha!

Hawa watu wanapata mlo wanapopewa platform kwenye shughuli kama hizi.Ila sio kila shughuli lazima waalikwe. Wengi hawajitambui
 
Lengo la kuwaalika ni kisiasa zaidi.

Imekaa katika kujitafutia uhalali hata kwa agenda zisizokuwa na kichwa wala miguu.
Hawa wote wanachumia tumboni. Ndio maana wakati wa uchaguzi wote dugu moja. Ila sidhani kama kichwani wana uwezo wa kueleza mambo ya maana kwa watu wa aina ile walioalikwa
 
Hawa wote wanachumia tumboni. Ndio maana wakati wa uchaguzi wote dugu moja. Ila sidhani kama kichwani wana uwezo wa kueleza mambo ya maana kwa watu wa aina ile walioalikwa

Kimsingi hawakupaswa kupewa nafasi pale wakiwamo pia wa chipukizi.

Ni wazi kuwa Kenyatta, Nyusi, Asumani, Kagame na waalikwa wengine hawakuwa wamekuja kwa ajili ya mambo miscellaneous.

Au Moderator ni JF peke yake?
 
Wametia aibu sana kuwaweka hao makatuni
Masanja na mwenzake
Nchii mambo muhimu wanapenda ingiza mambo yasiyokuwa na mantiki
Hata shilole si ajabu angepewa nafasi hapo

Ova
 
Wametia aibu sana kuwaweka hao makatuni
Masanja na mwenzake
Nchii mambo muhimu wanapenda ingiza mambo yasiyokuwa na mantiki
Hata shilole si ajabu angepewa nafasi hapo

Ova

IMG_20211211_115457_124.jpg
 
Sherehe zijazo najua watatuletea Ambaluti Kama mshehereshaji ccm ni kikundi Cha hovyo sana.
 
Kitendo alichokifanya Masanja ni Kibaya sana, ni utovu wa nidhamu kwa Wanyarwanda. Mimi binafsi nimechukizwa na kauli hii isiyo ya kistaarbu. Kwa niaba ya Watanzania ninawaomba radhi Wanyarwanda kwa kauli hii ya kijinga kabisa.

Naitaka serikali ya Tanzania iombe radhi na iwe inapitia maudhui ya kila mzungumzaji mbele ya hadhara wasije wakatuletea shida
 
Ni fundisho kubwa sana hili. Kuweka watu wa MIZAHA au COMEDIAN kwenye shughuli nyeti kama ile ni shida sana. Ipo siku ataalikwa mkutano wa dini halafu amuambie Padri ajadiliane na wenzake kuhusu KITIMOTO.
 
Sherehe zijazo najua watatuletea Ambaluti Kama mshehereshaji ccm ni kikundi Cha hovyo sana.

Ingependeza zaidi. Si umeona ya Hamisa wa Remmy mtoto wa kigogo?
 
Ni fundisho kubwa sana hili. Kuweka watu wa MIZAHA au COMEDIAN kwenye shughuli nyeti kama ile ni shida sana. Ipo siku ataalikwa mkutano wa dini halafu amuambie Padri ajadiliane na wenzake kuhusu KITIMOTO.

Kujifunza hao mbona heri kenge kusikia?
 
Back
Top Bottom