Uhuru na Haki Haiwezi ikaleta Amani na Maendeleo ya Watu; Amani na Maendeleo ya Watu ni Tunda la Uhuru na Usawa

Uhuru na Haki Haiwezi ikaleta Amani na Maendeleo ya Watu; Amani na Maendeleo ya Watu ni Tunda la Uhuru na Usawa

Zero:

Kwa sababu;

Mosi, Haki inahusiana na uhuru. Maana yake ni hivi, ukiwa na huru unaweza ukasema pasipo kusimamiwa wala kuelekezwa nini cha kusema, na hivyo una kuwa na haki ya kusema pasipo kuingiliwa.

Pili, tunafahamu haki ilikuwepo hata wakati wa mkoloni. Hivyo tulitafuta uhuru ili tupate usawa. Kwamba mtu mwafrika atakuwa sawa na mtu mweupe, mtu masikini atakuwa sawa na mtu tajiri. Na hakika palipo na usawa pana amani ya kutosha.
mkuu sijaelewa apo,kama haki ilikuwepo tangu mkoloni why tulitafuta uhuru ili hali " Haki inahusiana na uhuru"
 
Bujibuji:

Moja ya ladha ya utawala wa sheria, huwa kuna kuwepo na uhuru wa kuzungumza wenye kudhibitiwa kwa mujibu wa sheria. Na hivyo kila utakachoongea ni lazima kiwe na ushahidi na huo ndio uhuru wa kuongea. Leta ushahidi hapa hadharani... au kama unafanya propaganda nikuache uendelee na kazi yako hiyo ya propaganda.
Kwa hiyo huujui mkasa wa nyumba za Serikali?
 
mkuu sijaelewa apo,kama haki ilikuwepo tangu mkoloni why tulitafuta uhuru ili hali " Haki inahusiana na uhuru"
Haki ilikuwepo hata wakati wa uhuru. Kuna tukio moja liliwahi kumkuta Baba wa Taifa Hayati Mwl. J. K. Nyerere, 1942 wakati akiwa Tabora Boys... Alianzisha vuguvugu kupitia mdahalo wa kutaka walimu wa kiafrika wapatiwe nyumba za karibu na shule kama ambavyo walimu wa kizungu walikuwa wakipatiwa. Na yeye aliita ni haki ya walimu waafrika kwa kuwa ni walimu kama walimu wazungu. Lakini kumbe ni kitu asichokifahamu kuwa kwenye mikataba yao ya kazi wale walimu waafrika walifahamu kuwa haki yao ilikuwa si kuishi katika nyumba zile za shule, hiyo ilikuwa ni haki ya walimu wazungu.

Sasa baada ya kugundua hilo na hasa alipofika katika siasa za TAA, alifahamu kuwa Tanganyika tulikuwa hatuna usawa. Kwamba mzungu alipewa nafasi ya juu kuliko mtanganyika, na hivyo mzungu alikuwa na haki iliyozidi haki ya mtanganyika. Kwa hiyo hitaji la usawa na kuacha kunyonywa na wazungu ndio likawa hitaji la kitaifa na hata tukapata uhuru 1961, ambapo baada ya Tanganyika kuwa Jamhuri mtanganyika alihesabiwa kuwa mtu sawa na Muasia pamoja na mzungu.
 
Kinoamiguu:

Nazungumza kuhusu ujamaa na kujitegemea. Nazungumza kuhusu usawa na uhuru. Nazungumza kuhusu usawa katika mambo ya muhimu juu ya maisha ya watu, ikiwa ni pamoja na Kodi kwa wafanyabiashara, huduma za upatikanaji wa elimu bora, afya bora na maji bila kusahau miundombinu ya uhakika na bora. Tunataka kuwepo na upangiliaji mzuri wa makazi katika maeneo yote nchini, sio tu kwa maeneo ya osterbay, masaki, gangilonga n.k ila ni maeneo yote.

Ujamaa haupendelei watu wavivu ila inathamini na kuheshimu kazi ya kila mtu ambayo anaifanya. Ujamaa na kujitegemea inajenga usawa na uhuru kwa watu wakulima na wafanyakazi. Ni lazima ufanye kazi uishi kwa kipato chako. Heshima ya binadamu haipatikani kwa kuwa na gari zuri, jumba zuri, au mshahara mnono. Heshima ya binadamu inapatikana kwa kupata huduma za muhimu ikiwa ni afya bora na chakula bora, elimu bora na maji safi na salama. Na ndio kwa sababu hiyo serikali inasisitiza usawa na uhuru.

Kumbuka kumchagua Rais Dkt. Joseph Pombe Magufuli na CCM ili iyaendeleze hayo kwa miaka Mitano mengine.
Unaongea mambo meeeengi japo hujatwambia nani aliyesababisha hayo mambo yasiwepo mpaka leo nusu karne baada ya uhuru? Mkuu nchi hii haijawahi KUTAWALIWA na chama kingine zaidi ya hiking chama cha Wezi, wanafiki na waongo!
Hivi kiongozi mwadilifu anawezaje kutunga SHERIA INAYOZUIYA ASISHITAKIWE AWAPO/ ASIPOKUWEPO MADARAKANI?
Ivi mtu aliyekuwepo kiongozi kwa miaka yote leo anakuaje kusema kwamba yy ni wa mfano na yale yote yaliyotokea huko nyuma hakuwa sehemu YAke?
Unadhani uanhisi unaongea na watoto wasioelewa mambo! Pole sana
Ccm ni ileile hata wakikaa madarakani miaka 500 hawana uwezo wa kubadilisha kitu.
Anachokifanya wewe ni kuleta porojo porojo tu.
Watu wanalima wakivuna wanaporwa kama wale wa KOROSHO we unasema sijui heshima ya mtu?
Hivi mtu anayekunywa maji ya rope kule bahi hiyo heshima na usawa utaipata wapi?
 
Unaongea mambo meeeengi japo hujatwambia nani aliyesababisha hayo mambo yasiwepo mpaka leo nusu karne baada ya uhuru? Mkuu nchi hii haijawahi KUTAWALIWA na chama kingine zaidi ya hiking chama cha Wezi, wanafiki na waongo!
Hivi kiongozi mwadilifu anawezaje kutunga SHERIA INAYOZUIYA ASISHITAKIWE AWAPO/ ASIPOKUWEPO MADARAKANI?
Ivi mtu aliyekuwepo kiongozi kwa miaka yote leo anakuaje kusema kwamba yy ni wa mfano na yale yote yaliyotokea huko nyuma hakuwa sehemu YAke?
Unadhani uanhisi unaongea na watoto wasioelewa mambo! Pole sana
Ccm ni ileile hata wakikaa madarakani miaka 500 hawana uwezo wa kubadilisha kitu.
Anachokifanya wewe ni kuleta porojo porojo tu.
Watu wanalima wakivuna wanaporwa kama wale wa KOROSHO we unasema sijui heshima ya mtu?
Hivi mtu anayekunywa maji ya rope kule bahi hiyo heshima na usawa utaipata wapi?
Kinoamiguu:

Wewe umepaniki, nakushauri kanywe maji kisha uje tuendelee na mazungumzo mkuu.
 
Kinoamiguu:

Wewe umepaniki, nakushauri kanywe maji kisha uje tuendelee na mazungumzo mkuu.
Mm sijapaniki mkuu wewe tuendlee tu. Unayoongea wewe ni slogan zilzile. Wenzako tunaposema USAWA. Na haki TUNATAKA mtu mmoja raisi asipange mwenyewe Badala yetu hapana.
Mfano ni watz wangapi waliulozwa kupitia kwa wawakilishi wao kwamba
TUNATAKA ndege Badala ya Madawati?
Tukajenge uwanja wa ndege chato Badala ya musoma au kigoma?
 
Mm sijapaniki mkuu wewe tuendlee tu. Unayoongea wewe ni slogan zilzile. Wenzako tunaposema USAWA. Na haki TUNATAKA mtu mmoja raisi asipange mwenyewe Badala yetu hapana.
Mfano ni watz wangapi waliulozwa kupitia kwa wawakilishi wao kwamba
TUNATAKA ndege Badala ya Madawati?
Tukajenge uwanja wa ndege chato Badala ya musoma au kigoma?
Kinoamiguu:

Nimefurahi kusikia hujapaniki mkuu. Ni kweli kwamba tangu uhuru hata sasa, CCM kimeendelea kuwa ni chama tawala Tanzania, hata wakati ule wa TANU na ASP. Na kwa wakati wote huo, kimejitahidi sana katika kufanya mageuzi makubwa ya kiuchumi ili kuendana na mahitaji ya watanzania kutoka mahitaji yale ya wakoloni, ijapokuwa kimepitia wakati mgumu sana lakini kimefanikiwa.

Lengo la kutawala kwa chama kimoja mara baada ya uhuru lilikuwa ni zuri kwa maana kusudi lake ni kuwaunganisha watu kuwa wamoja katika falsafa moja kwa ujenzi wa nchi. Na hili limefanyika katika mataifa karibu yote duniani ambayo yalijikomboa kutoka ukoloni, ikiwemo Amerika yenyewe katika miaka ya 1780's. Lakini zilibadilisha mfumo ili kuongeza wigo wa ushiriki wa watu katika siasa za nchi na kuongeza demokrasia. Ndipo hapo mataifa mengine yaliingia katika vyama vingi huku zikitumia ama mfumo wa Serikali wa kibunge au Rais.

Mifumo yote hiyo, inaipa nguvu ama upande wa Bunge au Rais lakini nguvu hizo zitatoka kwa wananchi. Marekani yeye alichagua mfumo wa serikali wa Rais, badala ya ule wa kibunge kutoka kwa mkoloni wake Muingereza. Lengo ni kujipa uhuru kamili na kuachana kabisa na viashiria vya ukoloni, wa uingereza. Walichagua kumpa mamlaka Rais lakini waliipa nguvu Bunge kwa ajili ya kumshauri na kumsimamia Rais. Hii inamaana kwamba Urais ni dhamana ya wengi kwa ajili ya maslahi ya wengi. Tanzania tuliiga mfumo wa Serikali wa Amerika na wa uingereza tukaiweka pamoja na kupata mfumo ambao tunautumia sasa.

Tulifuata mfumo wa Serikali wa Rais na Bunge. Rais ni sehemu ya Bunge na kwamba mamlaka ya Rais na Bunge ni nusu kwa nusu. Serikali inafanya kazi zake kwa kushirikiana na Bunge. Kwamba katika utekelezaji wa majukumu ya serikali Rais ni kiongozi wa Serikali na Waziri Mkuu ni kiongozi wa Serikali Bungeni. Kwa hiyo Tangu uhuru hadi hivi leo hakuna jambo ambalo Rais amelitekeleza pasipo baraka za Bunge kwa maana ya wawakilishi wa wananchi kupitia wabunge. Ifahamike kuwa nchi yetu infuata mfumo wa demokrasi ya ushirikishwaji kwa kutumia wawakilishi wa wananchi, na huo ndio utawala wa sheria.

Kwenye kujenga uwanja wa ndege wa chato ushafahamu ni kwa namna gani ambapo serikali na Bunge limeweza kushirikiana vema. Hivyo basi ujenzi wa uwanja huo una baraka zote za Wananchi kupitia wawakilishi.

Nimekupa mfano huo wa stori ya Marekani ili tukalibiane katika kuifahamu hii mifumo ya serikali katika utendaji wake wa kazi. Kwamba katiba ya Tanzania imetoa mamlaka kwa wananchi kupitia bunge chini ya uongozi wa kiongozi wa Serikali Bungeni ambaye ni Waziri Mkuu.
 
Nimepoteza muda want kusoma utumbo mtupu kutoka Lumumba kwa wapiga magoti .
 
Acha kujichanganya na kujaribu kuchanganya wengine! Huwezi kuzungumzia usawa, bila haki kwani haki ndo inayoleta usawa! Maendeleo ya kweli hayawezi letwa katika nchi yoyote bila kwanza kuexercise haki na usawa kwa vitendo na sio kwa maneno matamu!
 
Na: McWenceslaus
01/10/2020.

Habarini za muda ndugu wanabodi wenzangu! Poleni kwa kazi na majukumu mengi ya siku. Baada ya kukaa kwa muda hivi, tukiwa tunatathiminu hali ya kampeni tangu mwanzo hata hivi leo, zikiwa zimesalia siku 27 kufika siku ya kufanya maamuzi ya kamchagua Rais, wabunge na madiwani. Kila mtu atakuwa ashapata kuona uelekeo sahihi wa nani ni Rais ajaye wa Tanzania. Na bila shaka asilimia kubwa ya watanzania wengi, wanauhakika na ushindi wa kishindo wa Rais Dkt. John Magufuli dhidi ya wagombea wengine kwa nafasi ya Rais Tanzania, msioamini subirini siku inakuja nanyi mtaamini. Ni kama ilivyokuwa kwa Thomaso mmoja wa mitume wa Yesu Kristo, ambaye hakuamini mwanzo lakini mwishowe aliamini. Leo ninakuja kuwa fahamisha Siri ya kauli ya HAKI na UHURU kama ambavyo imetumiwa na CHADEMA katika kampeni zake; na ukweli kuhusu UHURU na USAWA, katika kuleta AMANI na Maendeleo ya Watu. Nikuache uendelee....

Uhuru + usawa = Amani

Haki bila usawa ni sawa na mwili uliokosa chakula na matunzo, ni lazima mifumo yake ya mwili ifarakane na mwishowe ijifie yenyewe.

Na kwamba, haki ilikuwepo hapa nchini hata kabla ya uhuru. Moja ya sababu ya msingi ya kudai uhuru katika miaka ya 1960, ilikuwa ni kupigania haki na usawa katika mambo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, na hatimaye kuleta amani ndani ya taifa. Na hilo lilifanikiwa mnamo 09 disemba, 1961 ambapo watanzania walitambuliwa katika usawa na huru, hata hivi leo.

Leo hii tumeanza kusikia habari ya kuwa kuna kundi la watu wanaendelea kusikika humu nchini, wakisema "Amani ni tunda la Haki!" Huu ni uongo wa mchana kweupe peee. Hivyo basi, ni lazima tukawaambie wananchi kuwa, pasipo na usawa hakutakuwepo na amani. Ili kukanusha uongo huo. Tuseme kwa mfano, Paka anayo haki ya kumfukuza na kumtafuna panya; ni katika hali hiyo Panya ameshaonekana ni mnyonge mbele ya Paka, ni kwa sababu eti Paka anaitumia haki yake hiyo! Na kwa kusema ukweli, Panya huyu hawezi kufanya lolote la kumzuia Paka asitekeleze haki yake hiyo. Ni kwa sababu, nguvu hiyo ataitoa wapi, yeye ni mdogo paka ni mkubwa.

Hivyo katika jamii ya watu wenye hali tofauti ya kiuchumi, kiafya, kisiasa, rangi, itikadi n.k mfano wa Paka na Panya huyu, ni lazima msukumo mkubwa uwepo kwenye sera ya USAWA kuliko HAKI, kwa maana HAKI kwa asili huambatana na UHURU zaidi kuliko USAWA. Maana Palipo na HAKI pana UHURU; Na kwa sababu hiyo, ndiyo ilipelekea ndani ya azimio la Arusha 1967 chini ya chama cha TANU na baadaye CCM. Chama kilihimiza na kusisitiza kuwa ujamaa na kujitegemea ni siasa yenye lengo la kujenga jamii ya watu walio SAWA na HURU. Msukumo huo uliwekwa kwa sababu ya kutambua kuwa haki alikuwa nayo mkoloni ya kumnyonya mwafrika, lakini hakukuwepo na usawa wa kutambua kwamba mwafrika ni mtu ambaye anastahili heshima ya kutambuliwa utu wake. Na ndio maana palipo UHURU na USAWA ni lazima pawepo na AMANI, lakini palipo na haki na uhuru amani haiwezi kuwepo kabisa, ni sawa na yule Panya kwa Paka. Amani hiyo ipo kwa Paka pekee, lakini ni nani atakayeweza kusema kwamba Panya yule anayo amani, ukweli hayupo mtu huyo. Kwa Panya kukosa Amani, kwa sababu ya kuwepo kwa haki yake ya kukimbizwa na kutafunwa na Paka, inaifanya Amani ikosetafasiri nzuri kwa hakika.

Kwa kumalizia; katika kampeni za mwaka huu kuna ushindani baridi baina ya siasa ya ujamaa na siasa ya kibepari. Na ndio kwa sababu hiyo, Mgombea Lissu kupitia CHADEMA, amekuja na kauli mbiu ya uhuru na haki, na anajificha kwenye kivuli cha maendeleo ya watu kwa lengo la kuficha dhamiri yake ya kuukaribisha ubepari ndani ya Tanzania. Msukumo katika siasa za kibepari upo katika HAKI maana yake ni hivi, mfanyabiashara mkubwa na mfanyabiashara mdogo wote ni wafanyabiashara hawa hivyo watalipa kodi sawa kwa jina la biashara hiyo, hiyo ni HAKI sawa kwa wote na sio USAWA kwa wote. Katika ujamaa, msukumo mkubwa upo katika USAWA kwa wote, hii maana yake ni kwamba kila mfanyabiashara atalipa kodi kwa kadiri ya mapato yake yatokanayo na biashara yake... Huu usawa unafanya kuwepo kwa AMANI kwani kila mtu atachangia kwa kadiri ya uwezo wake. Na kila mtu atamuona mwenzake kuwa ni sawa kama alivyo yeye, vivyo hivyo kwa makundi na jumuiya zingine. USAWA ni mbegu bora ya kuleta AMANI ya kweli kwa wote.

Na katika kuendeleza nia hiyo ya dhati ya kudumisha UHURU pamoja na USAWA kwa ajili ya kuimarisha AMANI ya nchi yetu, serikali chini ya CCM na uongozi imara wa viongozi wa chama pamoja na Mwenyekiti wa chama na Rais wa nchi Dkt. John P. Magufuli; imeweza kuimarisha usawa kwa makundi yote na watu wa hali zote kwa kuwapatia haki za muhimu za huduma ya jamii. Ikiwa ni pamoja na elimu bure, huduma za afya nafuu na kuimarisha huduma ya mfuko wa TASAF, upatikanaji wa maji katika meneo yote ya mijini na vijijini na maeneo yenye viwanda na yasiyokuwa na viwanda n.k. Hivyo imeweza kuendeleza hali ya AMANI nchini hata sasa.

Uhuru + usawa = Amani
#chaguaCCM
#chaguaUjamaanaKujitegemea
#chaguaUsawanaUhuru
#chaguaMagufuli

Kazi inaendelea 2020-2025

Sauti ya Mdodomia.

01/10/2020
Yaani una subject haki kwenye usawa ?

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
JokaKuu:

Mkuu, Paka itambidi ale chakula. Je, Panya ni chakula cha Paka?

Huo ni mfano tu, lakini nilichotaka kusema ni kwamba palipo na haki pana uonevu; lakini palipo na usawa uonevu hauwezi kuwepo.

Mfano; Kuna haki za watoto, haki za wazazi, haki ya mwanamke, haki ya walemavu, haki ya muuaji, haki mwizi, haki chungu mzima. Na ikiwa utahitaji kutekeleza haki ya upande mmoja ni lazima haki ya upande wa pili uangamizwe au ife kwa muda.

Kwa misingi hiyo upande mmoja utakosa uhuru na hivyo kukosa amani. Ukiwa unatekeleza haki ya mwanamke ni dhahiri kuwa haki ya mwanaume itagandamizwa. Maana yake mwanamke atapewa kipaumbele kuliko mwanamke, tayari umeshawaweka katika makundi mawili mwanamke na mwanaume. Lakini kama utaweka usawa baina ya mwanamke na mwanaume, hapa patakuwa na umoja na sio makundi. Maana yake mwanamke atatendewa sawa na mwanamke si kwa sababu ya jinsia yake bali ni kwa sababu ya utu na ubinadamu wake.

..basically unacheza-cheza na maneno au lugha.

..ngoja kwanza tujaribu Uhuru, Haki, na Maendeleo.

..wakituzingua tutajaribu wanaohubiri amani kama unavyotaka.
 
Kama hujui maana ya haki sidhani kama utaelewa kuwa Usawa upo kwenye haki.
Usawa hauwezi kuwa kwenye haki, ila haki itapatikana ikiwa watu watakuwa huru. Na uhuru utakuwa na maana ikiwa watu watakuwa sawa, na huko ndipo ilipo amani.
 
Back
Top Bottom