Sikirimimimasikini
JF-Expert Member
- Dec 27, 2019
- 2,926
- 15,634
Mpango huo utakuwa sehemu ya ushirikiano wa AUKUS, mkataba wa usalama uliotangazwa na nchi hizo tatu mwaka jana.
Nchi hizo tatu (Uingereza, Marekani na Australia) zimelalamika kuwa mataifa pinzani yakiwemo Russia, China na North Korea yameshawaacha mbali ktk teknolojia ya makombora ya hypersonic, huku Russia ikiwa imeshayatumia mara kadhaa makombora hayo kwenye vita vya Ukraine.
Silaha za hypersonic ni zile zinazozidi kasi ya sauti mara tano. Ni vigumu zaidi kujilinda dhidi ya silaha hizo kwa sababu ya kasi yake na vilevile yanaruka katika mwinuko wa chini - nje ya mstari wa kuonekana kwa rada za ardhini - na yanaweza kurushwa katikati ya ndege.
Mnamo tarehe 19 Machi, Urusi ilidai kutumia kombora la hypersonic kuharibu ghala la silaha magharibi mwa Ukraine, na ujasusi wa jeshi la Marekani umependekeza kuwa vikosi vya Urusi vimezitumia mara kwa mara tangu wakati huo. Mashambulizi hayo yaliashiria matumizi ya kwanza ya makombora ya hypersonic katika mapigano.
=========
Nchi hizo tatu (Uingereza, Marekani na Australia) zimelalamika kuwa mataifa pinzani yakiwemo Russia, China na North Korea yameshawaacha mbali ktk teknolojia ya makombora ya hypersonic, huku Russia ikiwa imeshayatumia mara kadhaa makombora hayo kwenye vita vya Ukraine.
Silaha za hypersonic ni zile zinazozidi kasi ya sauti mara tano. Ni vigumu zaidi kujilinda dhidi ya silaha hizo kwa sababu ya kasi yake na vilevile yanaruka katika mwinuko wa chini - nje ya mstari wa kuonekana kwa rada za ardhini - na yanaweza kurushwa katikati ya ndege.
Mnamo tarehe 19 Machi, Urusi ilidai kutumia kombora la hypersonic kuharibu ghala la silaha magharibi mwa Ukraine, na ujasusi wa jeshi la Marekani umependekeza kuwa vikosi vya Urusi vimezitumia mara kwa mara tangu wakati huo. Mashambulizi hayo yaliashiria matumizi ya kwanza ya makombora ya hypersonic katika mapigano.
=========