Uislam na Ukristo siyo maadili ya Mtanzania na Mwafrika, ni moja ya nyenzo ya mmomonyoko wa maadili

Uislam na Ukristo siyo maadili ya Mtanzania na Mwafrika, ni moja ya nyenzo ya mmomonyoko wa maadili

Dini imeleta mafundisho mengi sana na ndio maana watu husema tumestaarabika maana kuna watu mpaka leo wana maadili na tabia za hovyo
Kinachomfanya MTU awe muungwana ni Elimu Sahihi. Siô Dini.
Dini kûna mafundisho àmbayo siô ya kiungwana.
Tusingefuata dini sidhani kama tungekuwa hivi
Pamoja na Dini kusema Usafi ni moja katika Imani lakini bado watu ni wachafu kupindukia
Mbona zîpo jamii Ambazo hazijafuata Dini za Uislam na ukristo na zîpo Mbali na wasafi. Mfano wachina
Kuna uzi unaongelea kuhusu uchafu wa mama ntilie wa Tz na ukifananisha na mama ntilie wa Rwanda kwa usafi

Mama ntilie wàpo wasafi na wàpo wachafu na wôte hawatagemei Dini
Sisi mbali na watu kusema wana dini fulani lakini bado kuna tatizo kubwa hata maadili ni tofauti
Kwani Vigodoro na kucheza uchi ndio maadili unayoona yanafaa
Sasa akija Padri au Shehe akakemea utamshangaa?
 
Pia dini zimeleta mambo mengine ya hovyo na ajabu ajabu, nafikiri kikubwa na kwamba Waafrika walichukua kila kitu kilicho kwenye na kufikiria kila yaliyoandikwa kwenye hivi vitabu ni matukio na maisha halisi(literally).
Tatizo la muafrika alishindwa kujikomboa kifikra tangu wazungu walipokuja na baadae waarabu
Hebu fikiria walisombwa na wengi kuuwawa waliojaribu kupinga
Mila na desturi zikafa na kuzikwa
Wazee wetu vyote walivyokuwa wanaamini na kufuata vikachomwa moto na mpaka lugha wakasahau kwa kuchanganywa wa huku na huko

Leo mpaka mtu mweusi alieko America hataki kuwa mwafrika kwa sababu babu yake aliitwa Malcolm au George

Kwa kweli tulibeba mambo yao yote na kuyafurahia ingawa babu zetu waliteseka sana
Leo hii kuna machafuko 🇬🇧 kisa mtoto aliekuwa anabaguliwa tangu mtoto shuleni na kuamua kuwachoma visu watoto wadogo wa kizungu
Mtoto ni mzaliwa wa hapa ila bado walimbagua sana

Inabidi tujielewe na kuwa proud to be Black
Sisi tamaduni zetu tunaziuwa wenyewe
Tulikuwa tuna dawa zetu kwa kutumia miti na mizizi ila Leo wamechoma moto kila sehemu na miti mingi imekwisha na kulazimika kutumia sumu zao tunazoziita dawa
Tuamke na kufanya yetu
Elimu waliyoiacha ni ya kuvumbua vitu na kukuza uchumi ila sisi tumeona tuwachape watoto fimbo sana ili wakariri na kuwaita wasomi

Msomi hata bawaba hawezi kutengeneza
 
UISLAM NA UKRISTO SIÔ MAADILI YA MTANZANIA NA MUAFRIKA NI MOJA YA NYENZO YA MMOMONYOKO WA MAADILI.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Kîla jamii inamaadili yake. Maadili yanatokana na ûtamaduni wa jamii Husika. Kîla jamii inautamaduni wake.

Maadili ni mafundisho yanayotolewa kwèñye jamii yenye kuonyesha Tàbia Njema na tàbia Mbaya na kutaka Watu wafuate mambo Mema.
Maadili ya jamii Moja huweza kutofautiana na maadili ya jamii zingine. Ingawaje Yapo maadili àmbayo yanafanana.

Kukiuka Maadili ya jamii yako ndîo huitwa MMOMONYOKO WA MAADILI.

Muafrika anamaadili yake kutokana na tamaduni Zake.
Wazungu wanamaadili Yao kutokana na tamaduni zào.
Waarabu wanamaadili Yao kutokana na tamaduni zào.
Wachina, wahindi n.k wôte wanamaadili Yao kutokana na tamaduni zào.

Kîla jamii ina Mila na desturi nzuri na Potofu. Mila na desturi au tuite maadili huwa potofu Kwa sababu mbalimbali lakini sababu kûbwa ni Wakati(Zama) na sababu ya pili utofauti Kimila.

Mfano, kile kinachoonekana NI maadili Mema Kwa jamii Moja siô ajabu kikawa NI maadili potofu Kwa jamii ñyiñgine
Mathalani, Ndoa za mitala NI maadili Mema Kwa jamii nyingi za kiafrika na Mashariki ya kati lakini Kwa jamii ya kizungu siô maadili

Ukeketaji ni maadili Mema Kwa Baadhi ya jamii za kiafrika lakini Kwa wazungu NI Mila Potofu.

Mahari ni maadili Mema Kwa jamii nyingi Duniani ikiwemo jamii za kiafrika lakini Kwa jamii nyingi za kizungu NI maadili potofu.

Upotofu na usahihi mara nyingi hutokana na mabadiliko ya kizama(kinyakati) na tofauti za kiutamaduni.

Ukristo na Uislam siô maadili ya Mtanzania na Muafrika Kwa ujumla.

Huwaga nashangaa nikisikia Mtu akiwaita Wengine Hawana maadili Wakati Muda huohuo MTU huyo NI muislam au Mkristo.
Muafrika mwenye maadili hawezi kuwa Muislam au Mkristo. Kuwa Muislam au Mkristo ni kukosa maadili ya kiafrika na pia ni mmomonyoko wa maadili.

Kukaidi, kukiuka, kutofuata maadili yako ya asili na kufuata maadili ya jamii ñyiñgine hiyo ndîo tofsiri halisi ya MMOMONYOKO WA MAADILI.

Maadili humong'onyolewa na vitu vingi lakini kikubwa zaidi ni Muingiliano WA tamaduni zaidi ya Moja Kwa kile kiitwacho utandawazi.

Huwezi Acha ûtamaduni wako na kuita tamaduni za Wengine ni maadili. Kitendo cha kuacha tuu na kusaliti ûtamaduni wako ni mmomonyoko wa maadili tosha.

Kabla ya Wageni kuja, waafrika walikuwa na maadili Yao Mema tuu. Hii haimaanishi hapakuwa na Mila mbaya na potofu.

Nilishasema kîla jamii inamila Zake nzuri na Mbaya.
Mila mbaya kama uchawi, Kutoa Watoto kafara, unyanyasaji WA kijinsia, n.k zilikuwepo Karibu jamii zote hata jamii za kizungu zilikuwa na Mila hizô.

Jamii za kiafrika zilikuwa zinaabudu katika Mungu Mmoja kupitia mizimu ya mababu kama ilivyo Kwa Waislam na Wakristo ambao huamini katika Mungu Mmoja katika mitume na Manabii.

Kabla ya ujio WA uislam na ukristo waafrika walikuwa na maadili kuliko Zama hizi baàda ya ujio wa Dini hizi.

Ûkienda kwèñye jamii Ambazo hazina Ukristo au Uislam zina maadili ukilinganisha na jamii Zenye Ukristo na Uislam.
Nenda Umasaini ndanindani, nenda Kwa Wahadzabe na watindiga Huko utajionea mwenyewe

Maadili ya kwèli hayafundishwi Kanisani au Misikitini. Maadili hufundishwa nyumbani.
Maadili yanauhusiano na asili ya Mtu na mîungu Yao.

Baadhi ya mafundisho ya kikristo na kiislam yanaweza kuwa mazuri Kwa kiwango cha juu lakini haimaanishi NI mafundisho Bora kuliko yale mafundisho ya asili Yenu, Wazazi wako, Babu zako Ambao wewe ndîo umetokea.

Maadili pia hufanyiwa matengenezo (reformations) ili yaendane na wakati Husika. Hata maadili ya kiislam na Kikristo yamefanyiwa marekebisho mengi tuu kufikia Hapo yalipo.

Maadili NI utambulisho yaani ûtamaduni. Mtu kutokuwa na maadili ya Kwao inamaanisha Hana utambulisho na Hana maadili na amemomonyoko kimaadili.

Yàani kikawaida Huwezi kuwa Muafrika Ukawa Mkristo au muislam alafu ukajiita unamaadili labda Kama hujui mantiki ya maadili yenyewe.

Unaweza Ukawa mwema na Mtu Bora Kwa kufuata tamaduni za kwetu zile zilizobora. Lakini zile zilizombaya ukaziacha.

Kûna wale watakaokuja na hoja ya Teknolojia.
Kwamba Kwa nini tunatumia Teknolojia za kigeni.
Mfano Simu au Magari n.k.
Tunaweza Kutengeneza Simu Kulingana na ubunifu wa tamaduni zetu.

Acha nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi.
Kwa Sasa Dar es salaam
Lakini haupingi uvaaji wa nguo za viwandani (ulizoletewa na hao waleta dini), matumizi ya simu, usafiri, na umesoma elimu yao😂😂
Si ni wabaya kwa nn usivikatae vyote?
 
1.Hakukuwa na kuoana kwa watu walio ndugu wa karibu.
2. Hakukuwa na mabishano kuhusu ushoga au mahubiri yanayohusu ushoga.
3. Hakukuwa na matapeli wanaodanganya watu wawape pesa watabarikiwa
4. Hakukuwa na mifarakano ya kidini, mfano vyakula, mavazi, vinywaji n.k
5. Ndoa zilikuwa zinadumu, hakuna kuoa na kuacha hovyo hovyo.

first off yote ulioyaorodhesha siyo Ukristo kwanza ni kinyume chake ni anti christ, pili kulikuwa hakuna kitu kama ndoa kama tuijuavyo leo hii kabla ya Ukristo kuingia kwetu, tulikuwa ni polygamy sasa kama polygamy ni bora klk Christian marriage hilo unaweza kuamua mwenyewe …
 
Kinachomfanya MTU awe muungwana ni Elimu Sahihi. Siô Dini.
Dini kûna mafundisho àmbayo siô ya kiungwana.

Mbona zîpo jamii Ambazo hazijafuata Dini za Uislam na ukristo na zîpo Mbali na wasafi. Mfano wachina


Mama ntilie wàpo wasafi na wàpo wachafu na wôte hawatagemei Dini
Kwa wengi wetu
Ukristo unasimama kwenye amri kuu mbili (ambazo ni kifupi Cha amri 10 za Mungu): Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa nguvu zako zote na kwa akili zako zote (Amri 1-3) na mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenywe (Amri 4-10). Sasa ni ipi kati ya hizo si Mila ya Kitanzania?
Hili la mpende jirani labda aliefuata msimamo kwa Dini ila sio maadili ya wengi
Mpaka leo ugomvi wa jirani ni mkubwa sana kwa baadhi ya watu na pia wafugaji na wakulima kwetu bado ni tatizo
Ukienda Misri utaona mto Nile ambapo wakulima na wafugaji wanaishi in harmony
Upande mmoja wa ziwa ni wakulima na upande mwingine ni wafugaji na kwenye ziwa wavuvi je ni raha iliyoje kama mtaelewana kama binadamu?

Kweli maisha yalikuwepo kabla ya dini kuja ila tumejifunza mema mengi pia ingawa wengine wanaona ni za kuja

Maadili ni jambo la kuzingatia sana na sisi hilo hatulifundishi popote zaidi ya kwenye dini na nyumbani ila mashuleni ni mwendo wa kukariri tu

Nani wa kumlaumu kwa hao vijana wanaochungulia wanawake wanaojifungua hospital ya Tabora ?
Hii ilikuwa kwenye taarifa za habari nchini
Je nani wa kulaumiwa?
Watoto lazima wafundishwe maadili na tabia njema kila mahali
 
1.Hakukuwa na kuoana kwa watu walio ndugu wa karibu.
2. Hakukuwa na mabishano kuhusu ushoga au mahubiri yanayohusu ushoga.
3. Hakukuwa na matapeli wanaodanganya watu wawape pesa watabarikiwa
4. Hakukuwa na mifarakano ya kidini, mfano vyakula, mavazi, vinywaji n.k
5. Ndoa zilikuwa zinadumu, hakuna kuoa na kuacha hovyo hovyo.
Yote hayo Mbona ni kinyume na Ukristo na uislam Wala hayaruhusiwi hayo kwa dini hizo
 
Nashindwa kutofautisha kati ya maadili na dini kwani dini ni nyenzo ya kuyafikia maadili mema

Ndani ya dini kuna maadili na tamaduni pamoja na mila hivyo dini ipo kwa ajili ya kufundisha maadili mema sio mabaya

Dini ni asili ya mwanadamu, ukiristo na uislam ni miongoni mwa dini(njia za kumjua Muumba) lakini zipo nyingi zaidi ambazo kimsingi zinaelekea kuhimiza maadili mema. Kuhusu kutofautiana ni mapokezi tu ya wafundishwaji

Kabla ya ujio wa waarabu na wazungu mataifa yote yalikuwa na dini ambazo pia zinaelekeza maadili mema.
 
Siwezi pinga kitu ambacho NI sahihi

Hao ambao siô waarabu wanafuata Dini ya waarabu àmbayo muanzilishi wake ni Muhammad

Hiyo siô Fact ni opinion za wanadini kujifagilia.
Hapa tujadili Fact.

Tunazungumzia maadili àmbayo msingi wake Mkûu ni ûtamaduni.
Kwèñye ûtamaduni kûna aspects nyingi kama Lugha, Dini, mavazi, chàkula, n.k.

Kwèñye Dini kîla jamii inadini na mîungu wake. Na hayo NI maadili ya kîla jamii.
Muhammaad ni mtume wa Mewisho aliyepewa Qur'an. Mitume yote kabla yake ilileta ujumbe huo huoi mmoja tu. Uislam.

Uislam ndiyo mfumo kamili wa maisha uliopo ambao hauna mfano wake.
 
Sio mmomonyoko, kimsingi ni mageuzi. Na hii ni kwasababu sio maadili yote yanatoweka tamaduni zikichanganyika. Kuna maadili ya jumla ambayo jamii zote zinafuata mfano watoto kuheshimu wazazi...

Tulichobadilishiwa ni mambo madogo tu kama mavazi, lakini maadili binafsi(subjective morality) ambayo hayachochewi na tamaduni yeyote ni ya jumla na kila mwanadamu anayafuata.

Yale haufundishwi unayajua kadri unavyoishi na viumbe wenzako, hata wanyama wana maadili yao....
 
Muhammaad ni mtume wa Mewisho aliyepewa Qur'an. Mitume yote kabla yake ilileta ujumbe huo huoi mmoja tu. Uislam.

Uislam ndiyo mfumo kamili wa maisha uliopo ambao hauna mfano wake.
Nenda China kawaambie hivyo uone jinsi watakavyokunyoosha kwenye re-education camps.
 
Kwa wengi wetu

Hili la mpende jirani labda aliefuata msimamo kwa Dini ila sio maadili ya wengi
Mpaka leo ugomvi wa jirani ni mkubwa sana kwa baadhi ya watu na pia wafugaji na wakulima kwetu bado ni tatizo
Ukienda Misri utaona mto Nile ambapo wakulima na wafugaji wanaishi in harmony
Upande mmoja wa ziwa ni wakulima na upande mwingine ni wafugaji na kwenye ziwa wavuvi je ni raha iliyoje kama mtaelewana kama binadamu?

Kweli maisha yalikuwepo kabla ya dini kuja ila tumejifunza mema mengi pia ingawa wengine wanaona ni za kuja

Maadili ni jambo la kuzingatia sana na sisi hilo hatulifundishi popote zaidi ya kwenye dini na nyumbani ila mashuleni ni mwendo wa kukariri tu

Nani wa kumlaumu kwa hao vijana wanaochungulia wanawake wanaojifungua hospital ya Tabora ?
Hii ilikuwa kwenye taarifa za habari nchini
Je nani wa kulaumiwa?
Watoto lazima wafundishwe maadili na tabia njema kila mahali
Udugu, kuwakarimu wageni, kuwasaidia wenye shida, kuwatunza wajane na yatima, wagonjwa na kuzikana wakati wa misiba, nk - kwa neno moja au mawili unaweza kusema ni kitu gani?
 
Tukiongelea maadili tunaongelea mfumo mzima wa maisha ya mwanadamu au utaratibu wa kuishi

Jinsi ya kula, kuvaa, kulala, kujamiiana(kuhusiana), kuongea, muonekano, mtazamo, hisia(kuhuruma, upendo, kutokuwa katili na roho mbaya n.k), kutembea na mengine mengi katika maisha ya mwanadamu yanatakiwa yafanyike ki maadili zaidi yaani ki tabia njema

Ukiangalia kwa undani dini nyingi zipo kwa ajili ya kuhamasisha mambo hayo kupitia imani za kiungu na uumbaji hata kabla ya ujio wa uislam na ukiristo katika jamii zetu
 
Back
Top Bottom