Uislam na Ukristo siyo maadili ya Mtanzania na Mwafrika, ni moja ya nyenzo ya mmomonyoko wa maadili

Uislam na Ukristo siyo maadili ya Mtanzania na Mwafrika, ni moja ya nyenzo ya mmomonyoko wa maadili

Hakuna jamii àmbayo haikutembea matako Wazi Kulingana na historia ya Dunia
Ndugu yangu mila zako ni ulizozikuta miaka hii kama uliona watu wanatembea matako wazi kama kweny vitabu basi fuata , ila tambua wazazi wako mazingra waliyokulea ndio mila zako sio za waliopita ....Dunia isingefika hapa hata wazungu walikuwa chini .

Vitabu vinaonyesha Adam alikuwa hajaendelea akafundishwa , zikaja zama kibao za mitume tofauti ndio maana waliishi mwaka 1800 leo hawapo walishapita.
 
Kama umejitambua kwa elimu ya mzungu basi ulichoandika ni unafiki , wazee wa zamani walikuwa smart na more resistant kuliko wa sasa , ilikuwaje dini zikaingia? Hpo hamna jibu bali dini ni mpango wa Mungu ndio maana zilisambaa mpaka ulaya.

Kusambaa Kwa Dini za kigeni hakukuwa Kwa hiyari. Wazee wetu walipoteza pambano kama vile unavyoona kinachoenda kutokea Kwa waarabu Hapo Mashariki ya Kati
Hakuna ushahidi wa babu wa mtu anajua zaidi ni maandisho ambayo ukienda kitabu kingine ukisoma yapo tofauti .

Unaposema mwafrika alikuwa na tamaduni zake ni unafiki hata kihistoria mwanadamu alitoka sehemu kwenda nyingine ili kupata ustaarabu na maendeleo, mwafrika alikuwa anakula nyama mbichi baadae akagundua moto mpaka kuanza kutengeneza zana zake mwenyewe...

Karne ya ngapi hiyo unaelezea hii Stori?

Hii inaonyesha lazima binadamu apate maendeleo kulingana na mabadiliko , dini za leo ndipo ambpo mwanadamu alipangiwa kuwepo leo kwa sababu hata maandiko kayasoma kweny vitabu ...Hiyo miaka ya kuishi pangoni mlikuwa mnajua kuandika?

Huwezi kusema unajua mila za muafrica wakati hata mwaka 1800 mwafrica alikuwa kashajitambua anaishi mbali na wanyama , Mila zako inategemea wazazi wako huwezi kusema sijui babu zako walikuweje huko nyuma .Mila sio conservativness mila zinabadilika kila siku kwa sababu binadamu anajifunza kulingana na mazingira.

Mila zinabadilika lakini hiyo haimaanishi zinakuwa Mila za jamii ñyiñgine.
Wanachopigania waarabu ndicho ulichoeleza Hapa.
Wao hawaogopi Mila zào kubadilika lakini hawataki zibadilike na kupoteza utambulisho waô na kuwa kama Mila za kizungu. Hata wachina nao wanafanya vivyohivyo
Basi usisome wala kutumia jf na simu kabisa maana babu zako hawakusoma , hata hao watu weupe nao walianzia chini kama mwafrika.
Hapa sijui Unazungumzia nini?
 
Ndugu yangu mila zako ni ulizozikuta miaka hii kama uliona watu wanatembea matako wazi kama kweny vitabu basi fuata , ila tambua wazazi wako mazingra waliyokulea ndio mila zako sio za waliopita ....Dunia isingefika hapa hata wazungu walikuwa chini .

Vitabu vinaonyesha Adam alikuwa hajaendelea akafundishwa , zikaja zama kibao za mitume tofauti ndio maana waliishi mwaka 1800 leo hawapo walishapita.

Maadili huyajui ndîo maana hujui hata unachokifafanua?
 
Hiyo ni teknolojia.
Hata wachina wanafuata tamaduni zao kwa sana na teknolojia imekua sana kwao.

Teknolojia inachochea utamaduni wa mahala ilhali dini zinaharibu tamaduni za wengine.

Mfano, huitaji kubadili jina lako (mfano Masanja) ili kutumia simu, ila watu wa dini watakuambia Masanja ni jina la mizimu mibaya, badili uitwe Gabriel ndiyo jina la mtakatifu.
Jina gani ambalo ulishawahi kuskia limekataliwa kwamba ni la mizim?
Mbona hata watumishi wenye majina makubwa majina yao ni ya kilugha (mwamposa, suguye,mwakasege, hananja nk).
Kwa hyo na kuvaa suruali na shati ni technology au ni utamaduni?
Vp na kuishi kwenye nyumba za kisasa ni teknolojia au utamaduni? Na umeiga kwa nan?
 
Kûna uhûsiano gàni Kati ya maadili na Teknolojia?

Maadili Unazungumzia kizuri na kibaya

Gari hata wewe unaweza Kutengeneza kama vile china wanavyofanya.

Teknolojia ya Afrika iliathiriwa zaidi baada ya ujio wa wakoloni.
Si ww unapinga kila kilicholetwa na mataifa ya nje ya Africa? Basi kataa kila kitu ikiwemo hiyo simu yako na nyumba unayoishi urudi mapangoni maana ndo asili ya Africa.
Halafu hunakatazwa kuabudu mti abudu kivyovyote unavyojiskia Kwan utapigwa?
 
kwann tuliacha science yetu ? hiyo ndo hoja
Kwan umekatazwa kuchukua ungo wako ukapata zako?
Ulishawahi kuskia sheria inayokataza matumizi ya tamaduni za asili?
Hiyo kuacha jiulize mwenyew maana umeacha bila kulazimishwa na mtu yeyote na haihusiani na dini maana umeamua mwenyew
 
Wote walewale wametokea sehemu moja na siasa zao wakazirithisha na huku
Siyo kweli kabisa.

Huujuwi Uislam ndiyo tatizo lako, unataka kufananisha na hizo biashara zingine.
 
Jina gani ambalo ulishawahi kuskia limekataliwa kwamba ni la mizim?
Mbona hata watumishi wenye majina makubwa majina yao ni ya kilugha (mwamposa, suguye,mwakasege, hananja nk).
Kwa hyo na kuvaa suruali na shati ni technology au ni utamaduni?
Vp na kuishi kwenye nyumba za kisasa ni teknolojia au utamaduni? Na umeiga kwa nan?
Huyo Mwamposa anaitwa Mwamposa?
Hilo ni jina la ukoo. Bila Shaka anaitwa Boniface.
Je umebatizwa? Kuna mkatoliki anabatizwa kwa jina lisilo la 'mtakatifu'?

Teknolojia ya kutengeneza mavazi imekuwa dunia nzima. Popote utakapoenda, Iwe China, Tanzania au au Japan l, watu wanavaa T-shirt na Jeans.
Suala ni wachina au wajapani bado wanavaa mavazi ya mtindo wa kwao kila mara mitaani na kwenye matukio mbalimbali ilhali wabongo hatuna hata vazi la kusema hili ni letu la kitamaduni. Labda uite wamasai.
 
UISLAM NA UKRISTO SIÔ MAADILI YA MTANZANIA NA MUAFRIKA NI MOJA YA NYENZO YA MMOMONYOKO WA MAADILI.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Kîla jamii inamaadili yake. Maadili yanatokana na ûtamaduni wa jamii Husika. Kîla jamii inautamaduni wake.

Maadili ni mafundisho yanayotolewa kwèñye jamii yenye kuonyesha Tàbia Njema na tàbia Mbaya na kutaka Watu wafuate mambo Mema.
Maadili ya jamii Moja huweza kutofautiana na maadili ya jamii zingine. Ingawaje Yapo maadili àmbayo yanafanana.

Kukiuka Maadili ya jamii yako ndîo huitwa MMOMONYOKO WA MAADILI.

Muafrika anamaadili yake kutokana na tamaduni Zake.
Wazungu wanamaadili Yao kutokana na tamaduni zào.
Waarabu wanamaadili Yao kutokana na tamaduni zào.
Wachina, wahindi n.k wôte wanamaadili Yao kutokana na tamaduni zào.

Kîla jamii ina Mila na desturi nzuri na Potofu. Mila na desturi au tuite maadili huwa potofu Kwa sababu mbalimbali lakini sababu kûbwa ni Wakati(Zama) na sababu ya pili utofauti Kimila.

Mfano, kile kinachoonekana NI maadili Mema Kwa jamii Moja siô ajabu kikawa NI maadili potofu Kwa jamii ñyiñgine
Mathalani, Ndoa za mitala NI maadili Mema Kwa jamii nyingi za kiafrika na Mashariki ya kati lakini Kwa jamii ya kizungu siô maadili

Ukeketaji ni maadili Mema Kwa Baadhi ya jamii za kiafrika lakini Kwa wazungu NI Mila Potofu.

Mahari ni maadili Mema Kwa jamii nyingi Duniani ikiwemo jamii za kiafrika lakini Kwa jamii nyingi za kizungu NI maadili potofu.

Upotofu na usahihi mara nyingi hutokana na mabadiliko ya kizama(kinyakati) na tofauti za kiutamaduni.

Ukristo na Uislam siô maadili ya Mtanzania na Muafrika Kwa ujumla.

Huwaga nashangaa nikisikia Mtu akiwaita Wengine Hawana maadili Wakati Muda huohuo MTU huyo NI muislam au Mkristo.
Muafrika mwenye maadili hawezi kuwa Muislam au Mkristo. Kuwa Muislam au Mkristo ni kukosa maadili ya kiafrika na pia ni mmomonyoko wa maadili.

Kukaidi, kukiuka, kutofuata maadili yako ya asili na kufuata maadili ya jamii ñyiñgine hiyo ndîo tofsiri halisi ya MMOMONYOKO WA MAADILI.

Maadili humong'onyolewa na vitu vingi lakini kikubwa zaidi ni Muingiliano WA tamaduni zaidi ya Moja Kwa kile kiitwacho utandawazi.

Huwezi Acha ûtamaduni wako na kuita tamaduni za Wengine ni maadili. Kitendo cha kuacha tuu na kusaliti ûtamaduni wako ni mmomonyoko wa maadili tosha.

Kabla ya Wageni kuja, waafrika walikuwa na maadili Yao Mema tuu. Hii haimaanishi hapakuwa na Mila mbaya na potofu.

Nilishasema kîla jamii inamila Zake nzuri na Mbaya.
Mila mbaya kama uchawi, Kutoa Watoto kafara, unyanyasaji WA kijinsia, n.k zilikuwepo Karibu jamii zote hata jamii za kizungu zilikuwa na Mila hizô.

Jamii za kiafrika zilikuwa zinaabudu katika Mungu Mmoja kupitia mizimu ya mababu kama ilivyo Kwa Waislam na Wakristo ambao huamini katika Mungu Mmoja katika mitume na Manabii.

Kabla ya ujio WA uislam na ukristo waafrika walikuwa na maadili kuliko Zama hizi baàda ya ujio wa Dini hizi.

Ûkienda kwèñye jamii Ambazo hazina Ukristo au Uislam zina maadili ukilinganisha na jamii Zenye Ukristo na Uislam.
Nenda Umasaini ndanindani, nenda Kwa Wahadzabe na watindiga Huko utajionea mwenyewe

Maadili ya kwèli hayafundishwi Kanisani au Misikitini. Maadili hufundishwa nyumbani.
Maadili yanauhusiano na asili ya Mtu na mîungu Yao.

Baadhi ya mafundisho ya kikristo na kiislam yanaweza kuwa mazuri Kwa kiwango cha juu lakini haimaanishi NI mafundisho Bora kuliko yale mafundisho ya asili Yenu, Wazazi wako, Babu zako Ambao wewe ndîo umetokea.

Maadili pia hufanyiwa matengenezo (reformations) ili yaendane na wakati Husika. Hata maadili ya kiislam na Kikristo yamefanyiwa marekebisho mengi tuu kufikia Hapo yalipo.

Maadili NI utambulisho yaani ûtamaduni. Mtu kutokuwa na maadili ya Kwao inamaanisha Hana utambulisho na Hana maadili na amemomonyoko kimaadili.

Yàani kikawaida Huwezi kuwa Muafrika Ukawa Mkristo au muislam alafu ukajiita unamaadili labda Kama hujui mantiki ya maadili yenyewe.

Unaweza Ukawa mwema na Mtu Bora Kwa kufuata tamaduni za kwetu zile zilizobora. Lakini zile zilizombaya ukaziacha.

Kûna wale watakaokuja na hoja ya Teknolojia.
Kwamba Kwa nini tunatumia Teknolojia za kigeni.
Mfano Simu au Magari n.k.
Tunaweza Kutengeneza Simu Kulingana na ubunifu wa tamaduni zetu.

Acha nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi.
Kwa Sasa Dar es salaam
Kwa hapa umetema madini mtani, si sahihi kuacha Mila zetu, hili jambo la Mila nilikuwa nalichukia sana miaka ya nyuma ila Sasa hivi sisimizi yeyote...

Ila Mila ikiwekwa na dini mixer anapatikana mtu Mmoja mzuri sana- A very civilized person.

Tumeziacha Mila zetu hususani wasomi ndio maana mabumunda wamekuwa wengi, Yani mtu ana masters na HAWEZI Unda chochote na akakiingiza sokoni kikaleta athari chanya kwenye jamii.

Tuna Laana, tumeacha Mila zetu, hatuwezi kufanya chochote Cha maana na ulimwengu wa kiroho unatutazama tu unasema watazurura sana Hawa.


Kila mtu anawaza kuwa msanii au mwanasiasa.

Hebu fikiria badala Iwe kwamba mtu maarufu na mwenye nguvu Tanzania ni mvumbuzi wa kitu flani ambacho kinasaidia jamii Nina uhakika hapa watu maarufu 30 kwenye nchi hii wakitajwa list itajazwa na watu wa michezo siasa Sanaa - Starehe, Starehe ndio...

Tumeacha Mila ushoga, usagaji - vitu vya kuletewa, unaongezeka, hivi Wazazi wangeenda kwao na kulia kuomba kimila haya matatizo Mbona ni madogo...
 
Huyo Mwamposa anaitwa Mwamposa?
Hilo ni jina la ukoo. Bila Shaka anaitwa Boniface.
Je umebatizwa? Kuna mkatoliki anabatizwa kwa jina lisilo la 'mtakatifu'?

Teknolojia ya kutengeneza mavazi imekuwa dunia nzima. Popote utakapoenda, Iwe China, Tanzania au au Japan l, watu wanavaa T-shirt na Jeans.
Suala ni wachina au wajapani bado wanavaa mavazi ya mtindo wa kwao kila mara mitaani na kwenye matukio mbalimbali ilhali wabongo hatuna hata vazi la kusema hili ni letu la kitamaduni. Labda uite wamasai.
Kumbe huna utamaduni 😂😂😂 basi washukuru waliikuletea hui utamaduni wa mavazi 😂😂
 
Jina gani ambalo ulishawahi kuskia limekataliwa kwamba ni la mizim?
Mbona hata watumishi wenye majina makubwa majina yao ni ya kilugha (mwamposa, suguye,mwakasege, hananja nk).
Kwa hyo na kuvaa suruali na shati ni technology au ni utamaduni?
Vp na kuishi kwenye nyumba za kisasa ni teknolojia au utamaduni? Na umeiga kwa nan?
Kwani NIDA wameshawahi kukataa jina lako?
 
Kiuchumi mbali.kijamii tuanzie
1
Kwa hapa umetema madini mtani, si sahihi kuacha Mila zetu, hili jambo la Mila nilikuwa nalichukia sana miaka ya nyuma ila Sasa hivi sisimizi yeyote...

Ila Mila ikiwekwa na dini mixer anapatikana mtu Mmoja mzuri sana- A very civilized person.

Tumeziacha Mila zetu hususani wasomi ndio maana mabumunda wamekuwa wengi, Yani mtu ana masters na HAWEZI Unda chochote na akakiingiza sokoni kikaleta athari chanya kwenye jamii.

Tuna Laana, tumeacha Mila zetu, hatuwezi kufanya chochote Cha maana na ulimwengu wa kiroho unatutazama tu unasema watazurura sana Hawa.


Kila mtu anawaza kuwa msanii au mwanasiasa.

Hebu fikiria badala Iwe kwamba mtu maarufu na mwenye nguvu Tanzania ni mvumbuzi wa kitu flani ambacho kinasaidia jamii Nina uhakika hapa watu maarufu 30 kwenye nchi hii wakitajwa list itajazwa na watu wa michezo siasa Sanaa - Starehe, Starehe ndio...

Tumeacha Mila ushoga, usagaji - vitu vya kuletewa, unaongezeka, hivi Wazazi wangeenda kwao na kulia kuomba kimila haya matatizo Mbona ni madogo...

Tunasema Mila zetu na maadili yetu mabaya kana kwamba hakuna maadili au Mila zetu zilizo nzuri
 
Back
Top Bottom