Uislamu haujakataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani, siungi mkono wasio waislamu kuzuiwa kula mchana

Uislamu haujakataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani, siungi mkono wasio waislamu kuzuiwa kula mchana

M
Mkuu kafiri maana yake ni kila asiyekuwa muislamu.

Kwa maana ni jina la jumla kwa kila asiyekuwa muislamu, badala ya uislamu kutamka dini zote ikaona iweke kwa ufupi tu kuwa wasiokuwa waislamu ni makafiri.

Hili jina linaonekana baya kwa sababu ya mindset zetu zimejengeka na tunalisikia likitajwa katika maeneo hatarishi.

Kama vile katika mambo ya kuuana utaskia anatajwa kaafiriii, mtu ataona hee kumbe kafiri hii ni jitu la kuuawa kabisa kumbe sivyo kabisa.

Hivyo kafiri ni jina la utambulisho kwa wasiokuwa waislamu mkuu.

Ni kama ukienda kwenye fani ya afya mgonjwa ataitwa mteja, utajiuliza kwamba mimi naumwa alafu naitwa mteja?


Kumbe Maana yake mteja ni mtu ambaye anakuja pale kutaka huduma.

Hivyo neno mteja ni jina la jumla kama ambavyo neno kafiri ni la jumla
Mke wangu anafanya kazi katika Kituo cha Afya. Kuna times ananiambia LEO WATEJA NI WENGI binafsi neno hili huwa linanikereketa.
 
Habarini za kutwa nyote.

Naomba niseme kwamba katika dini yetu ya uislamu hakuna pahala mtume kamkataza asiyekuwa muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna pahala qurani imekataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna sehemu wakati wa mtume imeonesha kwamba walikatazwa wasiokuwa waislamu wasile mchana wa ramadhani.

Katika masharti ya mtu kulazimika kufunga kwanza awe muislamu.

Kwa maana asiyekuwa muislamu hailazimiki kufunga,kama halazimiki kufunga maana yake ana uhalali wa kula mchana wa ramadhani kwa sababu sio muislamu.

Mtu anaweza akasema kwamba wamekatazwa wasile hadharani ?

Hadharani kwanza ni wapi kwa mujibu wa sheria ya dini ?

Watu wanakula kwenye migahawa hakuna anayekunywa chai na chapati anatembea pale kariakoo.

Hivyo kuhusu kula hadharani uislamu pia haujakataza kwa sababu neno hadharani ni pana katika muktadhwa huu.

Uislamu umekataza kwa muislamu ambaye hana udhuru wowote alafu akala mchana wa ramadhani,huyu anapata dhambi.

Lakini kuwakataza watu wasile mchana na kuwashambulia sio katika adabu za kiislamu kwa sababu

Kuna wagonjwa hawatakiwi kufunga.
Kuna wanawake wako kwenye siku
Kuna watoto
Kuna wazee
Kuna wasafiri
Kuna wasiokuwa waislamu

Hawa wote ruhusa kula mchana kwa mujibu wa ssheri ya uislamu wetu.

Sasa kama wanaruhusiwa kula mchana vipi wasiruhusiwe kula hadharani wakati hakuna katazo lolote la kula hadharani katika uislamu.

Allah anasema..

"Hakuna kulazimishana katika dini"

Asiye muislamu kumkataza asile mchana maana yake unamlazimisha akae na njaa jambo ambalo sheria ya dini imekataza.

Tutaheshimu sheria itakayowekwa na serikali lakini tunaomba sheria hizo zisinasibishwe na uislamu.

Ni bora uislamu ulaumiwe kwa sheria ambayo kweli imeiweka kama vile viboko kwa wazinifu n.k

Kuliko uislamu kulaumiwa kwa sheria ambayo haijaiweka kama hizi kukataza kula mchana wa ramadhani

Nakaribisha maswali.

Naomba kuwasilisha.
kati ya vitu ambavyo huwa vinanifanya nitamani tuachane na zanzibar, ni kuwachapa viboko wakristo ambao hawajafunga kula mchana, ni ukatili na ugaidi kabisa. hapo ndio huwa naiondoa kabisa zenji moyoni mwangu.
 
Kwanini hii misosi mnayafunga kula mchana huwa mnairundika mpka usiku na kibugia s bora msingewasaidia wenye uhitaji?
Mkuu usitishwe na picha za mitandaoni ambazo mara nyingi huoneshwa futari ya wenye uwezo. Kuna watu wanafuturu kipande cha muhogo na chai na hao ndio wengi.

Lakini pia kuna watu wanejitengenezea utaratibu wa kula vizuri zaidi wakati huu sawa na wewe unavyokula vizuri siku ya pasaka au krisimasi, hatuwezi kukupangia eti kile chakula ukawape wengine. Wapo watu wengi tu wanatoa kwa wenye uhitaji ila sio kwa njia ya maonesho
 
Habarini za kutwa nyote.

Naomba niseme kwamba katika dini yetu ya uislamu hakuna pahala mtume kamkataza asiyekuwa muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna pahala qurani imekataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna sehemu wakati wa mtume imeonesha kwamba walikatazwa wasiokuwa waislamu wasile mchana wa ramadhani.

Katika masharti ya mtu kulazimika kufunga kwanza awe muislamu.

Kwa maana asiyekuwa muislamu hailazimiki kufunga,kama halazimiki kufunga maana yake ana uhalali wa kula mchana wa ramadhani kwa sababu sio muislamu.

Mtu anaweza akasema kwamba wamekatazwa wasile hadharani ?

Hadharani kwanza ni wapi kwa mujibu wa sheria ya dini ?

Watu wanakula kwenye migahawa hakuna anayekunywa chai na chapati anatembea pale kariakoo.

Hivyo kuhusu kula hadharani uislamu pia haujakataza kwa sababu neno hadharani ni pana katika muktadhwa huu.

Uislamu umekataza kwa muislamu ambaye hana udhuru wowote alafu akala mchana wa ramadhani,huyu anapata dhambi.

Lakini kuwakataza watu wasile mchana na kuwashambulia sio katika adabu za kiislamu kwa sababu

Kuna wagonjwa hawatakiwi kufunga.
Kuna wanawake wako kwenye siku
Kuna watoto
Kuna wazee
Kuna wasafiri
Kuna wasiokuwa waislamu

Hawa wote ruhusa kula mchana kwa mujibu wa ssheri ya uislamu wetu.

Sasa kama wanaruhusiwa kula mchana vipi wasiruhusiwe kula hadharani wakati hakuna katazo lolote la kula hadharani katika uislamu.

Allah anasema..

"Hakuna kulazimishana katika dini"

Asiye muislamu kumkataza asile mchana maana yake unamlazimisha akae na njaa jambo ambalo sheria ya dini imekataza.

Tutaheshimu sheria itakayowekwa na serikali lakini tunaomba sheria hizo zisinasibishwe na uislamu.

Ni bora uislamu ulaumiwe kwa sheria ambayo kweli imeiweka kama vile viboko kwa wazinifu n.k

Kuliko uislamu kulaumiwa kwa sheria ambayo haijaiweka kama hizi kukataza kula mchana wa ramadhani

Nakaribisha maswali.

Naomba kuwasilisha.
Ujinga mtupu, yaani niache kula mchana kwa sababu ya dini ya mtu tena ya kuletewa? Siku nile aje mpuuzi eti aniulize kwanini nakula mchana haki ya nani huyo mtu aombe Mungu wake tu asiingie anga zangu. Atakula kichapo cha kufa mtu mpaka atajuta kuzaliwa.
 
kwani ni lazma ale watu wamuone?
Kuna mazingira unaweza ukakaa ukala.
Mwingine atataka kununua muhindi atembee nao
Turudi katika msingi wa imani Mtume anasema..

"Hakika matendo yanahukumiwa kutokamana na nia.."

Kama mimi nakula mbele ya aliyefunga na nia yangu ni kula kuna tatizo gani ?

Lakini pia kusema kwamba ni dharau huu ni muono wako tunauheshimu,lakini kuna ambao hawaoni kama ni dharau kula mbele ya aliyefunga na huu ni muono wao unatakiwa uuheshimu pia.

Kila mmoja ana maoni au muono wake usitake watu waheshimu muono wako tu.

Alafu mafundisho gani yanayosema kwamba kula mbele ya mtu aliyefunga sio ustaarabu ?

Kwa sababu kula ni kitendo chema katika uislamu,na kufunga ni kitendo chema katika uislamu.

Kwa hivyo mimi nikila mbele ya mtu aliyefunga kunakuwa na ubaya upi au dharau zipi ?
 
Ulazima ndp huo ustaarabu ninaosema.
Anunue chakula chake akae sehemu ale
Kwani ni lazima akila watu wasimuona ?

Kuna ulazima gani kwamba akila akajifiche wakati kula sio jinai kwa wale ambao hawalazimiki kufunga ?
 
Habarini za kutwa nyote.

Naomba niseme kwamba katika dini yetu ya uislamu hakuna pahala mtume kamkataza asiyekuwa muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna pahala qurani imekataza asiye muislamu kula mchana wa ramadhani.

Na wala hakuna sehemu wakati wa mtume imeonesha kwamba walikatazwa wasiokuwa waislamu wasile mchana wa ramadhani.

Katika masharti ya mtu kulazimika kufunga kwanza awe muislamu.

Kwa maana asiyekuwa muislamu hailazimiki kufunga,kama halazimiki kufunga maana yake ana uhalali wa kula mchana wa ramadhani kwa sababu sio muislamu.

Mtu anaweza akasema kwamba wamekatazwa wasile hadharani ?

Hadharani kwanza ni wapi kwa mujibu wa sheria ya dini ?

Watu wanakula kwenye migahawa hakuna anayekunywa chai na chapati anatembea pale kariakoo.

Hivyo kuhusu kula hadharani uislamu pia haujakataza kwa sababu neno hadharani ni pana katika muktadhwa huu.

Uislamu umekataza kwa muislamu ambaye hana udhuru wowote alafu akala mchana wa ramadhani,huyu anapata dhambi.

Lakini kuwakataza watu wasile mchana na kuwashambulia sio katika adabu za kiislamu kwa sababu

Kuna wagonjwa hawatakiwi kufunga.
Kuna wanawake wako kwenye siku
Kuna watoto
Kuna wazee
Kuna wasafiri
Kuna wasiokuwa waislamu

Hawa wote ruhusa kula mchana kwa mujibu wa ssheri ya uislamu wetu.

Sasa kama wanaruhusiwa kula mchana vipi wasiruhusiwe kula hadharani wakati hakuna katazo lolote la kula hadharani katika uislamu.

Allah anasema..

"Hakuna kulazimishana katika dini"

Asiye muislamu kumkataza asile mchana maana yake unamlazimisha akae na njaa jambo ambalo sheria ya dini imekataza.

Tutaheshimu sheria itakayowekwa na serikali lakini tunaomba sheria hizo zisinasibishwe na uislamu.

Ni bora uislamu ulaumiwe kwa sheria ambayo kweli imeiweka kama vile viboko kwa wazinifu n.k

Kuliko uislamu kulaumiwa kwa sheria ambayo haijaiweka kama hizi kukataza kula mchana wa ramadhani

Nakaribisha maswali.

Naomba kuwasilisha.
Kuna mifungo miwili inaendelea hivi sasa labda wameamua kuwakumbusha na wale majirani maana ya kufunga
 
Hili suala la kujificha wakati wa kula lingekaa kistaarbu, kuoneana huruma kwa mapenzi ingekuwa vyema na wala si kulazimishana.

Iwe ni hiyari, mtu kwa kumuonea huruma swahiba wake, rafiki yake jirani yake kwamba mwenzangu ana swaumu hivyo si vema nile mbele yake, ila akiamua kula muacheni ale. Ni kama vile mvuta sigara mstaarabu anaona aah, makaveli havuti sigara hivyo si vema nikaenda kuvuta nae akiwa karibu, mkeo mjamzito chakula fulani alikuwa anakioenda hapo kabla ila kwa sasa hawezi kukitia kinywani si vema ukanunua kwenda kukila mbele yake n.k n.k

Kwanza tunakubali soote hakuna kulazimishana katika dini.. Hii dini ni ya huruma na mapenzi japo watu(waislam tukichangia) tumeinajisi dini yetu, inaonekana ni dini ya ubabe, ugomvi kuchinjana chinjana n.k.

Enzi za mtume aliishi na watu wasiokuwa waislam
Kuna kisa kimoja cha umar ibn khattab kipindi cha uongozi wake, ilikuwa wale wadiojiweza wanapewa fungu(kwa sasa tunasema ama tunaweza fananisha na pensheni). Akamkuta mzee mmoja yuko dhaifu,ombaomba, kumuuliza vipi wewe pato lako unatumiaje, akasema yeye hapati chochote sababu yeye ni kafiri, umari akamuuliza ujanani mwako ulikuwa unatoa kodi, akajibu ndio, umar akawaamrisha wasaidizi wake aorodheshwe katika watu wanaopewa fungu, haiwezekani ujanani mwake alipe kodi vizuri tu kisha uzeeni asifaidike na alichotoa, jamaa akaanza kula pensheni

Hivi visa havipo kutufurahisha ila ni mafunzo kwetu, mtume aliishi na majirani wasiokuwa waislam vipi aliishi nao, kila mmoja ni muwakilishi wa Uislamu, huenda mtu asisome msahafu wala hadithi za mtume ila akajifunza uislam kupitia wewe.
Watu wamekuwa brainwashed mnoo, elimu hawana, allah aliposisitiza elimu alikuwa na maana yake, baada ya adamu kuumbwa cha kwanza kupewa ni elimu, mtume alipokabidhiwa utume ilifata ni elimu.

Tujitahidi kusoma, mwenye elimu ataendelea nayo akiendelea kuitafuta, ila pindi anapoona katosheka ndio ujinga unapoanzia.
 
Laiti misimamo kama hiyo Zanzibar ingekuwa inafanywa kwenye vitu vingine kama matamasha mziki na mambo mengine ya hovyo katika jamii ambayo kinyume na Uislamu ningewapa kongole.
 
Back
Top Bottom