Ujamaa uliofanywa na Nyerere ulikuwa umepingwa vikali sana na Karl Marx

Ujamaa uliofanywa na Nyerere ulikuwa umepingwa vikali sana na Karl Marx

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Habari.

Juzi kati nilikuwa nasoma na Kufasiri kitabu cha Karl Marx na Friedrich Engels, The Communist Manifesto. Kwenye kitabu hicho Marx anaeleza hatua hususa za ukuaji wa makabwela hadi kuja kuuondoa ubepari.

Anasema kuwa ulianza ukabaila. Katika huu ukabaila kulikuwa na wajasiriamali wa mijini ambao polepole wakaanza kupokonya nguvu za makabaila. Hawa wajasiriamali walipokua na kukomaa ndiyo wakaja kuwa mabepari.

Mabepari hawa hawakujali kitu zaidi ya faida. Waliwanyonya watu vibaya sana ili kukuza mitaji na kupata faida. Walau watwana wa enzi za ukabaila waliweza kuishi, makabwela waliotokana na ubepari walikuwa na hali mbaya sana. Hivyo anasema mwishowe makabwela watawatoa mabepari kwa nguvu na kuunda jamii isiyo na matabaka. Anasema mapinduzi ya makabwela yanakua polepole yakifuata mlolongo huu.

Sasa kwenye sehemu moja (Critical-utopian socialism and communism) anaeleza kuwa kuna watu, kabla hata makabwela hawajakomaa na kuweza kuwaondoa mabepari kama ilivyo ada, wao wanataka kuunda jamii isiyo na matabaka hewani tu.

Anasema ni waota ndoto ambao wanafikiri kwa kutumia maarifa wanaweza kuunda jamii ya kijamaa isiyo na matabaka bila kupitia hatua husika. Anadai kwa kufanya hivyo wanalazimika kukubaliana na mambo fulani ya mabepari, hivyo wanachounda kinakuwa siyo ujamaa wa kweli. Na pia wanazizimisha harakati zozote za makabwela kwa madai kuwa wanaunda jamii bora.

"Kwa hiyo basi, watu hawa wanapinga harakati zote za kisiasa, na hasa harakati za kimapinduzi; wanataka kufikia malengo yao kwa njia ya amani, na mipango ambayo hatma yake ni kushindwa, na kwa kutengeneza njia kwa ajili ya injili mpya ya kijamii."

Anadai ujamaa wa aina hiyo hatima yake ni kushindwa.

Ukiangalia utaona hii inafanana sana na ujamaa aliotaka kuunda Nyerere. Hakutaka kuacha makabwela wakue kwa ukuaji wao wa kiasili, alitaka kuunda jamii ya kijamaa kutokana na maono yake. Pengine ndiyo maana ulifeli.
 
Hebu toa wa nchi ambao ujamaa wa Karl Max ulifuata hizo hatua tajwa
Kwa maoni yangu Ujamaa kama alivyouwaza Marx bado haujatokea. Lakini naona nchi zinazosema ni social Democrats zinafuata kiasi. Kwao ubepari umeshakomaa, na taratibu tunaona makabwela wanachukua kutoka kwa mabepari kupitia kodi kubwa nk. Wengi, kama waliangukia kwenye huo Critical-Utopian socialism and communism(PEPO YA UJAMAA NA UKOMUNISTI)
 
Ujamaa ulitafsiriwa vibaya na wasomi mbalimbali. Ujamaa huu umebeba tofauti nyingi sana ukikagua. Ule wa ghana consiescism na humanism wa Zambia na ule Ubuntu wa SA. Ujamaa asili yake ni dhana za kifaransa zile za kipeasant. Ule ndo mtazamo halisi kabisa wa kinachotakiwa hapa. Inadai ardhi na ukulima na sio viwanda. Jean Jacquese (Kam sijakosea) aliliandika hili kabla ya Marx. Ujamaa umetokea katika mitazamo ya POPULISM.
Huu wa nyerere pia ulikuwa wa Aina yake kama ulivyo wa viongoz wengine
 
Kwa maoni yangu Ujamaa kama alivyouwaza Marx bado haujatokea. Lakini naona nchi zinazosema ni social Democrats zinafuata kiasi. Kwao ubepari umeshakomaa, na taratibu tunaona makabwela wanachukua kutoka kwa mabepari kupitia kodi kubwa nk. Wengi, kama waliangukia kwenye huo Critical-Utopian socialism and communism(EPO YA UJAMAA NA UKOMUNISTI)
Ujamaa kiuhalisia lazima utokee kwenye nchi yenye viwanda (maendeleo makubwa ya viwanda). Na ndo mana enzi hizo Marx aliitabir kuwa ENGLAND ndo utakuw nchi ya kwanza.

Kwa nchi za KIAFRIKA kutekeleza Sera za Ujamaa sio jambo jipya. Ila ni nje ya mawazo ya Marx. Ndo mana nchi ya kwanza ya kikomunist ilifeli Kwa sabb y wananchi wenyew kudai umagharibi. Kwan nchi za maghafrib zimeendelea Sana kiuchumi na teknojia. Tukitaka mambo yaende Sawa hapa hata mtazamo w maendeleo utafsiriwe upya. Ukijikita kwenye Uchumi na teknolojia, bhas ujue utadai ukapitalisti uwepo tu.
 
Ujamaa ulitafsiriwa vibaya na wasomi mbalimbali. Ujamaa huu umebeba tofauti nyingi sana ukikagua. Ule wa ghana consiescism na humanism wa Zambia na ule Ubuntu wa SA. Ujamaa asili yake ni dhana za kifaransa zile za kipeasant. Ule ndo mtazamo halisi kabisa wa kinachotakiwa hapa. Inadai ardhi na ukulima na sio viwanda. Jean Jacquese (Kam sijakosea) aliliandika hili kabla ya Marx. Ujamaa umetokea katika mitazamo ya POPULISM.
Huu wa nyerere pia ulikuwa wa Aina yake kama ulivyo wa viongoz wengine
Nafikiri hizi aina nyingine zote zilikuwa, kwa maneno ya Marx mwenyewe, "Kujenga ngome hewani." au "Injili mpya." ni watu waliotaka kuunda ujamaa kutokana na maono yao lakini kumbe una njia yake ya asili.
 
Nafikiri hizi aina nyingine zote zilikuwa, kwa maneno ya Marx mwenyewe, "Kujenga ngome hewani." au "Injili mpya." ni watu waliotaka kuunda ujamaa kutokana na maono yao lakini kumbe una njia yake ya asili.
Sorts of common ni kilimo. Ujamaa inadai Sana kilimo kuliko chochote kile. Ujamaa ni mbadala wa ukapitalisti. Kama ukapitalisti ni viwanda na miji bhas Ujamaa ni vijiji na kilimo. Tukitaka Yale magorofa kariakoo na posta yawe hayana thamani tuingie kwenye Ujamaa. Na ndo hapo wenye mitaji yao mule wamekufa
 
Ujamaa kiuhalisia lazima utokee kwenye nchi yenye viwanda (maendeleo makubwa ya viwanda). Na ndo mana enzi hizo Marx aliitabir kuwa ENGLAND ndo utakuw nchi ya kwanza.

Kwa nchi za KIAFRIKA kutekeleza Sera za Ujamaa sio jambo jipya. Ila ni nje ya mawazo ya Marx. Ndo mana nchi ya kwanza ya kikomunist ilifeli Kwa sabb y wananchi wenyew kudai umagharibi. Kwan nchi za maghafrib zimeendelea Sana kiuchumi na teknojia. Tukitaka mambo yaende Sawa hapa hata mtazamo w maendeleo utafsiriwe upya. Ukijikita kwenye Uchumi na teknolojia, bhas ujue utadai ukapitalisti uwepo tu.
Sahihi kabisa. Ujamaa wa Kimarx unatoka kwenye nchi ambayo iko mbali kiviwanda. Japo nina wasiwasi kama tulichokuwa tunafanya Wafrika kabla ya ukoloni kilikuwa ni ujamaa.
 
Sorts of common ni kilimo. Ujamaa inadai Sana kilimo kuliko chochote kile. Ujamaa ni mbadala wa ukapitalisti. Kama ukapitalisti ni viwanda na miji bhas Ujamaa ni vijiji na kilimo. Tukitaka Yale magorofa kariakoo na posta yawe hayana thamani tuingie kwenye Ujamaa. Na ndo hapo wenye mitaji yao mule wamekufa
Kweli, Marx alipendekeza hatua hizi kumi. Zinatisha kwa jamii ya sasa.

  • Kukomesha umiliki binafsi wa ardhi na kuweka kodi kwenye ardhi yote kwa ajili ya manufaa ya umma.
  • kodi kubwa inayotegemea kipato.
  • Kukomesha haki zote kuhusiana na urithi.
  • Kutaifisha mali za wahamiaji na waasi wote.
  • Kuweka biashara ya ukopeshaji mikononi mwa serikali, kwa kutumia benki na mtaji wa taifa, benki hiyo ikihodhi biashara hiyo.
  • Kuweka njia za mawasiliano na usafirishaji mikononi mwa serikali.
  • Kupanua viwanda na nyenzo zingine za uzalishaji zinazomilikiwa na serikali; kuanza kulima maeneo yaliyokuwa tupu, kuboresha ardhi kulingana na mpango wa pamoja.
  • Uwajibikaji sawa wa wote katika kazi. Kuanzishwa kwa majeshi ya uzalishaji, hasa katika kilimo.
  • Kuunganisha kilimo na viwanda; kuondoa polepole tofauti ya mijini na vijijini, kwa kutawanya watu kwa usawa katika nchi.
  • Elimu bure kwa watoto wote katika shule za serikali. Kukomesha ajira za watoto viwandani kama ilivyo sasa. Kuhusianisha elimu na uzalishaji wa viwandani nk.
 
Sahihi kabisa. Ujamaa wa Kimarx unatoka kwenye nchi ambayo iko mbali kiviwanda. Japo nina wasiwasi kama tulichokuwa tunafanya Wafrika kabla ya ukoloni kilikuwa ni ujamaa.
Si ujamaa. Sisi tulikuwa tuna tamaduni zetu na mifumo yetu ya kuishi tu. Huu mfumo waliotuachia wakoloni uliingia kinguvu na umeachwa Kwa haraka Sana ndo mana unatusumbua. Kwa mfumo Kam huu mpaka kutulia nao sisi Kam sisi tukajiendesha nao si jambo dogo. Mpaka Leo ndo mana tunawategemea. Hii kitaalam inaitwa social disorganization. Tunachodai Kwa wakoloni ni kwamba wametuachia mfumo magumu kuiendesha hatuwez ndo mana tunawategemea.
Nikutoe katika wasiwasi mfumo wa Mali binafsi afrika ulishakuwepo, hata matumiz ya hela Kilwa yalikuwepo. Waafrika tulikuwa katika mfumo usio wa kikapitalist Lakin sio ujamaa. Tuliishi katika MORAL ECONOMY
 
Ujamaa ulitafsiriwa vibaya na wasomi mbalimbali. Ujamaa huu umebeba tofauti nyingi sana ukikagua. Ule wa ghana consiescism na humanism wa Zambia na ule Ubuntu wa SA. Ujamaa asili yake ni dhana za kifaransa zile za kipeasant. Ule ndo mtazamo halisi kabisa wa kinachotakiwa hapa. Inadai ardhi na ukulima na sio viwanda. Jean Jacquese (Kam sijakosea) aliliandika hili kabla ya Marx. Ujamaa umetokea katika mitazamo ya POPULISM.
Huu wa nyerere pia ulikuwa wa Aina yake kama ulivyo wa viongoz wengine
Nimekuelewa naongezea nyama "Si kila andiko linakua sehemu ya muongozo wako bali akili yako na mazingira yako yanakufanya uandike yako na kuendeleza yaliyoandikwa na wengine"

Sent from my Infinix X572 using JamiiForums mobile app
 
Si ujamaa. Sisi tulikuwa tuna tamaduni zetu na mifumo yetu ya kuishi tu. Huu mfumo waliotuachia wakoloni uliingia kinguvu na umeachwa Kwa haraka Sana ndo mana unatusumbua. Kwa mfumo Kam huu mpaka kutulia nao sisi Kam sisi tukajiendesha nao si jambo dogo. Mpaka Leo ndo mana tunawategemea. Hii kitaalam inaitwa social disorganization. Tunachodai Kwa wakoloni ni kwamba wametuachia mfumo magumu kuiendesha hatuwez ndo mana tunawategemea.
Nikutoe katika wasiwasi mfumo wa Mali binafsi afrika ulishakuwepo, hata matumiz ya hela Kilwa yalikuwepo. Waafrika tulikuwa katika mfumo usio wa kikapitalist Lakin sio ujamaa. Tuliishi katika MORAL ECONOMY
Kabisa. Hii mifumo ya kikoloni, hasa huu wa soko huria hatuiwezi kabisa. Tulikuwa na mfumo mzuri ambao ulifanya tujitosheleze mahitaji yetu.
 
Kabisa. Hii mifumo ya kikoloni, hasa huu wa soko huria hatuiwezi kabisa. Tulikuwa na mfumo mzuri ambao ulifanya tujitosheleze mahitaji yetu.
Sera ya Soko huria ni ukapitalisti uliokomaa. Unazidisha umasikin Kwa maskin na unaongeza utajiri. Matatizo yote tunailaum Serikali sabb ndo pekee inayoweza kulainisha ugum wa huu mfumo. Tatizo la ajira, umasikin na magonjwa ni matatizo ya kawaida kwa mfumo wa kikapitalist. Sabb unataka survival of fit, mwenge nguv awe na nguvu. Yan maskini kutoka kwenye umasikin imekuwa ishu. Kama baba hajaajiriwa mtot kuajiriwa nako ni ishu. Kuna grup la watu haya matatizo wanarithishana.
Serikali peke yake inawez pindua hili au kuweka ahueni. Cha ajab walioko kweny mikakati ndo haohao wanufaika wa mfumo huo.
 
Ujamaa ni falsafa iliyolaaniwa kwa kumkataa Mungu.
Nani kasema?. Sayansi ya Kimarx haiamin kama umasikin na utajir ni mipango ya mungu. Wakat huohuo dini imesema mungu ameumba maskini ili wasidiwe na matajiri, mitihani ya mungu.
SWALI : una uhakika tukiingia kwenye mfumo wa umiliki wa wTu wote kwenye Mali kutakuwep na tajir au maskini?
 
Sahihi kabisa. Ujamaa wa Kimarx unatoka kwenye nchi ambayo iko mbali kiviwanda. Japo nina wasiwasi kama tulichokuwa tunafanya Wafrika kabla ya ukoloni kilikuwa ni ujamaa.
Ujamaa siyo umbile la binaadam,ni fantasy tu... nyerere alipopewa nchi alikua na umri wa miaka 39 tu!!..umri mdogo kupambanua Mambo ya miundo wa jamii,mahaba yalimuongoza badala ya tafakuri jadidi,walau angemsikiliza kambona wakajadiliana kwa 'nia swafi'
 
Sorts of common ni kilimo. Ujamaa inadai Sana kilimo kuliko chochote kile. Ujamaa ni mbadala wa ukapitalisti. Kama ukapitalisti ni viwanda na miji bhas Ujamaa ni vijiji na kilimo. Tukitaka Yale magorofa kariakoo na posta yawe hayana thamani tuingie kwenye Ujamaa. Na ndo hapo wenye mitaji yao mule wamekufa
hujui mambo.Wacha kupotosha!
 
Back
Top Bottom