Ujenzi Mkubwa unaoendelea Kigamboni(Dege Eco Village), ni mradi wa nani?

Ujenzi Mkubwa unaoendelea Kigamboni(Dege Eco Village), ni mradi wa nani?

Ni mradi wa ujenzi wa nyumba takribani 7,000. Mradi huu ni ubia kati ya kampuni ya Azimio na NSSF.

Bw Iqbal ni mwenye eneo hilo na mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Azimio.

Dkt Faustine Ndugulile
MB-Mbunge Kigamboni

Asante kwa taarifa. Ni sehemu ya mradi wa new Kigamboni?
 
nawapongeza wakazi wa kigamboni kwa kumpata mbunge mimi mbunge wangu hataki kuulizwa maswali mara ya mwisho tulionana wakati wa kampeni mwaka 2010
 
Huu ni mfano wa kuigwa kwa viongozi wetu kuja kujadiliana kwa hoja zinazoelimisha na kujenga jamii zetu kiujumla pongezi kwako Dr F. Ndugulile kwa kuwa nasi pamoja
 
Mimi leo nitakuwa msomaji tu mpaka kesho nifanikishe ya TANRODS yetu mh Mbunge
 
Si Kweli! Uvumi unaotoka na kutakuwa na taarifa sahihi. Mradi wa Mji Mpya wa Kigamboni ni mradi wa Serikali wa kujenga Mji mbadala pembezoni mwa DSM. Wazo la Mji Mpya wa Kigamboni ni zuri na wananchi wanaliunga mkono. Matatizo yapo kwenye utekelezaji. Matatizo yenyewe ni kama yafuatayo:
1. Sheria zinazosimamia mchakato huu ni nzuri (Sheria ya Ardhi na.4 ya mwaka 1999 na Sheria ya Mipango Miji na.8 ya 2007). Wanaovunja Sheria ni watendaji wa Wizara ya Ardhi na sio wananchi. Wananchi wanataka Serikali ifuate Sheria.
2. Ushirikishwaji: Watendaji wa Wizara ya Ardhi wanataka haki ya mwananchi kama mmiliki wa ardhi ianze na kuishia katika kulipwa fidia pekee. Wananchi wanataka wawe wadau katika mradi huu na kupewa kipaumbele cha kwanza kwenye ardhi yao.
3. Kumekuwa na usiri na sintofahamu kuhusu haki, Stahili na hatma za wananchi wa Kigamboni: Wananchi wanataka washirikishwe kikamilifu na haki zao ziwekwe wazi na waziafiki.
4. Ucheleweshaji mkubwa wa mradi: Kwa muda wa miaka Sita wananchi wa Kigamboni hawajanipa, hawakarabati, hawawezi kuuza Nyumba wala viwanja vyao na hawakopesheki kwenye mabenki. Hali inayoletea unyonge na kudumaza maendeleo yao binafsi.

Matatizo haya yakitatuliwa, mradi unaweza kupokelewa vizuri zaidi na wananchi.

Mheshimiwa Dr F. Ndugulile,

Je eneo la Potea/Puna pale kuna mipango miji yoyote ya maendeleo?
 
Last edited by a moderator:
Nami Nashukuru. Tuzidi kuwasiliana ili kubadilisha mawazo kuhusu ya msingi kwa Kigamboni na Taifa letu. Sisi Wabunge sio kwamba tunakuwa kila kitu, mengine ya msingi hutoka kwa wale tunaowawakilisha.

Dr hizo zitauzwa zitagawiwa bure kwa wananchi km mwalimu nyerere alivyofanya Magomeni ilala na kinondoni
 
Nami Nashukuru. Tuzidi kuwasiliana ili kubadilisha mawazo kuhusu ya msingi kwa Kigamboni na Taifa letu. Sisi Wabunge sio kwamba tunakuwa kila kitu, mengine ya msingi hutoka kwa wale tunaowawakilisha.
Kama robo yenu mngekuwa hivi hakika tungekuwa tumesogea hatua za uhakika zaidi!!!!!!!
Kwa mara nyingine tena nitoe pongezi kwako na kukusihi uendelee hivi!!

Mungu akubariki sana
 
Nami Nashukuru. Tuzidi kuwasiliana ili kubadilisha mawazo kuhusu ya msingi kwa Kigamboni na Taifa letu. Sisi Wabunge sio kwamba tunakuwa kila kitu, mengine ya msingi hutoka kwa wale tunaowawakilisha.

Saluti mkuu Dr. Ndugulile
 
Mimi leo nitakuwa msomaji tu mpaka kesho nifanikishe ya TANRODS yetu mh Mbunge

Bw Yericko Nyerere,

Wewe na wadau wenzako mlikuja kwangu na kunishirikisha katika jambo la jamii mnalotaka kulifanya. Binafsi nilimefurahia kuona wananchi wakichukua hatua kujiletea maendeleo na kutatua kero zinazowakabili.

Nimetimiza wajibu wangu kama nilivyoahidi. Nimetimiza kuwapatia kile mlichotaka. Bado mna wajibu wa kunipatia contacts za wale tuliowaongelea ili kukamilisha kazi yenu.

Hongereni kwa hatua mliyofikia, ni mfano wa kuigwa na inanipa wepesi kama mwakilishi wenu.
 
Mheshimiwa Dr F. Ndugulile,

Je eneo la Potea/Puna pale kuna mipango miji yoyote ya maendeleo?
Mkuu!

Hakuna Master Plan wala mchoro wa Mpango Miji kwa eneo hili. Vie vile Wizara ya Ardhi kupitia KDA imezuia upimaji.

Nimewaandikia barua na kuongea na viongozi wa Wizara hii ili waweze kuruhusu upimaji kwenye kata za Kimbiji, Kisarawe II na Pemba Mnazi.

Maendeleo ya wananchi yanakwenda kwa kasi zaidi kuliko Mipango ya Wizara ya Ardhi. Nimewashauri wao wasimamie miongozo na waachie Manispaa ya Temeke na sekta binafsi wapime na kuendeleza maeneo yao.
 
Huu ni mradi wa kifedhuli sanaaa!

Mbunge Dr F. Ndugulile hajasema ukweli kwani hiyo kampuni inajenga hayo maghorofa ni kwa ajili ya kuwauzia Wananchi ambao watabomolewa nyumba zao kwenye mradi wa heka Elfu 5 kwa ajili ya mji mpya wa Kigamboni.

Watakachofanya ni badala ya kumpa kila mwananchi hela yake aondoke (let say Mil 200) baada ya kubomolewa nyumba yake atapewa floor moja kwenye moja ya ghorofa hilo na kesi itakuwa imekwisha.

Kwanini Mwananchi apangiwe wapi pa kuishi na aina gani ya nyumba ya kuishi ! Huu mradi utaleta ngumi siku moja huko Kigamboni....
 
Huko ni kumwezesha mhindi,kwanini waingie ubiya naye na wasinunue wenyewe ardhi,huu ubia si wa bure nadhani hata Dau atakuwa na kahisa kake kupitia kwa huyo mhindi
 
Nami Nashukuru. Tuzidi kuwasiliana ili kubadilisha mawazo kuhusu ya msingi kwa Kigamboni na Taifa letu. Sisi Wabunge sio kwamba tunakuwa kila kitu, mengine ya msingi hutoka kwa wale tunaowawakilisha.

nakusalimu sana Dr.nina kaswali nakuomba sana unijibu
Mbona ujenzi wa hii barabara ya feri kibada via tungi umesimama kabisa au inasubiriwa 2015 kampeni hii barabara ya katini faraja kwa wengi ila ndio mbaya sana
 
The Fixer

Hili nalisikia kwako kwa mara ya kwanza...

Kama una ufahamu zaidi tuwasiliane. Ninavyojua miradi ni miwili tofauti. Nipo tayari kukupa contact zangu.
 
Back
Top Bottom