Ujenzi rahisi kwa kutumia interlock blocks, jenga popote, jenga sasa

Ujenzi rahisi kwa kutumia interlock blocks, jenga popote, jenga sasa

Yaani 50kgs za Cement unachanganya na udongo wenye uzito gani?
Nyie ni kampuni bila shaka mnafanya kazi kwa vipimo.
Hatupimi kwa kilo,na kama nilivyoelezea,ratio inategea na aina ya udongo uliyopo kwenye eneo lako,kuna jinsi ya kupima udongo ili kujua mchanganyiko wake,ukishajua ndio utajua mfuko mmoja upige tofali ngapi.
 
Interlock blocks au bricks ni aina ya tofali zinazofungamana kwenye ujenzi bila kutumia zege(motor) kuziunganisha,zinapigwa kwa saruji na udongo wenye mfinyazi kiasi. Tofali hizi zinatumia saruji kidogo sana(10%) tu ya udongo. Hizi tofali zipo miundo mingi sana lakini nitazungumzia aina ya Hydraform.
View attachment 2303148
Hydraform ndio waasisi wa teknolojia hii ya tofali lakini kulingana na soko kila sehemu wanatengeneza mashine.

Aina hii ni maarufu sana Tanzania
Mashine ya kupiga Hydraform inatumia hydrolic ambayo ina uwezo wa kupiga tofali zaidi ya 2000 kwa siku kwa kinu kimoja.

View attachment 2303149
Kuna mashine za mkono pia ambazo kwa kinu kimoja kinapiga tofali 400.
Uzuri wa Hydraform unapiga size unazotaka za urefu wa tofali na vipande vyake bila kuja kukata wakati wa ujenzi.
Urefu wa tofali huanzia nchi 18-24 na upana ni nchi 9 na 6 na kimo ni nchi 5.
Mfuko mmoja wa saruji unaweza kupiga tofali 80 mpaka 100 ikitegemea na aina ya udongo uliopo eneo lako.

URAHISI WA UJENZI WAKE HUU
1.Baada ya kuwa na tofali kinachofuata ni ujenzi au kupandisha boma lako. Tofali ya kwanza baada ya msingi ni kuset boma. Ujenzi wake ni rahisi kwa sababu hakuna haja ya motor kwenye kupandisha boma lako,utapachika tu ila utazingatia kanuni zote za ujenzi.

2.Hakuna haja ya plasta na skim baada ya ujenzi wako,hapo utaokoa saruji,mchanga,maji na gharama za fundi.

3.Kuhimili mitikisiko na vishindo hivyo si rahisi kuona nyumba hizi zikiwa na ufa sababu tofali zinapumua. Kama itatokea tetemeko au bomoa bomoa unaweza kuhama na tofali zako.

Faida ziko nyingi na kitaalamu ujenzi wa tofali za kufungamana unapunguza 40% ya gharama za ujenzi, mfano kama ulipanga kujenga kwa milioni 10 basi huenda ukatumia milioni 6 tu.

Karibu kwa mnaotaka kujenga,iwe ni kwa awamu kulingana na uwezo wako au kwa pamoja pia. Gharama zetu ni rafiki kabisa.

Kama una fundi wako karibu tukuuzie tofali. Kuna option mbili za kupata tofali.
1.Tofali moja tutakuuzia Tsh.650 kwa ndani ya Dar na maeneo ya jirani mikoani tutaelewana tu.
2. Tunaweza kukupigia tofali kwa Tsh. 250 ikiwa utanunua matirio yote mwenyewe.


View attachment 2303152

Kama una maoni au swali karibu uulize na utajibiwa iwezekanavyo.

MAWASILIANO YETU
Tupigie simu au WhatsApp 0625547181
Telegram t.me/ujenzirahisi
Facebook @ujenzirahisi
Instagram @ujenzirahisi
Tiktok @ujenzirahisi
KARIBU UJENZIRAHISI TUKUJENGEE UTAKAVYO,IWE NI KIDOGO KIDOGO AU KWA PAMOJA
Mku nyumba room sita kwa udhoefu wako inaweza kutumia tofali ngapi?
Asante
 
IMG_20220716_173336_735.jpg
 
Ongezea no 4.zinapunguza mda wa kujenga ndani ya wiki boma limesimama hii ni nzuri kwa wasio mda wa kusimamia ujenzi mfano wakaao nje ya nchi, au mikoani ndani ya mda wa likizo ya mwezi mmoja tu mtu anakabidhiwa nyumba yake, si unajua uaminifu hakuna we mtumie mtu akusimamie ujenzi ukutane na kituko, akiwa muungwana atajenga two in one yaani nae atajenga yake kupitia yako.
Je jins zinavyoshikan hakuna haja ya kuweka nguzo kwa ajili ya kuzisaidia hizo tofali??
 
Mfuko unatoa kwanzia 80 mpaka 100 kulingana na udongo wa eneo lako
Kwa hiyo hata mchangwa wa dar unaweza kujengea hiz tofali?? Na je kwa kupangana huko ikitokea tetemeko la ardhi haziwez kuleta balaa?? Au huwa zinawekewa nguzo??
 
Je jins zinavyoshikan hakuna haja ya kuweka nguzo kwa ajili ya kuzisaidia hizo tofali??
Hazihitaji sababu zinajilock zenyewe hivyo zinashikana kwa balance moja nyumba nzima, zinakuwa na nguvu ya uvutano moja.
 
Mkuu, una uhakika kabisa ujenzi wa kutumia tofali hizo una save hadi 40%?, maana mimi nilikuwa mmoja wa wasimamizi wa nyumba za NHC miaka ya 2015-2017, ambapo tulisimamia miradi yote ya NHC Tanzania, ikiwemo na ule wa Mikwambe+Mwongozo
 
Kwa hiyo hata mchangwa wa dar unaweza kujengea hiz tofali?? Na je kwa kupangana huko ikitokea tetemeko la ardhi haziwez kuleta balaa?? Au huwa zinawekewa nguzo??
Hakuna madhara kaka,hatutumii mchanga,ni udongo tu,wenye ufinyanzi kwanzia 7% mpaka 40%
 
Back
Top Bottom