Ujenzi wa Ghorofa Moja

Ujenzi wa Ghorofa Moja

Mkuu nilitaka nichangie ila nimeona comment za Robert Josephat, ZeMarcopolo, Kaka' na moghaka na wengine kadhaa wamefanya justice nilichotaka kuchangia. Nakushauri kwenye sehemu kama hii ambapo unaomba ushauri hususan wa aina mbili, angalia ule uliozidi kwa kuchangiwa na wadau wengi uufanyie kazi. Kama ulikua na option A na B halafu A ikachaguliwa na watu 9 na B watu 5 then you know what to choose.
Ni kama chadema yani. Majority likes ndo jibu. Kila la kheri kaka. Urudi kwenye uzi huu huu utuambie uli pursue option gani. We will use your site as a case study au practical example. Thanks mkuu.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Sasa, suala la supervision likoje hapa? I mean, ukishaweka mafundi na wameanza ujenzi, unasimamiaje kuhakikisha kuwa kila kitu kimeenda sawa sawa linapokuja suala la uchanganyaji?

Walau ukitaka kuhakikisha uchanganyaji wa zege unakuwa wa viwango vinavyotakiwa hakikisha unakuwa na mtaalamu siku hiyo ya uchanganyaji. Najua hata likizo ya wiki inakutosha kabisa kusimamia zoezi hili mkuu.
Muhimu sana

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Sijui kama haka kanakula tumilioni tungapi.... AMAFUMU ?

House-Exterior-3D-Model2.jpg

Duuh
Kaka hapa kiukweli jiandae na kama 100. Ila hiyo mia unahakikisha unaenda na mafundi sawa mwanzo mwenga. Ikiwezekana kushinda site kabisa. La sivyo utalia kwa gharama.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Nimevutiwa na hii mada sana, napenda nyumba ya ghorofa tatizo mifuko imechakaa.

Inawezekana sana ndugu yangu. Just focus and have it as a goal to accomplish. Don't stress on it too much and you will find yourself living your dream. It can be done. Play your part.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kwenye sekta ya ujenzi ,Haas ghorofa mkuu nakuaminiaga sana kwa kweli. Umatusaidia sana, na labda ndio anga zako hizi za kujidai.

Tatizo lipo ukihamia tu lile jukwaa pale juu unabadilika kabisa

Ha ha ha ha ha
Nani kakwambia ma engineer au watu wa kushinda site wanapendaga utani?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Naangalia option kujaribu kujenga kighorofa kimoja japo nilale juu, fundi ameniambia nichague kati ya option mbili
  1. kulaza matofali
  2. kutumia nguzo
Namaanisha kama nikilaza matofali floor slab ya juu itakua supported na hayo matofali bila nguzo. Kama nikiopt nguzo nitasimamisha matofali kawaida, niko tutani naombeni ushauri wataalamu ujenzi nitaanza soon ndio nafanya site clearance na kukusanya vifaa. Niko jijini

Sio rahisi sana kutoa ushauri hapa kuhusu jambo hili. Kwanza huyo "fundi" unayemzungumzia ni "Architect" au "Structural Engineer" (ama ni "Mason" tu)? Hao wawili kama walihusika katika kusanifu jengo hilo basi unahitaji ushauri wao.

Uamuzi wa kutumia nguzo ama la unaweza kuwa ni structural au unaweza kuwa achitectural (or both!). Kwa hivyo, hao watu wawili ni lazima upate ushauri wao kwa sababu wao ndio wanalijua jengo lango linavyotakiwa kuwa na pia wanaijua site yako (na zaidi wanao wajibu wa kitaaluma/kitaalamu). Kama kwa sababu moja ama nyingine hukuwatumia wataalamu hawa katika kusanifu jengo lako,basi ushauri wangu ni kuwa fuata mchoro kama ulivyo (usifanye mabadiliko, unless mmoja wapo wa wataalamu hao ametizama (review) kazi yako na kukushauri/kuafiki mabadiliko hayo). Kama hata mchoro huna, basi hiyo ni "shughuli" nyingine tena!

Tukizungumzia nguzo, watu wengi wanafikiri zaidi zege na nondo! Wanasahau kuwa nguzo inaweza pia kujengwa kwa hayohayo matofali kutegemeana na aina ya mzigo au forces inayozatamiwa kukabiliana nazo na pia muonekano unaotegemewa.

Kwa ujumla uamuzi wa suala lako unahitaji kuzingatia pamoja na yafuatayo:
(a) Site - aina ya udongo na uwezo wake (bearing capacity)
(b) Aina na kiwango ya mzigo unaokusudiwa kubebwa (dead loads, live loads)
(c) Kiwango na ukuwa wa matofali unaotegemea kutumia (6", 5" etc, ya mkono/ya machine, mangapi kwa mfuko wa cement - kuna matofali unaweweza kukwaruza kwa vidole tu unaona linapukuchika!)
(d) Muonekano uanotegemewa - Wakati mwingine nguzo zinaongeza "ladha" ya jengo!
(e) Flexibility (nimeona wadau kadhaa wameligusia hili)
(f) Ukubwa/upana wa vyumba (spans) - kama ni span kubwa kuna uwezekano wa kuwa na tensile stress kubwa kwenye vertical members. Matofali hayawezi kuhimili tensile stress.

Kwa hayo machache, unaweza kuona umuhimu wa kuongea kwanza na wataalamu wako kabla hujafanya mabadiliko.

Nakutakia mafanikio mkuu.
 
Duuh
Kaka hapa kiukweli jiandae na kama 100. Ila hiyo mia unahakikisha unaenda na mafundi sawa mwanzo mwenga. Ikiwezekana kushinda site kabisa. La sivyo utalia kwa gharama.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Mkuu hekimatele unanihakikishia kwamba nukiwa na 100m namiliki mjengo wa namna hiyo hapo juu?
Jee wewe ni engineer?
 
Last edited by a moderator:
Usikonde kaka ngoja nitafute hiyo 100m kwanza.

Komaa mkuu. Zichange mpaka zifike. Hakuna kuacha chenji chenji hovyo. Mambo ya tip na keep change punguza.
Misele ya baa na mitoko ya kula bata na kwio punguza kiduuuchu. Sio sana. tehe tehe teheeeeee.
Mpaka 100 ipatikane.
 
Sio rahisi sana kutoa ushauri hapa kuhusu jambo hili. Kwanza huyo "fundi" unayemzungumzia ni "Architect" au "Structural Engineer" (ama ni "Mason" tu)? Hao wawili kama walihusika katika kusanifu jengo hilo basi unahitaji ushauri wao.

Uamuzi wa kutumia nguzo ama la unaweza kuwa ni structural au unaweza kuwa achitectural (or both!). Kwa hivyo, hao watu wawili ni lazima upate ushauri wao kwa sababu wao ndio wanalijua jengo lango linavyotakiwa kuwa na pia wanaijua site yako (na zaidi wanao wajibu wa kitaaluma/kitaalamu). Kama kwa sababu moja ama nyingine hukuwatumia wataalamu hawa katika kusanifu jengo lako,basi ushauri wangu ni kuwa fuata mchoro kama ulivyo (usifanye mabadiliko, unless mmoja wapo wa wataalamu hao ametizama (review) kazi yako na kukushauri/kuafiki mabadiliko hayo). Kama hata mchoro huna, basi hiyo ni "shughuli" nyingine tena!

Tukizungumzia nguzo, watu wengi wanafikiri zaidi zege na nondo! Wanasahau kuwa nguzo inaweza pia kujengwa kwa hayohayo matofali kutegemeana na aina ya mzigo au forces inayozatamiwa kukabiliana nazo na pia muonekano unaotegemewa.

Kwa ujumla uamuzi wa suala lako unahitaji kuzingatia pamoja na yafuatayo:
(a) Site - aina ya udongo na uwezo wake (bearing capacity)
(b) Aina na kiwango ya mzigo unaokusudiwa kubebwa (dead loads, live loads)
(c) Kiwango na ukuwa wa matofali unaotegemea kutumia (6", 5" etc, ya mkono/ya machine, mangapi kwa mfuko wa cement - kuna matofali unaweweza kukwaruza kwa vidole tu unaona linapukuchika!)
(d) Muonekano uanotegemewa - Wakati mwingine nguzo zinaongeza "ladha" ya jengo!
(e) Flexibility (nimeona wadau kadhaa wameligusia hili)
(f) Ukubwa/upana wa vyumba (spans) - kama ni span kubwa kuna uwezekano wa kuwa na tensile stress kubwa kwenye vertical members. Matofali hayawezi kuhimili tensile stress.

Kwa hayo machache, unaweza kuona umuhimu wa kuongea kwanza na wataalamu wako kabla hujafanya mabadiliko.

Nakutakia mafanikio mkuu.
Gharama ya vile vibao ikoje na vinalipiwa wapi na kiasi gani?
 
Gharama ya vile vibao ikoje na vinalipiwa wapi na kiasi gani?
Vibao gani mkuu? Au unazungumzia stickers? Kama ni stickers inategemea ni vya bodi ipi na gharama ya mradi pia! Kuna ma engineer, wakandarasi, na wasanifu/wakadiriaji no wote hao nadhani wanatakiwa kuweka sicker kutoka kwenye bodi zao. Kama ni vibao kwa maana ya vibao tu, hiyo ni kazi ya fundi selemala na painter ili mradi yale maandishi yakidhi viwango/ matakwa tu.
 
ninamaanisha zile stickers zao,na je ni lazima kuweka kwa ujenzi wa ghoroma moja kwa nyumba tu ya kuishi kwa ujenzi wa hela ya mshahara ,sio zile za kujenga kama uyoga fasta?na hizo bodi zita play part ipi katika ujenzi huo,au ndio unawalipa tu hela bila kazi maalum?
 
Kila nikitaka kuacha jf roho inagoma,pamoja na kugombana sana humu na faida tunaipata sana tu
 
Idorome, Mimi pia ni Architect,

Fundi wako yupo sahihii, msikilize, ila zingatia ubora wa udongo hapo unapojenga hiyo nyumba yako.

Nyumba ya ghorofa moja haiitaji nguzo, ni kwa kufuata kasumba watu hujenga nyumba na nguzo, unaweza kujenga ghorofa moja bila nguzo, binafsi nimejenga ghorofa kadhaa hapa mjini (including yangu) bila nguzo na hazina tatizo hata kidogo,

Zingatio

Hakikisha tofari zinakuwa imara kama unachukua option 1. na kama hauamini tofati zako basi ni bora ukachukua option 2.

Ningejua unajenga wapi ningekueleza matofari mazuri yalipo.

spacarchitects@gmail.com
 
Mkuu nimeamua kutumia option ya kulaza matofali kwani sina mpango kubadili ramani na nimeona kwa mchoro wangu huenda ikawa ndio best option, uko sahihi kama ukitumia nguzo unaweza kumimina slab ya first floor bila kumaliza ground floor kwani kwa njia ya nguzo kila floor inajitegemea(kwa uelewa wangu)


safi sana mkuu, napenda kujifunza practical stages za ujenzi wa ghorofa

vipi umeamua kutumia nguzo au kulaza matofali?

hivi unaweza kumimina slab ya first floor bila kumalizia ground floor kwanza? hapa nina maana first floor itakuwa imebebwa na nguzo tu so inategemea uimara wa hizo nguzo
 
Duuh
Kaka hapa kiukweli jiandae na kama 100. Ila hiyo mia unahakikisha unaenda na mafundi sawa mwanzo mwenga. Ikiwezekana kushinda site kabisa. La sivyo utalia kwa gharama.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Hii mkuu jiandae si chini ya TZS 150m kama unataka itoke kama ninavyoiona pichani hapo!
 
Hiii nyumba si chini ya mil 250. Nina uzoefu
 
Back
Top Bottom