Ujenzi wa Ghorofa Moja

Ujenzi wa Ghorofa Moja

Vipi kuhusu ujenzi wa ghorofa moja kwa kutumia tofali za kuchoma hasa mkoa wa Morogoro?ushauri wenu wakuu

mkuu hii ni mpaka nguzo za zege huwezi kujenga bila nguzo
 
Idorome, Mimi pia ni Architect,

Fundi wako yupo sahihii, msikilize, ila zingatia ubora wa udongo hapo unapojenga hiyo nyumba yako.

Nyumba ya ghorofa moja haiitaji nguzo, ni kwa kufuata kasumba watu hujenga nyumba na nguzo, unaweza kujenga ghorofa moja bila nguzo, binafsi nimejenga ghorofa kadhaa hapa mjini (including yangu) bila nguzo na hazina tatizo hata kidogo,

Zingatio

Hakikisha tofari zinakuwa imara kama unachukua option 1. na kama hauamini tofati zako basi ni bora ukachukua option 2.

Ningejua unajenga wapi ningekueleza matofari mazuri yalipo.

spacarchitects@gmail.com

umenitia moyo sana mkuu hapo kwa red
 
Idorome, Mimi pia ni Architect,

Fundi wako yupo sahihii, msikilize, ila zingatia ubora wa udongo hapo unapojenga hiyo nyumba yako.

Nyumba ya ghorofa moja haiitaji nguzo, ni kwa kufuata kasumba watu hujenga nyumba na nguzo, unaweza kujenga ghorofa moja bila nguzo, binafsi nimejenga ghorofa kadhaa hapa mjini (including yangu) bila nguzo na hazina tatizo hata kidogo,

Zingatio

Hakikisha tofari zinakuwa imara kama unachukua option 1. na kama hauamini tofati zako basi ni bora ukachukua option 2.

Ningejua unajenga wapi ningekueleza matofari mazuri yalipo.

spacarchitects@gmail.com

Wewe ni architect lakini hujui spelling za neno TOFALI!!!
 
Hamna ki2 kama icho katika elimu ya uhandisi floor 1 kubebwa na tofali za kulala kinachofanyika ni kuangalia span almost less than 3m ndo angalau inaweza bebwa na tofali za kulala, na pia ki2 kingne ni imposed load(yaani mzigo)unaotegemewa kuwekwa na mtumiaji. In short usipende kumsikiliza fundi pasipo kupata technical detail kutoka kwa wataalamu (wahandisi) wa ujenz ki2 fundi anachokifanya ni ujenzi wa mazoea na si kitalaamu for more detail
Contact me.0659497070
 
Acha uongo kama huo na kama wewe ni engineer na kudisqualify hustail kuitwa mwandisi bali ni fundi wa darasa la saba. Na kama wewe ni archtect endelea kudesign hayo maboksi yako usipende kuingilia issu za uhandisi kwan kazi yako ni kusimamia frame work ya mchoro wako including vipimo,material quality na si kufanya kazi za structural,electrical or mechanical engineering
over mwenye uelewa na aelewe ivyo na asiye elewa anitafute ntamwelekeza zaidi ovaaa
 
Hello wakuu, kuna rafiki yangu ameezua slab yake ya ghorofa, kwa hiyo ana mirunda 500 na kila mmoja anauza 1300, marin boards 18mm 35 @ 30000 na mbao 4X2 zipo 100 kwa 3500, zote zimetumika mara moja, na site ipo tegeta salasala kwa anayependa ni PM nikuunganishe kama wataka kuziona na kununua
 
Zemacopolo hili gorofa lina ukubwa gani?

Linapokuja swala la slab kusema kwelie size matters yaani kama unataka mambo ya sqrm 180 basi andaa mfuko wa kutosha kwani kushona mkeka wa jamvi pale panalika sana nondo za 12mm na hazikimbiliki zitalika tuu. Mimi nimejenga 144sqrm na hapo zimelika nondo za kutosha.

Nimesema hapo awali kama una forecast ya cash ya kama 20 million per phase basi gorofa unaweza kujenga. Maana msingi wa gorofa utakula kuanzia 20 million kisha kujenga mpaka kwenye slab haifiki hata 8 million, then slab at least 25 million then unapandisha kwa at least 8 million then kufunika add another 15 million. hapo kama 70 million inakuwa imesimama. Baada ya hapo tukutane kwenye finishing.

Ukijipanga unaweza kaka. Nimimi nimethubut na nasema yoyote anaweza akijipanga.
Mkuu kwa hilo ghorofa la 144sqm, ulitumia tofali kama ngapi kwenye msingi tu?
 
mkuu umewahi kufika zenji? Jee unayajua maghorofa ya michenzani? yale majengo yana ghorofa tano, yamejengwa zaidi ya miaka 40 iliyopita na hayakutumia hata nguzo moja. yote yamejengwa kwa kulaza tofa, pia kuna jengo jengine liko mtendeni lina ghorofa nne nalo pia halikutumia nguzo bali tofali tu zimelazwa. hivyo kwa kagorofa kamoja we laza tu tofali
Mkuu jee foundation yake inatumia nondo? Au pia saruji tu
 
Kiongozi,

Mimi niko Dar es Salaam, Kibada.

Hapo kwa mahesabu ya harakaharaka unahitaji:

Mirunda 120
Marine boards 27
Cement mifuko 65
Mchanga lori 7ton trip 2
Kokoto lori 7ton trip 3
Nondo mm12 pcs180
Nondo mm8 pcs 40
Nondo mm16 pcs 36
Mbao 2X6 pcs pcs 40
Mbao 2X2 pcs 15
Mbao 2X4 pcs 10
Ufundi - maelewano ( kusuka nondo sh. laki 2. kupiga mbao laki 2, fundi laki 2, kumwaga zege laki 2 jumla laki 8)
Jumlisha na vikorokocho vingine kama misumari etc ambavyo bei yake sio deciding factor.

Kadirio la kati jumla ni sh. mil. 8.

Gharama hii inaweza kupungua kwa kiasi kikubwa iwapo vitatumika vifaa vya kukodi au used.
Mkuu

Hebu nipe ushauri, nataka kununua nondo huku nje zishasukwa ni za kuunganisha tu. Kila sheet 2m na urefu 3m, nataka kutumia kwa foundation concrete slab na ile juu slab ya pili, nataka kujua size ya kutumia.

Nyumba nataka nitumie forali za kulaza tu. Na upana wa nyumba 7 meter na urefu 8 meter foundations
Hebu nisaidie kunipa idea ya ujenzi
1454432172000.jpg
 
Naangalia option kujaribu kujenga kighorofa kimoja japo nilale juu, fundi ameniambia nichague kati ya option mbili
  1. kulaza matofali
  2. kutumia nguzo
Namaanisha kama nikilaza matofali floor slab ya juu itakua supported na hayo matofali bila nguzo. Kama nikiopt nguzo nitasimamisha matofali kawaida, niko tutani naombeni ushauri wataalamu ujenzi nitaanza soon ndio nafanya site clearance na kukusanya vifaa. Niko jijini
Hii project ulishaimaliza....
 
Huku ni kudanganyana kwamba waweza kulaza tofari ukajenga nyumba ya gorofa moja bila nguzo wala nondo
Mkuu uliyeomba ushauri usijaribu kitu kama hicho dunia imebadilika mabadiliko ya tabia nchi na majanga ya asili vimezidi.
Tumia nguzo imara kwa nyumba imara.
 
Faida za nguzo/columns.

1.zinapokea uzito kutoka kwenye beams na kupeleka mzigo/uzito ardhini.

2.zinazuia nyumba dhidi ya upepo mkali zikisaidiwa na beam/ringbeam.
(resistance of lateral forces due to wind or very heavy convectional rainfall).

3.zinashirikiana na ground beams kulifunga jengo na hivyo kupelekea
nyufa na matatizo mengine yatokanayo na tabia za udongo/tetemeko n.k
kuthibitiwa.

4.Kutumia nguzo katika jengo ni bora zaidi kwani ulifanya jengo
liwe kama limekamatwa ardhini na foundation bases tofauti na
kutumia tofari.

5.Vilevile tunavyotumia nguzo tunazidi kulidumisha jengo
kwa muda mrefu kwani ndani ya nguzo ni lazima pawekwe
nondo kwa hesabu maalum za kitaalamu tofauti na tofari.

Hivyo basi ni bora ukatumia ujenzi wenye kutumia zege na
nondo zaidi kuliko ule wenye kutumia cement na mchanga
pekee katika ujenzi wako.
Si ghorofa tu hata nyumba za kawaida ni bora kujenga kwa kutumia nguzo. Kuna wakati nyumba unaikuta ipo chini na barabara ipo juu, hivyo ni rahisi kuipandisha kama ina Nguzo. Uimara wa nyumba ni muhimu sana. Katika ujenzi kumbuka kuwa masikini ndiye hujenga nyumba na wala si tajiri kwani mdogomdogo huimarisha nyumba kuliko kujenga fasta.
 
Si ghorofa tu hata nyumba za kawaida ni bora kujenga kwa kutumia nguzo. Kuna wakati nyumba unaikuta ipo chini na barabara ipo juu, hivyo ni rahisi kuipandisha kama ina Nguzo. Uimara wa nyumba ni muhimu sana. Katika ujenzi kumbuka kuwa masikini ndiye hujenga nyumba na wala si tajiri kwani mdogomdogo huimarisha nyumba kuliko kujenga fasta.
Complications,
Nyumba ni ya chini, hizo nguzo za kazi gani??
Au unamaanisha zile zinazokaa pale barazani??
 
Complications,
Nyumba ni ya chini, hizo nguzo za kazi gani??
Au unamaanisha zile zinazokaa pale barazani??
Siimanishi za barazani nazungumzia za kwenye kona ili ziunganike na renta. Siyo Complications mkuu ila ni kuimarisha nyumba ili kireki zisikunyime usingizi
 
Inawezekana mkuu umeshamaliza hii project ile kwa faida ya wengine pia, options alizotaja mtoa mada zinakubalika isipokua tu ni lazima utambue kuna Fundi sio msemaji wa mwisho. Kama una architectural drawings tayari ni lazima upate na engineering drawings.
 
Siimanishi za barazani nazungumzia za kwenye kona ili ziunganike na renta. Siyo Complications mkuu ila ni kuimarisha nyumba ili kireki zisikunyime usingizi
Renta ni kodi au? linter sema
 
Back
Top Bottom