Ujenzi wa Uwanja wa Mpira Dodoma kwa msaada wa Mfalme wa Morocco umeishia wapi?

Ujenzi wa Uwanja wa Mpira Dodoma kwa msaada wa Mfalme wa Morocco umeishia wapi?

Mkuu kwani pale Dodoma tulitaka kujenga kwa pesa zetu?
Unaweza kumpangia cha kufanya yule anayekuja kukusaidia?
Mfalme mwenyewe (baada ya kufurahi) aliaahidi kutujengea buree uwanja mkubwa wa kisasa pale Dodoma.
Waswahili na msemo wetu
Ahadi ni Deni ila naona alitoa ila waizi wakaweka mifukoni
Au walimpiga Mfalme na ile miradi hewa wakasema leta asilimia kadhaa tuanze nazo wakauchuna na hataki kutusikia kabisa

Yaani ukweli utakuja kujulikana siku moja
 
Vipi maulid, ulikuwa upande gani katika munaqasha wa Mombasa, wanaoipinga au wanaoiunga mkono?
Sina upande, mimi ni Muislam. Wote wale wanajitahidi kwa namna yao na sina tatizo na wote.

Unafahamu walichokuwa wanabishana ni kipi? Maana naona umeitaja "Maulid" mimi nimeuona huo mnakasha, sikuona kuwa pale walikuwa wanapingana kuhusu Maulid. Rudia kuutazama.
 
karibu kwenye Uislam, siku ya kwanza utayoingia kwenye Uislam utaanza kuihisi raha yake.
Nijibu kwanza sababu za kitabu chenu kuandika kuwa jua unazama kwenye matope.


Sura ya Al-Kahf (Sura ya 18) verse 86


"حَتَّىٰ إِذَا بَلَغَ مَغْرِبَ الشَّمْسِ وَجَدَهَا تَغْرُبُ فِي عَيْنٍ حَمِئَةٍ وَوَجَدَ عِندَهَا قَوْمًا ۗ قُلْنَا يَا ذَا الْقَرْنَيْنِ إِمَّا أَن تُعَذِّبَ وَإِمَّا أَن تَتَّخِذَ فِيهِمْ حُسْنًا"

Nipe jibu
 
Tanzania haijali vipaumbele vya kwanza ambacho ni kuondoa Umasikini kwanza, ukiondoa umasikini wananchi wanajenga wenyewe hivyo viwanja.
Mfalme aliahidi kujenga kiwanja, sio pesa za serikali.
 
Wahuni Tu
Wahuni waliokula advance
Maana palitayarishwa kijengwe sehemu Inaitwa Nala njia kuelekea Singida mara puu Nzuguni kuelekea Moro

Mfadhili machale yakamcheza

Hapo nani Muhuni?!!

Bongo Nyoso hamfai kuanzia juu mpakabalozi wa mtaa na wananzego wote vicheche

Kilamtu anakula Kwa Urefu wa kamba yake
 
Unafahamu walichokuwa wanabishana ni kipi?
1695964985331.png
 
Huenda kuna mambo yamenipita, nimeona niulize hapa.

Ninakumbuka takribani miaka mitano iliyopita kulitokea ujio wa Mfalme wa Morocco hapa Tanzania wakati wa kipindi cha utawala wa Magufuli na ulikwenda sambamba na utiaji wa saini wa mikataba zaidi ya 10 (ambayo hatukuambia kwa kina kila mkataba unahusu nini) na mfalme yule kwa furaha akaahidi kutujengea mara moja msikiti mkubwa sana na uwanja wa kisasa sana pale Dodoma, tena bure!

Sasa muda umepita, kuna ukimya mzito, ahadi ya ujenzi wa uwanja upo kimya mnoo. Nini kinaendelea?
Mfalme wa Morocco ametutapeli kwa maneno? Mfalme katoa pesa na wajanja wa kijani wamezitafuna gizani?

NOTE: Tanzania (kwa kushirikiana na Kenya na Uganda) tunataka kuwa wenyeji wa AFCON 2027, na mkakati ni kuwa na viwanja vitatu, Uwanja wa Mkapa upo tayari unahitaji marekebisho machache), Zanzibar tayari wanarekebisha uwanja wao, hivyo kunabakia upungufu wa uwanja mmoja, na sasa tumesikia serikali imeanza mpango wa kujenga uwanja mpya Arusha, hivyo mabilioni ya pesa yatabidi kutengwa kwa kazi hiyo.
Mfalme wa Morocco hawezi tena kujenga kiwanja cha mpira maana nchi yake imekumbwa na tetemeko lililosababisha vifo vya maelefu ya wananchi na miundo mbinu kuharibiwa vibaya sana.

Walioko madarakani sasa hivi wanaelekeza nguvu nyingi Dar Es Salaam badala ya kuhakikisha kwanza Dodoma umekaa swa katika kila mahitaji ya miundo mbinu ya viwanja vya mpira, ndege, barabara, mashule, hospitali, na huduma zingine za kijamii zikidhi mahitaji na kushawishi mabalozi kuhamia huko ambako JPM aliwapa vinja vilivyopimwa bure.
 
Ilikuwa ahadi wakati wa vita ya kiuchumi,kwasasa vita hamna tena so ile ahadi imekufa
 
Wakati wa utawala wa magufuli nakumbuka tulitangaziwa kuwa mfalme wa morrocco atatujengea uwanja mkubwa wa mpira mkoa wa dodoma sijui ile ishu iliishia wapi...
Huenda ahadi ilitimizwa ila kuna wahuni waligawana mapato ya ahadi baada ya Magufuli kupumzika kwa amani.

Kwa sasa wapigaji wapo mstari wa mbele kula kwa urefu wa kamba zao.
 
Back
Top Bottom