Ujerumani yaruhusu upelekwaji wa vifaru vya Leopard 2 nchini ya Ukraine

Ujerumani yaruhusu upelekwaji wa vifaru vya Leopard 2 nchini ya Ukraine

Mtanga90

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2022
Posts
238
Reaction score
460
Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Anna Baerbock amesema "hatoizuia " Poland ikiwa itatuma vifaru vya Leopard 2 nchini Ukraine.

Ukraine imetoa wito kwa nchi za Magharibi kutoa vilivyotengezwa na Ujerumani ambavyo wanasema ivtawasaidia kuishinda Urusi.

Lakini Ujerumani bado haijatoa magari ya kivita, na sheria zake za usafirishaji wa silaha zinazuia nchi zingine kutuma zao.

Siku ya Jumapili, Bi Baerbock alisema Poland ilikuwa bado haijaomba ruhusa ya kuuza silaha hiyo nje.

"Kwa sasa swali halijaulizwa, lakini ikiwa tungeulizwa hatatuzuia ," aliiambia LCI TV ya Ufaransa Jumapili.

Wiki iliyopita, waziri mkuu wa Poland Mateusz Morawiecki alisema nchi hiyo iko tayari kutoa vifaru 14 ya Leopard 2 kwa Kyiv ikiwa Berlin itawaruhusu kufanya hivyo.

"Uwezo wa kutetea uhuru nchini Ukraine unaweza kutegemea hilo," alisema.

Vifaru vya Leopard 2 viliundwa mahsusi kushindana na vifaru vya Urusi T-90, ambavyo vinatumika katika uvamizi.

Inaaminika kuna zaidi ya 2,000 duniani kote na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alisema takriban 300 kati yavyo vitasaidia kuhakikisha kushindwa kwa Urusi.

Nchi nyingi washirika zimechanganyikiwa na Ujerumani kwa kusita kwake kutuma vifaru vyake vya Leopard 2.

Chini ya kanuni za sasa, Ujerumani lazima pia iidhinishe usafirishaji wowote wa vifaru vyake na nchi zingine, kama vile Poland.

Kufuatia mkutano wa zaidi ya nchi washirika 50 siku ya Ijumaa, Ujerumani ilikuwa bado haijajitolea kusambaza vifaru hivyo wala kutoa leseni ya kuuza nje. Lakini ilikanusha kuzuia usafirishaji wa vifaru hivyo kwa upande mmoja.

Katika taarifa ya pamoja siku ya Jumamosi mawaziri wa mambo ya nje wa Estonia, Latvia na Lithuania waliiambia Ujerumani "kutoa vifaru vya Leopard kwa Ukraine sasa".

Kwa nini vifaru Leopard inahitajika sana?

Kifaru cha Leopard 2 ni silaha ya kiwango cha kimataifa inayotumiwa na zaidi ya nchi kumi na mbili.

Ukraine inaona kifaru hicho kama sehemu nyingine muhimu ya ulinzi wake dhidi ya vikosi vya Urusi na Leopards zimetumiwa kivita nchini Afghanistan na Syria.

Kinachowafanya zivutie zaidi Kyiv ni kwamba karibu theluthi mbili ya Leopards zote zinazozalishwa bado ziko Ulaya. Kwa hivyo kupata Leopards kwenye mapambano ni jambo la moja kwa moja. Hilo pia hurahisisha matengenezo na ukarabati - vipengele muhimu vya mfumo wowote wa silaha.

Inafaa kukumbukwa katika haya yote kwamba Ujerumani inaipa Ukraine mifumo muhimu ya ulinzi wa anga, kama vile IRIS-T na makombora ya kutoka ardhini hadi angani ya Patriot, pamoja na magari ya kubeba wanajeshi

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz hapo awali amekuwa na mashaka juu ya ushiriki wa Ujerumani katika mizozo ya kijeshi, na ana wasiwasi juu ya kuchochea mzozo huo na kuihamakisha Urusi .

Kansela huyo alikutana na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron mwishoni mwa juma kusisitiza muungano wa nchi hizo mbili baada ya vita.

Ufaransa tayari imejitolea kupeleka mizinga mepesi kwa Ukraine, na Bw Macron alipendekeza kuwa inawezekana kwamba mizinga mikubwa ya Leclerc iliyotengenezwa na Ufaransa inaweza pia kuwasilishwa Ukraine.

Nchi nyingine zimejitolea kutuma mizinga, ikiwa ni pamoja na Uingereza, ambayo itatuma Challenger 2 14.

25cb0c90-9b01-11ed-8caa-69b4e6848359.jpg
 
Ujerumani walikua wanasita kutuma hivi vifaru maana siku zote nia yao ilikua kuisaidia Ukraine kujilinda, ila hivi vifaru balaa yake ni kwamba Ukraine sasa atakua na uwezo wa kupelekea mashambulizi, kwa kifupi sio kujilinda tena ila kulianzisha na kupiga.

Wasiwasi wa Ujerumani ni kwamba Ukraine wanaweza wakanogewa na kumfuata Mrusi mpaka Urusi ndani na kupitiliza Crimea hadi kukoleza vita na kubadilisha hali ambayo dunia inaweza ikaja kujutia maana Mrusi akipelekwa sana ndani anaweza akabonyeza manyuklia.

Nia ilikua kumfikisha Mrusi pale Crimea, ila asipigwe hadi ndani, na Ukraine hawajahakikishia kwamba hawatanogewa.

Hiki kifaru ni balaa sana

e57e8cf5d19e9cfdbdd2f3574cfe81be.jpg

====================

German Chancellor Olaf Scholz has decided to send Leopard 2 tanks to Ukraine, and allow other countries to do the same, reports in Germany say.
Leopard 2s are made in Germany and Berlin needs to approve their export.

Germany has been hesitant to send its own - or allow other nations to send theirs - over concerns it could escalate the conflict with Russia.

But now Mr Scholz has decided to send the at least a company of Leopard 2 A6 tanks, several German outlets say.
 
Hii Ni ishara nzuri kwa uungwaji Mkono wa Ukraine. Lakini hizi nchi ziwe Serious bhana. Unatumaje vifaru 14 tu? Urusi ameingiza zaidi ya vifaru 4000 nchini Ukraine japo zaidi ya 2000 vilishasambaratishwa na MANPADS za Ukraine. Kwahiyo Urusi ana vifaru zaidi ya 2000 nchini Ukraine vilivyoko mstari wa mbele.Sasa vifaru 14 vya Leopard vinawezaje kupambana na vifaru 2000 vya Urusi?

Ukraine inahitaji walau vifaru 400 vya Leopard ili kuirudisha nyuma jeshi la Urusi.
 
Hivi nyinyi mnao sema hivyo vifaru vya ujerumani havita wasaidia wanajeshi wa Ukraine hivi mnajua wale wanajeshi wa urusi walio kuwa wanavaa makanzu ndio wanaingia vitani walikua wanajiita sijuia chemu chem mnajua walipotelea wapi.
 
Hii Ni ishara nzuri kwa uungwaji Mkono wa Ukraine. Lakini hizi nchi ziwe Serious bhana. Unatumaje vifaru 14 tu? Urusi ameingiza zaidi ya vifaru 4000 nchini Ukraine japo zaidi ya 2000 vilishasambaratishwa na MANPADS za Ukraine. Kwahiyo Urusi ana vifaru zaidi ya 2000 nchini Ukraine vilivyoko mstari wa mbele.Sasa vifaru 14 vya Leopard vinawezaje kupambana na vifaru 2000 vya Urusi?

Ukraine inahitaji walau vifaru 400 vya Leopard ili kuirudisha nyuma jeshi la Urusi.

Mataifa ya magharibi yamekua yakiepuka kuisaidia Ukraine na silaha zenye uwezo wa kufanya escalation, wamekua wakisaidia tu kwa silaha zinazosaidia kwenye kujilinda, kwa mfano HIMARS inapiga ikiwa eneo moja, ila vifaru vinavamia kabisa mbele kwa mbele, imebidi sasa Ukraine wawezeshwe zaidi maana kwa Urusi kutuma wanajeshi 300,000 ambao aliokota mtaani, ni dhahiri Putin anataka viwe vita vya muda mrefu, na atapoteza sana.
 
Poland wanawashwa sana

Uwezo wenywewe wa kubattle wao kama wao hawana
 
Ujerumani walikua wanasita kutuma hivi vifaru maana siku zote nia yao ilikua kuisaidia Ukraine kujilinda, ila hivi vifaru balaa yake ni kwamba Ukraine sasa atakua na uwezo wa kupelekea mashambulizi, kwa kifupi sio kujilinda tena ila kulianzisha na kupiga.

Wasiwasi wa Ujerumani ni kwamba Ukraine wanaweza wakanogewa na kumfuata Mrusi mpaka Urusi ndani na kupitiliza Crimea hadi kukoleza vita na kubadilisha hali ambayo dunia inaweza ikaja kujutia maana Mrusi akipelekwa sana ndani anaweza akabonyeza manyuklia.

Nia ilikua kumfikisha Mrusi pale Crimea, ila asipigwe hadi ndani, na Ukraine hawajahakikishia kwamba hawatanogewa.

Hiki kifaru ni balaa sana

e57e8cf5d19e9cfdbdd2f3574cfe81be.jpg

====================

German Chancellor Olaf Scholz has decided to send Leopard 2 tanks to Ukraine, and allow other countries to do the same, reports in Germany say.
Leopard 2s are made in Germany and Berlin needs to approve their export.

Germany has been hesitant to send its own - or allow other nations to send theirs - over concerns it could escalate the conflict with Russia.

But now Mr Scholz has decided to send the at least a company of Leopard 2 A6 tanks, several German outlets say.
NATO mmeanza lini kutoa misaada na imesaidia kitu gani? saivi mmekuja na mbinu ya kijinga kuficha silaha karibu na maghala au viwanda vya Nuklia maana mwanzoni walivyoficha kwenye makazi ya watu walitunguliwa hukohuko na ni suala la muda tu. Hizo silaha zitatunguliwa kwenye hayo maghala na madhara yatawarudia wa ukreine wenyewe
 
NATO kwa mikwala tu awajambo. Stori za aina hii tumeanza kuzisikia toka kuanza kwa vita. Hivyo vifaru vitakapoanza kupigwa viberiti msije na excuse. Russia sio Bulgaria
Kama sio Bulgaria mbona zile siku tatu haziishi hadi wanalazimisha raia wa nchi zingine kuwasaidia kupigana. Bure kabisa.
 
Back
Top Bottom