Ujio wa SGR tishio kwa mabasi? Inabeba abiria 4000 sawa na trip 70 za mabasi

Ujio wa SGR tishio kwa mabasi? Inabeba abiria 4000 sawa na trip 70 za mabasi

Kipya kinyemi serikali hii imejaa uswahili,local people na mundane politicians ambao ndiyo wafanya biashara, train Hilo litahujumiwa ovyo ovyo utaona,hii nchi ya ovyo Sana ,self aggrandization ndo zinatawala,hivi Leo mabasi ya mwendo Kasi yako mangapi barabarani
 
Uswahiba,uswahiba! Nepotism, Nepotism, Nepotism, self aggrandization is going to kill the so called TRC public parastatals
 
Ndio maana nimeweka wahanga wakuu mkuu, Shabiby na Abood.. Ni njia yao kuu ya mapato. Though wengine wataathirika, basi zitazokosa wateja Dar-Moro-Dom zitaenda kubanana kwenye njia mpya..
Wahamie kusafirisha wilayani na mikoa mingine, Tanzania ni kubwa sana
 
Taarifa ya TRC imesema kwasasa treni ya mwendokasi inabeba wastani wa abiria 4000 kwa siku, hizi ni sawa na trip 70 za mabasi yenye uwezo wa kubeba abiria 57 kwa wakati mmoja.

Kituo kinachofata kitakuwa Dodoma pale mambo yatakapokamilika. Abood na Shabiby nadhani watakuwa waathirika wakuu kwenye hii saga.


Kiuchumi ina-save muda wa wasafiri, usalama ukizingatia usafiri wa reli ni salama zaidi kuliko barabara, inapunguza uchakavu wa barabara hasa ikianza kusafirisha mizigo. Upande wa pili itafinya sekta binafsi ya usafirishaji kwa wamiliki na wote wanaofaidika na mzunguko huo kama wakata tiketi, wahudumu, madalali, madereva na wamiliki wake wa malori na mabasi.

Hofu yangu ni kubakisha standard na sabotage kutoka kwa wafanyabiashara wa mabasi na malori, TRC watatoboa kweli?
Nadhani itabidi wabafilishe business model zao wahudumie maeneo ambayo hayana reli na ni mengi tu
 
Tanzania bado ni kubwa sana. Sio kila kitu ni Dar Dodoma.

Wanaweza anzisha Route ya Dodoma Mwanza, musoma, Bukoba, Arusha, moshi,kigoma,katavi nk.
Zile route zinazopita Dodoma kuja Dar. Waishie Dodoma watu wapande treni

Kuhusu mizigo. Maroli yaishie Dodoma. Mizigo isafirishwe kuelekea Dar na treni za mizigo wakati wa usiku.
Dodoma itakuwa na real Capital city
Kwa hiyo machungwa ya kutoka muheza tanga yaende Dodoma ili yasafirishwe na SGR?

Uchawa ukizidi unakua uenda-wazimu
 
Mbona tayari mambo yameishaanza mdogo mdogo.
Baada ya kuona watu wengi wanaotumia treni ya asubuhi na jioni kiwepo mimi mwenyewe kutoka Dar to Moro , na kuona inawasaidia sana watu tayari wameamua kuibadirisha nauli zake kuwa 20,000/= na kudai hiyo ni tran ya Express.
Na ile ambayo haina abiria wa kutosha ndio inaondoka saa tatu.
Na kuna tetesu kuwa hizo bei zitabadilika muda si mrefu na kuongezwa.
 
All that is immaterial Swali la maana zaidi je ni affordable ? Na kabla haujajibu kumbuka kwamba hii ni huduma na necessarily sio luxury
 
Kipya kinyemi serikali hii imejaa uswahili,local people na mundane politicians ambao ndiyo wafanya biashara, train Hilo litahujumiwa ovyo ovyo utaona,hii nchi ya ovyo Sana ,self aggrandization ndo zinatawala,hivi Leo mabasi ya mwendo Kasi yako mangapi barabarani
Kwa nauli niliyoisikia leo, Hilo Treni sasa ni kwa wenyenazo. Turudi tu kwenye mabasi kwani kilio chao ndo kimesikiwa.
 
Mbona tayari mambo yameishaanza mdogo mdogo.
Baada ya kuona watu wengi wanaotumia treni ya asubuhi na jioni kiwepo mimi mwenyewe kutoka Dar to Moro , na kuona inawasaidia sana watu tayari wameamua kuibadirisha nauli zake kuwa 20,000/= na kudai hiyo ni tran ya Express.
Na ile ambayo haina abiria wa kutosha ndio inaondoka saa tatu.
Na kuna tetesu kuwa hizo bei zitabadilika muda si mrefu na kuongezwa.
Yametimia!
 
Upande wa pili itafinya sekta binafsi ya usafirishaji kwa wamiliki na wote wanaofaidika na mzunguko huo kama wakata tiketi, wahudumu, madalali, madereva na wamiliki wake wa malori na mabasi.
Mbona imeanza kulalamikiwa ikiwa bado mbichi
 
Back
Top Bottom