Ujumbe kwa Prof. Assad: Hatutaki Rais anayesikiliza kila mtu na la kila Mtu!

Ujumbe kwa Prof. Assad: Hatutaki Rais anayesikiliza kila mtu na la kila Mtu!

wabongo tunataka Rais wa aina gani? anaesikiliza au asiesikiliza? tusifungane midomo tupige kura tujuane!!
Tunataka Katiba mpya ya nchi, ambayo itapunguza madaraka makubwa mno ya Rais aliyopo madarakani, mithili ya mungu-mtu!

Siyo kwamba tunataka Rais asikilize au asisikilize, bali afuate Katiba mpya ya nchi itakavyomtaka afanye mambo ya utumishi wa Umma. OVA
 
Pamoja na yoooote hayo lakini kuna shida naanza kuiona kwa babu Assad ni mtu wa kinyongo balaa bado ana mduku duku huoo😂 ilimpasa aongee yote siku moja kisha atulie zake lakini hii kila siku mara hiki mara kile atakuja atoe boko tutafutane hapa
 
Katika nchi 3 ambazo zitakua za mwisho kuendelea Africa au duniani ni pamoja na Tanzania. Sishangai tupo miongoni mwa mchi masikini sana duniani regardless rasilimali tulizonazo. Nchi hii ina tatizo kubwa la uongozi, ukitaka kunyoosha mambo utaitwa kila aina ya jina.
 
Mwanakijiji hajapinga katiba mpya ,muwe mnasoma na kuelewa,yeye anapingana na maoni ya professor Assad,ya kutaka kulazimisha mkuu wa nchi asikilize na kutetekeleza kila ushauri anaopewa.
Ndio maana mwanakijiji akasema hata katiba mpya ikija haitamlazimisha rais kufuata ushauri wa kila mtu.
Someni muelewe kwanza kabla ya kujibu hoja ya mleta mada
"Kutekeleza Kila ushauri anaopewa" Ndivyo alivyosema Prof?
 
Binafsi nikupe mfano mzee mwanakijiji:
Raia wanahitaji katiba ambayo Rais kama binadamu anaweza kudhibitiwa katika baadhi ya mazingira mfano mzir ni Rais Trump alipotaka kujenga ukuta wa Mexico kwakua wawakilishi waliona sio kipao mbele waligoma na still Rais inabdi asikilizeaoni ya wengi
 
Tatizo halipo kwenye kusikiliza au kutokusikiliza...., TATIZO lipo kwenye mambo mengi kuwepo kwa mtu mmoja (Ufalme) kwahio Rais inabidi apunguziwe meno na hayo Meno kupewa Taasisi...

Hakuna mtu mmoja mwenye akili au uwezo kuliko watu wote, kwahio vya kufanya na kufanyika vifanywe na Taasisi / wadau na wataalamu yeye pale ni kusimamia yaliyopangwa kwa mujibu wa makubaliano na sheria na sio vinginevyo...., Yaani ikibidi apungwe meno na kubaki Kibogoyo..., hayo Meno Ipewe Mahakama na Wananchi kwa kupitia Wabunge na Wananchi wawe na uwezo wa kumuondoa Mbunge wao wakati wowote akifanya ndivyo sivyo.....
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya maajabu makubwa ni hili la watu kuamini kuwa ujio wa Katiba Mpya utawapa Rais ambaye ataweza kudhibitiwa na "taasisi". Kwamba, Katiba Mpya itazuia Rais kufanya lolote na kuwa atakuwa analazimishwa kusikiliza mashauri mbalimbali. Prof. Assad ni miongoni mwa watu ambao amejionesha kukerwa mno na jinsi Magufuli alikuwa; hasikilizi, hapigwi maneno ya wataalam, na watendaji wenye maneno ya kitalaamu. Inawezekana siyo yeye tu bali wapo wengine ambao nao walikuwa wanakerwa kuwa Magufuli "hasikilizi". Na tunawaona wengine ambao nao wanafikia mahali pa kusema "Magufuli hakufanya lolote".

Sasa, wanataka tuwe na Rais ambaye anapewa ushauri na kila mtu na anatakiwa kusikiliza kila ushauri kwani asipousikiliza au kuukubali basi anakuwa "haambiliki". Inanikumbusha maneno yaliyosemwa wakati wa Nyerere; aliitwa pia "Haambiliki". Ati Magufuli alikuwa anawakera kwa sababu walitaka awasikilize na asiwaulize; akubali bila maswali! Sasa inawezekana wanaona Rais Samia ni wa kuambiwa kila kitu; kwamba wanampa mashauri ya kila namna na anaonekana anayafuata. Inawezekana wanaona kuwa Rais Samia anawakubalia kila mashauri hata ambayo matokeo yake siyo mazuri. WAnachofurahia ni kuwa wamelipata "sikio la mama".

Ndio maana tunaweza kuona wanashindana kukandia awamu ya tano (ambayo wao walikuwemo). Inaonekana kabisa kuwa ili mama akupe sikio inabidi umpapase kwa maneno mazuri ya kumkandia mtangulizi wake. Magufuli hakujenga kiwanda hata kimoja, uwekezaji ulipungua, maisha yalikuwa Magumu, watalii walikimbia, uchumi ulidorora... wanasema na kusema ili waseme "ila sasa awamu ya sita" mambo yamekavaa vizuri! Wanajaribu kutenda kana kwamba Rais Samia alishinda uchaguzi mahali bila ya Magufuli! Lakini hawa wanaotaka Rais anayesikiliza kila ushauri inabidi tuwakatae.

Tunawapinga na kuwakataa kwa sababu wanataka kumchukua Rais kuwa mateka wa fikra zao na mashauri yao. Watamshauri akikataa wataanza kusema "Rais hatusikilizi tena". Ukweli ni kuwa Rais - hata ije Katiba Haramu Mpya - hatakiwi kukubali ushauri wa kila mtu, hata kama ni maprofesa kama Assad. Anatakiwa kusikiliza na kuuliza; hatakiwi kukubali bila maswali! Na ni hatari zaidi kumtaka Rais awafurahishe kwa kuwa karibu na watu wenye kumsifia na kumwambia mambo mazuri.

Profesa Assad na watu wenye fikra kama zake hawamtakii mema Rais, wanamtega, na wanajaribu kumfanya awe Rais wa picha!

Hili tunawakatalia; waache ufyatu!

MMM
Rais kuwa msikivu ni kupitia mamlaka za kikatiba zilizowekwa kumshauri kama Bunge.

Rais anayejaribu kulicontrol Bunge ana kuwa na tabia kama za Magufuli, si msikivu tu, bali hata sheria zinazotungwa ni kwa maelekezo.

Prof Assad ni msomi na alilopendekeza ni kwa muktadha huo.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya maajabu makubwa ni hili la watu kuamini kuwa ujio wa Katiba Mpya utawapa Rais ambaye ataweza kudhibitiwa na "taasisi". Kwamba, Katiba Mpya itazuia Rais kufanya lolote na kuwa atakuwa analazimishwa kusikiliza mashauri mbalimbali. Prof. Assad ni miongoni mwa watu ambao amejionesha kukerwa mno na jinsi Magufuli alikuwa; hasikilizi, hapigwi maneno ya wataalam, na watendaji wenye maneno ya kitalaamu. Inawezekana siyo yeye tu bali wapo wengine ambao nao walikuwa wanakerwa kuwa Magufuli "hasikilizi". Na tunawaona wengine ambao nao wanafikia mahali pa kusema "Magufuli hakufanya lolote".

Sasa, wanataka tuwe na Rais ambaye anapewa ushauri na kila mtu na anatakiwa kusikiliza kila ushauri kwani asipousikiliza au kuukubali basi anakuwa "haambiliki". Inanikumbusha maneno yaliyosemwa wakati wa Nyerere; aliitwa pia "Haambiliki". Ati Magufuli alikuwa anawakera kwa sababu walitaka awasikilize na asiwaulize; akubali bila maswali! Sasa inawezekana wanaona Rais Samia ni wa kuambiwa kila kitu; kwamba wanampa mashauri ya kila namna na anaonekana anayafuata. Inawezekana wanaona kuwa Rais Samia anawakubalia kila mashauri hata ambayo matokeo yake siyo mazuri. WAnachofurahia ni kuwa wamelipata "sikio la mama".

Ndio maana tunaweza kuona wanashindana kukandia awamu ya tano (ambayo wao walikuwemo). Inaonekana kabisa kuwa ili mama akupe sikio inabidi umpapase kwa maneno mazuri ya kumkandia mtangulizi wake. Magufuli hakujenga kiwanda hata kimoja, uwekezaji ulipungua, maisha yalikuwa Magumu, watalii walikimbia, uchumi ulidorora... wanasema na kusema ili waseme "ila sasa awamu ya sita" mambo yamekavaa vizuri! Wanajaribu kutenda kana kwamba Rais Samia alishinda uchaguzi mahali bila ya Magufuli! Lakini hawa wanaotaka Rais anayesikiliza kila ushauri inabidi tuwakatae.

Tunawapinga na kuwakataa kwa sababu wanataka kumchukua Rais kuwa mateka wa fikra zao na mashauri yao. Watamshauri akikataa wataanza kusema "Rais hatusikilizi tena". Ukweli ni kuwa Rais - hata ije Katiba Haramu Mpya - hatakiwi kukubali ushauri wa kila mtu, hata kama ni maprofesa kama Assad. Anatakiwa kusikiliza na kuuliza; hatakiwi kukubali bila maswali! Na ni hatari zaidi kumtaka Rais awafurahishe kwa kuwa karibu na watu wenye kumsifia na kumwambia mambo mazuri.

Profesa Assad na watu wenye fikra kama zake hawamtakii mema Rais, wanamtega, na wanajaribu kumfanya awe Rais wa picha!

Hili tunawakatalia; waache ufyatu!

MMM
Mzee Mwanakijiji hakika kinachoendelea Tanzania ni kama tupo kwenye ndoto. Tulijinyambulisha na kujivunia tulipo kuwa na rais mwenye uthubutu kama Dkt Magufuli, ila sasa tumerudi kuwa wanyonge wenye msongo wa mawazo hata hatujui nini kimelikumba taifa letu hasa ukifikiria aliyefariki ktk level za rais, makamu wa rais na waziri Mkuu ni mtu mmoja tu na wengine wawili na baraza lote wapo. Yaani tunaona kabisa kuna coordinated efforts ambazo zinaonekana zipo organized na serikali ya Mama Samia na zina baraka za taasisi husika.

Ila kwa ufupi inaumiza sana kuona mtu ambaye masikini wanamlilia kila siku halafu kuna ka kikundi kana mdhihaki na kushusha kashfa ambazo ni za kubumba 😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭
 
Rais ambaye hasikilizi watu wake nae hatumtaki.tumejionea miaka mitano ya tabu na mateso kama siyo Mungu kuingilia kati hali ingekua mbaya sana muda huu.
Watu wake ni kina nani?
Je hao watu wake wote kwa umoja wao wanakubaliana kwa kila hoja?
Au unaamini wana hoja moja?

Kimsingi ni Raisi pekee ndio anayewajibika kwa maamuzi yote anayofanya. Kwa kuwa yeye ndio aliyepigiwa kura.

Je kama atasikiliza kila mtu huyo mtu atakayemshauri atawajibika kwa ushauri wake kama utakuwa na matokeo mabaya?

Tambua kuna maeneo mengi ambayo Rais anatakiwa asikilize ushauri kwa mujibu wa Katiba. Hao ndio wanatakiwa kusikilizwa na watawajibika kwa ushauri walioutoa. Hebu chukua mfano huu;

1. Wewe fala mmoja ushauri jambo A lifanyike.

2. Mimi fala mwingine nashauri afanye B badala ya A

3. Halafu yule fala mwingine aseme hao wote wapumbavu tufanye C.

Halafu wote sisi hatutoulizwa kwa chochote mambo yakienda mrama afuate ushauri upi sasa wa kwako au wa kwangu au yule?

Hebu fikiria tutakuwa na Raisi wa aina gani leo kasema A kesho B keshokutwa anasema C.

Nikupe mfano wa uwajibikaji.
Rais Clinton alikuwa anaziara ya kikazi Japan. Ndege yake ikachelewa kwa nusu saa.

Wamarekani wakashangaa inakuwaje Raisi achelewe nusu saa nzima? Wakaambiwa Mpambe wa Raisi alishauri Raisi anyoe kwanza kabla ya kupanda ndege kwa kuwa muonekano haukuendana na hadhi yake.

Mpambe wa Rais aliwajibishwa kwa kusababisha msafara wa Raisi kuchelewa kwa nusu saa.

Watu wengine wanatoa maoni sio Ushauri. Wa kumshauri wapo kikatiba na kisheria na wanalipwa sio wewe au mimi vidampa..
 
wabongo tunataka Rais wa aina gani? anaesikiliza au asiesikiliza? tusifungane midomo tupige kura tujuane!!
Tunataka Rais atakayesikiliza lakini halazimiki kufuata kila ushauri atakaopewa na MTU au kikundi chochote isipokuwa kama yeye na washauri wake wakiona upo ushauri mzuri aliopewa Rais ambao unatakiwa kufanyiwa kazi !! Lazima tukubali kwamba URais ni taasisi ambayo ndani yake inao washauri wa kila fani na wanalipwa kwa kazi zao hizo !!
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Mojawapo ya maajabu makubwa ni hili la watu kuamini kuwa ujio wa Katiba Mpya utawapa Rais ambaye ataweza kudhibitiwa na "taasisi". Kwamba, Katiba Mpya itazuia Rais kufanya lolote na kuwa atakuwa analazimishwa kusikiliza mashauri mbalimbali. Prof. Assad ni miongoni mwa watu ambao amejionesha kukerwa mno na jinsi Magufuli alikuwa; hasikilizi, hapigwi maneno ya wataalam, na watendaji wenye maneno ya kitalaamu. Inawezekana siyo yeye tu bali wapo wengine ambao nao walikuwa wanakerwa kuwa Magufuli "hasikilizi". Na tunawaona wengine ambao nao wanafikia mahali pa kusema "Magufuli hakufanya lolote".

Sasa, wanataka tuwe na Rais ambaye anapewa ushauri na kila mtu na anatakiwa kusikiliza kila ushauri kwani asipousikiliza au kuukubali basi anakuwa "haambiliki". Inanikumbusha maneno yaliyosemwa wakati wa Nyerere; aliitwa pia "Haambiliki". Ati Magufuli alikuwa anawakera kwa sababu walitaka awasikilize na asiwaulize; akubali bila maswali! Sasa inawezekana wanaona Rais Samia ni wa kuambiwa kila kitu; kwamba wanampa mashauri ya kila namna na anaonekana anayafuata. Inawezekana wanaona kuwa Rais Samia anawakubalia kila mashauri hata ambayo matokeo yake siyo mazuri. WAnachofurahia ni kuwa wamelipata "sikio la mama".

Ndio maana tunaweza kuona wanashindana kukandia awamu ya tano (ambayo wao walikuwemo). Inaonekana kabisa kuwa ili mama akupe sikio inabidi umpapase kwa maneno mazuri ya kumkandia mtangulizi wake. Magufuli hakujenga kiwanda hata kimoja, uwekezaji ulipungua, maisha yalikuwa Magumu, watalii walikimbia, uchumi ulidorora... wanasema na kusema ili waseme "ila sasa awamu ya sita" mambo yamekavaa vizuri! Wanajaribu kutenda kana kwamba Rais Samia alishinda uchaguzi mahali bila ya Magufuli! Lakini hawa wanaotaka Rais anayesikiliza kila ushauri inabidi tuwakatae.

Tunawapinga na kuwakataa kwa sababu wanataka kumchukua Rais kuwa mateka wa fikra zao na mashauri yao. Watamshauri akikataa wataanza kusema "Rais hatusikilizi tena". Ukweli ni kuwa Rais - hata ije Katiba Haramu Mpya - hatakiwi kukubali ushauri wa kila mtu, hata kama ni maprofesa kama Assad. Anatakiwa kusikiliza na kuuliza; hatakiwi kukubali bila maswali! Na ni hatari zaidi kumtaka Rais awafurahishe kwa kuwa karibu na watu wenye kumsifia na kumwambia mambo mazuri.

Profesa Assad na watu wenye fikra kama zake hawamtakii mema Rais, wanamtega, na wanajaribu kumfanya awe Rais wa picha!

Hili tunawakatalia; waache ufyatu!

MMM
Kati ya Prof Assad na wewe Mzee Mwanakijiji naona wewe ndiyo IMEFYATUKA vibaya. Hivi kweli unathubu kuunga mkono maamuzi ya KIIMLA yaliyofanywa na Magufuli kama Jeshi kuingia biashara ya korosho, kuwabomolea nyumba wakazi wa Kimara-Kinamba bila fidia, kujenga uwanja wa 3km runway kijijini kwake Chato, kukataa kutunza takwimu za COVID-19 na kuwapima Watanzania.

Rais ana wasaidizi wake na wapo pale kumsaidia. Hakuna binadamu anayejua kila kitu.

Hatutaki turudi kwenye ile hali ya ya yule hayawani tuliyemzika Chato ambaye akiamua kukupiga risasi anatuma kikundi chake kama alivyomfanyia Tundu Lissu
 
Raisi anapaswa kusikiliza wataalamu kisha apime na kufanya maamuzi. Atawajibika kwa maamuzi yake ikiwa ataenda kinyume na ushauri wa kitaalamu kwa mujibu wa sheria.
Kwa hiyo kwa vile watalaamu wanashauri asiende kinyume nao?
 
Kwamba Assad na wengineo wakisema kuwa Magufuli alikuwa hasikilizi maneno ya wataalamu, haimaanishi kuwa "Sasa, wanataka tuwe na Rais ambaye anapewa ushauri na kila mtu na anatakiwa kusikiliza kila ushauri kwani asipousikiliza au kuukubali basi anakuwa "haambiliki". "
Hata huo ushauri anaopewa Rais na wataam ni lazima uendane na misingi ya sheria na katiba! Mfano mzuri wa ushauri ambao Magufuli angetakiwa kupewa ni kwamba alikuwa anakiuka taratibu kutumia pesa kwa miradi ya utashi wake bila idhini ya bunge! Kama Bunge ingekuwa taasisi imara kitendo cha kukiuka ushauri huo kingempelekea bunge kumchukulia hatua ya impeachment!
 
Naunga mkono hoja. Katiba mpya haiwezi kutuondelea changamoto!!!
 
ukweli mpaka sasa Watanzania hatujajua tunataka nini, hata hicho tunachotaka tukipewa bado tutasema hapana hatukutaka hivi..

Kifupi, Watanzania ni kama binadamu aliyeruka stage katika ukuaji wake, binafsi naamini zipo stage ambazo Watanzania na WaAfrica tumeziruka na ndio chanzo cha kila kero tuliyonayo leo hii..

Yapo ya msingi sana yanayoonekana live ambayo kwa nguvu zetu wote tungeyapambania tungeweza kujinasua.... Mfano ELIMU DUNI KWA WATU WETU NI JANGA MPAKA SASA, kwa pamoja tungepigania hili kuna mambo tungeweza kuweka sawa sawia kabisa bila hata hii Katiba mpya.

MENTALITY YA KUJITEGEMEA NA WATU KUFANYA KAZI KWA BIDII, hili nalo halina na halihitaji Katiba mpya ila linaweza kuanza sasa au leo, Watu wote wafanye kazi kwa bidii na akili zetu zitoke kwenye mentality ya kumtegemea Mzungu baadala yake turudi kwenye akili za kujitegemea na kuwajenga watu wetu huko..

UZALENDO NA UPENDO BAINA YA WATANZANIA WENYEWE, sidhani kama hili nalo ambalo pia ni tatizo kwenye jamii linahitaji katiba mpya na ikija watu ndio watakuwa Wazalendo...Watanzania wenyewe kwa wenyewe tuna tatizo la kutopendana na kutokuwa wazalendo kwa Taifa letu kiasi.... Mentality hii inahitaji nguvu ya pamoja na mipango ya pamoja ili wote tulipende taifa letu na wenyewe pia kama watanzania tupendane popote pale...
 
Kwa hiyo kwa vile watalaamu wanashauri asiende kinyume nao?
Kuna wataalamu hapa Tanzania? Wangekuwepo yaliyokuwa yanafanyika awamu ya nne walikuwa hawaoni hadi taifa likafika hapo lilipofikia..kila mtu anataka kuiba hata vitu vyake mwenyewe..nchi hii haina wataalam imejaa wajinga tu, waliojaza elimu ya makaratasi kichwani..maarifa zero! wanachoweza sana ni kulamba viatu na kusifia sifia hata yasiyohitaji kusifiwa!
 
Back
Top Bottom